Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 4/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Nafsi
    Amkeni!—2015
  • Kifo Ni Adui Anayeweza Kushindwa
    Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Uhai Baada ya Kifo—Biblia Husema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Je! Nafsi Huendelea Kuishi Baada ya Kifo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 4/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Je! Inafaa kwa Mkristo kuruhusu uchunguzi wa maiti wa mtu wa ukoo?

BIBLIA haitoi maelezo ya moja kwa moja juu ya kuchunguzwa kwa maiti, lakini kuna mawazo fu-lani ya Kibiblia yanayohusika ambayo Mkristo anaweza kufikiria. Kisha uamuzi wa kibinafsi unaweza kufanywa kwa msaada wa maandiko na mambo fulani-fulani yanayohusu hali inayohusika.

Uchunguzi wa maiti ni kukatwa-katwa kwa viungo vya mwili kwa kupasuliwa ili kuchunguza maiti kuamua kisababishi cha kifo. Uchunguzi huo unaweza pia kutoa habari juu ya matokeo ya utendaji wa ugonjwa katika mwili. Maoni ya uchunguzi wa maiti ya dini fulani-fulani yameathiriwa na mafundisho yasiyo ya Kimaandiko. Kwa mfano, ensaiklopidia moja ya Kikatoliki husema hivi: “Mwili wa mfu wapaswa kutendewa kwa heshima kubwa ukiwa ndiyo makao ya zamani ya nafsi yake . . . Unakusudiwa kuinuka pamoja na nafsi yake, katika pindi ya ufufuo wa watu wote, uingie katika uzima wa milele . . . Kunaweza kuwa na kipindi fulani cha wakati katikati ya kifo halisi na kuondoka kwa nafsi.” Hata hivyo, Biblia huonyesha kwamba mtu (nafsi hai) anapokufa, anakuwa nafsi iliyokufa. (Mwanzo 2:7; 7: 21-23; Walawi 21:1, 11) Namna gani mwili wake? Kwa habari ya wote “wanadamu” na “wanyama” tunasoma hivi: “Wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.” (Mhubiri 3:18-20) Katika ufufuo, Mungu hatainua mwili ambao tangu hapo umekwisha kuwa mavumbi, bali yeye ataandaa mwili kama impendezavyo.​—Ona 1 Wakorintho 15:38, 47, 48.

Sehemu nyingine ya maoni ya Kibiblia juu ya wafu inaweza kufikiriwa kuhusiana na uchunguzi wa maiti. Mungu aliwaamuru Israeli hivi: “Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu; mimi ndimi [Yehova]. (Walawi 19:28; Kumbukumbu 14: 1,2; Yeremia 47:5; Mika 5:1) Ndiyo, haikuwapasa watu wa Mungu kuiga mataifa yaliyowazunguka katika kukatakata miili yao kama ishara ya kuhuzunikia wafu au kwa sababu nyinginezo zote za dini ya uwongo. Lazima amri hiyo iwe iliwatia moyo Waisraeli kuonyesha heshima kwa miili yao ikiwa uumbaji wa Mungu.​—Zaburi 100:3; 139:14; Ayubu 10:8.

Vivyo hivyo inawapasa Wakristo kuonyesha heshima inayofaa kwa miili yao, ambayo wameweka wakfu kwa Mungu. (Warumi 12:1) Wengine wameamua kwamba maoni hayo ya heshima kwa mwili yapaswa kuongozwa kufikiri kwao juu ya uchunguzi wa maiti. Wao wamehisi kwamba isipokuwa kuwe na sababu nyingine yenye kulazimisha, wao wangependelea kwamba mwili wa mtu mpendwa wa ukoo wao usikatwekatwe katika uchunguzi wa maiti. Huenda wakawa wanajua kwamba katika sehemu nyinginezo damu iliyotolewa kutoka katika maiti imepata kutumiwa kutiwa mishipani au kwa makusudi mengineyo, jambo ambalo wao hawakutaka kushiriki.a

Ni kwa sababu gani, basi, Wakristo fulani wameruhusu kuchunguzwa kwa maiti? Wao wanatambua kwamba Biblia haitoi maelezo yaliyo wazi juu ya utaratibu huu wa kitiba. Huenda pia wameona kwamba Waisraeli katika Misri waliruhusu matabibu ya Misri wawatie Yakobo na Yusufu dawa ya kuzuia maiti kuoza, jambo ambalo linaelekea lilihusu hatua fulani za upasuaji ili kuondoa viungo vya ndani vya mwili. (Mwanzo 50:2, 3, 26) Katika visa fulani leo, sheria ya nchi hutaka kwamba uchunguzi wa maiti ufanywe. Kwa mfano, ikiwa kijana, mwenye afya anakufa bila sababu yo yote iliyo wazi, huenda ikawa lazima kufanya upasuaji wa maiti. Kwa wazi, sheria inapodai kuwe na upasuaji wa maiti, Mkristo atakumbuka lile shauri la ‘kutii mamlaka iliyo kuu.​—Warumi 13:1, 7; Mathayo 22:21.

Hata katika kisa cha mtu ambaye amekuwa chini ya uangalizi wa daktari, na hivyo kinachoelekea kuwa kisababishi cha kifo kinajulikana, uchunguzi wa maiti huenda ukaandaa habari yenye kusaidia. Watoto walioachwa huenda wakataka kujua sababu hasa ili kuongeza habari juu ya historia ya kitiba ya jamaa yao. Habari kama hiyo inaweza kuathiri kiolezo au matibabu ya maisha yao wenyewe wakati ujao. Kuna sababu nyinginezo, pia, kwa nini wengine wanaruhusu uchunguzi wa maiti ufanywe. Ripoti ya uchunguzi wa maiti iliyo na maandishi ya uchunguzi wa visehemu vya mwili huenda ikawezesha jamaa istahili zile manufaa wanazopewa waliofiwa, kama vile kutoa ushahidi wa ugonjwa wa weusi wa mapafu unaohusianishwa na kuchimba makaa. Wengine hata wamehisi kwamba uchunguzi wa maiti ungezidisha amani ya akili yao kwa kuwasaidia kufahamu jambo lililosababisha au ambalo halikusababisha kifo cha mpendwa wao. Watu walio nje ya jamaa huenda pia wakahusika. Watu wa ukoo huenda wakahisi kwa moyo mweupe kwamba kuruhusu uchunguzi wa maiti huenda kukasaidia tabibu afahamu mwendo wa ugonjwa, na hivyo huenda akawa ametayarishwa vizuri zaidi kuwatibu wengine.

Kwa hiyo, inafaa Wakristo waonyeshe heshima kwa miili yao, lakini kuna mambo mengine ya hakika ambayo wanaweza kufikiria katika kuamua kama wataruhusu uchunguzi wa maiti ufanywe katika hali fulani.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari ya uwezekano wa kutumia viungo vya mwili vya kibinadamu kwa makusudi ya kutiwa katika mwili mwingine, ona Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1980, ukurasa 24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki