Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Kosa la Musa lilikuwa nini ambalo lilileta hasara ya kupoteza pendeleo la kuingia katika Nchi ya Ahadi? Je! ni kwamba yeye alipiga ule mwamba badala ya kusema nao tu, au ilikuwa kwamba yeye alishindwa kutukuza Yehova Mungu?
Inaonekana kwamba kosa la Musa lilikuwa zaidi ya kwamba yeye alipiga tu ule mwamba badala ya kusema nao, kama vile Mungu alivyokuwa ameelekeza.
Karibu na mwisho wa miaka 40 ya kutanga-tanga, Waisraeli walipiga kambi Kadeshi-barnea katika jangwa la Zini (au, Parani). Wao walikuwa wamepiga kambi huko makumi ya miaka kabla ya hapo, inaelekea kwa sababu macho matatu ya maji katika eneo hilo yanatokeza mahali penye rutuba palipo na usitawi, kama inavyoonekana katika picha inayoambatana na habari hii. Ingawa hivyo, katika pindi hiyo, maji yalikuwa haba, jambo ambalo huenda lilimaanisha kwamba watu hao hawangeweza kupata chakula kingi. Kwa hiyo wao waligombana na Musa, mwakilishi wa Mungu, wakisema: “Mbona ninyi mmetuongoza kutupandisha kutoka nchi ya Misri kutuleta mahali hapa paovu? Hapa si mahali pa mbegu na tini na mizabibu na mikomamanga, na hapana maji ya kunywa.”—Hesabu 20:5, NW.
Ndipo Mungu alipoambia Musa na Haruni: “Chukua ile fimbo na uite lile kusanyiko pamoja,... na lazima ninyi msema na lile jabali mbele ya macho yao, hilo lipate kweli kweli kutoa maji yalo; na lazima utwae maji, kwa ajili yao kutoka lile jabali na kuwapa kinywaji kusanyiko na wanyama-wa-beba-mizigo wao.” (Hesabu 20:8, NW) Ni jambo gani ambalo lilitokea baada ya hapo?
“Musa na Haruni wakaita lile kundi pamoja mbele ya lile jabali, na yeye akaendelea na kuambia hao, ‘Sikieni, sasa, ninyi waasi! Je! ni kutoka kwenye jabali hili kwamba sisi tutaleta maji kwa ajili ya ninyi?’ Kwa jambo hilo Musa akainua mkono wake juu na kupiga dharuba lile jabali kwa fimbo yake mara mbili; na maji mengi yakaanza kutoka.”—Hesabu 20:10, 11, NW.
Watu fulani wameonelea kwamba Mungu alielekeza Musa na Haruni ‘waseme na lile jabali,’ lakini wao ‘wakapiga dharuba lile jabali.’ Je! tofauti hiyo ilichukiza Yehova sana hivi kwamba yeye aambie Musa na Haruni kwamba Yeye hangewaruhusu waongoze Israeli kuingia Nchi ya Ahadi?
Haielekei kuwa hivyo. Uhakika ni kwamba miezi tu baada ya kule kutoka, watu hao walikuwa kwanza wamelalamika juu ya ukosefu wa maji. Jambo hilo lilitukia karibu na Mlima Sinai (Horebu), katika mahali ambapo palikuja kuitwa Meriba (katika eneo linaloonekana chini). Angalia jambo ambalo Mungu aliambia Musa katika pindi hiyo: “Mimi nasimama mbele ya wewe kule juu ya ule mwamba katika Horebu. Na lazima wewe upige dharuba juu ya ute mwamba, na ni lazima maji yatoke katika huo, na lazima watu wanywe hayo.” (Kutoka 17:2-7; 33:6, NW) Kwa hiyo, wakati Musa alipoambiwa aseme na ule mwamba kule Kadeshi, ingeweza kuwa yeye alikuwa na mwinamio wa kufanya jambo alilokuwa amefanya mapema kwa mwelekezo wa Mungu, hata ikiwa Mungu alimaanisha kwamba kusema na ule mwamba kungetosha.
Inaonekana kwamba jambo fulani zaidi liliongoza kwenye hukumu ya Mungu juu ya Musa na Haruni. Jambo hilo lingeweza kuwa lilikuwa nini? Musa aliambia watu wale wenye ugomvi: “Je! ni kutoka kwenye jabali hili kwamba sisi tutaleta maji kwa ajili ya ninyi?” Zaburi 106:33 (NW) inatupa sisi mwono wa ndani katika jambo hilo, kwa maana inaonyesha kwamba Musa alitenda kutokana na roho yenye uchungu na kwamba yeye alisema kwa haraka-haraka kwa midomo yake.’ Kwa maneno ya hasira, yeye alivuta fikira kwake mwenyewe na Haruni badala ya kuzivuta kwa Mmoja yule ambaye kwa kweli angeweza kuandaa maji kimuujiza. Hivyo, muda mfupi tu kabla Musa hajafa kwenye mpaka wa ile Nchi ya Ahadi, Mungu alirejeza kwenye kile kisa ambacho kilitukia Kadeshi-barnea na kuonyesha kwamba kosa la Musa lilikuwa kwamba yeye alishindwa ‘kutakasa Mungu mbele ya macho ya wale watu.’—Hesabu 27:12-14, NW.
Sisi tunaweza kuchukua somo kutokana na jambo hilo. Ingawa kwa uhakika ni jambo la maana kujizuia wenyewe na vitendo vya hasira, sawasawa na hivyo ni muhimu kuongoza roho yetu, hususa wakati watu wale wengine wanapopungukiwa. Sisi tukijiacha wenyewe tufadhaike kupita kiasi, sisi tungeweza kuanza kuona watumishi wa Mungu kwa msingi wa kibinadamu, badala ya kutambua kwamba wao bado ni “kondoo” za Mungu. Ni kweli, wao ni wasio wakamilifu na huenda wakafanya mambo ya kuudhi, lakini wao ni “watu wake, na kondoo wa malisho yake.” (Zaburi 100:3) Mungu aliacha Mwana wake afe kwa ajili ya watu hao, hivyo je! sisi hatupaswi kujitahidi kuwa wenye subira nao, tupunguze fikira tunazokaza juu ya jinsi ambavyo sisi tunahisi au tunaathiriwa na kukaza fikira zaidi juu ya msimamo wao pamoja na Mungu?
[Picha katika ukurasa wa 31]
Wakati wa masika katika mahali penye rutuba na usitawi karibu na moja la macho ya maji katika lile eneo la Kadeshi-barnea
[Credit Line]
Photos, pages 10, 31: Pictorial Archive (Near Eastern History)