“Tunaona ni Laiti Kila Mtu Duniani Angeweza Kukisoma!”
HIVYO ndivyo mwanamume mmoja alivyoandika akionyesha uthamini kwa kitabu, Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Barua yake inaonyesha maoni ya mamilioni ya watu ambao wamekiona kitabu hicho cha kurasa 256 chenye picha kuwa cha thamani kubwa sana katika kujibu maulizo juu ya chanzo na kusudi la uhai duniani.
Kikiwa kilitolewa mwaka jana kwenye mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova katika nchi mbalimbali, mamilioni ya nakala za kitabu hicho yameenezwa katika lugha nyingi. Kinasaidia watu waone kutokana na ushuhuda wa kisayansi na wa Kibiblia kwamba kuna Muumba kweli kweli aliyetufanya na kwamba yeye ana kusudi zuri ajabu kwa ajili ya wanadamu.
“Rahisi Kueleweka”
Kitabu hicho kimeandikwa kwa njia iliyo nyepesi kueleweka. Ni kama vile barua moja ilivyosema: “Naona ni lazima niwaeleze jinsi nimevutiwa na kichapo chenu. Ni nani, mwenye akili timamu, anayeweza kupinga njia yenu ya kiakili ya kueleza mambo kwa ukamilifu? Ninyi mmeweza kuifanya habari hii ya kindani sana na yenye maarifa makubwa ieleweke kwa urahisi wa ajabu—hilo likiwa ni tendo hodari sana unapofikiria ni uchunguzi mwingi sana wa uanachuo uliofanywa kuhusu kitabu hiki.”
Vivyo hivyo, mtu mmoja aliyekuwa akiamini mageuzi mwenye malezi ya kisayansi alisema: “Mimi nimeshangazwa sana na kueleweka wazi na nguvu za kuvutia za kitabu hiki kipya. Mimi nafikiri ndicho kitabu cha sayansi kilicho kizuri zaidi kwa kujenga uthamini wa uhai ambacho nimepata kusoma. Kina mambo magumu sana kisayansi, hata hivyo yako katika kiwango ambacho mtu ye yote anaweza kufahamu.
Mwingine alisema: “Kitabu chote ni ufundi wa ajabu. Picha na maandishi yaliyomo zimewekwa pamoja kwa njia ya kuvutia sana hivi kwamba hata wale ambao hawapendi kusoma habari za namna hii watashangazwa na namna rahisi na ya mkato iliyotumiwa. Njia ya heshima isiyo ya ufidhuli ambayo imetumiwa kuufunua ukweli itaandaa ushuhuda mwingi sana wa kujibu pasipo shaka lile ulizo lililo katika kichwa cha kitabu hiki.”
Picha Zinasaidia Kuufikia Moyo
Kuhusu picha zilizomo, mtu mmoja aliandika hivi: “Tunashidwa njia ya kuwashukuru kwa kitabu hiki cha kupendeza sana. Picha zilizomo ni zawadi za kupendeza za ustadi.”
Lakini zile picha mia kadha, kutia na nyingine za kupigwa kwa chombo cha upigaji picha, si zakuonyesha ustadi wa kupendeza tu. Zinafundishaa, zikikazia mambo yaliyo katika maandishi. Ni kama vile jamaa moja ilivyoandika: “Picha na urahisi wa kitabu chenyewe zimekuwa msaada mkubwa kwa wale kati yetu tunaoona mambo ya kisayansi kuwa magumu kueleweka.” Barua nyingine ilieleza hivi: “Picha na maandishi yaliyoandikwa pambizoni yanasaidia kabisa kuelewesha maana na katika kukumbuka mambo.”
Watu wanaguswa moyo hasa na sura ya 19, “Paradiso ya Kidunia Itakuja Karibuni.” Kuhusu picha zilizo katika sura hiyo, jamaa moja ya Australia iliandika hivi: “Hizo zinawaingia sana watu. Sisi tulijaribu kujiwazia wenyewe tukiwa humo katika Paradiso kama jamaa. Hakika Paradiso na kutumikia Yehova kwa umilele ni mambo yanayostahili kufanyiwa jitihada yo yote. Picha zenyewe zilitokeza machozi kwenye macho yetu.
Mwingine aliandika: “Ndicho kichapo cha kupendeza zaidi ambacho nimepata kuona kikichapishwa mpaka sasa na Mashahidi wa Yehova. Nilipofikia ukurasa 243 na kuiona picha ya kile kisichana na wale simba-milia, machozi yalianza kuja machoni.” Bado mwingine alisema: “Mimi nililia nilipokifungua-fungua kukitazama. Nililia kwa furaha.” Na bado mwingine, wa Kanada alisimulia hivi: “Kamba za moyo wangu zimevutwa-vutwa isivyo kawaida, na macho yanajaa machozi ya furaha.”
Bila shaka wewe unajua watu ambao wangefaidika kwa kupata nakala ya kitabu Creation. Mbona usiwapelekee nakala ya zawadi? Ona ukurasa unaofuata upate maelezo marefu.