Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 4/15 kur. 5-7
  • Kadiri Mpya ya Hekima ya Kimungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kadiri Mpya ya Hekima ya Kimungu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ile Siri Takatifu Yafunguka
  • Wakombolewa kwa Ukombozi
  • Lile Agano Jipya na Kile Kiumbe Kipya
  • Ile Dunia Paradiso
  • Fidia ya Kristo Njia ya Mungu ya Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Alilofanya Mungu ili Kuokoa Wanadamu
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • “Hekima ya Mungu Katika Siri Takatifu”
    Mkaribie Yehova
  • Usimamizi wa Kutimiza Kusudi la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 4/15 kur. 5-7

Kadiri Mpya ya Hekima ya Kimungu

“KWA HIYO Mungu akasema kwa Musa: ‘Mimi nitathibitika kuwa kile ambacho mimi nitathibitika kuwa.’ Na akaongeza: ‘Hivi ndivyo utakavyosema kwa wana wa Israeli, “Mimi nitathibitika kuwa amenituma kwenu.”’” (Kutoka 3:14, NW) Yehova alimweleza Musa kwamba kabla ya tukio hilo watumishi Wake hawakuwa wamefahamu kabisa umaana kamili wa jina Lake. Yeye ni Mungu wa kusudi na sikuzote yeye hutimiza penzi lake. Ikiwa hali zinataka hivyo, yeye anaweza kubadili njia yake ili atimize kusudi lake. Yeye ni mwenye hekima kadiri hiyo!

Shetani mwenyewe hakuthamini yaliyodokezwa na jina la Mungu. Inaelekea yeye alijua juu ya mti wa uzima katika shamba la Edeni. Ikiwa yeye angewaelekeza Adamu na Hawa kwenye mti huo, hilo lingeelekea kumweka Yehova katika hali ya kuchagua kati ya mambo mawili magumu: ama kushikamana na neno lake kwamba dhambi ingemaanisha kifo kwao au kushikamana na neno lake kwa habari ya mti wa uzima. (Mwanzo 2:9; 3:1-6) Vyo vyote iwavyo, Shetani alielekeana na jambo ambalo lingemkatisha tumaini.

Sasa Mungu alianza kuonyesha hekima ambayo haikutazamiwa na wana wake wa kiroho na ambayo hawakutangulia kufunuliwa. (Linganisha Waefeso 3:10.) Mungu alianza mfululizo wa matangazo na matukio ambayo kwa muda wa kipindi kirefu cha wakati yangeonyesha kwa njia ya ajabu sana hekima yake kubwa na uwezo wake wa kutimiza kusudi lake la milele, ambalo lilikuwa ni kuwa na dunia inayojaa wanadamu wenye furaha na washikamanifu ambao wangeishi milele katika Paradiso. (Mwanzo 1:27, 28) Tena na tena Mungu angezuia jitihada za Shetani za kuingilia jambo hilo.

Ile Siri Takatifu Yafunguka

Mara tu baada ya ule uasi wa kwanza, Mungu alichukua hatua. Yeye alikuwa na kikao cha mahakama kwa ajili ya watu hawa wawili wenye hatia na akashikilia uamuzi wake wa kifo kwa kutokutii. Namna gani juu ya Adamu na Hawa kula kutokana na ule mti wa uzima? “[Yehova] Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; kwa hiyo [Yehova] Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni.” —Mwanzo 3:17-23.

Wakati huo Mungu akachukua pia daraka la Mweneza Evanjeli au Mtangaza habari njema. Yeye alitamka unabii wa kwanza: “[Yehova] akamwambia nyoka, . . . Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa na wewe utamponda kisigino.” (Mwanzo 3:14, 15) Karne nyingi baadaye mtume Paulo alieleza hivi: “Kwa kuwa kiumbe [cha kibinadamu] kilitiishwa chini ya ubatili, si kwa penzi lacho chenyewe, bali kupitia yule ambaye alikitiisha, kwa msingi wa tumaini.” —Warumi 8:20, NW.

Ndiyo, mwanadamu baada ya hapo bila msaada, angekuwa katika kifungo cha kifo kilichorithiwa kutoka kwa Adamu bila msaada, lakini Mungu alikuwa akitangaza kusudi lake la kuokoa wazao watiifu wa Adamu. Lakini, ni nini uliokuwa “msingi wa tumaini”? Yeye angewaokoaje wanadamu na bado ashikamane na hukumu yake ya kifo kwa sababu ya dhambi? Hiyo ilikuwa iwe hekima ya Mungu iliyofichwa; ilihusu “ile siri takatifu iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo iliyopita na tangu vizazi vilivyopita.” (Wakolosai 1:26, NW; 1 Wakorintho 2:7, 8) Ijapokuwa waaminifu wa kale hawakuifahamu siri hiyo, walikuwa na tumaini kwamba kwa njia fulani Mungu angewafungua. Kwani, hata malaika walitamani sana kujifunza jinsi Yehova angetimiza kusudi lake! (1 Petro 1:10-12) Je! wewe unaifahamu siri takatifu hii?

Wakombolewa kwa Ukombozi

Polepole kwa muda wa karne nyingi, Yehova aliongeza habari kwenye ahadi yake ya kwanza kabisa. Alimwahidi Abrahamu mwaminifu uzao ambao kupitia huo baraka zingewajia wanadamu wote watiifu. (Mwanzo 22:15-18) Kupitia Yakobo yeye alifunua kwamba uzao huo angekuwa mfalme kutoka kabila la Yuda. (Mwanzo 49:10) Kufikia wakati huo wanadamu wenye kumwogopa Mungu waliamini ufufuo wa wafu, ijapokuwa hawangeweza kufahamu kabisa jinsi jambo hilo lingekuwa. (Ayubu 14:14, 15; Waebrania 11:19) Mwishowe Mungu alimwahidi Daudi kwamba Mfalme aliyekuwa akija, au Masihi, angekuwa mzao wa Daudi na angetawala mpaka wakati usiojulikana.—2 Samweli 7:16.

Manabii wote waliongeza visehemu kwenye ufahamu wa ile siri takatifu, lakini wanadamu hawangeweza kuona picha kamili. Hatimaye, wakati wa kuonekana kwa Masihi ulifika, na ndipo, baada ya muda mrefu, hekima hii ya Mungu iliyo ya namna nyingi sana ilipata kuwa wazi zaidi. Hiyo ilitegemea Yesu Kristo na mwandalio wa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu ukiwa ukombozi unaolingana kwa ajili ya wanadamu. Huo ukiwa ndio msingi, yaliyobaki ya kusudi tukufu la Yehova kupitia ule Ufalme yangeendelea mbele. Je! wewe unaufahamu ukombozi?

Katika Warumi, sura za tano na sita, Paulo anatoa elezo zuri juu ya huo. Kwenye Warumi 5:12 yeye anaeleza dhambi na kifo chetu tulichorithi. Anaendelea kuonyesha jinsi matokeo ya dhambi moja tu iliyofanywa na Adamu mkamilifu na kupoteza uhai kwa ajili ya wazao wake yangeweza kusawazishwa na uhai mwingine mkamilifu wa kibinadamu. Huo ulithibitika kuwa uhai wa yule “mwanadamu, Kristo Yesu.” (Mistari 15-21; ona pia 1 Timotheo 2:5, 6, NW) Kwa nini Yesu angeandaa ukombozi huo? Kwa sababu yeye alikuwa mwana wa Mungu, Yesu alikuwa “mtakatifu, asiyekuwa na uovu, asiyekuwa na waa lo lote, aliyetengwa na wakosaji.” (Waebrania 7:26; Luka 1:32, 33) Sisi hatuhitaji kujaribu kueleza yale mambo madogo madogo juu ya tabia za kurithiwa za uzawa wa Yesu. Malaika Gabrieli alimhakikishia Mariamu, mama ya Yesu, na sisi, kwamba hakuna lisilowezekana kwa Mungu. (Luka 1:37) Hivyo Yesu, ijapokuwa alizaliwa kutokana na mwanamke mzao wa Adamu, alikuwa Mwana wa Mungu—hasa mwanamume mkamilifu. Damu yake, au uhai, ilikuwa yenye thamani zaidi kupita damu ya wanyama wasiohesabika waliokuwa wametolewa dhabihu na makuhani wa Kiharuni wa Israeli kwenye hekalu katika Yerusalemu. Yeye alikuwa “Mwanakondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu!”—Yohana 1:29; 3:16.

Je! Mungu angeweza kufanya mpango huo kupitia Yesu na bado awe mwenye haki? Ikiwa Mungu alimwinua mwanaye kwenye uhai katika siku ya tatu, ni jambo gani lililopata ukombozi? Paulo anatuhakikishia kwamba Mungu ni mwenye haki. Fuatana na kusababu kwake: “Lakini kwa rehema yake wao wanafanywa wanyofu bure [ikiwa bila malipo], kwa ukombozi uliopatikana kupitia Yesu Kristo. Kwa kuwa Mungu alimwonyesha akifa hadharani akiwa dhabihu ya upatanisho ya kujifaidi nayo kupitia imani. Hiyo ilikuwa ili atetee haki yake mwenyewe (kwa kuwa katika uvumilivu wake, Mungu alipitilia dhambi za zamani za wanadamu)—ili atetee haki yake kwa wakati huu, na kuonyesha kwamba yeye ni mnyofu yeye mwenyewe, na kwamba yeye awafanya wale walio na imani katika Yesu kuwa wanyofu pia.” (Warumi 3:24-26, An American Translation) Sasa, hiyo inamaanisha nini? Kwa urahisi ni kwamba Yesu, akiwa mwanadamu wa nyama na damu, mkamilifu, alikufa hakika akiwa mwanadamu na anabaki mfu milele akiwa mwanadamu. Yeye alikufa “mara moja, alipojitoa nafsi yake.” (Waebrania 7:27) Hivyo ukombozi ni halali. Yesu alikufa katika mwili; katika siku ya tatu yeye “alifanywa kuwa hai katika roho.” —1 Petro 3:18, NW.

Lile Agano Jipya na Kile Kiumbe Kipya

Sasa sisi tutaona sehemu yenye kukamilisha ya ile siri takatifu. Kuwa kwa Yesu mwaminifu mpaka kifo kunamstahilisha kuwa Kuhani Mkuu na Mfalme wa Yehova. Kwa damu yake iliyomwagwa yeye anahalalisha agano jipya. Agano hilo jipya litatokeza washiriki wa kimbingu watakaotawala pamoja na Yesu wakiwa wafalme na makuhani. (Ufunuo 5:9, 10; 20:4, 6) Wao wanakuwa taifa jipya, “kiumbe kipya,” na kwa hakika hicho ni kitu!—Wagalatia 6:15, 16.

Fikiria: Mungu kupitia Kristo Yesu anachagua hesabu yenye kuwakilisha kutoka wanadamu, wanaume na wanawake. Yeye anaweza kuwatangaza kisheria kuwa waadilifu na kuwaita wawe wana wa kiroho. Kwa majira yake Mungu baada ya kifo chao, yeye huwafufua kwenye mbingu na kuwapa kutokufa, hata kama vile Mungu alivyomthawabisha Yesu. (1 Petro 1:3, 4) Lo! ni uhakika gani alio nao katika “kiumbe kipya” chake na ushikamanifu wao kwake! Lo! ni jibu kama nini kwa yule aliyewashtaki kwa uwongo mbele za Yehova! (Ufunuo 12:10) Ijapokuwa wao ni wasioweza kufa wakiwa pamoja na Kristo Yesu, wao kamwe kamwe hawatakosa ushikamanifu kwa Yehova. Lakini si hayo tu.

Ile Dunia Paradiso

Kristo Yesu, pamoja na wafalme na makuhani washiriki wake wa kimbingu, watahakikisha kwamba kusudi la Yehova kwa mwanadamu na dunia litatimizwa kwa ukamili wakati wa Utawala wa Mileani wake. Akitumia manufaa za ukombozi, Yesu atawafufua wafu na, atawaleta walio waaminifu miongoni mwao na waokokaji wa mwisho wa mfumo huu mbovu, atawaleta waaminifu kwenye ukamilifu wa kibinadamu. Wakati uo huo, dunia itafanywa kuwa paradiso. Wale wote ambao wakati huo watakataa jitihada ya mwisho ya Shetani ya kuwapotosha watapewa uzima mkamilifu wa kibinadamu milele. Shetani na umati wake wote wenye uovu wataangamizwa milele. Amani na umoja vitaenea katika uumbaji wote, ukitetea kikamili enzi kuu ya Yehova na utawala wake wa upendo. Wote malaika na wanadamu watakuwa wameonyesha upendo mshikamanifu kwa Muumba na Mungu wao. —Ufunuo, sura ya 20.

Sasa sisi tunaweza kuifahamu vizuri zaidi ile siri takatifu. Sasa sisi tunaona hekima ya Yehova inayopita hata ubuni wake wa kuumba katika malimwengu ya mimea na wanyama. Sisi tuna sababu nzuri ya kupaaza sauti hivi: “O kina cha mali ya Mungu na hekima na maarifa! Jinsi hukumu zake hazichunguziki . . . Kwa sababu kutoka kwa yeye na kwa yeye na kwa ajili ya yeye kuna vitu vyote. Kwa yeye kuwe utukufu milele. Amina.—Warumi 11:33-36, NW.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Matokeo ya dhambi moja ya Adamu mkamilifu na kupotezwa kwa uhai wake kungeweza kusawazishwa. Jinsi gani? Na uhai mwingine mkamilifu wa kibinadamu, ule wa Yesu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki