Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 12/1 kur. 4-7
  • Kuponya kwa Kutumia Imani Je! Kunatoka kwa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuponya kwa Kutumia Imani Je! Kunatoka kwa Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tofauti Kubwa-Kubwa
  • ‘Wewe Huna Imani!’
  • Kuponya​—Zawadi Ambayo Ilipitilia Mbali
  • Sababu ya Kujihadhari
  • Wakati Mkristo ni Mgonjwa
  • Je! Uponyaji wa Imani Hukubaliwa na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • ‘Uponyaji wa Kimuujiza’ Leo—Je, Unatoka kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Kuponywa Kimuujiza kwa Wanadamu Kuko Karibu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Jinsi Imani Iwezavyo Kusaidia Wagonjwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 12/1 kur. 4-7

Kuponya kwa Kutumia Imani Je! Kunatoka kwa Mungu?

MWANAMUME huyo alikuwa amekuwa mgonjwa kwa miaka 38. “Je! wewe unataka kuwa na afya nzuri?” Yesu akauliza. Kama wewe ungalikuwa mwanamume huyo, je! wewe ungalijibu, ndiyo? Yesu alimwambia: “Inuka, inua machela yako na utembee.” Tokeo la maneno hayo lilikuwa nini? “Mwanamume huyo akawa papo hapo mwenye afya, na yeye akainua machela yake na kuanza kutembea.”—Yohana 5:5-9, NW.

Tendo hodari hilo la ponyo la kimungu lilikuwa moja tu la matendo mengi ambayo Yesu alifanya wakati wa huduma yake ya kidunia. (Mathayo 11:4, 5) Leo waponyaji-kwa-imani wanadai kwamba bado Mungu anafanya maponyo hayo, na wao wanategemezwa na shuhuda za maelfu ya watu ambao wanadai kuwa wameponywa nao.

Tofauti Kubwa-Kubwa

Funzo la Biblia linafunua tofauti kadha kubwa-kubwa kati ya maponyo yanayoripotiwa katika Biblia na yale yanayoripotiwa na waponyaji-kwa-imani leo. Yesu na wanafunzi wake, kwa mfano, hawakutoza kamwe malipo kwa maponyo yao. “Ninyi mlipokea bure, toeni bure,” Yesu akafundisha. (Mathayo 10:8, NW) Hivyo wao walifuata mfano uliowekwa na Elisha, ambaye alikataa zawadi kutoka kwa mwanamume jina lake Naamani ambaye Elisha alimponya ukoma. (2 Wafalme 5:1, 14-16) Basi, wakati waponyaji-kwa-imani wanapotoza malipo kwa utumishi wao, wao wanavunja kanuni hiyo ya Kimaandiko.

Inastahili kuangaliwa pia kwamba maponyo yaliyofanywa katika nyakati za Biblia yalikuwa ama ya papo kwa hapo au yalifanyika katika kipindi kifupi cha wakati. Wakati mtume Petro alipoona mwanamume mmoja “ambaye alikuwa mwenye kulemaa kutoka tumbo la uzazi la mama yake,” yeye aliambia mwanamume huyo: “Katika jina la Yesu Kristo yule Mnazareti, tembea!” Usimulizi unafunua hivi: “Papo kwa hapo nyayo za miguu [ya yule mwanamume mwenye kulemaa] na mifupa ya vifundo vya miguu yake ikafanywa imara; na, akiruka juu, yeye akasimama na kuanza kutembea.” (Matendo 3:1-8, NW) Jisomee wewe mwenyewe mifano mingine kwenye Matendo 5:15, 16 na 14:8-10.

Hata hivyo, maponyo ya kuponya kwa imani leo mara nyingi yanachukua siku kadha, majuma, au hata miezi ili kupata matokeo! Unaostahili kuangaliwa, pia, ni uhakika wa kwamba waponyaji-kwa-imani wanaelekea kukaza fikira juu ya magonjwa yanayopata utendaji wa mwili au wa akili tu, kama vile upofu, kupooza, au uziwi—maradhi ambayo mara nyingine yana msingi wa kiakilini. Anaonelea hivi mpasuaji Paul Brand: “Mara tatizo la kiungo cha mwili likiisha kuwa wazi kwa njia isiyoweza kufanyiwa ubishi—miguu yenye kukosekana, macho, au matundu ya nywele yenye kukosekana—ni mara haba miujiza inapotukia.” Hata hivyo, Yesu aliponya “kila namna ya ugonjwa na kila namna ya kutoweza,” kutia na kasoro zilizoonekana wazi katika viungo vya mwili, kama vile mkono uliokunjamana.—Mathayo 9:35; Marko 3:3-5, NW.

‘Wewe Huna Imani!’

Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu wengi walio na magonjwa makubwa ya kusikitisha wanahudhuria ‘krusedi za maponyo’ na kurudi nyumbani wakiwa wagonjwa zaidi ya wakati wo wote ule. Waponyaji-kwa-imani wanatoa maelezo ya kuondolea mbali kushindwa kwao kwa kudai kwamba, ‘Watu hao hawana imani!’ Hata hivyo, hilo linasikika kuwa jambo la udanganyifu. Kama vile Dakt. William Nolen alivyoonelea: “Tofauti na tabibu yule wa kawaida, mponyaji anayeponya kwa kutumia njia isiyo ya kimwili halazimiki kamwe kupata lawama wakati kuponya kwake kunaposhindwa. Lazima mimi nikiri kwamba ningependa niwe na ule uchaguzi wa kukimbilia udhuru fulani wakati ninapokutana na mgonjwa ambaye mimi siwezi kuponya.”

Wala manabii wa Mungu, Yesu, wala wanafunzi wa Yesu hawakuwa kamwe na uhitaji wa kutoa udhuru wa kwamba mtu asiyejiweza hakuponywa kwa sababu yeye hakuwa na imani. Ni kweli, ukosefu wa imani huenda ukawa ulipunguza hesabu ya watu ambao walijitokeza mbele kuja kuponywa. Lakini kwa wale ambao walijitokeza mbele, sikuzote ponyo kamili lilitokea!—Marko 6:5, 6.

Kwa kweli, katika visa fulani watu ambao kwa wazi hawakuwa na imani waliponywa. Kwa mfano Naamani, yule mkuu wa jeshi la Shamu hakuwa na itikadi kamili kwamba angeweza kuponywa ukoma wake kwa njia ambayo nabii Elisha alielekeza. Ni baada tu ya ponyo lake kwamba yeye alikiri hivi: “Hapa, sasa, mimi kwa uhakika najua kwamba hakuna Mungu ko kote katika dunia ila katika Israeli.” (2 Wafalme 5:11-13,15, NW) Hivyo udhuru usio na uzito wo wote ambao unatolewa na waponyaji-kwa-imani unaanguka kabisa kwa kukosa msingi.

Kuponya​—Zawadi Ambayo Ilipitilia Mbali

Lakini je! si kweli kwamba zawadi za kimuujiza za kuponya zilikuwa kwa wingi miongoni mwa Wakristo wa mapema? (1 Wakorintho 12:9) Ndiyo, lakini kulikuwa na sababu nzuri kwa miujiza ambayo ilitukia huko nyuma. Kwa mileani moja na nusu, taifa la Israeli wa kimwili lilikuwa watu wachaguliwa wa Mungu; lakini katika karne ya kwanza ya Wakati wa Kawaida wetu, taifa la Israeli lilikataliwa kwa sababu ya ukosefu wa imani na mahali palo pakachukuliwa na kundi jipya la Kikristo. Wakristo hawa wa mapema walihitaji msaada unaopita ule wa kawaida ili kuitia nguvu imani yao na kuupa ushuhuda ulimwengu wa nje kwamba wao walikuwa na tegemezo la Yehova Mungu.

Hivyo, zawadi za kimuujiza, kutia na kuponya, zilipewa kwa lile kundi changa la Kikristo. Hizo zilitumika kuwa “ishara” kwa wasio na itikadi na kuwa njia ya kuijenga imani ya wenye itikadi. (1 Wakorintho 14:22) Hata hivyo, karibu miaka elfu mbili baadaye, Ukristo hauwi tena katika utoto mchanga. (Linganisha 1 Wakorintho 13:9-13.) Ni muda mrefu ambao umepita tangu Biblia ilipokamilika nayo inaenezwa kwa mamilioni ya nakala. Kwa hiyo Wakristo wa kweli leo wanaweza kwa urahisi kuelekeza watu wasio na itikadi kwenye kurasa zayo kwa kuunga mkono mambo ambayo wao wanafundisha. Madhihirisho ya kimuujiza hayahitajiwi tena.

Paulo alizidi kuonyesha kwamba zawadi za kufanya matendo yapitayo yale yaliyo asili ya mwanadamu ‘zingeondolewa mbali.’ (1 Wakorintho 13:8, NW) Zawadi hizo zilipokezwa kwa wengine kwa njia ya moja kwa moja na mitume wa Kristo Yesu peke yao au zikapokezwa wao wakiwapo. (Matendo 8:18-20; 10:44-46; 19:6) Baada ya kifo cha mitume, madhihirisho ya kimuujiza yalikoma.

Cyclopedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature kilichotungwa na McClintock na Strong (Buku la 6, ukurasa wa 320) kinaonelea kwamba ni “taarifa isiyobishaniwa kwamba wakati wa mamia ya kwanza ya miaka baada ya kufa kwa mitume sisi tunasikia kidogo au hatusikii lo lote juu ya kufanywa kwa miujiza na Wakristo wa mapema.”

Sababu ya Kujihadhari

Yesu Kristo alionya kwamba wakati ungekuja ambapo wengi wangemwambia: “Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?” na bado Yesu angewaambia wao: “Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.” (Mathayo 7:22, 23) Basi, ni jambo gani linaloleta yale yanayoonekana kama mafanikio katika kufanya “miujiza mingi” ikiwa si roho ya Mungu?

Katika visa fulani, udanganyifu wa kabisa kabisa unaonekana kuwa unahusika. Kwa mfano, The Herald, karatasi yenye habari ya Zimbabwe, iliripoti juu ya watu watatu ambao mponyaji-kwa-imani anayejulikana sana alitangaza kuwa walikuwa wameponywa. Karatasi yenye habari hiyo ilifunua wazi huo kuwa udanganyifu: “Mtoto mmoja bado hawezi kusikia wala kusema; mtoto mmoja hakuwa kamwe kiziwi wala bubu; na mwanamke mmoja ambaye alikuwa kiziwi kabisa bado hawezi kusikia.”

Nyakati nyingine, kuponya kwa imani kunaonekana kuwa kuna tokeo fulani la kumtuliza kwa muda mwenye kuteseka. Katika visa vingine—hasa ambapo kipindi kirefu cha wakati kinapita kabla ya hilo ponyo kujidhihirisha lenyewe—inaonekana kwamba utendaji wa mwili kujiponya wenyewe kiasili unahusika. Katika kitabu Science and the Paranormal, Dakt. William Nolen anadai kwamba “karibu asilimia 80 ya wagonjwa ambao wanakuja kwa [tabibu wa kawaida] wana magonjwa ambayo yamejiwekea yenyewe mipaka—yaani, magonjwa ambayo yatapona yenyewe tu.” Basi, baada ya muda fulani kupita mponyaji-kwa-imani anaweza kwa urahisi kujitwalia sifa kwa ponyo.

Kwa kumaliza, Biblia inaonya kwamba “Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru” katika jaribio la kudanganya. (2 Wakorintho 11:14) Kwenye 2 Wathesalonike 2:9, 10, Paulo alieleza hivi zaidi: “Yule [asiyefuata sheria] ambaye kuja [kuwapo, NW] kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote [“aina zote za miujiza,” The Jerusalem Bible] na ishara na ajabu za uwongo; na katika madaganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea.” Kwa hiyo jihadhari! Mara nyingi kuponya kwa imani kunahusisha ndani nguvu za kishetani! “Nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani,” akaonya Paulo. “Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana [Yehova, NW] na kikombe cha mashetani.”—1 Wakorintho 10:20, 21.

Wakati Mkristo ni Mgonjwa

Kweli, wakati mtu ni mgonjwa, huenda ponyo la kimuujiza likaonekana kama uwezekano wenye kuvutia. Ingawa hivyo, angalia kwamba Epafrodito mfanya kazi mwenzi wa mtume Paulo alikuja kuwa mgonjwa karibu ya kufa. (Wafilipi 2:25-27) Timotheo mwandamani wa karibu wa Paulo ivyo hivyo alitaabishwa na “visa vya mara kwa mara vya ugonjwa.” (1 Timotheo 5:23, NW) Hata hivyo, Paulo hakuponya ye yote wa wanaume hao kimuujiza. Na wakati Paulo alipohitaji matibabu yeye mwenyewe, huenda akawa alitumia utumishi wenye kutolewa na Luka, “yule tabibu mpendwa” ambaye alisafiri pamoja naye.—Wakolosai 4:14, NW.

Vivyo hivyo leo, Mkristo ambaye ni mgonjwa sana anaweza kutafuta msaada wa tabibu mwenye kustahili au mzoeza-mwili, akiepuka kujiingiza-ingiza katika maponyo yanayovuviwa na mashetani au katika utabibu-bandia unaopatikana sana katika nchi nyingi leo. Yeye anaweza pia kusali, si kuomba ponyo la kimuujiza, bali kuomba hekima ya kushughulika na ugonjwa ule. (Yakobo 1:5) Anaweza pia kusihi kwa bidii kwamba Yehova ‘amtegemeze [akiwa, NW] mgonjwa kitandani.’—Zaburi 41:3.

Ni wazi kwamba, linaweza kuwa jambo la kuvunja sana moyo wakati sayansi ya tiba inapokuwa haiwezi kuponya maradhi fulani. Hata hivyo, hata wakati anapokuwa mgonjwa Mkristo lazima ajitahidi ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi,’ si kuruhusu hangaiko juu ya afya lifunike mahangaikio ya kiroho kabisa. (Wafilipi 1:10, NW) Yeye anaweza kujitegemeza kwa tumaini la kuishi chini ya Ufalme wa Mungu wakati “hapana mwenyeji atakayesema, mimi mgonjwa.”—Isaya 33:24; 65:17-19.

Kwa kweli, tumaini hilo la ulimwengu mpya wenye uadilifu ni la thamani kubwa zaidi ya ahadi tupu-tupu za waponyaji-kwa-imani. Fikiria Peter, mwanamume mmoja kipofu anayeishi katika Akumadan, Ghana. Yeye alitumia jumla ya miaka 26 katika makanisa tofauti-tofauti ya kuponya kwa imani akiwa na matumaini ya kwamba upofu wake ungeponywa. Lakini hakuna mponyaji-kwa-imani ambaye alifungua macho yake. Ndipo, alipokuwa bado akihudhuria kanisa moja la kuponya kwa imani, yeye alifikiwa na Mashahidi wa Yehova.

Mashahidi walieleza kutokana na Biblia kwamba chini ya Ufalme wa Mungu ponyo la jumla la hali zote za kutoweza lingetukia. Jambo hilo lilifungua macho ya ufahamu ya Peter. Kwa kujawa na uthamini wa kweli nzuri ajabu za Biblia, yeye akawa mtangazaji wa wakati wote wa Ufalme wa Mungu na ametumikia akiwa hivyo kwa miaka zaidi ya mitatu! Yeye anatazamia mbele kwenye wakati ambapo kwa njia halisi, “macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.”—Isaya 35:5, 6.

Kwa msaada wa Neno la Mungu, maelfu wengine wamejihurisha wenyewe kutoka kuweka itibari yenye makosa katika waponyaji-kwa-imani.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Ni mara chache sana waponyaji-kwa-imani wanapoponya watu walio na matatizo katika viungo vya mwili

[Picha katika ukurasa wa 7]

Mkristo ambaye ni mgonjwa anasali kuomba nguvu za kuvumilia. Yeye anatazama mbele pia kwenye ulimwengu mpya, ambako “hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki