Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 9/15 kur. 4-7
  • Ile Gharika—Onyo Kutokana na Wakati Uliopita

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ile Gharika—Onyo Kutokana na Wakati Uliopita
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hali Zinazolingana na Hizo
  • Zile Siku za Mwisho
  • Inawezekana Kuokoka
  • Huu Ndio Wakati Tunaopaswa Kuwa Wenye Kulinda Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Ulimwengu Ulioharibiwa
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • Je! Wewe Walaani Vikali Ulimwengu Kupitia Imani Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Simulizi la Noa na Gharika Kuu—Je, Ni Hekaya Tu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 9/15 kur. 4-7

Ile Gharika​—Onyo Kutokana na Wakati Uliopita

KATIKA historia ndefu ya wanadamu, kumekuwa na misiba yenye kuletwa na nguvu za asili ambayo imekuwa mikubwa kama ule mlipuko wa Mlima St. Helens, au mikubwa zaidi. Lakini hakuna ye yote kati ya hiyo imelingana na ile Gharika kubwa sana ya siku za Noa. Gharika hiyo ilikuwa kubwa sana na yenye uharibifu mwingi sana hata ikabaki bila kufutika katika mawazo ya wanadamu duniani pote.

Kuna hadithi mbalimbali 150 za kimapokeo kuhusu Gharika kutoka sehemu nyingi tofauti za dunia, kutia na na Babulonia, Roma, India,, Australia, na yale mabara mawili ya Amerika. Ingawa hadithi hizo za kimapokeo zinatofautiana katika maelezo madogo-madogo, kuna upatano wa ujumla wa kwamba kilichosababisha Gharika ni kosa fulani katika adili, kwamba wanadamu waliharibiwa duniani pote, na kwamba jamaa moja iliokoka ikiwa katika safina au mashua. Ni msiba wa duniani pote tu ambao ungeweza kukumbukwa mahali pengi hivyo na kwa muda wa kudumu.

Mwanachuo mmoja wa Biblia aliandika hivi: “Upatano ulio kati ya masimulizi hayo ni uthibitisho usiokanika wa kwamba hadithi hiyo ya kimapokeo haikutungwa tu; hadithi ya kutungwa haifanani na nyingine, haiwi ya ulimwenguni pote; basi hadithi hiyo ya kimapokeo ina msingi wa kihistoria; ni matokeo ya tukio ambalo kwa kweli lilitukia katika vile vipindi vya mwanzo-mwanzo wa wanadamu.” Lakini mbona msiba huo uliotokea zamani za kale ni onyo kwa kizazi kinachoishi sasa?

Ni jambo la maana sana kwetu tuziangalie hali zilizofanya Gharika itokee. Ufanani wazo na hali za ulimwengu leo unaifanya Gharika iwe na maana kwetu. Hivi ndivyo masimulizi ya kihistoria katika kitabu cha Biblia cha Mwanzo yanavyozieleza hali hizo: “[Yehova] akaona ya kuwa maovu ya wanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. Mungu akaiona dunia, na tazama, imeharibika; maana kila mwenye mwili amejiharibia njia yake duniani.”​—Mwanzo 6:5, 12.

Ulimwengu wa wanadamu ulikuwa uvunjifu wa adili kwa ujumla, kila elekeo la mawazo lao likiwa baya wakati wote. Matokeo ni kwamba “dunia ikajaa dhuluma.” (Mwanzo 6:11) Watu walitoa maisha zao kabisa wafuatie tamaa za vitu vya kimwili na za ngono. Yesu Kristo alivuta fikira kwenye jambo hilo aliposema hivi: “Kama vile walivyokuwa katika siku hizo kabla ya gharika, wakila na kunywa, wanaume wakioa na wanawake wakiozwa, mpaka siku ile ambayo Noa aliingia ndani ya safina; nao hawakujali mpaka ile gharika ikaja na kuwafagilia mbali wote, ndivyo kutakavyokuwa kuwapo kwa Mwana wa mtu.” (Mathayo 24:38, 39, NW) Jambo pekee lililowapendeza ni kutosheleza tamaa zao za kimwili.

Noa alikuwa ametoa onyo la mapema kwa miaka mingi, lakini kizazi hicho kikakataa kuliamini. Wao hawakuwa wamepata kamwe kuona gharika ya jinsi hiyo. Kwa hiyo kwa sababu mambo yaliendelea kuwa kama hapo kwanza, walikuwa kama viziwi wasilisikie onyo. “Hawakujali.” Wao hawakuona ni kitu hata kama onyo hilo lilikuwa limetoka kwa Muumba wao kupitia Noa.

Lakini Mungu alimwambia Noa hivi: “Mwisho wa kila mwenye mwili umekuja mbele zangu; kwa sababu wameijaza dunia dhuluma, basi nitawaharibu pamoja na dunia.” (Mwanzo 6:13) Wakati Gharika ilipokuja, Noa na jamaa yake walihifadhiwa kwa sababu walilitii onyo na wakafuata maagizo ya Mungu. Lakini kwa sababu gani yote hayo yatupendeze sisi kwa njia ya pekee?

Hali Zinazolingana na Hizo

Kama ilivyokuwa katika siku zilizotangulia Gharika, jeuri imekuwa njia ya maisha hasa tangu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, Jeuri ya kisiasa kati ya nchi na nchi imetokeza vita vilivyo na uharibifu na ukali mwingi zaidi ya wo wote katika historia ya kibinadamu. Jeuri hiyo imeenea ikafikia miji, barabara, na nyumba za watu; hata inakuwa tisho kwa wasafiri. Zaidi ya hilo, televisheni, sinema, na vitabu vya hadithi vinakuwa sana-sana na habari zenye jeuri.

Ulinganifu mwingine ni njia ya kisasa ya maisha. Kutosheleza tamaa za ngono na vitu vya kimwili ndilo jambo linaloshughulisha kabisa kizazi cha sasa. Duniani pote, tunaona uvunjifu wa adili ambao umetokeza magonjwa yanayoambukia sana watu kupitia ngono. Uzinzi, uasherati, na ngono zinazofanywa na watu wa jinsia moja ni mambo yanayofanyika sana. Kama kile kizazi kilichokuwa kabla ya Gharika, kizazi cha sasa kinapenda anasa za kimwili na mali kuliko jinsi kinavyopenda Mungu.

Kwa kuwa Mungu ‘alihuzunika’ kwa sababu ya mwenendo mbaya kabisa wa watu waliokuwako kabla ya Gharika, Je! si jambo linalopatana na akili kukata shauri kwamba angejisikia ivyo hivyo kwa sababu ya mwenendo mbaya unaofuatwa sana ulimwenguni pote? Je! tendo aliloutenda ulimwengu huo wa siku za Noa halipasi kuwa onyo kwa kizazi cha sasa? Je! si jambo la akili kufikiri kwamba yeye atakata shauri lile lile kama tunavyoona kwenye Mwanzo 6:5-7? Mungu alipouona ubaya wa wanadamu, “akahuzunika moyo. [Yehova] akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi.” Kupitia waandikaji wa Biblia walioongozwa na roho, Mungu ametangaza kwamba atafikiliza hukumu kama hiyo juu ya kizazi chenye kufuatia anasa kinachoishi leo. Kizazi hicho kinayakaribia maangamizi yaliyo makubwa zaidi katika historia ya kibinadamu.

Zile Siku za Mwisho

Akiutazama wakati wetu, mwandikaji wa Biblia aliyeongozwa na roho kuandika barua ya pili kwa Timotheo anaisimulia hali ya mambo iliyozorota tunayoiona sasa ulimwenguni pote. Katika sura ya 3, 2Tim 3 mistari 1 mpaka 4, yeye anasema: “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu.”

Yesu Kristo alitoa unabii pia juu ya siku za mwisho wa mfumo huo wa mambo. Katika unabii wake alinena juu ya jeuri nyingi kabisa ambayo tumeona tangu Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, akisema: “Kwa maana taifa litainuka juu ya taifa na ufalme juu ya ufalme.” (Mathayo 24:7, NW) Yeye alinena pia juu ya kutokutii sheria kulikoenea sana leo na woga ambao watu wanao kuhusu wakati ujao. “Kwa sababu ya kuongezeka kwa kutokutii,” Yesu akasema, “upendo wa wengi zaidi utapoa.” (Mathayo 24:12, NW) Alisema pia kwamba wanadamu ‘wangezimia kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa na watu.”​—Luka 21:26, NW.

Maneno “siku za mwisho” yanamaanisha kwa kizazi hiki cha sasa jambo lile lile yaliyomaanisha kwa kizazi cha kabla ya Gharika​—mwisho wa sehemu iliyo na nguvu zaidi ya mfumo huo wa mambo ya kibinadamu. Kwenye 2 Wathesalonike 1:8, 9, Paulo mwandikaji wa Biblia aliyeongozwa na roho anasema, kupitia Yesu Kristo, Mungu ‘atawalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake.’

Waokokaji wa Gharika walikuta kwamba kile kizazi kilichokuwako kabla ya Gharika kilikuwa kimefagiwa kikatoka duniani. Wale watu na vitu vyote walivyokuwa wameishi kwa ajili yavyo havikuwapo tena. Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati kisasi cha Mungu kitakapokomesha kizazi cha sasa chenye jeuri. “Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo.”​—Zaburi 37:10.

Inawezekana Kuokoka

Ulinganifu uliopo kati ya kizazi kilichokuwako kabla ya Gharika na kizazi chetu hauhusu ubaya wa watu na kuharibiwa kwao tu. Kama vile walivyokuwako waokokaji wa Gharika ndivyo kutakavyokuwa waokokaji wa mwisho wa mfumo wa sasa wa mambo. Waokokaji wa Gharika walikuwa watu wapole ambao hawakuishi kama watu wale wengine kwa ujumla. Wao walikuwa wapenda uadilifu waliomtii Mungu na kusikiliza maonyo yake. Tunaambiwa hivi kwenye Mwanzo 6:8, 9: “Noa alipata upendeleo machoni pa Yehova. . . . Noa alikuwa mwanamume mwadilifu. Yeye alijithibitisha kuwa asiye na kosa kati ya watu wa rika lake.” (NW) Kwa habari yake na waokokaji wenzake, mtume Petro aliandika kwamba Mungu “hakukosa kuadhibu ulimwengu wa kale, bali alimlinda Noa, mhubiri wa uadilifu, salama pamoja na wengine saba wakati alipoleta gharika juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu.”​—2 Petro 2:5, NW.

Tunahakikishiwa na manabii wa Mungu, kutakuwa na umati mkubwa wa waokokaji kutoka uharibifu wa Mungu unaokuja wa mfumo wa sasa wa mambo. Wao, pia, watakuwa watu wapole ambao ni wapenda uadilifu na walio watiifu kwa maagizo ya Mungu kama vile Noa alivyokuwa. Baada ya kutabiri uharibifu wa waovu, mtunga zaburi anasema: “Bali wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”​—Zaburi 37:11; Ufunuo 7:9, 13, 14.

Yesu alitabiri kwamba habari njema za Ufalme wa Mungu zingetangazwa ulimwenguni pote katika siku za mwisho. Hiyo ndiyo njia inayotumiwa kukusanya watu wenye nia na uadilifu duniani ili waje kuokolewa. Yesu alionyesha jambo hilo katika mfano wake juu ya kutenganisha kondoo watoke kati ya mbuzi. Naye alimalizia mfano huo kwa kusema kwamba watu wasio waadilifu wanaofanana na mbuzi ‘wangeondoka wakaingie katika kukatiliwa mbali kwa milele, lakini waadilifu wanaofanana na kondoo waingie katika uzima wa milele.’​—Mathayo 25:31-46, NW.

Ingawa Gharika ilitukia wakati ulio mbali sana na siku zetu, kwa wazi hiyo ni onyo kwetu tusiwe watu wasiotaka kusikiliza. Kumbukumbu linaloihusu liliandikwa, kama Biblia inavyosema, “ili kutufundisha sisi.” (Warumi 15:4) Hilo ni onyo tusije tukaishi kwa njia ya ulimwengu ya kutenda jeuri, kufuata tamaa mbaya za miili yetu, na kufuatia vitu vya kimwili bila kumsikiliza Muumba wetu. Yeye habadiliki. Mungu alikifutilia mbali kizazi kilichokuwa kabla ya Gharika kwa sababu ya ubaya wacho. Kwa sababu iyo hiyo, yeye atakifutilia mbali kizazi hiki cha sasa na mfumo wote uliomo wa serikali za kisiasa, biashara ya kufuatia vitu vya kimwili tu, na dini ya uwongo.

Ili tuuokoke mwisho wa mfumo wa mambo, ni lazima tusikilize onyo tunalopata kutokana na yaliyotukia wakati uliopita. Ni lazima tujithibitisha kuwa wapenda uadilifu, kama walivyofanya wale waokokaji wanane wa Gharika. Na ili tuokolewe ni lazima tufuate shauri lililo kwenye Sefania 2:3: “Itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya [Yehova].

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kama vile Noa na jamaa yake walivyoiokoka Gharika, wewe pia unaweza kuwa kati ya waokokaji wenye furaha wa mwisho wa mfumo huu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki