Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w94 6/1 kur. 3-4
  • Kwa Nini Upendezwe na Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Upendezwe na Dini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Dini Inaweza Kutosheleza Mahitaji Yetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Walijitoa Wenyewe kwa Hiari​—Nchini Albania na Kosovo
    Masimulizi ya Mashahidi wa Yehova
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Kwa Nini Kuchukua Dini Kwa Uzito?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
w94 6/1 kur. 3-4

Kwa Nini Upendezwe na Dini?

KATIKA kila nchi duniani, watu hupendezwa na dini. Kwa upande ule mwingine kuna watu wengi sana pia ambao husema kwa wazi kwamba hawapendezwi na dini. Lakini, je, wao walihisi hivyo sikuzote?

Asili ya kibinadamu ni kwamba mtu huwa hatosheki kikweli akiwa na vitu vya kimwili pekee. Wanadamu huhitaji kuwa na hali ya kiroho. Kuwako kila siku kunakotegemea mahitaji ya kimwili pekee, kukiwa na vipindi vya mara kwa mara vya tafrija, hakuridhishi kikamili mahitaji ya mtu ya ndani kabisa. Tofauti na wanyama, wanadamu hutaka kujua, ‘Kusudi la uhai ni nini?’ ‘Uhai huu mfupi unaotia ndani mambo mengi mazuri na pia mambo mengi mabaya, je, ndio uu huu tu?’ Je! hujapata kuuliza maswali kama hayo?

Hata hivyo, mamilioni mengi ya watu walio hai leo walikulia katika mazingira yaliyozuia kupendezwa na dini kokote kwa maana. Huenda uvutano huo ukatoka kwa wazazi wao, kwa walimu wao, kwa marika wao, au hata kwa serikali yao.

Skalabrino, ambaye ni kijana kutoka Albania, alieleza kwamba chini ya utawala wa Ukomunisti watu walifundishwa kwamba hakuna Mungu. Zaidi ya hayo, ingekuwa hatari kwao kuongea juu ya dini; kufanya hivyo kungewasababisha wafungwe gerezani. Hata hivyo, katika 1991, alipokuwa Uswisi akiwa mkimbizi, alipewa fursa ya kujifunza Biblia. Yeye alikubali. Kwa nini?

Katika Albania yeye alikuwa amesikia kwamba kulikuwa na kitabu kiitwacho Biblia, lakini kwa kweli yeye hakujua jambo lolote juu yacho. Hivyo, mwanzoni huenda isiwe tamaa ya kuelewa Biblia hasa iliyomchochea ajifunze. Ingawa aliambiwa kwamba angekuwa akijifunza juu ya kusudi la Mungu kwa ajili ya wanadamu na dunia, aliona hiyo ikiwa fursa ya kufanyia maendeleo matumizi yake ya lugha iliyotumiwa mahali hapo. Lakini, upesi alipata kwamba yale aliyokuwa akijifunza yaliridhisha tamaa ya kiroho ya kindani yenye nguvu sana aliyokuwa nayo. Moyo wake ulichangamshwa na ahadi ya Mungu ya ulimwengu mpya ambamo amani ingeenea, ulimwengu ambamo watu wangeweza kuishi milele na kufurahia wingi wa vitu vyote vinavyohitajiwa kwa uhai. Kupendezwa kwake kulifikia upeo alipojifunza kwamba yeye na familia yake wangeweza kuwa sehemu ya ulimwengu mpya huo. Akiwa hawezi kujiwekea habari njema hiyo, alipigia simu familia yake katika Albania ili kushiriki habari hiyo nao.

Aleksei, aliyeishi Urusi, alishangaa pia juu ya jinsi ujuzi sahihi ulivyoweza kuathiri maisha ya mtu. Akiwa amelemewa na matatizo na asiweze kupata elezo lenye kuridhisha juu ya kusudi la uhai, alipanga kujiua. Hata hivyo, kwanza alikwenda Finlandi ili kumtembelea rafiki fulani. Akiwa njiani katika gari-moshi, aliongea juu ya matatizo yake pamoja na maabiria wenzake. Mlikuwa na Shahidi wa Yehova miongoni mwao, ambaye alimsihi ajifunze Biblia kwa sababu hiyo hutoa utatuzi wa matatizo ya jinsi hiyo. Yeye alikuwa mwenye kutia shaka. Kwenye safari ya kurudi, alikuwa na ono lilo hilo. Wakati huu ni Shahidi mwingine aliyezungumza naye na kumwambia kwamba yeye alikuwa amekuwa na matatizo ya namna hiyo lakini Biblia ilikuwa imemsaidia ayashinde. Yeye pia akamtia moyo mtu huyo ajifunze Biblia. Alipowasili nyumbani, simu ililia. Huyo alikuwa rafiki mwingine, aliyekuwa akijifunza na Mashahidi na alikuwa na furaha sana. Mtu huyo alikuwa akianza kung’amua kwamba labda Biblia ingeweza kuandaa alichohitaji, lakini alijua kwamba yeye hangeweza kuielewa bila msaada. Alikubali kuwa na funzo la Biblia nyumbani la kawaida pamoja na Mashahidi wa Yehova, akaanza kuhudhuria mikutano yao. Upesi alielewa ni kwa nini wale wanaofinyanga maisha zao kulingana na yale ambayo Biblia hufundisha ni wenye furaha sana, ingawa wao pia hukabili matatizo yaliyo ya kawaida kwa wanadamu.

Akiwa na ufahamu wa kindani kuhusu asili ya kibinadamu, Yesu Kristo alisema hivi: “Mtu hawezi kuishi kwa kutegemea mkate pekee.” (Mathayo 4:4, The New English Bible) Alisema hivi pia: “Wenye furaha ni wale wenye kufahamu uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3, New World Translation) Wao wana furaha kwa sababu wanafahamu kwa makini uhitaji wao, wanachukua hatua zifaazo ili kuuridhisha uhitaji huo, na hupata baraka ya Mungu. Hata hivyo, uhitaji wetu wa kiroho hauridhishwi kwa kujiunga na kanisa fulani tu au kwa kuhudhuria mahubiri fulani ya kidini. Dini iliyo ya kidesturi hasa huenda ikawa na uvutano wa kihisiamoyo, lakini je, hiyo huandaa masuluhisho halisi kwa matatizo ya maisha? Hata ingawa dini yafundisha imani fulani za msingi zifaazo, ikiwa inashindwa kuandaa uelewevu wa kweli juu ya kusudi la uhai, je, itaridhisha uhitaji wako wa kiroho? Jambo lililo la maana hata zaidi ni, je, kuzoea dini ya jinsi hiyo kutaongoza kwenye uhusiano mzuri na Mungu? Bila uhusiano huo, uradhi wa kweli utakosekana.

Kwa habari hiyo watu wengi wanatafuta kitu fulani ambacho hawajapata bado.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Je! mahitaji yako ya kiroho yataridhishwa kwelikweli kwa kujiunga na kanisa fulani?

[Picha katika ukurasa wa 4]

Wengi wamepata kwamba wanapoielewa Biblia, maisha yanakuwa yenye maana zaidi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki