Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 5/15 kur. 21-23
  • Msaada Katika Kufanya Maamuzi Yenye Hekima

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaada Katika Kufanya Maamuzi Yenye Hekima
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jifunze Kutokana na Wakati Uliopita
  • Wakabiliwa na Uamuzi
  • Kufaidika na Shauri Lenye Hekima
  • Usikose Kujua Hila za Shetani
  • Kupata Kuwajua Wakristo wa Kwanza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Kitabu Cha Biblia Namba 46—1 Wakorintho
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Kitabu Cha Biblia Namba 47—2 Wakorintho
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Je, Umoja wa Kikristo Unawataka Watu Wafanane?
    Amkeni!—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 5/15 kur. 21-23

Msaada Katika Kufanya Maamuzi Yenye Hekima

ALICE alifanya uamuzi usio wa hekima ambao uligeuka kuwa msiba. “Mimi nilijiondoa mwenyewe kutoka kwa Yehova na tengenezo lake,” anakubali. Ingawa mwishowe alirudi, ilimchukua zaidi ya miaka 13 kufanya hivyo—“miaka yenye huzuni” ndivyo anavyoiita.

Mkristo hapaswi kukadiri kidogo hatari ya kufanya maamuzi yasiyo ya hekima kuhusiana na utumishi wake kwa Mungu. Si kwamba maamuzi yasiyofaa yanafanywa kimakusudi baada ya kufikiria mambo ya uhakika yanayofaa. Nyakati nyingine yanafanywa tu kwa msingi wa maitikio ya kisilika. Maono ya moyoni yakiisha faulu kufunika suala kana kwamba kwa wingu nao moyo usiokamilika unatoa maongozi yasiyofaa juu ya uwezo wa kufikiri, umizo la kila namna ya huzuni laweza kutokea.

Kweli kweli, “moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote.” (Yeremia 17:9) Hata hivyo, Biblia, inatuambia jinsi tunavyoweza kujilinda wenyewe. “Hekima inapoingia katika moyo wako,” yasema, “utambuzi wenyewe utakuhifadhi wewe.” (Mithali 2:10, 11, NW) Lakini tunaifanyaje hekima iingie katika moyo wetu?

Jifunze Kutokana na Wakati Uliopita

Jaribu hili. Jiweke mwenyewe katika hali ya watumishi wa Mungu wa kwanza-kwanza walioelekeana na hali zenye kujaribu zinazofanana na zako. Tuseme, kwa mfano, kwamba hali fulani katika kundi la Kikristo la kwenu inakufanya uhangaike. Jaribu kufikiria hali inayolingana na hiyo inayotajwa katika Biblia.

Namna gani kundi la Kikristo la karne la kwanza kule Korintho? Wazia kwamba ni mwaka 54 au 55 W.K. na wewe ni mshiriki wa kundi la Korintho. Umekuwa Mkristo kwa miaka miwili au mitatu. Ilikuwa furaha kama nini kuja kujua maarifa ya ukweli wakati wa miezi 18 ya Paulo kukaa kule! Lakini sasa, mambo yanaonekana kuwa mabaya.

Mwelekeo wa kufanyiza vikundi vya marafiki wachache na vikundi vyenye kuleta farakano unatokeza kutopatana kundini, na kutisha kuwa umoja walo. (1 Wakorintho 1:10, 11) Kuvumiliwa kwa mwenendo usio wa adili kunahatirisha roho yalo. (1 Wakorintho 5:1-5) Kuonyesha hadharani tofauti kati ya washiriki wa kundi mbele ya mahakama za kisheria za kilimwengu kunaharibu sifa nzuri yalo.—1 Wakorintho 6:1-8.

Ukiwa ungali unawaza mwenyewe kuwa katika Korintho wa kale, unahangaishwa kwamba wengine wa washiriki wa kundi wanagombana sikuzote juu ya mambo ambayo kwa kweli ni ya umaana mdogo tu. (Linganisha 1 Wakorintho 8:1-13.) Unahuzunishwa na mashindano, husuda, hasira, na kutokuwa na utaratibu unakoona. (2 Wakorintho 12:20) Kweli kweli, unasumbuliwa na wachache wenye kutakabari wanaofanya maisha ya Kikristo kuwa magumu isivyo lazima. (1 Wakorintho 4:6-8) Unaudhika kusikia kwamba wengine hata wanatilia shaka cheo na mamlaka ya mtume Paulo, wakifanya mashtaka yasiyo haki, na kudhihaki ukosefu wake wa ufasaha akiwa msemaji. (2 Wakorintho 10:10; 12:16) Unaona wasiwasi isije kuwa kwamba wale wanaoendeleza waziwazi maoni yao ya kibinafsi wangeweza kuharibu imani ya kundi katika mafundisho ya kidini ya msingi.—1 Wakorintho 15:12.

Wakabiliwa na Uamuzi

‘Haipasi kamwe kuwa hivi,’ wapiga kite. ‘Kwa sababu gani wazee hawasahihishi mambo? Jambo fulani limekuwa baya sana.’

Je! wewe utaliacha kundi katika Korintho, ukiamua kwamba ungekuwa katika hali bora zaidi ukimtumikia Mungu mahali penginepo? Au pengine hata utaamua kwamba ingekuwa bora zaidi kuacha kushirikiana kabisa na Wakristo wenzako? Je! utaruhusu matatizo hayo yapoze furaha yako na uhakika wako kwamba Yehova Mungu na Yesu Kristo ndio wanaosimamia mambo? Je! utasitawisha roho ya kulalamika na kuchambua, ikikufanya utilie shaka makusudio ya Wakristo wenzako? Je! utapunguza mwendo katika kazi ya kuhubiri, ukitoa sababu kwamba kuna umaana mdogo sana wa kuelekeza wanaopendezwa kwenye kundi kama hilo?

Kwa kutazama hali bila upendeleo kutoka mahali panapofaa leo, huenda ukaliona kuwa ni jambo rahisi kusema kwamba uamuzi wako ungalikuwa kukaa kwa ushikamanifu karibu na kundi la Mungu, kujapokuwa kutokamilika kwalo. Lakini ukikabiliwa na hali kama hiyo leo, je! ungeweza kudumisha akili iliyo wazi na moyo uliotulia? Je! ungeamua leo kama vile unavyofikiri ungaliamua ikiwa ungekuwa ukishi wakati huo?

Kufaidika na Shauri Lenye Hekima

Wakristo Wakorintho waliofanya uamuzi wenye hekima walikuwa wale waliokaa karibu na kundi. Walihisi kama alivyohisi Petro miaka mingi mapema. Wakati baadhi ya wanafunzi walipoacha kushirikiana na Yesu, Petro alisema: “Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.” (Yohana 6:68, 69) Kwa wazi, ni kwa kukaa tu karibu na tengenezo la Mungu kwamba tunaweza kunufaika kutokana na shauri lalo.

Katika makundi mapya, kama hilo huko nyuma katika Korintho, si jambo lisilo la kawaida kwa kutokamilika kwa kibinadamu kusababisha tatizo ambalo huenda likataka kutolewa kwa shauri lenye nguvu. Lakini katika kutoa shauri kwa Wakristo katika Korintho, Paulo alikumbuka kwamba kwa kadiri kubwa walio wengi wao walikuwa wangali “wapenzi.” (1 Wakorintho 10:14; 2 Wakorintho 7:1; 12:19) Yeye hakusahau kwamba Yehova huwatolea fadhili zisizostahilika na msamaha wale wanaoitikia mwelekezo Wake.​—Zaburi 130:3, 4.

Bila shaka, kwa kuwa kundi la Kikristo huvuta watu wa kila aina, wengine wanachukua muda mrefu zaidi kuitikia mwelekezo huo kuliko wanavyofanya wengine. Iko hivyo kwa sababu mbalimbali. Mabadiliko fulani ni magumu zaidi kufanywa kuliko mengine. Pia, kila mtu mmoja mmoja ni tofauti katika muundo wa kimwili na kiakili, mazingira, malezi, na hali. Kwa hiyo ni jambo lenye hekima kama nini kuepuka kuwa mwenye kulaumu kupita kiasi na kukumbuka kwamba “[upendo] husitiri wingi wa dhambi”! (1 Petro 4:8) Ingawaje, ikiwa Yehova na Mwanaye wana nia ya kuvumilia kutokamilika kwa kibinadamu na kutokomaa katika kundi lao, je! haitupasi sisi kudhihirisha roho iyo hiyo?​—1 Wakorintho 13:4-8; Waefeso 4:1, 2.

Kama ungalikuwa katika kundi la Korintho wa kale, ukisikiliza shauri imara lakini lenye upendo la Paulo kungekukumbusha kwamba Kristo, akiwa kichwa cha kundi la Kikristo, anapendezwa sana na masilahi yalo. (Mathayo 28:20) Hilo lingejenga uhakika wako katika ahadi ya Yesu ya kuweka wafuasi wake wakiwa wameunganishwa kadiri walivyoitikia msaada ulioandaliwa kupitia “mtumwa mwaminifu mwenye akili. (Mathayo 24:45-47; Waefeso 4:11-16) Ndiyo, na maneno ya Paulo yangalikusaidia udumishe furaha na uimara hata chini ya hali zenye kujaribu. Ungalikuwa mwenye uhakika kwamba Mungu angekupa wewe nguvu ushinde gumu lo lote ambalo huenda akaruhusu liwepo kwa muda.

Hiyo si kusema kwamba Mkristo hapaswi kusema lo lote ikiwa hali mbaya zinasitawi katika kundi. Huko nyuma katika Korintho, wanaume wakomavu kama vile Stefana, Fortunato, Akaiko, na wengine kutoka nyumbani mwa Kloe, walitenda. Kwa wazi wao walimjulisha Paulo juu ya hali hiyo. (1 Wakorintho 1:11; 5:1; 16:17) Lakini wakiisha kufanya hivyo, wakiwa na uhakika waliacha mambo mikononi mwake. Juhudi kwa ajili ya uadilifu haikuwafanya wapoteze uhakika katika ukichwa wa Kristo au kuwafanya ‘waghadhibike dhidi ya Yehova.’—Mithali 19:3, NW.

Juhudi yetu kwa ajili ya uadilifu wetu leo itatuzuia sisi hata kufikiria wazo la kupunguza mwendo katika mgawo wetu tuliopewa na Mungu wa kuhubiri habari njema. Kufanya hivyo kungedhihirisha ukosefu wa hangaikio kwa ajili ya masilahi ya wengine, na kungekuwa kushindwa kufanya yale ambayo Kristo anatutaka tufanye. “Kwa hiyo, ndugu zangu wapendwa,” akashauri Paulo, “mwe imara, bila kuondoleka, sikuzote mkiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana, mkijua kwamba kazi yenu yenye bidii si ya bure kuhusiana na Bwana.”—1 Wakorintho 15:58, NW.

Usikose Kujua Hila za Shetani

Magumu ya kundi kama yale yaliyokuwako katika Korintho nyakati nyingine yanaweza kuwa vigumu zaidi kuyashughulikia kuliko mateso ya moja kwa moja. Shetani anatumia hali kama hizo kwa faida yake mwenyewe katika jaribio la kutufanya sisi tufanye maamuzi yasiyofaa yatakayotuondoa mbali na Yehova. Lakini ‘sisi hatukosi kujua hila za Shetani.’—2 Wakorintho 2:11, NW.

Paulo aliwaambia Wakristo wa Korintho kwamba wangeweza kunufaika kutokana na kuchunguza maandishi juu ya watumishi wa Mungu wa kwanza-kwanza. “Sasa mambo hayo yaliendelea kuwapata kuwa mifano,” akasema juu ya Waisraeli, “nayo yaliandikwa kuwa onyo kwa sisi ambao juu yetu miisho ya mifumo ya mambo imefika.” (1 Wakorintho 10:11, NW) Vivyo hivyo, sisi leo tunaweza kunufaika kutokana na kuchunguza kwa uangalifu maandishi ya Wakristo wa kwanza. Kwa mfano, tunaweza kufikiria yale yaliyotukia katika Korintho. Kutafakari juu ya jinsi tungalifanya maamuzi yanayofaa wakati huo kutusaidia tuepuke kufanya maamuzi yasiyofaa sasa.

Baada ya “miaka yenye huzuni” 13 ya kutokuwapo, Alice anasema hivi kuhusu mkutano wake wa kwanza katika Jumba la Ufalme: “Mimi niliogopa kuongea nisije nikalia. Nilikuwa nyumbani—nyumbani kweli kweli. Singeweza kuamini hilo.” Kwa hiyo azimia, yajapokuwa magumu ambayo huenda yakazuka, kushikamana na uamuzi wako wenye hekima wa kutoliacha kamwe tengenezo la Yehova! Baraka zako katika kushirikiana na watu wa Mungu zitakuwa tele. Nazo zitakuwa hazina mwisho.—Mithali 2:10-15, 20, 21.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki