Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Je! kuna tofauti kati ya “kuumba” (creation) na “nadharia ya kuumba” “creationism”?
Ndiyo, kuna tofauti. Neno hili “kuumba,” likiwa linaonekana mara 18 katika Biblia ya New World Translation of the Holy Scriptures, laelekeza kwa kufaa kwenye utendaji wa kuumba wa Yehova. (Kwa mfano, ona Warumi 1:20, 8:21; 2 Kor. 5:17, NW) Usemi huu “nadharia ya kuumba’’ haupatikani katika Biblia.
Kamusi inayoitwa Webster’s Third New International Dictionary (chapa ya mwaka 1971) inafasili “kuumba” (creation) kuwa ni “tendo la kuumba,” na neno “creationism” kuwa “fundisho au nadharia ya kuumba.” Kamusi iyo hiyo inafasili “ism” kuwa “fundisho maalum, kisa, mfumo, au nadharia—mara nyingi ikitumiwa kwa dharau.”
Miaka hii ya kuanzia 1980 “nadharia ya kuumba” imekuwa “fundisho” halisi kwa sababu imekubaliwa na vikundi vya kisiasa vyenye kuchochea uvutano juu ya maongozi ya kiserikali, kama vile kikundi kinachoitwa Moral Majority. Sasa huo si usemi usiopendelea upande wo wote, bali unatia ndani maoni ya wale wenye kuichukua Biblia kihalisi, kama vile maoni yasiyo ya akili ya kwamba Mungu aliumba dunia na kila kitu juu yayo kwa siku sita, kila moja ikiwa yenye saa 24. Sasa kuna zaidi ya vitabu 350 vinavyoenezwa ili kuunga mkono wazo lisilo na ushahidi la “nadharia ya kuumba.” Mashahidi wa Yehova wanayakataa katakata makisio ya kipumbavu na “nadharia ya kuumba” na wanaunga mkono yale ambayo Biblia inafundisha hasa juu ya “kuumba.”
Ili upate jibu kamili zaidi kwa swali la juu, tafadhali ona makala yenye kichwa “Evolution, Creation, or Creationism—Which Do You Believe?” katika kurasa 12-15 za gazeti-jenzi letu la hili, yaani, Awake la tarehe ya Machi 22, 1983.