Sala Zataka Kazi
“[Yehova, NW] yu mbali na wasio haki; bali huisikia sala ya mwenye haki.“—MITHALI 15:29.
1. Ni hali gani moja ambayo ni lazima itimizwe ikiwa Mungu atajibu sala zetu?
MATAKWA yote ya Yehova ni ya hekima, haki, na ya upendo. Kwa vyo vyote si mazito. (1 Yohana 5:3) Hiyo ircatia ndani matakwa yake kwa habari ya sala, ambayo mojapo ni kwamba sisi tuongoze maisha zetu kupatana na sala zetu. Mwendo wetu wa tendo lazima umpendeze Yehova Mungu. Kama sivyo, tungemtazamiaje afikirie kwa upendeleo maombi yetu na sala zetu za kusihi?
2, 3. Kwa sababu gani Yehova hakujibu sala za Waisraeli, kama inavyoonwa kwa maneno ya Isaya, Yeremia, na Mika?
2 Hii ni sehemu moja ya sala ambayo inapuuzwa na walio wengi wa wale walio katika Jumuiya ya Wakristo, sawa na ilivyopuuzwa na Waisraeli waasi-imani katika siku za Isaya. Ndiyo sababu Yehova alimwagiza nabii wake amwakilishe kama akisema: “Mwombapo maombi mengi, sitasikia . . . Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya; jifunzeni kutenda mema.“ (Isaya 1:15-17) Ndiyo, ikiwa Waisraeli hao walitaka kibali cha Mungu, iliwapasa watenda katika njia iliyopendeza yeye. Kama ambavyo imekwisha kusemwa kwa kufaa: “Ikiwa ungetaka Mungu akusikilize unaposali, ni lazima wewe umsikilize Yeye wakati Yeye anaposema.“
3 Kwa kweli, kwa kurudia-rudia Yehova Mungu aliona lazima ya kuwakumbusha watu wake Israeli juu ya kweli hizi. Hivyo twasoma hivi: “Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria, hata sala yake ni chukizo“ kwa Mungu. “[Yehova, NW] yu mbali na wasio haki; bali huisikia sala ya mwenye haki.“ (Mithali 28:9; 15:29) Kwa sababu ya hali hii, Yeremia aliomboleza hivi: “Umejifunika nafsi yako kwa wingu, maombi yetu yasipite.“ (Maombolezo 3:44) Kweli kweli, onyo ambalo Mika aliongozwa na roho kutoa lilitimizwa: “Ndipo watakapomwomba [Yehova, NW], asiwaitikie; naam, atawaficha use wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.“—Mika 3:4; Mithali 1:28-32
4. Ni jambo gani linaloonyesha kwamba hata miongoni mwa watu wa Yehova wengine hawathamini uhitaji wa kazi zinazopatana na sala zao?
4 Hivyo ni jambo la maana kabisa kuishi kupatana na sala zetu. Je! ni jambo la lazima kukazia uhakika huo leo? Ndivyo kweli kweli, si kwa sababu tu ya hali ilivyo katika Jumuiya ya Wakristo bali pia kwa sababu ya hali ya baadhi ya watu wa Yehova walio wakfu. Kati ya zaidi ya wahubiri 3,000,000 wa habari njema mwaka jana, zaidi ya 37,000 walitengwa na ushirika kwa sababu ya mwenendo usiomfaa Mkristo. Hiyo inajumlika kuwa uwiano wa karibu mmoja kati ya 80. Inawezekana sana, walio wengi wa hao watu mmoja mmoja walikuwa wakisali angalau mara kwa mara. Lakini, je! walikuwa wakitenda kupatana na sala zao? Hata kidogo! Hata baadhi ya wazee ambao wamekuwa katika utumishi wa wakati vote kwa miongo ya miaka walikuwa miongoni mwa wale waliotiwa nidhamu katika njia moja au nyingine. Huzuni kubwa kama nini! Kweli kweli, “anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asije akaanguka,“ asije akatenda katika njia inayofanya sala zake zisikubalike na Muumba wake
Sababu kwa Nini Sala Zataka Kazi
5. Ili Yehova ajibu sala zetu, ni lazima tuthibitisheje unyofu wetu?
5 Ili sala zetu zisikiwe na Yehova Mungu, si kwamba tu lazima sisi tuwe safi kiadili na kiroho bali pia ni lazima sisi tuthibitishe unyofu wa sala zetu kwa kufanyia kazi yale tunayosali kwa ajili yayo. Sala peke yayo haiwezi kuwa badala ya jitihada ya unyofu, na yenye kuongozwa na akili. Yehova hatatufanyia sisi yale ambayo tunaweza kujifanyia wenyewe kwa kutumia kwa bidii shauri la Neno lake na kufuata mwongozo wa roho yake takatifu. Inatupasa sisi kuwa na nia ya kufanya yote tuwezayo katika habari hii ill yeye awe na msingi wa kujibu sala zetu. Hivyo, ‵haitupasi sisi kuomba zaidi ya yale tuliyo na nia ya kufanyia kazi,ʼ kama alivyosema mtu Fulani kwa kufaa.
6. Ni kwa sababu gani mbili inatupasa sisi kusali?
6 Hata hivyo, huenda swali likaulizwa: ‵Kwa nini tusali ikiwa tutalazimika kufanyia kazi yale tunayoyaomba?ʼ Inatupasa sisi tusali kwa angalau sababu mbili nzuri. Kwanza, kwa sala zetu tunakiri kwamba vita vyote vizuri hutoka kwa Mungu. Yeye ndiye Mpaji wa kila upaji mzuri na mkamilifu—nuru ya jua, mvua, nyakati za mavuno, na mengine mengi sana! (Mathayo 5:45; Matendo 14:16, 17; Yakobo 1:17, NW) Pili, iwe jitihada zetu zitafaulu au zitashindwa inategemea baraka ya Yehova. Kama tusomavyo kwenye Zaburi 127:1, NW: “Isipokuwa Yehova mwenyewe ajenga nyumba, ni kazi bure kwamba wajenzi wayo wamefanya kazi ngumu juu yayo. Isipokuwa Yehova mwenyewe alinda mji, ni kazi bure kwamba mlinzi amekaa macho.“ Kuonyesha jambo ilo hilo ni maneno haya ya mtume Paulo kwenye 1 Wakorintho 3:6, 7: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.“
Baadhi ya Mifano ya Kale
7, 8. (a) Ni tukio gani katika maisha ya Yakobo linaloonyesha kwamba yeye alithamini kwamba kazi ni lazima ziambatane na sala? (b) Mfalme Daudi alitoa mfano gani kuhusiana na jambo hili?
7 Maandiko yanaripoti visa vingi kuonyesha kwamba watumishi waaminifu wa Yehova walifanyia kazi yale waliyosali kwa ajili yayo. Acheni tuzungumzie mifano michache iliyo kiwakilisho. Kwa sababu mjukuu wa Abrahamu Yakobo alipata baraka ya uzaliwa wa kwanza, ndugu yake mkubwa Esau alimwonea chuki yenye kuua. (Mwanzo 27:41) Miaka 20 hivi baadaye, wakati Yakobo alipokuwa akirudi nchi ya uzaliwa wake kutoka Padanaramu akiwa na jamaa kubwa na kundi kubwa la mifugo, alisikia kwamba Esau alikuwa anakuja kumlaki. Akikumbuka uhasama wa Esau, Yakobo alisali kwa bidii kwa Yehova kwa ajili ya ulinzi kutokana na ghadhabu ya ndugu yake. Lakini je! yeye aliachia mambo hapo? Sivyo, kabisa. Yeye alipeleka zawadi kwa ukarimu mbele yake, akitoa sababu hivi: “Nitamsuluhisha kwa zawadi inayonitangulia.“ Na ndivyo ikawa, kwa kuwa wakati ndugu hao wawili walipokutana, Esau alimkumbatia Yakobo na kumbusu.—Mwanzo sura za 32, 33.
8 Daudi alitoa mfano mwingine wa kufanyia kazi yale tunayosali kwa ajili yayo. Wakati mwanaye Absalomu alipojitwalia kiti chake cha ufalme, mshauri wa Daudi Ahithofeli alijiunga na Absalomu. Kwa hiyo Daudi alitoa sala ya bidii ya kusihi ya kwamba shauri la Ahithofeli lingeweza kuzuiwa. Je! Daudi alisali tu iwe hivyo? Hapana, yeye alimwagiza mshauri wake mshikamanifu Hushai ajiunge na Absalomu iii aweze kuzuia shauri la Ahithofeli. Na hivyo ndivyo mambo yakawa. Absalomu alitenda juu ya shauri baya alilopewa na Hushai, akikataa shauri la Ahithofeli.—2 Samweli 15:31-37; 17:1-14; 18:6-8.
9. Nehemia alionyeshaje kwamba yeye alithamini kwamba sala zataka kazi?
9 Bado mfano mwingine ambao unaweza kutajwa kwa kutupa sisi shauri la upole ni ule wa Nehemia. Yeye alikuwa na mradi mkubwa wa kutimiza—kujenga upya kuta za Yelusalemu. Hata hivyo, maadui wengi walikuwa wakifanya shauri bovu pamoja dhidi yake. Nehemia alisali na kufnya kazi pia, sawa na vile tunasoma: “Tulimwomba dua mungu wetu, tena tukaweka walinzi mchana na usiku.” Tangu hapo na kuendelea nusu ya vijana wa Nehemia walikaa chonjo kulinda ile nusu nyingine, wale waliokuwa wakijenga ukuta.—Nehemia 4:9, 16.
Mfano wa Yesu
10, 11. Ni mifano gani ya Yesu inayoonyesha kwamba alitena kupatana na sala zake?
10 Yesu Kristo alituwekea sisi mfano mwema wa kufanyia kazi yale tunayosali kwa ajili yayo. Yeye alifundisha sisi kusali hivi: “Acha jina lako litakaswe.” (Mahayo 6:9)NW Lakini yesu pia alifanya yote awezayo ili wasikilizaji wake waweze kutakasa jina la baba yake, Vivyo hivyo, Yesu hakusali tu: “Baba ulitukuze jina lako.” (Yohana 12:28) Hapana, yeye alifanya yale angeweza kufanya ili kutukuza jina la baba yake na kuwafanya wengine wafanye ivyo hivyo.—Luka 5:23-26; 17:12-15; Yohana 17:4.
11 Akiona uhitaji mkubwa wa kiroho waliokuwa nao watu, Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno [Yehova Mungu], apeleke watenda kazi katika mavuno yake.” (Mathayo 9:37, 38) Je! Yesu aliachia mambo hapo? Sivyo hata kidogo! Mara baada ya hilo, yeye alituma wale mitume wake 12 wawili wawili katika safari ya kuhubiri, au ‘kuvuna,’ Baadaye, Yesu alituma wale waeneza evanjeli 70 wafanye kazi iyo hiyo.—Mathayo 10:1-10; Luka 10:1-9.
Kutumia Ile Kanuni
12. Kazi ina maana gani katika sala zetu kwamba Mungu atupe sisi riziki yetu ya kila siku?
12 Kwa wazi, Yehova Mungu anatutarajia sisi tutende kwa kupatana, tutende kupatana na sala zetu, hivyo kuthibitisha unyofu wetu. Yesu alituambia tusali hivi: “Utupe leo riziki yetu.“ (Mathayo 6:11) Kwa kufaa, basi, wafuasi wake wote wanamwomba Mungu jinsi iyo hiyo. Lakini je! sisi tunamtazamia Baba yetu wa kimbingu ajibu sala hiyo bila sisi kufanya lo lote juu yayo? Bila shaka sivyo. Ndiyo sababu sisi tunasoma hivi: “Nafsi ya mtu mvivu hutamani“—pengine hata kwa kusali—“asipate kitu.“ (Mithali 13:4) Mtume Paulo alionyesha jambo ilo hilo kwenye 2 Wathesalonike 3:10 akisema: “Ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.“ Kusali iii tupate riziki yetu ya kila siku lazima kuambatane na nia ya kufanya kazi. Kwa kupendeza, kwa hekima Paulo alisema kwamba wale ambao ‵hawataki kufanya kaziʼ haiwapasi kula chakula. Wengine wanaotaka kufanya kazi huenda wakawa bila kazi ya kuajiriwa, wakawa wagonjwa, au wakawa wazee wasiweze kufanya kazi. Wao wanataka kufanya kazi, lakini hilo linapita hali zao. Kwa sababu hiyo wao wanaweza kusali kwa kufaa kwa ajili ya riziki yao ya kila siku na kutumaini kuipokea.
13. Ili Yehova ajibu sala zetu za kuomba roho yake takatifu, ni lazima sisi tufanye nini?
13 Yesu pia alitushauri sisi tumwombe Baba yake wa kimbingu roho takatifu Yake. Kama vile Yesu alivyotuhakikishia, Mungu ana nia zaidi ya kutupatia sisi roho takatifu kuliko vile wazazi wa kidunia walivyo na nia ya kuwapa watoto wao vitu vizuri. (Luka 11:13) Lakini je! tungetazamia Yehova Mungu atupe roho yake takatifu kimuujiza, bila jitihada yo yote kwa upande wetu? Sivyo kabisa! Ni lazima tufanye yote tuwezayo tupokee roho takatifu. Kuongezea kusali kwa ajili yayo, tunahitaji kujilisha kwa juhudi Neno la Mungu. Kwa sababu gani? Kwa sababu Yehova Mungu hatoi roho yake ikiwa sisi tunapuuza ile njia ya kidunia anayotumia Yehova leo, “yule mtumwa mwaminifu mwenye akili,“ anayewakilishwa na Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Bila msaada kutoka kwa huyu “mtumwa“ hatuweza kufahamu maana kamili ya tunayosoma ama kujua jinsi ya kutumia yale tunayojifunza.—Mathayo 24:45-47
14, 15. (a) Ili Yehova ajibu sala zetu za kuomba hekima, ni lazima sisi tushirikianeje? (b) Hilo linaonyeshwaje na mfano wa Mfalme Sulemani?
14 Hii kanuni ya kwamba sala zinataka kazi pia inatumika katika maneno haya ya mwanafunzi Yakobo, ndugu-nusu wa Yesu: Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.“ (Yakobo 1:5; Mathayo. 13:55) Lakini je! Mungu anatupatia sisi hekima hii kwa muujiza fulani? Hasha. Kwanza kabisa, ni lazima sisi tuwe na mwelekeo unaofaa, kama tusomavyo: “Wenye upole atawafundisha njia yake.“ (Zaburi 25:9) Na Mungu anawafundishaje “wenye upole“? Kwa njia ya Neno lake. Tena, ni lazima sisi tutie jitihada kulifahamu na kulitumia, kama inavyoonyeshwa kwenye Mithali 2:1-6: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara, na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, . . . Ndipo utakapofahamu [woga wa Yehova, NW], na kupata kumjua Mungu. Kwa kuwa [Yehova, NW] huwapa watu hekima.“
15 Wakati Mfalme Sulemani aliposali apewe hekima na Mungu akajibu sala yake kimuujiza, je! ile kanuni ya kwamba sala zinataka kazi ilitumika pia? Ndiyo, ilitumika, kwa kuwa akiwa mfalme wa Israeli, Sulemani alitakwa kuandika nakala yake mwenyewe ya Sheria, aisome kila siku, na kuitumia katika maisha yake. Lakini wakati Sulemani alipoenda kinyume cha maagizo yayo, kama vile kwa kuongeza wake na farasi, kazi zake hazikupatana tena na sala zake. Kama matokeo, Sulemani akawa mwasi-imani na alikufa akiwa hivyo “mpumbavu.“—Zaburi 14:1; Kumbukumbu 17:16-20; 1 Wafalme 10:26; 11:3, 4, 11.
16. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba sala zetu juu ya kushinda udhaifu wa kimwili lazima ziambatane na kazi?
16 Ile kanuni kwamba kazi lazima ziambatane na sala pia inatumika wakati tunapomwomba Mungu msaada iii kushinda zoea fulani la kichoyo lililokwisha imarika sana ndani yetu. Hivyo dada mmoja painia alikubali kwamba alikuwa mzoevu wa vipindi vya televisheni vya mfululizo-hadithi siku baada ya siku, akivitazama kuanzia saa 5 asubuhi mpaka saa 9:30 alasiri kila siku. Alipojifunza kutokana na hotuba ya mkusanyiko mmoja jinsi programu hizo zenye kuonyesha mambo ya uasherati zilivyokuwa zenye kudhuru, yeye alimpelekea Mungu jambo hilo katika sala. Hata hivyo, ilimchukua muda fulani kushinda zoea hilo. Kwa sababu gani? Kwa sababu, kama alivyosema: ʼMimi ningesali nishinde zoea hilo na kisha ningetazama programu hizo hata hivyo. Kwa hiyo nikaamua kukaa katika utumishi wa shambani siku nzima ili nisiweze kuwa na kishawishi hicho. Hatimaye nilifikia hatua ya kwamba ningeweza kuzima televisheni asubuhi na kuiweka imezimwa siku nzima.’ Ndiyo kuongezea kusali ili kuushida udhaifu wake, ilimapasa yeye afanye kazi ili aushinde.
Sala na Kutoa Ushuhuda Kwetu
17-19. (a) Ni mambo gani hakika yanayoonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakitenda kupatana na sala zao? (b) Ni mfano gani wa mtu mmoja unaoonyesha jambo ilo hilo?
17 Hakuna sehemu ambayo katika hiyo ile kanuni ya kwamba sala zataka kazi inakuwa ya kweli zaidi ya kazi ya kuhubiri Ufalme. Hivyo, Mashahidi wa Yehova wote si kwamba tu wanasali kwa ajili ya ongezeko katika wavunaji bali pia wanajitumikisha wenyewe katika kazi hiyo. Kama matokeo, wameona maongezeko yenye kustaajabisha katika nchi moja baada ya nyingine. Kutoa mfano mmoja tu: Katika 1930 kulikuwako shahidi mmoja tu wa Yehova akihubiri katika Chile. Leo, Shahidi huyo mmoja amekuwa si elfu moja tu bali wapatao 30,000. (Isaya 60:22) Je! haya yalikuwa matokeo tu ya sala? Hapana, kazi ilihusika pia. Kwani, katika 1986 pekee, Mashahidi wa Yehova katika Chile walitumia zaidi ya saa 6,492,000 kwenye kazi ya kuhubiri!
18 Ndivyo inavyokuwa wakati kazi ya kuhubiri inapopigwa marufuku. Si kwamba tu Mashahidi wanasali kwa ajili ya ongezeko bali pia wanaendelea kuhubiri kisirisiri. Basi, ijapokuwa upinzani wa wakuu wa serikali, maongezeko yanatukia katika nchi hizi. Hivyo, katika nchi 33 ambako Mashahidi wa Yehova wanaelekeana na upinzani kama huo wa wakuu wa serikali, katika mwaka wa utumishi wa 1986 walitumia zaidi ya saa 32,600,000 kwenye kazi yao ya kuhubiri na walifurahia ongezeko la asilimia 4.6!
19 Bila shaka, ile kanuni ya kwamba sala zataka kazi pia inatumika kwa watu mmoja mmoja. Huenda sisi tukasali kwa Yehova tupate funzo la Biblia la nyumbani lakini huenda tusiwe tukifanya yote tuwezayo ili kupata moja. Hilo ndilo lililokuwa ono la painia mmoja. Akiwa na funzo la Biblia moja tu, mwanamke huyo alisali awe na zaidi. Je! yeye aliachia mambo hapo? Hapana, lakini yeye aliweka maandishi ya huduma yake kwa uangalifu naye alipata kuona kwamba kwenye ziara zake za kurudia yeye hakuwa akizungumza juu ya kuwa na funzo la Biblia la nyumbani. Akiendelea katika upande huu, upesi yeye akawa na mafunzo ya Biblia mawili zaidi.
19 Of course, the principle that prayers require works also applies individually. We may pray to Jehovah to get a home Bible study but may not be doing all we can to obtain one. That was the experience of one pioneer. Having only one Bible study, she prayed to have more. Did she let matters go at that? No, but she carefully took note of her ministry and found that on her return visits she was not bringing up the subject of having a home Bible study. Proceeding along this line, she soon had two more Bible studies.
20. Ile kanuni ya kwamba sala zataka kazi inaweza kuelezwaje kwa muhtasari??
20 Mifano mingine mingi ingeweza kutolewa kuthibitisha kwamba sala zataka kazi. Kwa mfano, kuna ile inayohusiana na mahusiano ya kibinafsi katika jamaa au kundini. Lakini ile mifano iliyokwisha tajwa yapasa kutosha kuonyesha wazi kabisa kwamba sala zataka kazi. Hilo ni jambo linalopatana sana na kufikiri kuzuri, kwa kuwa hatuwezi kumtazamia Yehova Mungu afikirie maombi yetu kwa kibali ikiwa sisi tunamuudhi kwa mwenendo wetu wenyewe. Kwa sababu hiyo ni lazima pia sisi tufanye yote tuwezayo kupatana na sala zetu ikiwa tutamtazamia Yehova atufanyie yale ambayo sisi hatuwezi kufanya wenyewe. Kweli kweli, kanuni za Yehova ni za hekima na haki. Zinapatana na akili, na ni kwa manufaa yetu wenyewe kwamba tunatenda kupatana nazo.
Je! Wewe Unakumbuka
◻ Ni takwa gani kuhusiana na sala ambalo wengi katika Israeli wa kale walipuuza?
◻ Kwa sababu gani Mungu hatendi kwa njia yenye kupita kiasi kwa kutaka kwamba tufanye kazi na vilevile tusali kwa ajili ya tunayotamani
◻ Ni mifano gani ya kale inayoonyesha kwamba watumishi wa Yehova walifanyia kazi yale waliyosali kwa ajili yayo?
◻ Ili Mungu ajibu sala zetu za kuomba roho yake takatifu na hekima, ni lazima sisi tuwe tukifanya nini?
◻ Ile kanuni ya kwamba sala zataka kazi inatumikaje katika huduma yetu ya shambani?
[Picha katika ukurasa wa 17]
Yesu aliwahimiza wanafunzi wake kusali kwa ajili ya wavunaji zaidi. Lakini yeye pia aliwatuma nje kwenye kazi ya kuhubiri, au ‘kuvuna’
[Picha katika ukurasa wa 18]
Je! wewe unasali kwa ajili ya msaada wa kuongoza vizuri utazamaji wako wa televisheni? Basi tumia ile kanuni ya kwamba sala zataka kazi kwa kuizima televisheni yako.