Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 5/1 kur. 10-14
  • Njaa Yenye Kuleta Kifo Katika Wakati wa Utele

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Njaa Yenye Kuleta Kifo Katika Wakati wa Utele
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Njaa Yenye Kuleta Kifo
  • Ni Jinsi Gani Ni Wakati wa Utele?
  • Yusufu, Mhifadhi Uhai
  • Mwigizo Unafunuka Hatua kwa Hatua
  • Yusufu Akiwa Misri
  • “Je, Tafsiri Si za Mungu?”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Yehova Hakumsahau Yosefu Kamwe
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Je! Wewe U Mwenye Rehema Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Kuhifadi Uhai Katika Wakati wa Njaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 5/1 kur. 10-14

Njaa Yenye Kuleta Kifo Katika Wakati wa Utele

“Watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa.”​—ISAYA 65:13.

1, 2. (a) Mataifa yanang’ang’ana na matatizo gani bure tu?(b) Biblia inaelekeza kwenye tumaini gani linalolingana na hali za kikweli?

WOGA mwingi sana kuhusu njaa unaning’inia juu ya ulimwengu mzima! Ikitoa elezo juu ya hali hiyo hatari, makala moja ya mhariri katika gazeti The Boston Globe ilisema hivi: “Ulimwengu wenye watu karibu bilioni moja wanaoishi karibu na kufa-njaa lazima upate njia za kusaidia mataifa yaliyo maskini zaidi ili yafurahie kitu kinachokaribia ule wingi wa mavuno yanayopatikana na mataifa yaliyo matajiri zaidi.” Hata hivyo, mataifa yale pia ya-nayoitwa kuwa ni yenye maendeleo ya kiufundi hayawezi kudai kuwa yameepuka kabisa upungufu wa chakula. Hayo yameshindwa pia kutokeza programu ya kuhakikisha kwamba raia wao wote watalishwa. Watu wenye huruma ya kibinadamu wanaojali wanang’ang’ana na tatizo hilo linalokua. Je! kuna suluhisho?

2 Makala ya mhariri iliyotanguliwa kutajwa ilikubali wazi hivi: “Upande ulio wa kufisha moyo zaidi wa ulaji chakula cha hali ya chini . . . ni kwamba ulimwengu una uwezo kabisa wa kulisha kila mtu.” Hata hivyo mjeledi wa njaa kubwa ya chakula na ufaji-njaa unaendelea kusonga mbele. Mbona jambo hilo liwe hivyo? Muumba wetu mwenye upendo ameuandalia vitu vya kutosha umaya-maya wote wa mabilioni ya watu wa dunia. Katika kuitayarisha dunia iwe makao ya wanadamu, yeye aliifanya iweze kuzaa vyakula maridhawa, vinavyozidi kiasi kinachohitajiwa na wote. (Zaburi 72:16-19; 104:15, 16, 24) Hata katika nyakati hizi za taabu-taabu, sisi tunahakikishiwa kwamba Mwandalizi Mkuu wetu atawatolea chakula cha kuwatosha wale wanaotegemea Chanzo kinachofaa. Kupitia Yule ambaye yeye alimpa kuwa Msimamizi wa Chakula mkuu anatuambia hivi: “Endeleeni . . . kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu [wa Mungu], na mambo yote hayo mengine [mahitaji ya kimwili ya maisha] mtaongezewa.”​—Mathayo 6:33; 1 Yohana 4:14, NW.

Njaa Yenye Kuleta Kifo

3. Ni njaa gani ya chakula iliyo ya umaana mkubwa zaidi, nayo ilitabiriwaje?

3 Jambo la kuelekezewa umaana ulio mkubwa zaidi duniani leo ni njaa ya chakula cha kiroho yenye kutia majonzi. Inahusiana moja kwa moja na ukosefu wa amani. Jamii ya kibinadamu inatanga-tanga huku na huku, ikitafuta juu-chini njia ya kutokea. Mungu mwenye nguvu zote alisababisha nabii wake aandike juu ya hali hiyo karne nyingi zilizopita, akisema: “Angalia, siku zinakuja, asema Bwana [Yehova], ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya [Yehova]. Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la [Yehova], wasili-one.”​—Amosi 8:11, 12.

4, 5. (a) Kwa sababu gani wengine hawampati Mungu ingawa wanamtafuta? (b) Yesu alitofautianaje na viongozi wa kidini wa siku zake? (Mathayo 15:1-14)

4 Hata hivyo, je! kuna njia ya kutoka katika mgogoro huo? Mtume Paulo anajibu ndiyo, akitutia moyo kwa maneno haya: “Mungu aliyeufanya ulimwengu . . . [aliwekea wana-damu] nyakati alizoziamuru tangu zamani, na mipaka ya makazi yao; ili kumtafuta Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.”​—Matendo 17:24-27.

5 Ikiwa Mungu “hawi mbali na kila mmoja wetu,” mbona watu wengi wanapapasa-papasa wakimtafuta wasimpate? Ni kwa sababu wao wanamtafuta mahali-mahali pasipofaa. Ni wangapi wanaojiita Wakristo wanaokiendea kibinafsi kitabu kile kikuu cha mafundisho ya Ukristo, Biblia Takatifu, ili wapate mashauri? Ni wangapi wale wanaoitwa eti “wachungaji” wanaotumia Neno la Mungu kuwafundisha “kondoo”? (Linganisha Ezekieli 34:10.) Yesu aliwaambia viongozi wa kidini wenye kiburi wa siku zake kwamba wao ‘hawakuyajua maandiko wala uweza wa Mungu.’ (Mathayo 22:29; Yohana 5:44) Hata hivyo, Yesu aliyajua na hata akafundisha watu Maandiko hayo, wale ambao yeye alihisi huruma kwa ajili yao “kwa sababu walikuwa hoi na wenye wasiwasi kama kondoo wasio na mchungaji.”​—Mathayo 9:36, HNWW.

Ni Jinsi Gani Ni Wakati wa Utele?

6. Kwa habari ya utele wa kiroho, Yehova anarudiaje kuwapa watumishi wake uhakikisho?

6 Yehova anawapa uhakikisho na kitia-moyo wale wanaotafuta kumjua yeye kwa moyo mweupe. Katika kukaripia wachungaji wa uwongo wa kidini, yeye anasema hivi kupitia nabii wake Isaya: “Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi bali ninyi mtatahayarika.” (Isaya 65:13, 14) Lakini Mungu anaandaaje utele kwa ajili ya watumishi wake mwenyewe? Ni lazima sisi tufanye nini ili tushiriki kwa furaha katika uandalizi wake wa kuhifadhi uhai, kujapokuwa na njaa kubwa ya kiroho leo?

7. Ni mwigizo gani wa kale ulioandaliwa kwa upendo kwa ajili ya kitia-moyo chetu leo?

7 Kwa kuwa kuokoka kunategemea kabisa kujua kwetu matakwa ya Mungu na kuyatenda kwa imani, inatupasa tuliendee Neno la Mungu kwa furaha, tukitafuta kujua mapenzi yake kwetu sisi na kutambua njia yake ya kushughulika pamoja nasi. (Yohana 17:3) Kwa kusudi hilo, sasa tutafikiria mwigizo wa Kibiblia unaolingana na linalotukia leo. Mhu-sika Mkuu katika mwigizo huo ni Yusufu mzee wa ukoo. Kama vile Yehova alivyofanya uandalizi wa hekima kwa ajili ya watu Wake kupitia Yusufu, ndivyo Yeye anavyoongoza kwa upendo wale wanaomtafuta Yeye leo.​—Linganisha Warumi 15:4; 1 Wakorintho 10:11, maelezo ya chini (*) NW katika Biblia ya Marejezo; Wagalatia 4:24.

Yusufu, Mhifadhi Uhai

8, 9. (a) Ni ulinganifu gani tunaopata katika nyakati za baadaye kwa Yusufu, Yakobo na Farao? (b) Sisi wenyewe tunaweza kuhusikaje katika utimizo huo?

8 Akiwa mhifadhi uhai, Yusufu mwana wa Yakobo alishiriki fungu la kuvutia sana. Je! hilo linaonyesha jambo fulani katika nyakati za baadaye? Basi, fikiria uvumilivu wa Yusufu wa kutendwa na ndugu zake mambo ambayo hakustahili, kukabili kwake michunguzo na majaribu katika nchi ya kigeni, imani yake isiyotikisika katika kudumisha ukamilifu, na kupandishwa cheo awe msimamizi mwenye hekima katika wakati wa njaa yenye kuleta uangamivu. (Mwanzo 39:1-3, 7-9; 41:38-41) Je! hatuoni ulinganifu katika mwendo wa maisha ya Yesu?

9 Ni kupitia kupatwa na janga kwamba Yesu akawa Mkate wa Uzima katikati ya ulimwengu wenye kukosa sana chakula cha “kuyasikia maneno ya [Yehova].” (Amosi 8:11; Waebrania 5:8, 9; Yohana 6:35) Katika mahusiano yao na Yusufu, Yakobo na hata Farao wanatukumbusha juu ya Yehova na mambo anayotimiza kupitia Mwanaye. (Yohana 3:17, 34; 20:17; Warumi 8:15, 16; Luka 4:18) Walikuwako wengine pia walioshiriki katika mwigizo huu wa maisha ya halisi nasi tutafikiria sehemu zao kwa kupendezwa. Bila shaka tutakumbushwa juu ya tegemeo letu wenyewe juu ya Yusufu Mkubwa Zaidi, Kristo Yesu. Tunapiga asante kama nini kwamba yeye anatuhifadhi tusipatwe na njaa yenye kuleta kifo wakati wa “siku za mwisho” hizi zinazozidi kuwa mbaya!​—2 Timotheo 3:1, 13.

Mwigizo Unafunuka Hatua kwa Hatua

10. (a) Yusufu alitayarishwaje kwa ajili ya daraka alilopaswa kutimiza? (b) Ni sifa gani alizoonyesha kwanza-kwanza maishani?

10 Katika siku za Yusufu, hakuna mwanadamu angaliweza kujua mapema ni mambo gani ambayo Yehova alikuwa amewawekea watu Wake akibani. Lakini kufikia wakati ambao Yusufu aliitwa kutimiza fungu lake muhimu, Yehova alikuwa tayari amemzoeza na kumkamilisha kwa habari za sifa zake. Kuhusu maisha yake ya kwanza-kwanza usimulizi unasomwa hivi: “Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.” (Mwanzo 37:2) Yeye alionyesha ushikamanifu kwa mapendezi ya baba yake kama vile Yesu alivyokuwa mshikamanifu bila kuyumba-yumba katika kulisha kundi la kondoo za Baba yake katikati ya “kizazi kisichoamini, kilichopotoka.”​—Mathayo 17:17, 22, 23.

11. (a) Kwa sababu gani ndugu-nusu za Yusufu walikuja kumchukia? (b) Ni hali gani inayofanana na hiyo iliyohusu Yesu Kristo?

11 Baba ya Yusufu, Israeli, akaja kumpenda yeye zaidi ya ndugu zake wote na akampendelea kwa kuagiza ashonewe kanzu ndefu yenye milia-milia. Kwa sababu hiyo, ndugu-nusu za Yusufu “wakaanza kumchukia yeye, na hawakuweza kusema naye kwa amani.” Walipata sababu zaidi ya kumchukia alipokuwa na ndoto mbili walizozifasiri kumaanisha kwamba yeye angewatawala. Kwa njia inayofanana na hiyo, viongozi miongoni mwa Wa-yahudi walikuja kumchukia Yesu kwa sababu ya ushikamanifu wake, kufundisha kwake kwa njia yenye usadikishi, na kwa sababu ya baraka ya Yehova iliyoonekana wazi juu yake.​—Mwanzo 37:3-11; Yohana 7:46; 8:40, NW.

12. (a) Kwa sababu gani Yakobo alihangaikia masilahi ya wana wake? (b) Ni ulinganifu gani tunaopata kati ya mwenendo wa Yusufu na ule wa Yesu?

12 Baada ya muda fulani, ndugu za Yusufu wakawa wanalisha kondoo karibu na Shekemu. Baba ya Yusufu alihangaika kwa kufaa kwa sababu kule ndiko Shekemu alikuwa amemwingilia Dina kinguvu, hivi kwamba Simeoni na Lawi wakiwa pamoja na ndugu zao, wakawa wamewaua wanaume wa mji huo. Yakobo alimwomba Yusufu aende akaone masilahi yao na kumrudishia habari. Ijapokuwa ndugu zake walikuwa na uhasama kumwelekea, Yusufu alijiondokea papo hapo akawatafute. Kwa namna inayofanana na hiyo, Yesu aliukubali kwa furaha mgawo wa Yehova hapa duniani, hata ingawa ungemaanisha taabu kubwa wakati wa kukamilishwa kwake awe Wakili Mkuu wa wokovu. Katika uvumilivu wake, Yesu akawa mfano mzuri kama nini kwetu sote!​—Mwanzo 34:25-27; 37:12-17; Waebrania 2:10; 12:1, 2, NW.

13. (a) Ndugu-nusu za Yusufu walifunguliaje chuki yao? (b) Huzuni ya Yakobo inaweza kulinganishwa na nini?

13 Ndugu-nusu kumi za Yusufu wakamwona akija kwa mbali. Papo hapo hasira yao ikawaka dhidi yake, nao wakatunga hila ya kumwondolea mbali. Kwanza walipanga ku-mwua. Lakini kwa kuogopa kuhusu daraka lake akiwa mzaliwa wa kwanza, Reubeni akawashinda kwa maneno ili wamtupe Yusufu ndani ya birika la maji lililo kavu, akitazamia kurudi baadaye na kumweka huru. Hata hivyo, wakati huo, Yuda akawasadikisha ndugu zake wamwuze kama mtumwa kwa Waishmaeli fulani ambao msafara wao ulikuwa ukipita. Ndipo ndugu hao wakachukua kanzu ndefu ya Yusufu na kuichovya ndani ya damu ya beberu na kumpelekea baba yao. Yakobo alipoichunguza alipaaza sauti: “Ndiyo kanzu ya mwanangu, mnyama mkali amemla; bila shaka Yusufu ameraruliwa”. Lazima iwe kwamba Yehova alihisi kihoro kama hicho juu ya taabu ya Yesu alipokuwa akitimiza mgawo wake duniani.​—Mwanzo 37:18-35; 1 Yohana 4:9, 10.

Yusufu Akiwa Misri

14. Mwigizo huo wa kale unaweza kuwa na manufaa gani kwetu leo?

14 Haitupasi kamwe kukata shauri kwamba matimizo ya matukio hayo ya mwigizo unaohusu Yusufu yanatukia kwa mfuatano ule ule kabisa wa kitarehe kama ilivyotukia kule nyuma. Bali, tunapata kule nyuma mfululizo wa vielelezo ambavyo ni vya kutupa sisi maagizo na kitia-moyo leo. Ni kama vile mtume Paulo anavyosema: “Yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini. Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa mfano wa Kristo Yesu; ili kwa moyo mmoja na kwa kinywa kimoja mpate kumtukuza Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.”​—Warumi 15:4-6.

15. Kwa sababu gani Yusufu na nyumba na Potifa walifanikiwa?

15 Yusufu alipelekwa Misri, na kule akauzwa kwa Mmisri jina lake Potifa, mkuu wa walinzi wa Farao. Yehova alithibitika kuwa pamoja na Yusufu, aliyeendelea kuishi kwa kufuata kanuni nzuri sana ambazo baba yake alikuwa amekaza kikiki ndani yake, hata ingawa yeye alikuwa mbali sana na nyumba ya baba yake. Yusufu hakuachilia mbali ibada ya Yehova. Bwana wake, Potifa, alikuja kuthamini sifa za Yusufu zenye kutokeza na kumweka juu ya watu wa nyumba yake yote. Yehova aliendelea kuibariki nyumba ya Potifa kwa sababu ya Yusufu.​—Mwanzo 37:36; 39:1-6.

16, 17. (a) Yusufu alikutanaje na jaribu zaidi la ukamilifu? (b) Yaliyompata Yusufu gerezani yanaonyesha mwelekezo gani wa mambo?

16 Kule ndiko mke wa Potifa alijaribu kumtongoza Yusufu. Yeye akaendela kumkataa. Siku moja mwanamke huyo akashika kwa ghafula kanzu yake, lakini yeye akakimbia, akiiacha mkononi mwake. Mbele ya Potifa, mwanamke huyo alimshtaki Yusufu juu ya kufanya utongozi usio wa adili, na Potifa akaagiza Yusufu atupwe ndani ya gereza. Kwa muda fulani yeye alifungwa kwa pingu za chuma. Lakini kwa muda wote wa majanga yaliyompata gerezani, Yusufu aliendelea kuthibitisha kwamba alikuwa mwanamume wa ukamilifu. Hivyo, mtunza-gereza alimweka awe na kabidhi ya kutunza wafungwa wote.​—Mwanzo 39:7-23; Zaburi 105:17, 18.

17 Baada ya muda kupita, mnyweshaji mkuu wa Farao na mkuu wa waokaji wali-mchukiza yeye na wakatiwa gerezani. Yusufu alipewa mgawo wa kuwahudumia. Tena, Ye-hova akaelekeza mambo kwa maarifa. Wakuu wale wawili wa barazani walipata ndoto zili-zowafadhaisha. Baada ya kukazia kwamba “fasiri ni za Yehova,” Yusufu aliwaambia yaliyomaanishwa na ndoto hizo. Na sawa na vile Yusufu alivyokuwa ameonyesha, siku tatu baadaye (katika siku ya uzaliwa wa Farao) mnyweshaji alirudishwa kwenye cheo chake, lakini mkuu wa waokaji akanyongwa.​—Mwanzo 40:1-22, NW.

18. (a) Yusufu alikujaje kukumbukwa? (b) Maana ya ndoto za Farao ilikuwa nini?

18 Ingawa Yusufu alikuwa amemlalamia sana mnyweshaji aseme na Farao kwa ajili yake, miaka miwili ilipita kabla ya mwanamume huyo kumkumbuka Yusufu. Hata hivyo, lililomfanya amkumbuke ni kwa sababu tu Farao alipata mara mbili ndoto zenye kumfadhaisha katika usiku mmoja. Kulipokuwa hakuna ye yote wa makuhani wazoea-uchawi wa mfalme ambaye angeweza kufasiri maana ya ndoto hizo, mnyweshaji alimwambia Farao kwamba Yusufu angeweza kufasiri ndoto. Kwa hiyo Farao akapeleka neno kwamba Yusufu aletwe, ambaye kwa unyenyekevu alielekeza kwenye chanzo cha fasiri za kweli, akisema: “Mungu atampa Farao Majibu ya amani.”

“Nalikuwa nikisimama ukingoni mwa mto [Naili]; na tazama, ng’ombe, saba wanatoka mtoni, wanono, wazuri, wakajilisha manyasini. Kisha, tazama, ng’ombe saba wengine wakapanda baada yao, dhaifu, wabaya sana, wamekonda; katika nchi yote ya Misri sijaona kama hao kwa udhaifu. Na hao ng’ombe waliokonda, wabaya, wakawala wale ng’ombe saba wa kwanza, wale wanono. Na walipokwisha kuwala haikutambulikana ya kwa-mba wamewala, bali wakaonekana wabaya kama kwanza. . . .

“Kisha nikaona katika ndoto yangu, na tazama, masuke saba yanatokeza katika bua moja, mema, yamejaa. Na tazama, masuke saba membamba, dhaifu, yamekaushwa na upepo wa mashariki, yakatokeza baada yao. Na hayo masuke dhaifu yakameza yale masuke saba mema. Nami nikawaambia hao waganga [makuhani wazoea-uchawi, NW], wala hakuna aliyeweza kunionyesha maana yake.”​—Mwanzo 40:23–41:24.

19. (a) Yusufu alionyeshaje unyenyekevu? (b) Ni ujumbe gani uliotolewa na fasiri ya ndoto hizo?

19 Lo! ndoto za kiajabu kama nini! Mtu ye yote angewezaje kueleza maana yazo? Yusufu alieleza, lakini si kwa ajili ya utukufu wa kibinafsi. “Ndoto ya Farao ni moja; Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya.” Ndipo Yusufu akaendelea kuufunua ujumbe ule thabiti wa kiunabii juu ya ndoto zile, akisema:

“Tazama, miaka saba ya shibe [utele, NW] inakuja, katika nchi yote ya Misri. Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi. . . . Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.”​—Mwanzo 41:25-32.

20, 21. (a) Farao alitendaje kwa kupata onyo lile? (b) Kufikia hapa, Yusufu na Yesu wanaweza kulinganishwaje?

20 Farao angeweza kufanya nini juu ya njaa hiyo kubwa ya chakula iliyokuwa ikikaribia? Yusufu alipendekeza kwamba Farao afanye tayarisho kwa kuweka mtu mwenye akili na hekima juu ya nchi ili aweke akibani mavuno ya ziada ya miaka ile mizuri. Kufikia sasa Farao alikuwa ametambua sifa za kutokeza za Yusufu. Akiivua pete yake ya muhuri kutoka mkononi mwake mwenyewe na kuitia mkononi mwa Yusufu, kwa njia hiyo Farao alimweka rasmi awe juu ya nchi yote ya Misri.​—Mwanzo 41:33-46.

21 Yusufu alikuwa na umri wa miaka thelathini aliposimama mbele ya Farao, umri ule ule ambao Yesu Kristo alikuwa nao alipobatizwa na kuanza huduma yake yenye kutoa uzima. Makala inayofuata itaonyesha jinsi Yusufu alitumiwa na Yehova katika kutangulia kuwa kivuli cha “Wakili Mkuu [wa Yehova] na Mwokozi” katika wakati wa njaa kubwa ya chakula cha kiroho kwa kuhusiana kipekee na siku zetu wenyewe.​—Matendo 3:15; 5:31.

◻ Ni kwa njia gani maradufu njaa ni tisho leo?

◻ Ni sifa gani nzuri sana ambazo Yusufu alisitawisha alipokuwa pamoja na ndugu-nusu zake?

◻ Sisi tunaweza kujifunza nini kutokana na mambo yaliyompata Yusufu kwanza-kwanza katika Misri?

◻ Tendo la Yehova la kumjali Yusufu na watu wenye kukumbwa na njaa kubwa ya chakula linatuhakikishia nini?

[Maswali ya Funzo]

[Sanduku katika ukurasa wa 13]

Mchanga-habari katika safu ya gazeti Sunday Star (Toronto, Machi 30, 1986) alisema hivi juu ya yale yanayoitwa eti makanisa makubwa-makubwa: “Mahali yanaposhindwa vibaya ni katika kutosheleza njaa ya kiroho yenye kina kirefu ya wanaume, wanawake na vijana wa leo.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki