Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 1/1 uku. 19
  • Watoto-Mashahidi wa Shule Wapongezwa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto-Mashahidi wa Shule Wapongezwa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Mwalimu Abadili Maoni Yake
    Amkeni!—2009
  • Kumsifu Yehova Shuleni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Ninawezaje Kuwa na Uhusiano Mzuri na Mwalimu Wangu?
    Vijana Huuliza
  • Watoto wa Shule wa Naijeria Wabarikiwa kwa Ajili ya Uaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 1/1 uku. 19

Watangazaji wa Ufalme Waripoti

Watoto-Mashahidi wa Shule Wapongezwa

JE! WEWE, kama mwanafunzi katika shule, unaogopa-ogopa juu ya kusema wazi kutetea imani yako? Mambo yaliyoonwa yaliyo hapa chini yanafunua kwamba Mashahidi vijana hawa hawakuogopa kutegemeza imani yao ya Kikristo na wakapongezwa kwa kufanya hivyo.

◻ Kwenye shule moja katika Australia, wanafunzi walipewa mgawo kuandika insha juu ya Krismasi, lakini mwalimu alisema kwa Shahidi mmoja wa miaka 11 hivi: “Mimi najua wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova, kwa hiyo huwezi kuandika juu ya miadhimisho ya Krismasi. Wewe unaweza kuandika insha tofauti juu ya ‘Historia ya Krismasi.’” Dada kijana yule alikusanya insha yake, akitumia habari zinazofaa kutokana na vichapo vya Sosaiti na vitabu vingine vya marejezo. Kwa mshangao wa darasa, mwalimu alieleza kwamba habari hizo zilikuwa nzuri kabisa na sahihi kihistoria. “Kati ya insha zote ambazo mimi nimepokea, yako ndiyo iliyo bora zaidi katika darasa,” akasema mwalimu. Kwa tokeo la jambo hilo, Shahidi yule kijana aliangusha broshua moja ya Shule, magazeti 15, kitabu kimoja cha Ujana, na vitabu viwili vya Kuishi Milele kwa mwalimu wake na wanafunzi wenzake.

◻ Katika shule nyingine katika Australia, watoto-Mashahidi wanane walisimamiwa na mwalimu-mbadala kila alasiri kwa majuma matatu ya mwisho-mwisho wa masomo ya shule, kwa kuwa wao hawakushiriki katika utendaji mbalimbali wa Krismasi. Baadaye mwalimu huyo wa kike alimweleza hivi mama ya baadhi ya watoto hao: “Sehemu ambayo mimi nilishiriki ilikuwa kidogo. Hesabu kubwa kidogo ya walimu wamekuja na kuuliza ni jinsi gani mambo yanavyoendelea. Mimi nimewaambia: ‘Si kitu hata kama ninyi mnafikiri nini juu ya dini yao na njia ambayo wao wanajiondoa katika utendaji fulani-fulani, hiki ndicho kikundi cha watoto wazuri zaidi ambao mimi nimepata kufanya kazi nao.’” Majuma machache baadaye wakati mwanamke huyo alipofikiwa katika huduma ya nyumba kwa nyumba, yeye alisema: “Na kabla sijasahau, je! ninyi mliwapasha wengine habari ambazo nilisema juu ya wale watoto shuleni? Mimi nataka kila mtu ajue.”

◻ Kutoka United States linakuja hili jambo lililoonwa la mwanafunzi-msichana wa miaka 17 wa kidato cha nne katika shule ya sekondari ambaye alikuta darasa lao la somo la sheria likiwa limejihusisha sana katika mazungumzo juu ya haki zinazohusiana na uhuru wa dini na mtenganisho wa kanisa na Serikali. Mbili za kesi zenye kuhusika zilikuwa juu ya Mashahidi wa Yehova na lile suala la damu. Dada kijana yule aliiona ripoti hiyo iliyokuwa ikizungumzwa kuwa yenye kupendelea upande mmoja na isiyo haki kwa habari ya kweli za Biblia juu ya damu na akaambia mwalimu wake hivyo. Mwanamume huyo alijibu kwa kumpa dada nafasi ya kuhutubia darasa. Kabla ya hotuba yake, wanafunzi walifikiria kwamba mahakama zilikuwa zimefanya uamuzi unaofaa katika kulazimisha Mashahidi watiwe damu mishipani bila ya wao kutaka. Lakini baada ya kusikia hoja ile yenye msingi wa Biblia, darasa lile lilipiga kura ya wote pamoja dhidi ya maamuzi ya mahakama. Dada yetu alifurahi wakati wengi wa wanafunzi wale walipomfikia na kuomba habari zaidi kuhusu itikadi za Mashahidi wa Yehova. Yeye sasa anasema anathamini kwa ukamili zaidi kwamba shule ni eneo lake la pekee.

Ndiyo, ninyi watoto wa shule mna eneo lisilo na kifani. Kwa kadiri ambavyo ninyi mnakuwa na nafasi, endeleeni kwa fadhili kuwasaidia wanafunzi wenzenu wajifunze juu ya lile kusudi zuri ajabu la Mungu, na ninyi mtapata pongezi si kutoka kwa wengine tu bali kutoka kwa Yehova mwenyewe!—Ayubu 40:14.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki