Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 10/1 kur. 8-9
  • Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Mahubiri Yenye Sifa Zaidi ya Yote Yaliyopata Kutolewa
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Mahubiri Maarufu ya Mlimani
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Ninyi Ni Chumvi ya Dunia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Wenye Furaha Ni Watu Wanaomtumikia “Mungu Mwenye Furaha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 10/1 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Ni Akina Nani Walio na Furaha Kweli Kweli?

KILA mtu anataka kuwa mwenye furaha. Akitambua hivyo, Yesu anaanza Mahubiri ya Mlimani yake kwa kueleza ni akina nani walio na furaha kweli kweli. Kama vile tunavyoweza kuwazia, jambo hilo linavuta papo hapo fikira za wasikilizaji wake walio wengi sana. Hata hivyo, bila shaka maneno yake ya utangulizi yanaonekana na watu wengi kama kwamba yanapingana.

Akielekeza maelezo yake kwa wanafunzi wake, Yesu anaanza hivi: “Wenye furaha ni ninyi maskini, kwa sababu ufalme wa Mungu ni wenu. Wenye furaha ni ninyi mnaoona njaa sasa, kwa sababu mtajazwa. Wenye furaha ni ninyi mnaolia sasa, kwa sababu mtacheka. ‘Wenye furaha ni ninyi wakati wo wote watu wanapowachukia . . . Furahini siku hiyo na kuruka, kwa maana, tazameni! thawabu yenu ni kuu mbinguni.”

Hayo ni masimulizi ya Luka ya utangulizi wa mahubiri ya Yesu. Lakini kulingana na kumbukumbu la maandishi ya Mathayo, Yesu anasema pia kwamba wapole, wenye rehema, walio safi moyoni, na wenye kuamanika ni wenye furaha. Yesu anasema kwamba wao ni wenye furaha kwa sababu watairithi dunia, wataonyeshwa rehema, watamwona Mungu, na wataitwa wana wa Mungu.

Lakini, analomaanisha Yesu juu ya kuwa wenye furaha si kufanya shangwe wala kucheka-cheka, kama wakati mtu anapokuwa na mambo ya kumfurahisha-furahisha. Furaha ya kweli ina kina kirefu zaidi, ina wazo la kuridhika, mtu kujisikia ametosheka na anatimiza mambo maishani.

Kwa hiyo Yesu anaonyesha kwamba wale walio na furaha kweli kweli ni watu wanaotambua uhitaji wao wa kiroho, wanaosikitishwa na hali yao yenye dhambi, na wanaopata kumjua Mungu na kumtumikia. Basi, hata kama wakichukiwa au kuteswa kwa kufanya mapenzi ya Mungu, wao wana furaha kwa sababu wanajua wanapendeza Mungu na watapokea thawabu yake ya uzima wa milele.

Lakini, wengi wa wasikilizaji wa Yesu, sawa na watu wengine leo wanaamini kwamba kuwa tajiri, mwenye ufanisi, na kufurahia anasa ndiyo mambo yanayomfanya mtu awe mwenye furaha. Yesu hajui hivyo katika maoni yake. Akionyesha tofauti ambayo bila shaka inashangaza wengi wa wasikilizaji wake, yeye anasema:

“Ole wenu ninyi matajiri, kwa sababu mnapata kitulizo chenu kwa ukamili. Ole wenu ninyi mnaojazwa sasa, kwa sababu mtaona njaa. Ole ninyi mnaocheka sasa, kwa sababu mtaomboleza na kulia. Ole, wakati wo wote watu wanaposema vizuri juu yenu, kwa maana mambo kama hayo ndiyo babu zao waliowatendea manabii wa uwongo.”

Yesu anamaanisha nini? Kwa sababu gani kuwa na mali, kufuatia anasa kwa kucheka, na kufurahia sifa za wanadamu kunaleta ole? Ni kwa sababu wakati mtu anapokuwa na vitu hivyo na kuvithamini sana, utumishi kwa Mungu, ambao ndio pekee unaoleta furaha ya kweli, unaondolewa katika maisha yake. Wakati ule ule, Yesu hakumaanisha kwamba kuwa maskini tu, mwenye njaa, na mwenye kuomboleza ndiko kunafanya mtu awe mwenye furaha. Lakini, mara nyingi watu hawa wenye hali za shida wanaweza kuitikia mafundisho ya Yesu, na kwa njia hiyo wao wanabarikiwa kupata furaha ya kweli.

Ndipo, akiambia wanafunzi wake, Yesu anasema: “Ninyi ndinyi chumvi ya dunia.” Bila shaka, yeye hamaanishi kwamba wao kwa halisi ni chumvi. Bali chumvi inahifadhi vitu. Rundo kubwa la chumvi liliwekwa karibu na madhabahu kwenye hekalu la Yehova, na makuhani wenye kusimamia shughuli zilizoendeshwa humu waliitumia kuyakoleza matolea.

Wanafunzi wa Yesu ni “chumvi ya dunia” katika maana ya kwamba wao wanakuwa na matokeo yenye hifadhi juu ya watu. Kwa kweli, ujumbe wanaochukua utahifadhi maisha za wote watakaouitikia! Utaingiza katika maisha za watu hawa sifa za udumifu, ushikamanifu na uaminifu, uzuie kuoza ko kote kwa kiroho na kiadili ndani yao.

“Ninyi ndinyi nuru ya ulimwengu,” Yesu anawaambia wanafunzi wake. Taa haiwekwi chini ya kikapu bali inawekwa juu ya kinara cha taa, kwa hiyo Yesu anasema: “Vivyo hivyo acheni nuru yenu ing’ae mbele ya watu.” Wanafunzi wa Yesu wanafanya hivyo kwa ushuhuda wao wa waziwazi, pia kwa kutumikia wakiwa mifano inayong’aa ya mwenendo unaopatana na kanuni za Biblia. Luka 6:20-26; Mathayo 5:3-16, NW.

◆ Ni akina nani walio na furaha kweli kweli, na kwa sababu gani?

◆ Ni akina nani wanaopokea ole, na kwa sababu gani?

◆ Ni kwa njia gani wanafunzi wa Yesu ni “chumvi ya dunia’’ na “nuru ya ulimwengu”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki