Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 11/15 kur. 4-7
  • Je! Dini Inaweza Kutosheleza Mahitaji Yetu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Dini Inaweza Kutosheleza Mahitaji Yetu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kutosheleza Mahitaji Yetu ya Kimwili
  • Kwa Nini Upendezwe na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Tafuta Ufalme, Si Vitu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Je! Dini Imetosheleza Mahitaji Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Furahia Kazi Yako
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 11/15 kur. 4-7

Je! Dini Inaweza Kutosheleza Mahitaji Yetu?

TUTAKULA nini? Tutakunywa nini? Tutavaa nini? Kuna uharaka kuhusu maulizo haya, hasa inapokuwa vigumu sana kupata mahitaji ya lazima ya maisha. Hata hivyo, angalia kwamba Yesu Kristo alisema: “Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini.” (Mathayo 6:25) Je! hilo linaonekana kuwa jambo geni? Hata hivyo, mtu akikosa chakula, mavazi, na makao, anachohitaji ni msaada wenye mafaa, si kile ambacho huenda wengine wakakiona kuwa maneno matupu ya kidini.

Yesu hakuwa mwenye kukosa huruma, wala yeye hakuwa akijaribu kuepa suala hilo. Yeye aliyajua sana mahitaji ya watu. Hata hivyo, yeye alijua hatari iliyo halisi sana. Inapohusu kutosheleza mahitaji yetu, ni vyepesi sana kukazia maishani mwetu kutegemea vitu vya kimwili na kuhisi kwamba Mungu si wa maana sana. Basi, tunahitaji kunyoosha mambo yetu ya kutanguliza.

Tutanyoosha mambo yetu ya kutanguliza ikiwa sisi tutafuata shauri la Yesu: “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki [uadilifu, NW] [ya Mungu] na hayo yote mtazidishiwa.” (Mathayo 6:33) Tukifuata shauri hilo, dini—dini ya kweli inayotegemea kweli za Biblia—inaweza kutosheleza mahitaji yetu.

Hata hivyo, Yesu hakuwa mtu asiyeona jinsi mambo yalivyo hasa hivi kwamba adokeze kwamba kuwa tu mmoja wa wanafunzi wake na kufuata mafundisho yake ya kidini kungetatua matatizo yetu mara moja; wala yeye hakumaanisha kwamba wanafunzi wake wapaswa kuketi kitako tu na kungojea Mungu awaandalie kimuujiza. Kwani, huenda kila mmoja angekuwa Mkristo ikiwa hilo lilimaanisha kuwa huru mara hiyo kutoka kwa magumu ya maisha! Alilomaanisha Yesu ni kwamba Baba yake, Yehova Mungu, anaandaa kila kitu kinachohitajiwa kutosheleza mahitaji yetu. Ndiyo sababu Yesu alisema hivi pia: “Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.”—Mathayo 6:32.

Pia Yehova anatosheleza mahitaji yetu ya kiroho yenye umaana wa muhimu. Kupitia kwa Maandiko Matakatifu, yeye ametupa sisi mwongozo wa kuelekeza maisha zetu katika njia nzuri zaidi iwezekanayo. (Isaya 48:17) Mungu amesimamisha ushirika wa waabudu wanaotoa tegemezo linapohitajiwa. (Matendo 4:34) Yeye pia anajiingiza kuwasaidia watumishi wake kupitia kwa roho yake takatifu, au kani yenye kutenda. (Luka 11:13; Wagalatia 5:22-25) Tena, Mungu amefanya uandalizi ili arudishe Paradiso duniani.—Luka 23:43, NW; Ufunuo 21:1-4.

Kutosheleza Mahitaji Yetu ya Kimwili

Sasa ebu zifikirie nyingine za kanuni za Biblia ambazo zimewasaidia watu watosheleze mahitaji yao ya kimwili. Mtume Mkristo Paulo aliandika:

“Na tujitakase nafsi-zetu na uchafu wote wa mwili na roho.” (2 Wakorintho 7; 1)

Ebu wazia matatizo yote ambayo tunaweza kukimbia tukiepuka kujichafua kwa tumbako, dawa za kulevya zisizo halali, na vitu vingine vinavyouchafua mwili. Na tunakuwa afadhali namna gani tusipotapanya-tapanya pesa, wakati, na mawazo kwa vichapo visivyo na adili na starehe zinazoweza kuchafua roho yetu!

Pia Maandiko yanasema hivi:

“Usiwe miongoni mwao wanywao divai wazito, miongoni mwao walio walaji wa nyama walafi. kwa kuwa mlevi na mlafi ataingia katika umaskini, na usingizi mzito utamvika mtu matambara halisi.” (Mithali 23:20,21, NW)

Ona tokeo la mwisho la ulevi na ulafi —umaskini na matambara. Wengi leo—hata watu ambao ni wanadini sana—wanaendelea kuwa katika umaskini kwa sababu wanajiingiza katika matumizi ya vileo kupita kiasi au ni wazoevu wa vitu vinavyochafua mwili. Kuepuka vitu kama hivyo ili kujipatanisha na viwango vya Biblia kunaweza kutusaidia sana kutosheleza mahitaji yetu ya chakula, mavazi, na makao.

Kanuni nyingine ambayo imewasaidia Wakristo watosheleze mahitaji yao inaonwa katika maneno ya mtume Paulo:

“Sisi tuna utumainifu kwamba tuna dhamiri nyofu, maadamu sisi tanataka kujiendesha wenyewe kwa unyofu katika mambo yote.” (Waebrania 13:18, NW)

Kuwa wanyofu katika mambo yao yote kumewawezesha Wakristo wengi wajiruzuku wenyewe na jamaa zao. Kumewaletea sifa nzuri, na hivyo wengine wanaelekea kufanya biashara pamoja nao. Mtu mnyofu huenda sikuzote asiwe na mengi kimwili, lakini kwa kawaida ana mahitaji ya lazima ya maisha na anahifadhi staha yake mwenyewe.

Linalohusiana kwa ukaribu sana na hili ni lile shauri:

“Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe.” (Waefeso 4:28)

Kutumia kanuni hii kumewasaidia wengi wapate na kushikilia kazi ya kuajiriwa kwa sababu wao ni wenye kutibarika. Kwa sababu hiyo, wanaweza kujiruzuku wenyewe na jamaa zao. Badala ya kuambukizwa na roho ya ulimwengu huu, inayojifanya haioni mazoea mengi ya kukosa unyofu, Wakristo ni wanyofu, na jambo hili linaleta matokeo mazuri.

Ili kutoa kielezi: Mmoja wa Mashahidi wa Yehova katika Japani alitaka kufanya kazi kwa saa chache kila juma ili awe na wakati zaidi kwa ajili ya mambo ya kiroho. Hata hivyo, alipotoa ombi lake, mwajiri-kazi wake alimfukuza kutoka katika kazi yake. Kwa sababu hiyo, mama ya mwajiri-kazi huyo alimwuliza: “Je! wewe ulimfuta kazi yule mwanamume anayetegemeka zaidi?” Mambo yakawa mabaya zaidi kwa Shahidi huyo alipoumiza mgongo wake akifanya kazi nyingine. Muda mfupi baadaye, yeye alikutana na mwajiri-kazi wake wa zamani, ambaye alikuwa amekasirika kwa sababu alikuwa tu amepata kujua kwamba mmoja wa waajiriwa wake alikuwa amekuwa akiiba dhahabu, platinamu, na pete kutoka katika kampuni yake ya vito vyenye thamani. Mara hiyo mwajiri-kazi huyo akamwomba Shahidi arudi kazini, wakati huu kwa masharti yake mwenyewe. Mwanamume huyo alitaka mfanyakazi mnyofu.

Kulingana na mtume Paulo, Mkristo apaswa ‘afanye kazi kwa juhudi’ si kujiandalia yeye mwenyewe tu bali pia “apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.” (Waefeso 4:28) Nyakati za uhitaji, Wakristo wa kweli sikuzote wana nia ya kuwasaidia wengine. Jamaa moja katika Fiji ilipata kuona jambo hili wakati nyumba yao ilipoharibiwa vibaya sana na kimbunga walipokuwa kwenye mkusanyiko wa Kikristo. Waliporudi nyumbani, walipata tamasha ya uharibifu. Lakini pia wao walipata waamini wenzao ambao walitumia mali zao kwa furaha kuandalia jamaa hiyo makao na msaada wa kujenga upya nyumba yao. “Ni jambo lenye kufariji,” akasema haba yule, “unapojua kwamba kuna Wakristo ambao wanakujali wewe sana.”

Yesu Kristo alihisi huruma kubwa sana kwa walio na uhitaji. Katika pindi nyingi, yeye binafsi alitoa msaada kwa walio na upungufu katika njia moja au nyingine. Bila shaka, Yesu alijua kwamba mradi mfumo huu wa mambo uliofisidika unaruhusiwa kuwapo, umaskini na matatizo mengine ya kijamii yataendelea kuwapo. (Yohana 12:8) Kwa hiyo, ijapokuwa yeye alifanya mengi kuwasaidia watu kimwili, mkazo halisi wa huduma yake ulikuwa kutosheleza mahitaji yao ya kiroho.

Wakati umati ambao njaa yao ilikuwa imetoshelezwa ulipomfuata Yesu Kapernaumu, yeye alitoa maelezo haya yenye maana sana: “Ninyi mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba. Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa.” (Yohana 6:26, 27) Yesu alimaanisha nini?

Yesu alimaanisha kwamba kuna hatari ambayo watu wangeishirikisha na yeye na wanafunzi wake kwa faida ya kimwili tu. Lakini yeye alijua kwamba hili halingeleta manufaa yenye kudumu. Kwa hiyo yeye alisema: “Wenye furaha ni wale wanaoona uhitaji wao wa kiroho, kwa kuwa ufalme wa mbingu ni wao. Wenye furaha ni wale ambao wana njaa na kiu kwa uadilifu, kwa kuwa wao watajazwa.”—Mathayo 5:3, 6, NW.

Zaidi ya njaa ya chakula cha kimwili, kuna njaa ya ukweli na utimizo wa kiroho. Furaha ya kweli inatokea wakati njaa hii ya kiroho inapotoshelezwa. Jumuiya ya Wakristo imetokeza jamii inayofikiria mambo ya kimwili tu. Dini za Mashariki zimewaacha watu katika giza la kiroho. Lakini ibada ya kweli​—dini ya Yesu Kristo—imetosheleza mahitaji ya kiroho ya watu. Inaweza kufanya vivyo hivyo kwako wewe. Maandalizi haya yanaweza kuwa yako ikiwa wewe utayatumia kwa faida.

Mathalani, kutoka kwa Mkristo aliyeshiriki katika kutoa ushuhuda barabarani, mwanamume kijana mmoja katika Mauritius alikubali nakala za Mnara wa Mlinzi na jarida jenzi Amkeni! Juma lililofuata, yeye alirudi ili apate magazeti zaidi. Alieleza kwamba yeye alikuwa akifikiria kujiua mwenyewe kwa sababu ya matatizo yake ya kifedha, lakini magazeti yale yalikuwa yamemsaidia ang’amue kwamba kuna Mungu anayetujali sisi. Njaa ya kiroho ya mwanamume huyo kijana ilikuwa inaanza kutoshelezwa.

Je! sisi tutapata kuona wakati ambao mahitaji yetu yote ya kiroho yatatoshelezwa kikamili? Biblia inaahidi kwamba tutaona. Kwa kweli, watu wamechoka kusikia ahadi moja baada ya nyingine kuhusu mambo mazuri yatakayokuja. Wametamaushwa mara nyingi. Lakini sisi tunaweza kuwa na uhakika katika ahadi za Biblia. Mtungaji wayo, Yehova Mungu, anatimiza kila ahadi anayofanya. Yoshua alieleza jambo hili katika njia nzuri alipowakumbusha Waisraeli wenzake hivi: “Nanyi nyote mnajua mioyoni mwenu, na rohoni mwenu, ya kuwa halikuwapungukia ninyi hata neno moja katika mambo hayo mema yote aliyoyanena BWANA [Yehova, NW], Mungu wenu, katika habari zenu; yote yametimia kwenu, hapana neno lo lote mlilopungukiwa.”—Yoshua 23:14.

Utatuzi wa kweli kwa matatizo yetu yote unategemea utimizo wa ahadi za ajabu za Mungu za kusafisha dunia nzima. (Ufunuo 11:18) Mahitaji yetu yote yatatoshelezwa wakati Ufalme wake utakaporudisha Paradiso duniani, kutimiza ahadi yake ya kwanza kwa aina ya wanadamu. (Mathayo 6:9, 10) Halafu sisi hatutasikia ‘sauti ya kulia wala ya kuomboleza’ kutoka kwa watu ambao mahitaji yao hayawezi kutoshelezwa. Kupitia kwa kazi ya unyofu na kutumia kanuni za kimungu, wao watafurahia maisha kamili, yenye kutosheleza.—Isaya 65:17-25.

Maria, aliyekuwa mtawa wa kike Mkatoliki aliyetajwa mwanzoni, alipata uhakika huu. Yeye aling’amua kwamba yeye alikuwa ameishi katika giza la kiroho kwa miaka mingi, akitaabishwa na hofu juu ya wakati ujao na akikosa kuona maana halisi ya maisha. Lakini kujifunza kweli ya Biblia kulibadili yote hayo. “Mimi nilitoka gizani nikaingia katika nuru inayong’aa zaidi,” akasema. (Zaburi 43:3; Mithali 4:18) Jambo hili halikumsaidia tu kutosheleza mahitaji yake ya kimwili ya wakati huo bali pia kutosheleza njaa na kiu chake cha kiroho. Ndiyo, dini —dini ya kweli—inaweza kutosheleza mahitaji yako.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Dini ya kweli itatosheleza mahitaji yetu yote

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki