Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 1/1 kur. 8-9
  • Mtazamo-Kimbele wa Utukufu wa Ufalme wa Kristo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mtazamo-Kimbele wa Utukufu wa Ufalme wa Kristo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Mtazamo-kimbele wa Utukufu wa Ufalme wa Kristo
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
  • Kugeuka Sura​—Wamwona Yesu Katika Utukufu
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kusudi la Kugeuka (kwa Yesu)
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Jinsi Kugeuka Umbo kwa Kristo Kwakuathiri Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 1/1 kur. 8-9

Maisha na Huduma ya Yesu

Mtazamo-Kimbele wa Utukufu wa Ufalme wa Kristo

YESU amesimama akiwa njiani kwenda Kaisaria Filipi, na yeye anafundisha kutano la watu pamoja na mitume wake. Yeye anafanya tangazo hili la kuwagutusha: “Kwa kweli mimi nasema kwenu ninyi kwamba pana baadhi ya wale ambao wanasimama hapa ambao hawataonja kifo hata kidogo mpaka kwanza wao waone yule Mwana wa binadamu akija katika Ufalme wake.”

Yesu angeweza kuwa anamaanisha nini? lazima wanafunzi wawe wanashangaa wakitaka kujua. Karibu juma moja baadaye, Yesu anachukua Petro, Yakobo, na Yohana pamoja naye na wao wanapanda mlima mrefu sana. Inawezekana kuwa ni usiku, kwa kuwa wale wanafunzi ni wenye usingizi. Wakati Yesu anaposali, yeye anageuka sura mbele yao. Uso wake unaanza kung’aa kama jua, na mavazi yake yanakuwa maangavu kama nuru.

Ndipo, maumbo mawili, yanayotambulishwa kuwa “Musa na Eliya,” yanatokea na kuanza kuambia Yesu juu ya ‘mwondoko wake ambao utatukia kule Yerusalemu.’ Mwondoko huo kwa wazi unamaanisha kifo cha Yesu na ufufuo utakaofuata baada ya hapo. Hivyo, maongezi hayo yanathibitisha kwamba kifo chake chenye kunyenyekeza si jambo la kuepukwa, kama vile Petro alivyokuwa ametamani.

Sasa wakiwa macho kabisa, wale wanafunzi wanatazama na kusikiliza kwa mshangao mkubwa. Ingawa hii ni njozi, inaonekana kama halisi sana hivi kwamba Petro anaanza kushiriki katika ile tamasha, akisema: “Bwana, ni vizuri kwetu sisi kuwa hapa. Ikiwa wewe unataka, mimi nitasimamisha mahema matatu hapa, moja kwa ajili yako wewe na moja kwa ajili ya Musa na moja kwa ajili ya Eliya.”

Wakati Petro anapokuwa akisema bado, wingu jangavu linawafunika, na sauti kutoka lile wingu inasema: “Huyu ni Mwana wangu, yule mpendwa, ambaye mimi nimekubali; sikilizeni yeye.” Kwa kusikia ile sauti, wale wanafunzi wanaanguka kifudifudi. Lakini Yesu anasema: “Inukeni na msiwe na woga.” Wakati wao wanapofanya hilo, wao hawaoni mtu isipokuwa Yesu.

Wakiwa njiani kuteremka mlima siku inayofuata, Yesu anaamuru: “Msiambie mmoja ye yote ile njozi mpaka yule Mwana wa mtu ainuliwe juu kutoka kwa wafu.” Mwonekano wa Eliya katika ile njozi unatokeza swali katika akili za wanafunzi. “Kwa sababu gani,” wao wanauliza, “waandishi wanasema kwamba Eliya lazima aje kwanza?”

“Eliya tayari amekwisha kuja,” Yesu anajibu, “na wao hawakumtambua yeye.” Hata hivyo, Yesu anasema juu ya Yohana yule mbatizaji, ambaye alitimiza fungu la kazi linalofanana na la Eliya. Yohana alitayarisha ile njia kwa ajili ya kuja kwa Kristo, kama vile Eliya alivyofanya kwa ajili ya Elisha.

Njozi hiyo inathibitika kuwa yenye kutia nguvu kama nini, kwa wote Yesu na wanafunzi wale! Ile njozi ni, kama inavyoweza kusemwa, utangulizi wa maono ya utukufu wa ufalme wa Kristo. Wale wanafunzi ni kama kwa kweli waliona yule “Mwana wa mtu akija katika ufalme wake,” sawasawa na vile Yesu alikuwa ameahidi juma moja mapema. Baada ya kifo cha Yesu, Petro aliandika juu ya wao kuwa walikwisha ‘kuwa mashahidi wenye kujionea kwa macho utukufu wa adhama ya Kristo wakati sisi tulipokuwa pamoja na yeye katika ule mlima mtakatifu.’

Mafarisayo walikuwa wamedai kutoka kwa Yesu ishara ya kuthibitsha kwamba yeye alikuwa ndiye mmoja yule aliyeahidiwa katika Maandiko kuwa Mfalme mchaguliwa wa Mungu. Wao hawakupewa ishara yo yote kama hiyo. Kwa upande ule mwingine, wanafunzi wa Yesu wenye uhusiano wa ndani na yeye wanaruhusiwa kuona mgeukosura wa Yesu kama uhakikisho wa maunabii ya Ufalme. Hivyo, baadaye Petro aliandika: “Kwa hiyo sisi tunalo neno la unabii lililohakikishwa zaidi.” Mathayo 16:28–17:13; Marko 9:1-13; Luka 9:27-37; 2 Petro 1:16-19, NW.

◆ Ni jinsi gani watu fulani waliona Kristo akija katika Ufalme wake kabla ya wao kuonja kifo?

◆ Katika ile njozi, Musa na Eliya waliongea na Yesu juu ya nini?

◆ Kwa sababu gani njozi hii ilikuwa msaada wenye kutia nguvu wanafunzi wale?

[Picha ya ukurasa nzima katika ukurase wa  9]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki