Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 9/15 kur. 3-4
  • Utafutaji wa Rafiki za Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utafutaji wa Rafiki za Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Si “Rafiki” Wote Walio Rafiki za Kweli
  • Kuwa Mchaguzi
  • Chagua Marafiki Wako kwa Hekima
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Wataka Rafiki za Namna Gani?
    Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Tunawezaje Kuchagua Marafiki Wazuri?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Marafiki Wazuri na Wabaya
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 9/15 kur. 3-4

Utafutaji wa Rafiki za Kweli

KIJANA mmoja mwanamume aliumia vibaya katika aksidenti ya pikipiki. Kwa majuma mengi alilala katika hali ya kutokuwa na fahamu ndipo akaanza kupata nafuu polepole. “Kama ningekuwa na rafiki wengi wazuri kama nilivyo na wazoeani wengi ningepata nafuu ya haraka zaidi,” yeye akasema. ‘Wengi wa rafiki niliokuwa nao kabla ya aksidenti hii wameniacha. Lakini rafiki wazuri wanaweza kusaidia sana mtu apone.’

Hali hiyo ni ya kawaida sana katika ulimwengu wa leo usio na urafiki. Wale wanaoitwa ati rafiki wanaweza kuwa wengi wakati mambo yote yanapokuwa sawa. Lakini wakati tukio baya linapopata mtu, wao wanatoweka. Kwa kawaida ni vigumu kupata rafiki za kweli.

Hata hivyo, kuwa na rafiki mmoja au wawili wa kweli, wachangamfu, kunafanyiza tofauti kubwa sana maishani. Wastadi wanaochunguza habari hii wanasema: “Tamaa nyingi ya kutaka mahusiano ya kibinafsi yaliyo karibu zaidi ni kichwa kikubwa [cha habari] katika nyakati zetu.” Na kama vile msemo mmoja wa kale unavyosema: ‘Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki.’

Wakati mmoja, watu walikuwa wakihangaikia wengine zaidi na walikuwa na nia ya kusaidia rafiki au jirani zao. Lakini kipindi kile cha Vita ya Ulimwengu ya Kwanza kilichotokeza badiliko kubwa kilifanya uhusiano wa kibinadamu kwa ujumla uwe mbaya zaidi. Sasa mwelekeo ulio wa kawaida ni wa kukosa shukrani, wa kutohurumia wengine, na wa mimi kwanza.

Hali hiyo ya mambo inayosikitisha ilitabiriwa karne 19 zilizopita kwa maneno haya: “Katika siku za mwisho itakuwa vigumu sana kuwa Mkristo. Kwa maana watu watajipenda wao wenyewe tu na pesa zao; wao watakuwa wenye kiburi na wenye kujisifu, wakimcheka Mungu kwa dharau, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani kwao, na wabaya kweli kweli. Wao watakuwa wana vichwa vigumu na wasikubali kamwe maoni ya wengine; wao watakuwa waongo wa daima na wafanya-matata na watafikiri ukosefu wa adili si kitu. Wao watakuwa wajeuri na wakali, na watawacheka kwa dharau wale wanaojaribu kuwa wema. Wao watasaliti rafiki zao.”—2 Timotheo 3:1-4, The Living Bible.

Lo! ni hali ya kuhuzunisha na hata hivyo iliyo sahihi kama nini juu ya ulimwengu leo! Na ni wazi haitupi tumaini kubwa la kupata rafiki za kweli. Ijapokuwa hivyo, hata sasa inawezekana kuwa na rafiki za kweli. Nao ni wenye thamani kubwa kama nini! Sikuzote unaweza kuwaendea upate msaada, mashauri, faraja, na uandamani mchangamfu. Lakini ni jambo la muhimu kupambanua kati ya walio na wasio rafiki za kweli.

Si “Rafiki” Wote Walio Rafiki za Kweli

Kijana mwanamume aliyeumia katika aksidenti ambaye alitajwa pale mwanzoni alikuwa mshiriki wa kikoa cha mpira na alikuwa na “rafiki” wengi. Mara nyingi washiriki wa vilabu au jumuiya ndogo-ndogo huunda mahusiano ya kufurahisha. Lakini “urafiki” wa namna hiyo huenda usiwe imara sana. Tena kuwa na “rafiki” wengi halafu uwapoteza wote ni jambo la kuvunja moyo sana, kama vile kijana huyo alivyogundua. Kujipatia wazoeani ni jambo rahisi; kuwa na rafiki za kweli sivyo kulivyo.

Matajiri au wale walio katika cheo cha juu wanaweza kwa urahisi kuwa na “rafiki” wengi. Kame vile Biblia inavyosema: “Walio matajiri wana rafiki wengi.” “Kila mtu hujaribu kupata upendeleo wa watu mashuhuri; kila mtu hudai urafiki wa wale wanaotoa mapendeleo.” (Mithali 14:20; 19:6, Today’s English Version) Lakini je! ni wangapi kati yao wanaokuwa na makusudio mengine ya kando-kando? Na ikiwa watu hawa wenye kuonyeshwa sana urafiki wanapoteza utajiri au hadhi, baada ya muda mfupi huenda wakawa bila rafiki kabisa.

Mara nyingi watu wenye sura za kuvutia wanakuwa na “rafiki” wengi pia—wengi wa hao wakiwa wamevutwa na hali za kimwili. Lakini “urafiki” huo unaweza kudhuru sana na unaweza kutoweka katika joto la taabu kama ukungu. Kwa hiyo kuna uhitaji wa kweli wa . . .

Kuwa Mchaguzi

Ndiyo, kuna hekima katika kuwa mchaguzi kuhusu rafiki. Rafiki za uwongo mara nyingi ni warairai wakubwa wanaotafuta upendeleo wakiwa na kusudio fulani la kando-kando. “Mtu anayerairai jirani yake anatandazia miguu yake wavu.”—Mithali 29:5, The Jerusalem Bible.

Basi, fikiria kwa uangalifu kikundi cha rafiki zako za sasa. Je! wao wanakutolea mavutano ya mema au ya mabaya? Je! wao ni wenye kujifikiria wenyewe tu, wenye kushikilia kauli yao tu, au wenye majivuno? Je! wao wanatenda mambo upesi bila kufikiri na kufurahia kujasiria mambo yaliyo hatari? Mwelekeo wao ni nini kuhusu watu wa jinsia tofauti? Je! wao ni waungwana na wenye heshima au wanazoeana kupita kiasi na watu wa jinsia tofauti, labda hata kukosa adili? Je! waandamani wako wa kawaida wamethibitika kuwa wasio na unyofu, watu wasiotegemeka? Je! wao ni watumiaji dawa za kulevya? Wanywaji wa kupindukia? Ikiwa ndivyo, wewe umo hatarini. Huenda wewe ukawa u mnyofu, safi, na mnyenyekevu, lakini kumbuka: “Mashirika mabaya yanaharibu mazoea yenye mafaa.”—1 Wakorintho 15:33, NW.

Hatari kubwa katika kuwa na waandamani wabaya ni kwamba utawaiga wao. Watakupaka njia zao na mielekeo yao polepole, labda bila ya wewe kuhisi hivyo. Ni kama Biblia inavyosema: “Endelea kuandamana pamoja na wenye hekima nawe utakuwa mwenye hekima. Ukiwa na urafiki pamoja na watu wapumbavu, wewe utaharibiwa.”—Mithali 13:20, TEV.

Ni rahisi kuchukua hatua isiyo ya kweli katika kujipatia rafiki. Lakini usivunjike moyo. Kungali kuna mamilioni ya watu wazuri sana wenye urafiki katika ulimwengu. Hivyo unaweza kupataje rafiki hao wa kweli?

[Picha katika ukurasa wa 4]

Waandamani wako wanaweza kuwa na mavutano yenye nguvu juu yako wewe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki