Maisha na Huduma ya Yesu
Matayarisho ya Kukabiliana na Mateso
BAADA YA kuwaagiza mitume wake katika njia za kuendesha kazi ya kuhubiri, Yesu anawaonya juu ya wapinzani. Yeye anasema: “Tazameni! mimi natuma ninyi kama kondoo kati ya mbwa-mwitu . . . Jilindeni ninyi dhidi ya watu; kwa kuwa watawatoa ninyi kwenye mahakama za mahali, na wao watawapiga ninyi mijeledi katika masinagogi yao. Kwani, ninyi mtaitwa mbele ya magavana na wafalme kwa ajili yangu.”
Yajapokuwa mateso makali watakayokabili wafuasi wake, Yesu anawatia moyo kwa kuwaahidi hivi: “Wakati wanapowatoa ninyi, msiwe wenye wasiwasi juu ya jinsi au yale ambayo ninyi mtasema; kwa kuwa yale ambayo ninyi mtasema yatapewa kwenu ninyi katika saa hiyo; kwa kuwa wale wanaosema si ninyi tu, bali ni ile roho ya Baba ambayo inasema kupitia ninyi.”
“Zaidi,” Yesu aendelea, “ndugu atamtoa ndugu kwenye kifo, na baba mtoto wake, na watoto watainuka dhidi ya wazazi na watawafanya wauawe.” Anaongezea hivi: “Ninyi mtakuwa vitu vya kuchukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu; lakini yeye ambaye amevumilia mpaka mwisho ndiye ambaye ataokolewa.”
Kuhubiri ndilo jambo lenye maana ya kwanza, hivyo Yesu anakazia uhitaji wa kutumia akili ili wawe huru kuendeleza kazi hiyo. “Wakati wao wanatesa ninyi katika mji mmoja, kimbilieni mwingine,” akasema yeye, “kwa kuwa kweli mimi nasema kwenu ninyi, Ninyi hamtamaliza kamwe mzunguko wa miji ya Israeli mpaka Mwana wa mtu awasili.”
Ni kweli kwamba Yesu alitoa agizo hili, onyo, na kitia-moyo kwa mitume wake 12, lakini hayo pia yalikusudiwa kwa ajili ya wale ambao wangeshiriki katika kuhubiri ulimwenguni pote baada ya kifo na ufufuo wake. Hilo linaonyeshwa na uhakika wa kwamba yeye alisema wanafunzi wake ‘wangechukiwa na watu wote,’ si na Waisraeli pekee ambao kwao mitume walitumwa kuhubiri. Zaidi ya hilo, kwa wazi mitume hawakuitwa mbele ya magavana na wafalme wakati Yesu alipowatuma nje katika kampeni yao ya muda mfupi ya kuhubiri. Isitoshe, wakati huo waamini hawakutolewa kwenye kifo na washiriki wa jamaa zao.
Hivyo alipokuwa akisema kwamba wanafunzi wake hawangemaliza mzunguko wa kuhubiri kwao, “mpaka Mwana wa mtu awasili,” Yesu alikuwa akituambia sisi kwa njia ya kiunabii kwamba wanafunzi wake hawangemaliza mzunguko wa dunia yote inayokaliwa na watu kwa kuhubiri juu ya Ufalme wa Mungu uliosimamishwa kabla ya mfalme Yesu Kristo aliyetukuzwa kuwasili akiwa afisa mfishaji wa Yehova kwenye Har–Magedoni.
Akiendelea kutoa maagizo yake ya kuhubiri, Yesu anasema: “Mwanafunzi hawi juu ya mwalimu wake, wala mtumwa juu ya bwana yake.” Hivyo wafuasi wa Yesu lazima watazamie kutendewa vibaya na mateso kama yale yale yeye alipata kwa kuhubiri Ufalme wa Mungu. Hata hivyo yeye anaonya kwa upole hivi: “Msiwe wenye kuogopa wale ambao huua mwili lakini hawawezi kuua nafsi; afadhali mwe wenye kuogopa yeye ambaye anaweza kuharibu nafsi na mwili pia katika Gehenna.”
Yesu aliweka mfano katika jambo hili. Bila woga yeye alivumilia kifo badala ya kukana ushikamanifu wake kwa Yeye aliye na uwezo wote, Yehova Mungu. Ndiyo, ni Yehova ambaye anaweza si kuharibu tu “nafsi” (kumaanisha katika habari hii mataraja ya wakati ujao ya mmoja akiwa nafsi inayoishi) ya mtu bali anaweza hata kufufua mtu afurahie uzima wa milele Lo! Yehova ni Baba wa kimbingu mwenye upendo, na huruma kama nini!
Halafu Yesu anawatia moyo wanafunzi wake kwa mfano ambao unakazia utunzaji wenye upendo wa Yehova kwa ajili yao. “Je! si mashore wawili huuzwa kwa sarafu moja yenye thamani ndogo?” yeye auliza. “Hata hivyo hata mmoja wao hataanguka chini bila ya Baba yenu kujua. Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote. Kwa hiyo msiwe na woga: ninyi ni wenye thamani zaidi kuliko mashore wengi.”
Ujumbe wa Ufalme ambao Yesu anawatuma wanafunzi wake kutangaza utawagawanya washiriki wa jamaa, kwa kuwa washiriki fulani wa jamaa wanaukubali na wengine wanaukataa. “Msifikiri mimi nilikuja kuweka amani juu ya dunia,” yeye akaeleza, “mimi nilikuja kuweka, si amani, bali upanga.” Hivyo, ili mshiriki wa jamaa aukubali ukweli wa Biblia uhodari unahitajiwa. “Yeye ambaye ana shauku kubwa zaidi kwa ajili ya baba au mama kuliko kwa ajili yangu mimi hanistahili mimi,” Yesu akasema, “na yeye ambaye ana shauku kubwa zaidi kwa ajili ya mwana au binti kuliko kwa ajili yangu mimi hanistahili mimi.”
Akimalizia maagizo yake, Yesu anaeleza kwamba wale wanaopokea wanafunzi wake wanampokea yeye pia. “Na ye yote ambaye anampa mmoja wa hawa walio wadogo kikombe kimoja tu cha maji baridi anywe kwa sababu yeye ni mwanafunzi, mimi nawaambia ninyi kweli kweli, yeye hatapoteza kamwe thawabu yake.” Mathayo 10:16-42, NW.
◆ Yesu aliwapa wanafunzi wake maonyo gani?
◆ Ni kitia-moyo na faraja gani aliyowapa?
◆ Ni kwa sababu gani maagizo ya Yesu yanatumika pia kwa Wakristo wa kisasa?
◆ Ni kwa njia gani mwamafunzi wa Yesu hawi juu ya mwalimu wake?