Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 9/1 uku. 7
  • “Washika-Ukamilifu” Mikusanyiko katika Ufilipino

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Washika-Ukamilifu” Mikusanyiko katika Ufilipino
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Mikusanyiko Uthibitisho wa Udugu Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Njoni Kwenye “Ongezeko la Ufalme” Makusanyiko ya Wilaya ya 1984!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Njia ya Mungu ya Maisha” Mkusanyiko wa Wilaya na wa Kimataifa wa 1998
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Yehova Anawakutanisha Watu Wake Wenye Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 9/1 uku. 7

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

“Washika-Ukamilifu” Mikusanyiko katika Ufilipino

MFULULIZO wa mikusanyiko 23 ya mwaka 1985 ya “Washika-Ukamilifu” iliyofanywa katika Ufilipino ilipata mafanikio ya ajabu kwa kila njia. Hudhurio lililounganishwa la watu 213,734, ambalo ni ongezeko la asilimia 27 juu ya tarakimu ya mwaka uliopita, lilikuwa zaidi ya mara mbili na nusu za hesabu ya jumla ya wahubiri waliomo nchini. Jambo hilo linaonyesha kwamba kuna watu wengi wanaopendezwa wenye kuhudhuria mikusanyiko. Pia, watu 2,223 walibatizwa, hiyo ikiwa ni asilimia 14.5 juu ya mwaka uliopita.

Katika Tuguegarao Cagayan, ilitazamiwa kwamba watu 12,000 ndiyo wangehudhuria mkusanyiko, lakini 24,327 wakaja! Kituo kimoja cha redio kilifanya mahoji ya dakika 30 pamoja na akina ndugu, na bila shaka jambo hilo lilisaidia kutokeza hudhurio hilo zuri sana. Mwenye kuhoji aliuliza ni jinsi gani sisi tunafanikiwa kudumisha amani na utaratibu kwenye mikusanyiko yetu. Akaelezwa kwamba washiriki wote wa Tengenezo letu wanajitahidi kufuata kanuni za Biblia za upendo na amani. Kwa hiyo wakati wo wote tunapokuwa na mikusanyiko kama huo, hakuna kugombana-gombana. Mwenye kuhoji alistaajabu akasema: “tengenezo lenu ni zuri kama nini! Matengenezo mengine hayawezi kufanya hivi. Wakati wo wote yanapokuwa na mkutano wa watu wengi kama huu, sikuzote kunakuwa na visa vibaya.”

Kwenye mkusanyiko uo huo, mwalimu mmoja kwenye Chuo Kikuu cha Mkoa wa Cagayan alitoa maoni haya: “Hudhurio lilikuwa kubwa sana; wajumbe walikuwa wenye nidhamu; kulikuwa na ushirikiano kati yao; walionyesha kujitoa kamili kwa huduma. Ijapokuwa wajumbe walikuwa wengi sana, mahali penyewe palikuwa peupe-pe kwa usafi; kulikuwa na utaratibu na hakuna visa visivyofaa vilivyotukia, na hiyo inathibitisha tu kwamba Mashahidi wanafuata kidini mambo wanayojifunza kutokana na Maandiko.”

Mwenye kutoa ruhusu ya kukusanyika kwenye Uwanja wa Rizal wa Ukumbusho katika Manila alieleza hivi wakati wa mkusanyiko: “Mimi navutwa na mpango wa kusanyiko lenu. Sosaiti yenu ina mipango iliyotengenezwa vizuri, na ni sasa tu kwamba mimi nimeshuhudia aina hii ya utaratibu wa Mashahidi kwa sababu ni sasa tu mimi nimeona kusanyiko kama hili.”

Kwenye mkusanyiko wa mjini Calbayog, wahubiri 7 walihudhuria kutoka kikundi kilicho peke yacho nao wakaja na watu wenye kupendezwa 14. Kwa kuthamini uhitaji wa kuwapo penye karamu hii ya kiroho, jamaa moja ya kutoka Palawan ilitumia karibu asilimia 20 ya mapato yao ya kila mwaka ili kuhudhuria Mjini Puerto Princesa.

Wajumbe wengi wa kigeni walisafiri kwenda kwenye mkusanyiko wa Manila, na karibu asilimia 80 kati yao walikuwa katika namna fulani ya utumishi wa wakati wote. Ilikuwa jambo la kuchangamsha moyo kuona jinsi akina ndugu walivyotiwa moyo na ule mchezo wa kuigiza “Wakati Ujao Wako​—ni wa Kushidaniwa,” uliohusu utumishi wa wakati wote. Mjini Iloilo, watu watatu wenye kushiriki katika mchezo huo wa kuigiza walivutwa sana moyoni wakati wa mazoezi mpaka wakapeleka maombi ya upainia wa kawaida hata kabla ya kusanyiko kuanza. Mjini Ormoc, mwenye kiti wa mkusanyiko alisimulia kwamba mara tu baada ya mchezo wa kuigiza, wahubiri sita waliomba maombi ya painia wa kawaida.

Hakika roho ya Yehova inavuta mioyo ya watu “wajitoe kwa hiari” katika siku hizi za mwisho. (Zaburi 110:3) Mikusanyiko hiyo ya “Washika-Ukamilifu” katika Ufilipino imewatia moyo sana akina ndugu na watu wa kupendezwa walio kule.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki