Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 10/1 kur. 4-7
  • Je! Unaweza Kuipata Dini ya Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Unaweza Kuipata Dini ya Kweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Silika ya Kuua” Yaondolewa Mbali
  • Kutotamani “Dola Ile ya Ziada”
  • Maoni Yanayofaa Juu ya Kazi
  • Maisha ya Jamaa Yenye Furaha Zaidi
  • Lile Swali Kubwa “Kwa Sababu Gani” Lajibiwa
  • Dini ya Ki-Siku-Hizi Ni Yenye Mafaa kwa Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Uamuzi wa Kutumia Maisha Yangu Katika Utumishi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Funzo la Familia Ambalo Huleta Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Matatizo ya Kifedha—Kuna Msaada Gani?
    Furaha​—Namna ya Kuipata
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 10/1 kur. 4-7

Je! Unaweza Kuipata Dini ya Kweli?

RONALD—aliyetajwa katika makala iliyotangulia—alifikiri ilimpasa aache kabisa utafutaji wake wa dini ambayo ingeweza kumpa msaada na mwongozo wenye mafaa. Lakini yeye aliamua kujipa nafasi ya mwisho ya kujaribu. “Ikiwa kweli kweli kulikuwa na Mungu fulani, mimi nilitaka yeye ajue kwamba nilikuwa nikimtafuta kwa unyofu,” yeye akasema. Kwa hiyo usiku mmoja Ronald alisali hivi: “Ikiwa wewe ni Mungu mwenye upendo kweli kweli, wewe nitafute mimi unipate kwa sababu kwa miaka kadha mimi nimekutafuta wewe nisipate kitu.”

Siku chache baadaye akiwa mahali pake pa kazi, Ronald aligawiwa kufanya kazi ya zamu pamoja na mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Alianza kuuliza huyo mwanamke maswali kuhusu Biblia. Majibu yaliamsha udadisi wake. Baada ya muda mfupi akaanza kujifunza Biblia kwa ukawaida. Alienda pia kwenye mikutano ya kundi la Mashahidi wa Yehova la eneo la kwao.

Miezi sita baadaye Ronald alisadikishwa kwamba alikuwa amepata dini iliyompa kichocheo cha kurekebisha maisha yake kwa njia yenye mafaa zaidi sana. Baada ya miaka mitatu ya kushirikiana na Mashahidi wa Yehova, katika barua moja aliyoandikia gazeti Mnara wa Mlinzi alieleza manufaa fulani alizopata kutokana na ushirika huo.

“Silika ya Kuua” Yaondolewa Mbali

Ronald anaandika hivi: “Manufaa ya kwanza kutokana na kujifunza ukweli [fundisho la Biblia] ilikuwa kuweza kuzuia vyema zaidi hasira yangu. Kwa muda mrefu nilihusika katika [judo na karate]. . . . Nilikuwa nikifanya mazoezi kwa muda wa saa sita mpaka nane kwa siku, na sikuzote ilikaziwa kikiki ndani yangu nisitawishe silika ya kuua.”

Kupigana na kuua si njia zenye matokeo za kutatua mahitilafiano pamoja na mwanadamu mwenzako. Basi, dini yenye mafaa ni kani ya kuleta amani. Biblia inasema kwenye Warumi 12:18, NW: “Iweni wenye kuamanika pamoja na watu wote.” Mashahidi wa Yehova hawazoezi miili yao kwa pigano, wala hawatafuti kujihami kwa kujifunza kutumia bunduki. Wao wanajulikana duniani pote kwa msimamo wao wenye amani, wa kutokuwamo katika wakati wa vita.

Kwa kuona kani yenye mafaa au mambo yanayoweza kutimizwa na dini ya namna hiyo, mtawa wa kike wa Roma Katoliki aliandika katika gazeti moja la Kiitalia la kanisa hivi: “Ulimwengu ungekuwa tofauti kama nini ikiwa sisi sote tungeamka asubuhi moja tukiwa tumeamua kwa uthabiti kutochukua silaha tena, . . . sawasawa na Mashahidi wa Yehova!”

Mwelekeo huo wa kuamanika ulio miongoni mwa Mashahidi umechangia kufanyiza udugu wa ulimwenguni pote wa watu zaidi ya milioni tatu katika nchi 208. Wao wanatendeana kama rafiki za kweli kweli, bila kujali ni wa taifa, kabila, au cheo gani cha kijamii. Jambo hilo ni lenye mafaa sana katika ulimwengu wenye uhasama, hasa wakati msaada unapohitajiwa. Eva, mwanamke kijana wa Sweden—ambaye ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova—aliona jambo hilo.

Alipokuwa akitembelea Ugiriki, Eva alipatwa na ugonjwa wa ngozi inayofunika ubongo. Akiwa amekosa fahamu, na mwenye sumu katika damu na kuvuja damu ndani mwilini, yeye aliharakishwa kwenye hospitali moja katika Athene, ambako hakujua mtu ye yote. Baba yake katika Sweden alipashwa habari kwa simu. Yeye akapigia simu mzee mmoja katika kundi la kwao la Mashahidi wa Yehova. Mzee huyo akawapigia simu Mashahidi aliowajua katika Athene. Eva alifikiwa kwa haraka na waamini wenzake Wagiriki asiopata kamwe kukutana nao.

Jambo hilo linaleta akilini mfano ambao mtume Paulo alitumia, akionyesha jinsi umoja na uhurumiano yanavyofanya kazi pamoja. Yeye alisema kwenye 1 Wakorintho 12:25, 26: “Kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. Na kiungo kimoja kikiumia viungo vyote huumia nacho.”

Hilo ndilo jambo ambalo Eva aliona katika Ugiriki. Kwa karibu majuma matatu rafiki zake wapya hawakumwacha yeye bila mtu wa kumtumikia. Yeye alipona na akarudi nyumbani kwake. Anasema: “Mimi niliona kweli kweli manufaa za udugu wenye upendo.”

Kutotamani “Dola Ile ya Ziada”

Acheni tuirudie barua ya Ronald. Baada ya kusimulia jinsi itikadi yake mpya ilivyomsaidia kuzuia hasira yake, aondolee mbali ile “silika ya kuua,” na kuwa mwenye kuamanika zaidi, yeye anasema kwamba fundisho la Biblia lilimpa maoni yenye usawaziko juu ya kazi na pesa. “Mimi nilikuwa mwendesha-kompyuta namba moja wa mwajiri-kazi wangu.” Ronald anasema, “na nilikuwa nikikosa kuwa pamoja na jamaa na rafiki zangu ili tu nifanye kazi ya ziada. Nilifanya kazi nyakati za usiku kwa miaka zaidi ya saba. Sikuzote niliitaka ile dola ya ziada.”

Tamaa hiyo ya kutaka “ile dola ya ziada” inaweza kuja kuleta madhara baadaye, madhara ya kifo. “Kwa watu fulani, pesa zinamaanisha usalama. Kwa watu fulani zinamaanisha mamlaka. Kwa wengine zinamaanisha wataweza kununua upendo, na kwa kikundi fulani cha nne zinamaanisha mashindano na kuupata ushindi,” anasema daktari wa akili Jay Rohrlich, ambaye wateja wake sana-sana ni wakubwa wanaoshughulikia pesa wa kutoka wilaya ya Wall Street ya New York.

Ikieleza juu ya taarifa hiyo, ripoti moja katika gazeti Science Digest inasema: “Itikadi ya kwamba pesa zinaweza kutokeza mambo hayo . . . inaongoza mara nyingi kwenye ukosefu wa uwezo wa kufanya ngono, ukosefu wa usingizi, mitokeo ya ghafula ya ugonjwa wa moyo na kuwa na matatizo pamoja na mwenzi wa ndoa na watoto.” Shauri la Biblia ni: “Msiwe na tabia ya kupenda fedha.” Ronald alijifunza jambo hilo na kulitumia. Alipata kwamba hilo lilikuwa jambo lenye mafaa sana.—Waebrania 13:5.

Maoni Yanayofaa Juu ya Kazi

Mara nyingi utafutaji wa pesa unashawishi watu wajilazimishe kupanda cheo katika kazi ya maisha yao. Jambo hilo linaweza kuletea hata watu wenye afya nzuri sana mikazo mikali na pambano la maoni ya moyoni—hata kufikia kujiua. “Mwanamume mmoja, aliyekuja kazini asubuhi moja akapata kwamba dawati yake ilikuwa imehamishwa, alipanda juu kabisa ya jengo lile na kuruka chini.” Dakt. Douglas LaBier alisimulia jambo hilo katika hoji moja la U.S.News and World Report lenye kushughulika na ukamatano ulio kati ya kazi za maisha na matatizo ya kimoyoni.

“Linalohitajiwa,” anasema Dakt. LaBier “ni maisha yaliyoendelezwa zaidi, na moja ambayo hayategemei sana kazi fulani ya maisha. Kuongezea mambo kama vile ulaji wa kutosha, pumziko na mazoezi, watu wanaotaka maisha zenye usawaziko zaidi wanahitaji kufikiria kufanya mambo mengi zaidi pamoja na jamaa zao na kuendeleza uwezo wa kufanya mambo yasiyohusiana na kazi ya maisha yao ambayo yanawapa furaha.”

Mashahidi wa Yehova wanajifunza kutokana na Biblia kusawazika kwa habari ya pesa na kazi. Mhubiri 4:4, 6 (NW) ansema juu ya kazi ngumu inayohusu “ushindani wa mmoja kuelekea mwingine” na kusema: “Ni zuri zaidi konzi la pumziko kuliko konzi maradufu la kazi ngumu na kujitahidi kufuatia upepo.” Ronald alipata hiyo kuwa hekima yenye mafaa. Alipunguza kazi yake ya kimwili ili awe na wakati mwingi zaidi kwa ajili ya masilahi za kiroho na kwa ajili ya jamaa na marafiki wake.

Maisha ya Jamaa Yenye Furaha Zaidi

Ndipo Ronald anaposema katika barua yake kwamba mashauri ya Biblia juu ya ndoa na maisha ya jamaa yamemsaidia kushughulika kwa hekima zaidi na hali za jamaa. Jambo hilo ni la maana sana sasa wakati maisha ya jamaa yanapoelekea kuvunjika katika mahali pengi. Nchi zenye maendeleo ya viwandani zinaripoti ndoa chache zaidi, talaka nyingi zaidi, na hesabu inayopungua ya watoto wanaozaliwa.

Elekeo hilo linagutusha kwa sababu katika jamaa ndipo ambapo baadhi ya mahitaji yaliyo ya msingi zaidi ya kibinadamu yanapotoshelezwa. Katika uchunguzi mmoja, gazeti Sydney Morning Herald la Australia liliuliza watu 2,000 ni jambo gani kati ya yanayofuata ambalo liliwapa uradhi mkubwa zaidi: kazi, jamaa, rafiki, utendaji mbalimbali wa kujifurahisha, mali, au dini. Watu wengi ajabu waliipa “jamaa” mahali pa kwanza.

Mashahidi wa Yehova wanapendezwa na kuendeleza jamaa zao zikiwa zenye nguvu. Kwa mfano, katika muda wa miaka mitano tu iliyopita, magazeti yao mawili Mnara wa Mlinzi na Amkeni! (yenye jumla ya mwenezo wa nakala zapata milioni 22 katika lugha zaidi ya 100) yamekuwa na makala zapata 60 zenye mafaa kuhusu kushughulika na hali tofauti-tofauti katika maisha ya jamaa. Bila shaka, dini yenye msingi wa Biblia inayosaidia watu watunze jamaa zao kwa njia ya hekima na upendo ni yenye mafaa.

Lile Swali Kubwa “Kwa Sababu Gani” Lajibiwa

Ronald anamalizia barua yake kwa kusema: “Kuna jambo moja ambalo mara nyingi linakuja akilini wakati mimi ninaposoma gazeti la habari, kutazama habari za televisheni, kuongea pamoja na wafanya kazi wenzangu, au kuambia wengine juu ya imani yangu. Hilo ni kwamba kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova kunanipa mimi jibu kwa moja la maswali yanayoulizwa mahali pengi zaidi sana katika ulimwengu —Kwa sababu gani kuna uhalifu, jeuri, vita, ukosefu wa adili, magonjwa, msukosuko wote huu, zaidi ya kuwako matatizo yote yale ya kila siku? Kujua kwamba mfumo huu na matatizo yao ni ya muda tu kumeinua uzito mkubwa kutoka kwenye mabega yangu.”

Biblia inafunua ni nini kinachosababisha hali ya leo ya ulimwengu yenye kufadhaisha. Inaeleza ni kwa sababu gani kusudi la awali la Muumba kufanya dunia hii iwe makao ya paradiso kwa wanadamu halijawa halisi bado. Inaeleza jinsi Mungu atakavyoondoa duniani mavutano yote yenye kuvuruga na kusimamisha paradiso ya kudumu ili watu waifurahie milele.—2 Petro 3:9-13

Ili dini iwe yenye thamani yenye mafaa, ni lazima izae tunda jema. Ni lazima itokeze watu bora. Ni lazima iweze kueleza ni kwa sababu gani mambo yako kama yalivyo duniani leo. Na inapasa ikaze kikiki tumaini hakika kwa wakati ujao katika akili na mioyo ya watu. Ronald alitafuta dini ya namna hiyo, na akaipata. Nafasi iyo hiyo ingali wazi kwako wewe.—Mathayo 7:17-20.

[Picha katika ukurasa wa 5]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki