Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 4/15 uku. 30
  • Je! Unakumbuka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unakumbuka?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Habari Zinazolingana
  • Yubile ya Yehova—Wakati Wetu Kufurahi Sana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Yehova Ameandaa Njia ya Kukuweka Huru
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 4/15 uku. 30

Je! Unakumbuka?

Je! wewe umefikiria kwa uangalifu matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi? Ikiwa ndivyo, inaelekea utaweza kukumbuka mambo yafuatayo:

◻ Ni kwa sababu gani haimpasi Mkristo kusherehekea Krismasi?

Sababu moja ni kwamba sherehe ya Krismasi ilikuwa na mwanzo wake katika mwadhimisho wa kipagani wa Saturnalia, ile sherehe ya Kiroma ya mungu wa kilimo Saturni. Neno la Mungu lasema: “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa.” (2 Wakorintho 6:14-17) Mkristo hawezi kujitenga na wasioamini hali angali anaadhimisha sherehe yenye mwanzo wa kipagani.​—12/15, ukurasa 6.

◻ Yubile ya Kikristo ni nini?

Ni kukombolewa kunakohusu “kweli” inayoweza kuwaweka wanadamu huru kutoka “sheria ya dhambi na mauti.” Kweli hiyo inategemea “Mwana,” Yesu Kristo. (Yohana 8:31-36; Warumi 8:1, 2,21)​—1/1, ukurasa 21.

◻ Yubile ya Kikristo inaadhimishwa wakati gani?

Katika Pentekoste 33 W.K., Yubile ya Kikristo ilianza kuadhimishwa na wale waliokusudiwa uzima katika mbingu. Kwa wanadamu wanaoamini watakaofurahia uzima wa milele duniani, watapata Yubile kuu ya Kikristo wakati wa Mileani, kwa kuwa dhambi na kutokamilika kote kulikorithiwa kutafutiliwa mbali.​—1/1, kurasa 21,22, 27.

◻ Ni kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova hawaendeshi shule kwa ajili ya watoto katika Esia na kwingineko?

Kwa sababu ya mambo yanayosemwa na Biblia, ni lazima kwanza Mashahidi wa Yehova wahangaikie agizo lao la kuhubiri ule ujumbe wa maana sana kuhusu UfaIme wa Mungu. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Si kwamba hawafahamu kuteseka kwa kibinadamu na matendo yasiyo ya haki katika mfumo uliopo, na wanasaidia kadiri wawezavyo. Hata hivyo wao wanatambua kwamba ponyo la kweli limo, si mikononi mwa wanadamu, bali katika ukombozi ambao Ufalme wa Mungu utaleta karibuni. (Zaburi 146:3-10)​—1/15, ukurasa 7.

◻ Ni nyuso (sehemu) zipi za imani tunazoweza kujifunza kutokana na mifano ya Abeli, Enoki, Noa, Abrahamu, na Musa?

Imani kama ya Abeli inazidisha uthamini wetu kwa dhabihu ya Yesu. Imani ya kweli inatusaidia tuwe wajasiri, kama Enoko. Kama vile Noa, imani inatusukuma sisi tufuate maagizo ya Mungu. Imani ya Abrahamu inakazia ndani yetu uhitaji wa kutii Mungu na kutumaini ahadi zake. Inatupasa tubaki bila doa kutokana na ulimwengu na kusimama kwa ushikamanifu pamoja na watu wa Mungu, kama Musa alivyotoa mfano.​—1/15, ukurasa 20.

◻ Ni katika njia gani utafiti unaweza kuwa ama baraka ama laana?

Utafiti wenye afya juu ya Muumba wetu, mapenzi yake, na makusudi yake unaweza kuwa wenye kuridhisha sana na kunufaisha, ukileta furaha na burudiko maishani mwetu. Kwa upande mwingine, utafiti usiozuiwa unaweza kutuongoza katika ziwa la tope la makisio na nadharia za binadamu, na kuharibu imani halisi na kujitolea Mungu.—2/1, ukurasa 29.

◻ Yesu alimaanisha nini aliposali hivi: “Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke.”? (Mathayo 26:39)

Yesu alihangaikia lile shtaka la kukufuru ambalo aliona lingetupwa juu yake. Huo ndio uliokuwa uhalifu mbaya zaidi ambao Myahudi ye yote angekuwa na hatia yao. Kwa hiyo, kifo chake chini ya hali hiyo kingeonekana kikimletea suto Baba yake wa kimbingu.​—2/15, ukurasa 13.

◻ Ikiwa mtu analazimika kuvumilia mateso au dhiki, ni nini ulio mwendo wa hekima kuchukua?

Ni bora kwake kuwa na saburi, akimtegemea Mungu kwa tumaini’ apate faraja, na kumkaribia Yeye zaidi. Jambo hilo litaifanya iwe rahisi kwa mtu huyo kuvumilia mambo mengine yanayofanana na hayo maishani bila ya kupoteza tumaini. (Maombolezo 3:25-31)​—2/15, ukurasa 24.

◻ Ni nani walio zile “kabila kumi na mbili za Israeli” waliotajwa na Yesu kwenye Luka 22:28-30?

Hao wanawaakilisha jamii zote za wanadamu watakaohukumiwa na Kristo na makuhani wadogo wake 144,000 kuhusiana na kuumbwa upya kwa yote ambayo Yehova amekusudia kwa dunia hii. (Mathayo 19:28)​—3/1, ukurasa 28.

◻ Ni nini linalomaanishwa na amani ya kimungu, nayo inaweza kupatikanaje?

Amani ya kimungu ni hali tulivu ya akili na moyo, hali tulivu ya ndani, bila kujali yale ambayo huenda yakawa yanatukia. (Zaburi 4:8) Inaweza kupatikana tu kutokana na uhusiano uliokubaliwa pamoja na Mungu, unaowezeshwa na dhabihu ya ukombozi wa Kristo Yesu. (Wakolosai 1:19, 20)​—3/15, kurasa 11, 14, 15.

◻ Tuna misaada gani leo ya kutusaidia kupata kujua Mungu kwa ukaribu sana?

Tuna Biblia na pia utimizo ulio wazi wa karne nyingi wa unabii mbalimbali wa Biblia. Vilevile, tuna maandishi ya Gospeli ya maisha, kazi, na maneno ya Yesu Kristo, ambaye juu yake Paulo aliandika hivi: “Ni katika yeye [Kristo] kwamba ujazi wote wa sifa ya kimungu unakaa kimwili.” (Wakolosai 2:9, NW)​—4/1, ukurasa 6.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki