Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 10/1 uku. 21
  • Je! Wewe Una Shukrani kwa Huduma Inayofanywa Waziwazi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Una Shukrani kwa Huduma Inayofanywa Waziwazi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Habari Zinazolingana
  • Fundisha Peupe Na Kutoka Nyumba Kwa Nyumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kuhubiri Nyumba kwa Nyumba
    Huduma ya Ufalme—2006
  • Kwa Nini Huduma ya Nyumba kwa Nyumba Ni ya Maana Sasa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Nyumba kwa Nyumba Bila Kuacha
    Huduma Yetu ya Ufalme—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 10/1 uku. 21

Ripoti ya Watangazaji wa Ufalme

Je! Wewe Una Shukrani kwa Huduma Inayofanywa Waziwazi?

HUDUMA ya nyumba kwa nyumba inapatana na Maandiko, na Mashahidi wa Yehova wanajulikana ulimwenguni pote kwa sababu ya kufanya sehemu hiyo ya utumishi wao. (Matendo 20:20, 21) Yesu aliwaambia wafuasi wake hivi: “Mtapokea nguvu wakati roho takatifu itakapofika juu yenu ninyi, na ninyi mtakuwa mashahidi wangu mimi katika Yerusalemu na katika Yudea yote na katika Samaria na kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.” (Matendo 1:8, NW) Andiko la Matendo 5:42 (NW) linaonyesha kwamba Wakristo hao wa kwanza walienda “nyumba kwa nyumba“bila kuacha.

Katika Haiti kulikuwa na mkabiliano uliohusu huduma ya nyumba kwa nyumba ya Mashahidi wa Yehova. Jambo hilo lilitokea wakati painia wa pekee mmoja alipokuta mwanamke mwenye kufuata sana Uprotestanti. Wakati wa maongezi ndugu huyo akaonyesha kwamba ni Mashahidi wa Yehova peke yao wanaohubiri nyumba kwa nyumba kama vile Biblia inavyopanga. Mwanamke huyo akajibu kwamba washiriki wa kanisa lake wangeweza kwenda nyumba kwa nyumba na wamepata kufanya hivyo pindi fulani. Pasipo shaka, Jumamosi iliyofuata, Shahidi huyo alikuta kikundi kimoja kikienda nyumba kwa nyumba, kikiwa kimeelekezwa na mwanamke huyo. Walikuwako watu karibu 100 katika kikundi hicho. Kwa kujivunia sana tendo hilo, mwanamke huyo akamwita ndugu yule ashuhudie tendo hilo hodari.

Juma moja baadaye, mwanamke huyo huyo akaongoza kikundi kingine na kufurahia kumwonyesha ndugu jambo hilo. Lakini, ndugu akasema kwamba waliokuwapo walikuwa karibu nusu tu ya hesabu iliyokuwapo juma lililotangulia. Kufikia Jumamosi ya nne kikundi hicho kilikuwa kimepungua kufikia watu 20, na katika Jumamosi ya tano mwanamke yule akawa peke yake. Kwa unyenyekevu, yeye alimjia ndugu na kukubali wazi hivi: “Ni Mashahidi wa Yehova peke yao walio na ukweli, kwa kuwa ni wao pekee yao wanaoweza kuendelea kufanya kazi ya kutoa ushuhuda juma baada ya juma bila kuacha.”

Painia wa pekee yule akamtolea mwanamke huyo funzo la Biblia ambalo lingemwonyesha ni sababu gani Mashahidi wanaweza kuendelea kuhubiri nyumba kwa nyumba na kwa sababu gani wengine hawawezi. Mwanamke huyo akakubali kwa unyenyekevu. Yeye na mume wake wakaanza kujifunza na kufanya maendeleo mazuri. Wote wawili sasa wanashirikiana na Mashahidi wa Yehova wakiwa watangazaji wa Ufalme wenye bidii nyumba kwa nyumba!

Huduma ya nyumba kwa nyumba ni uandalizi mzuri ajabu na wenye upendo ambao Yehova amepanga ili utumiwe kuwatafuta walio na moyo mnyofu na kuwasaidia wajifunze juu ya matakwa yake kwa uzima. Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wanafurahia kushiriki katika sehemu hiyo na nyinginezo za utumishi mtakatifu wanaomtolea Mungu. Mwelekeo wao unafanana na ule wa mtume Paulo, aliyesema: “Ninamshukuru Kristo Yesu Bwana yetu, ambaye alinipa uwezo, kwa sababu alinichukua kuwa mwaminifu kwa kunigawia huduma.”​—1 Timotheo 1:12, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki