Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 11/1 kur. 26-31
  • Matatizo ya Jamaa Yatatuliwa na Mashauri ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Matatizo ya Jamaa Yatatuliwa na Mashauri ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Hisia-Mwenzi” ni ya Maana Sana
  • Linda Moyo wa Mtoto Wako
  • Tumia “Hekima Yenye Mafaa”
  • Tegemea Yehova
  • Malezi ya Mtoto—Maoni Yaliyosawazika
    Amkeni!—1997
  • Malezi ya Mtoto—Dini na Sheria
    Amkeni!—1997
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
  • Nishughulikeje na Mzazi Wangu Aliyeondoka Nyumbani?
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 11/1 kur. 26-31

Matatizo ya Jamaa Yatatuliwa na Mashauri ya Biblia

1, 2. (a) Ni nini baadhi ya visababishi fulani vya jamaa zilizofarakana? (b) Kwa sababu gani matatizo ya wale walio katika jamaa zilizofarakana yawe ya kufikiriwa na wote? (1 Wakorintho 12:26)

“WANAWAKE [wanachagua] kupata talaka, watoto kutokuhesabiwa kuwa urithi wa wazazi wao, . . . badala ya kukosa uaminifu kwa Kristo,” akaandika Arnobius, mtu mwenye kudai kuwa Mkristo wa karne wa nne.a Ndiyo, hata ijapokuwa hivyo bado upinzani mkali wa kidini wenye kuletwa na watu wasioamini ulizigawanya jamaa. Yesu alitabiri kwamba wale ambao ‘wangependa’ washiriki wa jamaa yao kuliko yeye hawangemstahili. Kwa sababu hiyo “upanga” ungekuwapo ukitokeza mgawanyiko katika nyumba fulani, kwa sababu ya mwamini kuonyesha kiasi kidogo cha upendo kwa jamaa yake, “naam, na hata nafsi yake mwenyewe.” (Mathayo 10:34, 37; Luka 14:26) Upinzani huo umeendelea kuzivunja-vunja jamaa katika siku zetu.

2 Ingawa Mkristo anaweza kufanya yote anayoweza ili ndoa ibaki ikiwa imeungana, wenzi wengine wasioamini wanakataa katakata ‘kukubali kukaa’ na yule Mkristo, halafu mtengano au talaka inafuata. (1 Wakorintho 7:12-16) Jamaa zilizofarakana zinatokea pia kwa sababu, wakati wa “umalizio wa mfumo huu wa mambo,” upendo kwa Mungu na sheria zake, kutia ndani zile zinazohusu ndoa, ‘umepoa.’ (Mathayo 19:6, 9; 24:3,12, NW) Katika United States kadiri ya talaka iliongezeka kwa asilimia 236 kati ya mwaka 1960 na 1980! Watu fulani walihusika katika talaka kabla ya kuwa Mashahidi wa Yehova. Kwa kuwa ndoa karibu tatu kati ya tano za wenye kupeana talaka katika United States zina watoto, wale walio katika jamaa zilizovunjika-vunjika, wanakabili matatizo yenye kuwavaruga sana. Kwa kawaida wakati watu wanapojifunza ukweli wa Neno la Mungu, maisha yao ya jamaa yanapata maendeleo, lakini watu fulani walipeana talaka kabla ya kuwa Mashahidi wa Yehova. Nyakati nyingine hata Mkristo ambaye hakutumia mashauri ya Biblia kwa bidii nyumbani kwake amekuja mwishowe kujikuta katika talaka. (Yohana 13:17) Wazazi Wakristo wanaweza kufanya nini chini ya hali hizo walee watoto wampende Yehova?

“Hisia-Mwenzi” ni ya Maana Sana

3. Ni taabu gani inayosababishwa na talaka?

3 Katika siku za Malaki wanaume fulani Waisraeli walikuwa wakitaliki wake zao kwa hila. ‘Kulia na kuugua’ kwa wanawake hao waliokataliwa huku wakiomba sana msaada wa Mungu kulikuwa ni kama ‘kunaifunikiza madhabahu ya Yehova kwa machozi.’ (Malaki 2:13-16) Kuvunja ndoa leo kunaleta maumivu vivyo hivyo, hata kama kuna sababu thabiti za Kimaandiko za uvunjiko huo. Ingawa mume na mke wanataabika, watoto mara nyingi ndio wanaotaabika hata zaidi.

4. (a) Ni kwa njia gani mbalimbali watoto wanataabika wakati wazazi wao wanapopeana talaka? (b) Mzazi anaweza kumsaidaje mtoto?

4 Hata talaka ile ikileta kitulizo cha kutokutendwa vibaya, nyakati nyingine mtoto anaona ni kama kwamba ulimwengu wake umebomoka-bomoka. Kwa hiyo inahitajiwa kabisa mzazi anayeamini aonyeshe upendo na ufahamu unaozidi sana ule wa kawaida katika kushughulikia hali hiyo. “Sikuzote mimi nilikuwa pale katikati. Nilihisi kwamba nimegawanyika,” akaeleza kijana mmoja ambaye baba yake Mkristo alijipatia talaka ya Kimaandiko wakati mvulana huyo alipokuwa na umri wa miaka mitano. “Mimi nilifungia ndani yangu jinsi nilivyohisi hasa. Kufanya hivyo kulisababisha vipindi vya kushuka moyo.” Kusaidia mtoto ashughulike na maoni hayo ya moyoni yenye kumwingia sana kunahitaji mzazi awe na “hisia-mwenzi” (kujisikia kama mtoto mwenyewe) na kuwa na ‘huruma nyororo sana.’ (1 Petro 3:8, NW) Huenda mtoto yule akawa mnyamavu kwa sababu ya hatia, akihisi kwamba kwa njia fulani ni mwenye lawama kwa talaka ile. Mzazi anahitaji kueleza kwa subira kwamba anampenda mtoto na kwamba talaka haikusababishwa na kosa lake.

5. Kwa sababu gani mzazi Mkristo ajitahidi kukomesha hali za uadui za yule aliyekuwa mwenzi wake?

5 Kuoneana uchungu kati ya wazazi kunaweza kuzidi sana, hasa wakati masuala ya kidini yanapohusika. Hata hivyo, badala ya “kulipa dhara kwa dhara au kutukana kwa kutukana,” mzazi yule anayeamini anapaswa afikirie masilahi ya mtoto. (1 Petro 3:9, NW) Katika kitabu chake Growing Up Divorced (Kukua Katika Hali ya Talaka), Linda Francke anasema hivi: “Wazazi ambao wanaonyeshana uadui wanafanya matatizo ya watoto hao yawe magumu zaidi na hata yenye uharibifu. Kwa sababu ya kutokutaka kuleta hatari ya kujitenga na mzazi mmoja huku akishirikiana na yule mwingine, mtoto anaweza kujiweka kando asiwe na uhusiano unaofaa pamoja na wazazi wote wawili.” Ndiyo, si kwamba tu “wivu wenye uchungu na wenye ugomvi” ni mambo mabaya bali yanaweza hata kutenganisha mtoto na wewe. (Yakobo 3:14, 16) Mashambulizi ya maneno yanayosemwa bila kufikiri dhidi ya mzazi yule mwingine asiyeamini yanaweza kuumiza sana mtoto. (Mithali 12:18) Ikiwa yule aliyekuwa mwenzi wa ndoa ambaye ni mpinzani anaendeleza magombano, ‘kwa kadiri ambavyo inakutegemea wewe [mwamini], uwe mwenye kuamanika pamoja na watu wote.’​—Warumi 12:18-21, NW.

Linda Moyo wa Mtoto Wako

6. Baada ya uamuzi kufanywa juu ya atakayekuwa akitunza mtoto, ni tatizo gani linaloweza kupata wazazi fulani?

6 Haki ya kubaki na watoto ili kuwatunza ikiisha kuamuliwa, mara nyingi bado kutakuwa na magumu ya kushindana nayo. “Moja la matatizo yale makubwa-makubwa,” inasema ripoti kutoka tawi la Sosaiti yetu katika Australia, “ni kwamba mzazi anaelekea kulegea akiisha kupewa haki ya kubaki na mtoto ili amtunze . . . Hata mzazi aliye katika ukweli anaweza kuacha kuona ile sababu ya msingi iliyomfanya yeye atake kupewa haki ya kuwatunza watoto. Sababu ya kwanza inapasa kuwa kuwalea wakiwa waabudu wa kweli wa Yehova.” Kufanya hivyo kunahitaji jitihada ya daima.​—Waefeso 6:4, NW.

7. (a) Kwa sababu gani mtoto afundishwe kumheshimu mzazi yule aliyeondoka? (b) Unaweza kuzungumzaje na mtoto kwa kumpa sababu ikiwa yule asiyeamini anajihusisha katika mwenendo usio wa Kikristo?

7 Bila shaka, mara nyingi mahakama inatoa haki za kwamba mzazi yule ambaye sasa hana haki ya kubaki na mtoto awe akitembelewa na mtoto huyo. Je! haki hizo zinaweza kuheshimiwa na bado moyo wa mtoto uwe ukilindwa? Ndiyo, na kwa kadiri ambavyo inafaa inampasa mtoto amwonyeshe heshima inayostahili yule mzazi asiyeamini. Ikiwa, anapotembelea, yule asiyeamini anahusika katika mwenendo usio wa Kikristo, badala ya kukuza chuki kwa kumlaani mzazi huyo, yule mwamini anaweza kumweleza mtoto kwamba Mungu ameweka viwango vya mwenendo katika Biblia na kwamba “kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu,” yule Hakimu wa mwisho. (Warumi 14:12) Hata hivyo, eleza wazi kwamba mwenendo huo haupaswi kuigwa. Onyesha kwa akili kwamba ingawa watu fulani hawaishi kwa kufuata viwango hivyo, baadaye wengi wanabadilika kwa sababu ya kuona mfano wa Kikristo katika mtoto na aliyekuwa mwenzi wa ndoa. Kwa njia hiyo, huenda ikawezekana mtoto awe na kadiri fulani ya heshima kwa mzazi huyo. Tofauti zinazohusu dini zilizo kati ya watu wawili waliopeana talaka hazipasi kuzuia mzazi asiwe na matokeo mazuri juu ya mtoto. Yule mzazi Mkristo ataacha “kiasi chake kijulikane na watu wote.” (Wafilipi 4:5, NW) Ingawa hivyo, namna gani yule asiyeamini akijaribu kubomoa mazoezi ya kimungu?

8. Wazazi wawili walitayarishaje watoto wao kwa ajili ya ziara za kwenda kuwaona wapinzani waliokuwa wenzi wao wa ndoa?

8 Kufanya matayarisho kwa ajili ya ziara hizo ndio ufunguo! Mama mmoja Mkristo ambaye mtu aliyekuwa mume wake aligeuka akawa mwasi-imani aliripoti hivi: “Mimi nilikuwa nikijifunza pamoja na watoto kabla ya ziara ile juu ya jinsi mwenendo wao ungemhusu Yehova. Tulikuwa tukiigiza hali ambazo zingeweza kutokea. Mimi nilikuwa nikisema: ‘Baba yenu akisema hivi au vile, ninyi mngejibuje?’ “Mwanamke mwingine Mkristo aliyepewa talaka kwa sababu aligeuka akawa Shahidi anaongeza hivi: “Kabla [vijana wangu wawili matineja] hawajaondoka kwenda kumtembelea baba yao katika ziara ya mwisho-juma, tunakuwa na sala kuomba Yehova awe pamoja nao na kuwasaidia kutolea baba yao ushahidi, hasa kwa kuwa na mwenendo mzuri sana.”

9. Wazazi Wakristo wanaweza kuigaje mfano wa mama ya Musa?

9 Huenda mzazi asiyeamini mwenye haki za kutembelea mtoto akajaribu kumshawishi-shawishi kwa kumpa zawadi nyingi, vitumbuizo vya bei kubwa, na raha nyingine za kitafrija. Yokebedi, mama ya Musa, (na Amramu, ikiwa bado alikuwa hai) bila shaka alisaidia kuitengeneza hisia ya Musa ya kujua mambo yaliyo ya adili alipokuwa angali mdogo sana, kwa kuwa alijua ni mambo gani yangemkabili akipokezwa mikononi mwa binti ya Farao. (Kutoka 2:1-10) Ingawa alizikabili zile “hazina za Misri” zenye kushawishi, Musa alifanya uchaguzi wake mwenyewe wa kufuata kanuni za kimungu. Yeye ‘alihesabu’ mapendeleo yake ya kiroho kuwa ni mali za kweli! (Waebrania 11; 23-26) Inawapasa wazazi Wakristo vivyo hivyo watayarishe watoto wao kukabili vishawishi hivi kwa kuzungumza habari za Kimaandiko zinazoelekeza fikira hasa juu ya hazina za kiroho.b Mara nyingi watoto wanafanikiwa kugundua kwamba mzazi anasingizia tu kuwa anafurahia kuwapa vitu na kumbe kusudio lake la kufanya hivyo ni kuwavuta upande wake ili yeye ndiye apendwe nao kwa shauku.​—Mithali 15:16, 17.

10. Katika hali inayopita kiasi, ni baadhi ya mambo gani ambayo mzazi anapaswa kufikiria?

10 Katika visa fulani vinavyopita kiasi, huenda ziara hizo zikaelekea kuletea mtoto dhara fulani kubwa. Mzazi angepaswa aamue jambo la kufanya chini ya hali hizo, akikadiria katika sala dhara hilo linaloelekea kutokea lina ukubwa gani, ni msaada gani wa kisheria unaopatikana, na kama kuna uwezekano wa kukataza zile haki za mtoto kutembelea mzazi yule mwingine.c Epuka vitendo vya haraka-haraka ambavyo vingeweza kufanya wewe utiliwe mashaka kama unafaa kuwa mzazi.​—Wagalatia 6:5; Warumi 13:1; Matendo 5:29; 1 Petro 2:19, 20.

Tumia “Hekima Yenye Mafaa”

11. Wakati mzazi Mkristo anaposhindwa kupata haki ya kuwa akitunza mtoto, lazima yeye atambue nini?

11 Namna gani ikiwa yule mzazi Mkristo ndiye peke yake aliye na haki za kuwa akienda kutembelea watoto wake? Ikiwa mtoto hayumo tena katika nyumba ya Kikristo, mzazi huyo ana uongozi kidogo wa kiroho wa kumpa mtoto yule. (1 Wakorintho 7:14) Kwa mfano, ingeelekea kuwa Abrahamu aliyekuwa mzee mwaminifu wa ukoo alisisitiza kwamba Ishmaeli mwanaye aoe mwabudu mwenzake, kama Isaka. Lakini Ishmaeli, ambaye alikuwa kijana-tineja, na Hajiri (Hagari) mama yake walipokwisha kufukuzwa watoke katika jamaa hiyo, Abrahamu hakuweza kuzuia Hajiri asimpangie Ishmaeli kuoa Mmisri ambaye kwa wazi hakuwa mwabudu wa Yehova.​—Mwanzo 21:14, 21; 24:1-4.

12. (a) Ni lazima mzazi Mkristo ambaye hakupewa haki ya kumtunza mtoto atumie nini? (b) Toa mfano wa jinsi Mkristo anaweza ‘kutumia hekima afanikiwe.’

12 Hata hivyo mzazi Mkristo ambaye hakupewa haki za kubaki na mtoto ili amtunze anaweza kufanya mengi kukaza ndani yake upendo wenye kina kirefu kwa Yehova ijapokuwa huenda akawa na nafasi chache za kufanya hivyo. Ili atende hivyo, ni lazima mzazi huyo ‘alinde hekima yenye mafaa na uwezo wa kufikiri.’ (Mithali 3:21, NW) Ndiyo, mengi zaidi yanahitajiwa, si wingi tu wa jitihada. “Iwapo chuma hakipati, wala mtu hakinoi; ndipo hana budi kutumia nguvu zaidi [asipate matokeo mengi]. [Kwa hiyo] yafaa kutumia hekima, na kufanikiwa.” (Mhubiri 10:10) Kwa mfano, pindi kwa pindi huenda yule asiyeamini akatokeza mambo ya udhuru tu ili kuzuia mzazi yule mwingine asiweze kumwona mtoto. Badala ya kufanyiza mpambano papo kwa hapo, huenda mzazi akapata matokeo mazuri zaidi kwa kutumia Mithali 25:15: “Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; na ulimi laini huvunja mfupa.” Subira na upole zinaweza kulainisha hata mtu aliye na nia ilyo ngumu kama mfupa, ingawa si rahisi kuzionyesha wakati mtu anapokabiliwa na vizuizi visivyo vya haki. (Linganisha 2 Timotheo 2:23-25.) Mara nyingi mabishano yanaweza kuepukwa kwa kufika katika wakati uliopangwa na kufuata madokezo yanayoruhusika (si kinyume cha Maandiko) kuhusiana na mtunzaji mtoto ambao umepewa na mzazi anayekaa naye. Ikiwa unahangaishwa na jambo la kwamba yule asiyeamini anamwambia mtoto mambo ya kubomoa heshima yako, kumbuka 1 Petro 2:15; “Kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu.” Kuweka mfano mwema kutawezesha mtoto aone ni nani aliye katika upande unaofaa.​—Mithali 20:7.

13. Mzazi anayeamini anaweza kufanyaje ziara iwe yenye faida kweli kweli?

13 Wakati wa ziara hizo, jitahidi kuingiza Neno la Mungu ndani ya moyo wa mtoto kwa kujifunza naye binafsi habari za kiroho na kwa kwenda naye kwenye mikutano ya kundi, wakati wote inapowezekana. Hata ikiwa kuna vizuizi vigumu vya kisheria, bado mzazi huyo anaweza kutaja-taja kazi za uumbaji wa Mungu kwa njia ya kikawaida tu, na kwa njia nyinginezo asaidie mtoto huyo kumpenda Mungu. (Warumi 1:19, 20: Mathayo 6:28-30) Yesu alizitambua hali za kupungukiwa kwa wasikilizaji wake. Yeye “alikuwa akisema nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulisikia.” (Marko 4:33, 34) Kwa hiyo zaidi ya kuzungumza mambo mazito ya kiroho, jihusishe pamoja na mtoto katika utendaji mwingine wenye kujenga, kama vile kutembelea pamoja na marafiki wema, kutia na wengine walio wa umri wa mtoto huyo. (Mithali 13:20) Furahieni tafrija inayofaa mkiwa pamoja. Fanya ziara hiyo iwe pindi itakayopendwa sana na mtoto. Kumtia nidhamu kwa kiasi kunaonyesha upendo. (Mithali 13:24) Lakini, nyakati nyingine matatizo yanaweza kuelekea kuwa mazito mno. Mikazo inatoka pande nyingi. Mambo yote hayo yanaweza kuvumiliwaje?

Tegemea Yehova

14. Ni uhakikisho gani tulio nao kutokana na Zaburi 37:23, 24?

14 Kwa habari ya mtu ambaye Yehova ‘anafurahia’ mwendo wake wote wa maisha, Daudi aliandika hivi: “Ingawa huenda yeye akaanguka, hatavurumishwa chini, kwa maana Yehova anautegemeza mkono wake.” (Zaburi 37:23, 24, NW) Ndiyo, huenda nyakati nyingine Mkristo anayeng’ana mikazo ya jamaa iliyofarakana ‘akaanguka’ katika maana ya kupatwa na mambo yanayomvuruga mawazo, hali za kukata tamaa, na mabadiliko ya kisheria au ya kifedha, lakini yeye ‘hatavurumishwa chini kwenye uharibifu.’ Au kama vile The New Berkeley Version inavyofasili kifungu hicho: “Wakati aangukapo, yeye hatakuwa amepiga chini na kumalizika.” Kwa sababu gani? Kwa sababu Yehova anamtolea mkono wake wa kuweza kupitia roho takatifu yake na waabudu wake wenye upendo.​—Yakobo 1:27.

15, 16. Jamaa fulani zilizofarakana zimepewaje riziki, na jambo hilo likatimiza ahadi gani?

15 Mtu mmoja mpinzani aliyekuwa mume wa mwanamke Mkristo alipokwisha kupewa haki ya kuwatunza watoto wake wawili wadogo, mwanamke huyo alisema hivi: “Wakati mambo yalipoondolewa kabisa katika uwezo wa mikono yangu, nilijifunza kweli kweli kutegemea Yehova. Nimejifunza kukubali mambo anayoruhusu na kutokujaribu kutumia nguvu nifanye mambo yasiyo mikononi mwangu mwenyewe. Bado ninaendelea kujifunza. Ni somo gumu.” Lakini, yeye anatumia kwa ukamili haki zake za kuwatembelea watoto na amejipatia faraja si kutokana na mume wake wa sasa, ambaye ni mzee Mkristo mwaminifu, bali pia kutokana na wengine katika kundi.

16 Mkristo mwingine aliyekuwa na mume ambaye akageuka akawa mwasi-imani na kukaa na watoto kwa miezi kadha kinyume cha uamuzi wa mahakama, alisema hivi: “Mimi nilishuka sana moyo hata nikafikiria ningebomoka-bomoka. Jambo moja tu lililonizuia kurukwa na akili wakati wa kipindi hicho lilikuwa kujihusisha katika huduma ya shambani.” Binti yake, aliyekuwa na umri wa miaka 7 wakati huo, alichukua msimamo imara upande wa Yehova hata akavumilia kupigwa-pigwa mara kadha na baba kwa sababu alikataa kusoma vitabu vyake vya uasi-imani. Binti alipomrudia mama yake, alikuwa amepiga moyo konde ashikamane na Yehova kwa ukaribu hata zaidi. Watumishi hao na wengine waaminifu wameona Zaburi 54:2-7, NW: “Ee Mungu, sikia sala yangu;. . . tazama! Mungu ni msaidiaji wangu; Yehova yuko kati ya wale wanaotegemeza nafsi yangu. . . . Kwa maana yeye alinitoa katika kila taabu.” Ndiyo, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tutapata tegemezo la Yehova!—1 Wakorintho 10:13.

17. Wazazi walio katika jamaa zilizofarakana wanaweza kusaidiaje watoto wao, na thawabu inaweza kuwa nini?

17 Kwa hiyo ikiwa wewe ni mzazi aliye katika jamaa iliyofarakana, uwe mwepesi kujali maoni ya ndani ya mtoto wako. Imarisha moyo wake kwa Neno la Mungu. Ikiwa wewe huna haki zaidi isipokuwa zile za kumtembelea tu, basi uwe na “hekima yenye mafaa” unapozitumia hizo kwa ukamili. Uwe na tumaini hakika kwamba Neno la Mungu lililopandwa linaweza kuwa na nguvu nyingi katika moyo wenye kuitikia. (1 Wathesalonike 2:13) Kuona mtoto akija kumpenda Yehova kunaistahili sana jitihada yote.

[Maelezo ya Chini]

a Kichapo Against the Heathen Kitabu cha Pili, 5.

b Ona “Nafasi ya Vijana Iliyo Kubwa Zaidi” katika toleo letu la Agosti 15, 1985, na pia “Wazionaje Mali?” katika kitabu Kupata Faida Zote za Ujana Wako, kilichochapishwa na Sosaiti yetu.

c Kifungu cha Sheria Kisichobadilika-badilika cha Ndoa na Talaka katika United States kinasema hivi: “Mzazi ambaye hakupewa haki ya kumtunza mtoto ameruhusiwa haki za kiasi za kumtembelea mtoto huyo isipokuwa kama mahakama imefanya kesi fulani ikapata kwamba matembezi hayo yangehatirisha afya ya kimwili ya mtoto au yaharibu sana ukuzi wake wa maoni ya moyoni.”

Je! Wewe Unakumbuka.

◻ Mzazi Mkristo aliyepewa haki ya kutunza mtoto anaweza kulindaje moyo wa mtoto?

◻ “Hekima yenye mafaa” itasaidiaje mzazi anayeamini ambaye amepewa haki za kutembelea tu mtoto?

◻ Ni uhakikisho gani unaotolewa kwenye Zaburi 37:23, 24, na Yehova anatimizaje ahadi hiyo?

[Picha katika ukurasa wa 29]

Tumia haki za kutembelea mtoto kwa kusudi la kukaza ukweli ndani ya moyo wake, lakini unganisha jambo hilo na utendaji mwingine unaofaa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki