Kujihadhari Dhidi ya “Amani na Usalama” Kama Linavyotungwa na Mataifa
“Wakati wo wote wanaposema: “Amani na usalama!”—1 WATHESALONIKE 5:3, NW.
1, 2. (a) Kwa sababu gani kutafuta amani kumekuwa ndilo jambo la hekima zaidi? (b) Hivyo, mifumo ya kisiasa yenye kupingana itakubaliana juu ya nini?
HAKUJAPATA kamwe kuwa na wakati ambao ulimwengu mzima wa wanadamu umekosa usalama kama ulivyo leo. Kuna hisia ya hofu kuu juu ya vita ya ulimwengu ya tatu yenye kuhusu mataifa yaliyoendelea sana kijeshi ambayo yana ile ambayo sasa inaonekana kuwa ndiyo silaha mkataa kwa silaha zote —kombora la nyukilia. Uwezo wa mataifa kutendesha kazi nyukilia yenyewe ya atomi kwa kufuatia vita ni kama umewafikisha kwenye umbali wote wanaoweza kufikia katika kuua wanadamu kwa wingi sana. Kwa sababu hiyo, jambo lililo la hekima zaidi limekuwa kufanya amani.
2 Ndiyo, kweli kweli, kwa maana katika muhula wetu vita ya ulimwengu ya tatu yenye kutumia silaha kama hizo ingemaanisha tu kujiua kwa ulimwengu wote, huku wakiwako watu waliolipuliwa wakawa ni kama hawakubakia kitu au wenye kuangamia kutokana na matokeo ya maangamizi ya kinyukilia. Wana-siasa na maamiri wa kijeshi wenye kuona mbali wanahisi jambo hilo kwa njia iliyo wazi sana. Wao hawataki wawe na daraka la kulaumiwa kwa afa hilo la duniani pote. Hivyo, mifumo ya kisiasa yenye kupingana kweli kweli itaona inafaa kufikia patano fulani, ndiyo, kuifuata falsafa ile yenye hekima ya kilimwengu ya kusema “shika lako, nami nishike langu.”
3. Ni kwa sababu gani mataifa yatatangaza “Amani na usalama”?
3 Hata hivyo, mataifa hayatumainiani kwa ukamili. Kwa tahadhari ya kujilinda, wanadumisha majeshi yao yakiwa na zana zenye nguvu kabisa. Kwa sababu hiyo, je! ni kwa sababu ya upendo wa moyo mweupe, ulio wa kweli kwa mtu na mwenzake wakiwa washiriki wa jamii ile ile moja ya kibinadamu kwamba watawala wataungana katika kufanya tangazo lile la “Amani na usalama” kwa ajili ya ulimwengu wote wa wanadamu? Hapana, bali itakuwa ili kutuliza-tuliza hofu zile ambazo kwa haki zimewapata watu.—1 Wathesalonike 5:3, NW.
Viongozi wa Kidini na Itikio la Halaiki ya Watu kwa Tangazo Linalokuja
4, 5. (a) Ni itikio gani la halaiki ya watu kwa tangazo linalokuja huenda tukatazamia? (b) Ijapokuwa viongozi wa kidini wataunga mkono tangazo linalokuja, ni maswali gani yanayotokea juu ya kama Mungu ataliunga mkono?
4 Wakati mwishowe tangazo hilo litakapofanywa, itikio la halaiki ya watu linapasa kuwa zuri kuzunguka dunia yote. Bila shaka viongozi wa kidini wa ulimwengu, kutia na viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo, Wakatoliki na Waprotestanti, watashangilia hatua hiyo ya kimataifa. Vyo vyote upepo uvumavyo, ndivyo viongozi wa kidini wanavyoenda ili wabaki wakipendelewa na wingi wa watu na kupata usaidizi na mafikirio ya kufadhiliwa kisiasa.
5 Hata hivyo, kuungwa mkono kwa mpango huo wa kisiasa wenye kutangazwa kwa sauti kubwa na viongozi wa kidini hakumaanishi kwamba Mungu wa ulimwengu wote mzima, kutia na dunia yetu, atauunga mkono. Wakiwa katika majengo yao ya kidini, huenda viongozi wa kidini wakatoa sala ndefu zenye kusemwa kwa sauti kubwa kwa kusikiwa na wateja wao wa kidini na kuomba baraka ya kimungu juu ya hatua zilizochukuliwa na chombo kile cha kisiasa kilichopo kwa ajili ya amani na usalama wa kimataifa. Lakini je! sala zote hizo za uzito, ambazo makundi yenye kusikiliza wanazimalizia kwa kutoa “Amina” yenye nguvu, zinakubalika kwa yule Mungu wa ulimwengu wote mzima? Je! yeye anaweza kuwa na amani pamoja na ulimwengu uliogawanyika kidini, ambao sala zao za kuomba amani na usalama zimefanyizwa kulingana na kiolezo cha migawanyo na madhehebu za kidini zisizokubaliana?
6, 7. (a) Kama Wayahudi wa nyakati za kale, ni mwendo gani wa tendo ambao Jumuiya ya Wakristo imechukua? (b) Ni nini litakalotokea kwa sababu ya viongozi wa kidini kuunga mkono tangazo la “Amani na Usalama”?
6 Hapana mahali pengine ambapo madai ya kwamba Mungu anaunga mkono yanasikika kwa sauti kubwa kuliko katika mataifa ya Jumuiya ya Wakristo. Lakini yule Mungu wa ulimwengu wote mzima siye anayetawala juu ya Jumuiya ya Wakristo. Jumuiya hiyo imefuata mwendo unaofanana na ule wa Waisraeli wa kale. Wakati wao walipoacha kuridhika na mpango wa Yehova kwa serikali yao na wakaanza kufikiri kwamba muundo wa kisiasa wa mataifa ya kipagani yaliyowazunguka ulifaa zaidi, walimwendea Samweli nabii wa Yehova wakamwomba awawekee mfalme juu yao. Samweli alichukizwa sana na kuhuzunikia sana jambo hilo. Sembuse Mungu ambaye yeye alikuwa nabii wake.
7 Yehova kwa kufaa alihisi ameudhika kwa sababu ya ombi hilo la kuondoka kwenye muundo wake wa kitheokrasi juu ya Israeli. Kama vile alivyomwambia Samweli nabii wake: “Hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.” (1 Samweli 8:4-9) Huo ulitangulia kuwa mfano wa mwendo ambao Jumuiya ya Wakristo imechukua katika karne hii ya 20. Kwa hiyo mshangilio wa viongozi wa kidini wakati ujao juu ya tangazo la “Amani na usalama” halitakuwa na tokeo zuri, halitakuwa na baraka ya kimungu.
Kufanya Wanadamu Waache Kujihadhari
8. Inaelekea ni jukumu gani ambalo Umoja wa Mataifa utakuwa nalo katika tangazo linalokuja, na kwa sababu gani tengenezo hili linafanya wanadamu waache kujihadhari?
8 Huenda Umoja wa Mataifa ukajisifia kuwa na washiriki 159 leo, kutia ndani karibu mataifa yote. Bila shaka katika wakati wake Umoja wa Mataifa utakuwa mbele kabisa kwa habari ya kutoa tangazo linalokuja la “Amani na usalama!” Jambo la kusikitisha ni kwamba, tengenezo hilo la ulimwengu wote linafanya mabilioni ya wanadamu waache kujihadhari. Kwa sababu gani? Kwa sababu amani hiyo, hata ingawa itaungwa mkono na matengenezo yote ya kidini ya ulimwengu huu, kutia na yale ya Jumuiya ya Wakristo, haimaanishi amani pamoja na Muumba wa ulimwengu wote mzima, ambaye ana uwezo wa kupa uhai na kuuchukua kulingana na uamuzi wake wa mambo muhimu katika mbingu na duniani.
9, 10. Msimamo wa Mashahidi wa Yehova ni nini kwa habari ya “Amani na usalama” kama linavyotungwa na mataifa, na kwa sababu gani?
9 Katika unabii wa Isaya, Muumba anasema hivi waziwazi kabisa: “Mbingu ni kiti cha enzi changu, na dunia ni kibago cha miguu yangu.” (Isaya 66:1, NW) Mataifa yaliyo chini hapa juu ya kibago cha miguu yake hayakipambi kwa tengenezo lao la Umoja wa Mataifa. Yanajitahidi kisiasa kudumisha amani na usalama wa duniani pote na kwa njia hiyo kuufanya Umoja wa Mataifa uendelee kuwapo. Mashahidi wa Yehova walio wakfu duniani hawawezi kujiunga na ulimwengu katika kutegemea hatua za kibinadamu zinazochukuliwa ili kuleta amani na usalama wa mataifa ya kilimwengu. Wao wanayathamini kwa moyo maneno ya Yakobo 4:4, NW: “Wazinzi wa kike, je! hamjui kwamba urafiki na ulimwengu ni uadui na Mungu? Ye yote, basi, anayetaka kuwa rafiki ya ulimwengu anajifanya mwenyewe kuwa adui ya Mungu.”
10 Ingawa wao hawafanyi utendaji wa kupinga amani na usalama itakayotungwa na mataifa, Mashahidi wa Yehova hawawezi kuipendekeza kwa mamilioni ya watu wanaotafuta mahali pa mponyoko wakati taabu ya ulimwengu iliyo kubwa kupita zote itakapofoka na kukomesha mfumo huu wa mambo. (Mathayo 24:21) Kwa maana mfumo mpya wa mambo ya Mungu ndio utakaoleta usalama wa ulimwenguni pote chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani,” Yesu Kristo.—Isaya 9:6, 7, NW.
11. Viongozi wa kidini waliuonaje mnuio wa kuunda Ushirika wa Mataifa baada ya Vita ya Ulimwengu ya Kwanza?
11 Historia inatoa ushuhuda wa kushindwa kwa njama za kibinadamu kuleta amani. Tunakumbuka kwamba mwishoni mwa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza katika 1918, Ushirika wa Mataifa ulinuiwa kuwa kizuio cha vita ya ulimwengu. Baraza la Muungano wa Makanisa ya Kristo Katika Amerika liliushangilia mnuio huo na kusema: “Ushirika huo si manufaa ya kisiasa tu; badala ya hivyo huo ni wonyesho wa kisiasa wa Ufalme wa Mungu duniani.” Lakini je! huo wenye kuitwa ati wonyesho wa kisiasa wa ufalme wa kidunia wa Mungu uliiletea dunia amani na usalama wa kudumu?
12. (a) Ufunuo 17:8 umetimizwaje? (b) Ni nani anayeendelea kupanda juu ya mgongo wa “mnyama-mwitu wa rangi nyekundu kama damu,” na kwa muda gani?
12 Kama yule “mnyama-mwitu wa rangi nyekundu kama damu” aliye wa mfano, wa Ufunuo sura ya 17 (NW), ambaye yule kahaba wa kale, ‘Babuloni Mkuu,’ amejiketisha juu yake, ndivyo Ushirika wa Mataifa ulivyoingia katika “lile shimo refu sana” ilipotokea Vita ya Ulimwengu ya Pili katika 1939. Hiyo ilimpa mpandaji wake kahaba wajibu wa kuruka chini. Baada ya kumalizika kwa Vita ya Ulimwengu ya Pili katika 1945, Umoja wa Mataifa uliundwa uwe mfuataji wa Ushirika wa Mataifa uliopatwa na msiba. Huo una washiriki wanaozidi kwa mbali wale waliokuwa wa Ushirika, kwa hiyo unapasa kuwa tengenezo lenye nguvu zaidi linalostahili kutumainiwa kwa uhakika zaidi na ulimwengu wa wanadamu. Hivyo ikawa kwamba katika 1945 yule “mnyama-mwitu wa rangi nyekundu kama damu” aliye wa mfano alipanda juu “kutoka ndani ya lile shimo refu sana,” na yule kahaba wa mfano, ‘Babuloni Mkuu,’ tena akapanda juu ya mgongo wake, ambapo yeye bila kuona aibu ameketi mpaka leo hii. (Ufunuo 17:3, 5, 8, NW) Lakini sasa hataketi kwa muda mrefu, kulingana na unavyotabiri Ufunuo 17:16–18:24. Kwa sababu gani sivyo?
13. (a) Umoja wa Mataifa ni nini? (b) Ulitanguliaje kuwekewa kivuli cha kuufananisha zamani za kale?
13 Kwa kweli Umoja wa Mataifa ni muungano wa kilimwengu ulio dhidi ya Yehova Mungu na Mashahidi wake walio wakfu duniani. Umoja huo ni mpango wa hila, huku mataifa ya kilimwengu wakifanya shauri pamoja na kutafuta njama watakayotenda dhidi ya tengenezo lionekanalo la Yehova Mungu duniani. Wakati wa huu “umalizio wa mfumo wa mambo,” jambo hilo lilifananishwa na mpango wa hila unaotajwa kwenye Isaya 8:12.—Mathayo 24:3, NW.
Mtegemee Yehova kwa Amani na Usalama
14. Kwa sababu gani ufalme wa Israeli wa makabila kumi uliingia katika muungano pamoja na Shamu, na ni swali gani lililoukabili ufalme wa Yuda?
14 Kabla ya wakati wa Isaya taifa la Israeli la makabila 12 lilikuwa limegawanyika kwa sababu ya suala la umaliki. Hiyo ilikuwa baada ya utawala mtukufu wa Mfalme Sulemani. Makabila kumi yaliyojiondoa yawe upande wa kaskazini yalisimamisha ule uliokuja kuitwa ufalme wa Israeli, ukiwa na mji mkuu Samaria. Makabila mawili yaliyobaki, makabila ya Yuda na Benyamini, yalibaki yakiwa mashikamanifu kwa nasaba ya kifalme ya Mfalme Daudi kwenye mji mkuu wa Yerusalemu. Ufalme wa Israeli wa makabila kumi uligeuka kwa uadui dhidi ya ufalme wa Yuda wa makabila mawili. Baadaye, ufalme wa Israeli ukafanya ushirika pamoja na ufalme wa Shamu, uliokuwa na mji wao mkuu Dameski. Wazo lilikuwa kuupindua ufalme wa Yuda na kuutiisha. Je! basi ufalme wa Yuda uingie katika muungano pamoja na taifa jingine lenye nguvu ili kuliweza shambulio kali la taifa la Israeli lenye kuungana na taifa la kipagani la Shamu?—Isaya 7:3-6.
15. (a) Watu fulani katika ufalme wa Yuda walipendelea nini, na mwelekeo huo ulionyesha nini? (b) Nabii Isaya alinenaje dhidi ya mwelekeo huo?
15 Walikuwako watu fulani katika ufalme mdogo wa Yuda waliopoteza imani katika Yehova Mungu wa kitaifa. Wao walipendelea kufanya muungano, au mpango wa hila, pamoja na ufalme fulani hodari wa kipagani wa ulimwengu huu. Kwa kutetea jambo hilo la kutaka ufalme wa Yehova wa Yuda ujitie katika nira isiyo ya uaminifu pamoja na ufalme fulani wa ulimwengu wenye kukana Mungu, wengine walikuwa wakisema, “Ni mpango wa hila!” kwa kuwaambia waliobaki bila kuamua katika ufalme wa Yuda. Hivyo walionyesha hawakuwa na imani na tumaini hakika katika Mungu ambaye hekalu lake lilikuwa katika Yerusalemu. Nabii Isaya aliongozwa na roho ya Mungu aseme dhidi ya mpango huo wa hila, akisema hivi katika sura ya 8, mstari wa 12, NW: “Ninyi watu msiseme kamwe, ‘Ni mpango wa hila!’ kwa habari ya mambo yote yale ambayo watu hawa wanaendelea kusema, ‘Ni mpango wa hila!’ na shabaha ya hofu yao ninyi watu msiihofu kamwe, wala msiitetemee kamwe.”
16, 17. Ni nini kilicholetea watu wa kale wa Yehova amani na usalama wa kweli, na jambo hilo lilionyeshwaje wakati Senakeribu Mfalme Mwashuri alipotisha Yerusalemu?
16 Watu waliokuwa katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova walipata amani na usalama kwa sababu ya Yehova kuwa pamoja nao. Jambo hilo lilionyeshwa wakati mtawala yule Mwashuri Senakeribu alipotuma halmashauri ya maafisa watatu wa cheo cha juu ikamwombe Mfalme Hezekia na watu wa Yerusalemu kuisalimu amri yake kwa ushinde. Mkuu na mnenaji Mwashuri, Rabshake, alisimama mbele ya kuta za Yerusalemu na kwa majivuno makuu akamtolea madharau Yehova Mungu ili kudhoofisha au kuharibu tumaini hakika ambalo Wayahudi walikuwa nalo katika Yeye. Mfalme Hezekia alienda hekaluni akaliweka jambo hilo mbele za Yehova Mungu akiwa ametiwa kihoro kingi na tendo hilo la kumshushia heshima Mungu yule mmoja aliye hai na wa kweli Yehova, na akiwa anaihisi kwa kufaa hatari ya Yerusalemu mbele ya umaya-maya huo wa Waashuri. Yehova alitoa jibu linalofaa kwa kufurahia wonyesho huo wa imani adhimu katika yeye na jinsi alivyokimbiliwa ili aionyeshe enzi kuu yake ya ulimwengu wote mzima. Isaya nabii wake alijiunga kusema maneno ya uthibitisho. Rabshake Mwashuri mwenye kutisha hakupewa jibu lo lote, sawasawa na vile Mfalme Hezekia alivyokuwa ameagiza.—2 Wafalme 18:17-36; 19:14-34.
17 Bila shaka kwa kustaajabishwa sana na jambo hilo, Rabshake aliirudia kambi ya Senakeribu, ambaye wakati huo alikuwa akipigana dhidi ya Libna. (2 Wafalme 19:8) Baada ya kusikia ripoti ya Rabshake, Senakeribu alipelekea Hezekia barua za kutisha, akionya hivi: “Asikudanganye Mungu wako unayemtumaini, akisema, Yerusalemu hautatiwa katika mikono ya mfalme wa Ashuru.” (2 Wafalme 19:9, 10) Baada ya usiku kuingia, Yehova Mungu alimjibiza kwa njia yake mwenyewe Rabshake, mnenaji huyo wa Ashuru, na Yeye mwenyewe akazijibu barua zenye kutisha za Senakeribu kuthibitisha kwamba Yeye alikuwa mkuu kuliko mungu wa Waashuri mwenye kufanya nchi nyingine ziwe koloni zake. Kikomo cha usimulizi wa mfululizo wa vituko hivyo, kama unavyotolewa kwenye 2 Wafalme 19:35, kinasema: “Ikawa usiku uo huo malaika wa Bwana [Yehova, NW] alitoka, akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! hao walikuwa maiti wote pia.” Wakati Waashuri waliobaki, kutia na Mfalme Senakeribu na labda Rabshake, walipoamka wakati wa mapambazuko, waliona tamasha ile ya kuogofya sana huku na huku ya majeruhi wa vita waliouawa na Yehova Mungu.
18. (a) Tokeo lilikuwa nini kwa habari ya Senakeribu mwenye kutaka makuu? (b) Usimulizi huo wa kihistoria unapasa kuwatolea mfano gani Mashahidi wa Yehova wa leo?
18 Kwa kushindwa katika mbinu zake za kutaka makuu dhidi ya tengenezo la Yehova na kufedheheshwa kweli kweli, Senakeribu alifanya haraka kurudi “mwenye haya ya uso” kwenye mji mkuu wake wa kitaifa, Ninawi, akaenda tu kuuawa na wawili wa wanaye. (2 Nyakati 32:21; 2 Wafalme 19:36, 37) Milki ya Ashuru haikutisha tena tengenezo lionekanalo la Yehova. Hilo lilikuwa tendo la hali ya juu kweli kweli, la kuondoa malawama juu ya enzi kuu ya ulimwengu wote mzima ya Mungu Aliye Juu Zaidi. Zaidi ya hilo, kulindwa kwa Yerusalemu ni mfano mzuri kabisa unaoonyesha ni nani ambaye Mashahidi wa Yehova leo wanapaswa kumtegemea kwa uhakika kamili wa kupata amani na usalama wenye kuendelea na usioweza kuvurugwa—si mpango wa hila ya kisiasa bali Yehova Mungu.
Kuendelea Kujihadhari
19. Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi itaendelea kufanya nini?
19 Ili kukusaidia wewe uendelee kujihadhari, Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi itaendelea kutoa katika vichapo vyayo maonyo ya wakati wayo kwa watu wote wanaosoma, ili wewe usije ukapatikana bila kujihadhari na tangazo la kusingizia linalokuja la “Amani na usalama,” kama linavyotungwa na mataifa ya mfumo huu wa mambo wa kale.
20. Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova hawatashiriki kwa vyo vyote kusaidia watu wategemee “Amani na usalama” unaokuja, na kwa hiyo sasa ni wakati wa nini?
20 Mashahidi wa Yehova walio wakfu hawawezi kwa vyo vyote kushiriki kusaidia watu waitegeimee “Amani na usalama” utakaotangazwa na mataifa ya kilimwengu yakiwa na uhakika: wala hawawezi kuwapongeza wenye kutunga “Amani na usalama” huo wa kimataifa na, wakati uleule, Yehova Mungu awe pamoja nao. Wao wanajihadhari dhidi ya kuungana pamoja na mataifa ya mfumo huu wa mambo wa kale. Wanajikumbusha daima kwamba “taifa” jipya, lililo kando na lililo tofauti sana na Ushirika wa Mataifa, lilizaliwa katika mwaka ule wa 1919 baada ya vita. “Taifa” jipya hilo linaendelea kukua na kupanuka katika dunia yote, sawasawa na.ilivyotabiriwa kwenye Isaya 60:22: “Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa hodari.; Mimi, BWANA [Yehova, NW], nitayahimiza hayo wakati wake.” Ndiyo, sasa ndio wakati wa watu wote kujihadhari dhidi ya “Amani na usalama” unaokuja kama linavyotungwa na mataifa.
Wewe Ungejibuje?
◻ Inaelekea ni nini litakalokuwa itikio la halaiki ya watu kwa tangazo la “Amani na usalama”?
◻ Ni nini kilichotangulia kuwa kivuli chenye kufananishwa na “mpango wa hila” wa Isaya 8:12, NW?
◻ Ni jinsi gani UM unafanya wanadamu waache kujihadhari?
◻ Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova hawatapatikana bila kujihadhari?
[Picha katika ukurasa wa 18]
Bila shaka UM utakuwa mbele kabisa katika tangazo linalokuja la “Amani na usalama!”
[Picha katika ukurasa wa 21]
Rabshake mkuu Mwashuri alimtolea madharau Mungu wa Israeli, lakini tokeo lilionyesha kwamba amani na usalama wa kweli unakuja kutokana na