Maswali Kutoka kwa Wasomaji
■ Kwa sababu gani ni wachache sana wa Mashahidi wa Yehova ambao wanashiriki sehemu ya ule mkate na ile divai kwenye mwadhimisho wa kila mwaka wa Chakula cha Jioni cha Bwana?
Hiyo ni kwa sababu, tofauti na yale makanisa ya Jumuiya ya Wakristo, Mashahidi wa Yehova wanakubali lile fundisho la Biblia kwamba hesabu ndogo ya wanadamu itapata uhai wa kimbingu na wale wengine wa watumishi waaminifu wa Mungu watathawabishwa kwa uhai wa milele duniani.
Makanisa yamefundisha kwa muda mrefu kwamba mbinguni ndiyo thawabu kwa wote ambao wanafurahisha Mungu; wale wengine wote wanaenda kwenye moto wa mateso. Biblia inasema vingine. Maandiko yanaonyesha kwa uwazi kwamba ni wanadamu fulani tu, kama vile mitume, ambao watatawala pamoja na Kristo mbinguni. Yesu alisema kwamba hao ni “kundi dogo.” Biblia inasema kwamba hesabu yao ni 144,000. (Luka 12:32; Ufunuo 14:3, 4) Wengi ambao walitumikia Yehova kwa uaminifu na wakawa na kibali chake walikufa kabla Yesu hajafungua ile njia ya kwenye uhai wa kimbingu. (Mathayo 11:11; Waebrania 10:19-21) Na baada ya ule uchaguzi wa wale “kundi dogo,” mamilioni ya wengine wamekuwa Wakristo wa kweli. Kwa washikamanifu wote hao ambao si wa lile “kundi dogo,” Biblia inatoa mbele yao lile tazamio la uhai usio na mwisho katika paradiso ya kidunia iliyorudishwa. (Zaburi 37:20, 29; Ufunuo 21:4, 5) Lakini ni kwa sababu gani watu hao hawashiriki sehemu ya ule mkate na divai pia? Yesu alionyesha kwamba kushiriki sehemu ya ile mifano wakati wa kile Chakula cha Jioni cha Bwana kulikuwa kwa wale tu ambao wameitwa kwenye uhai katika mbingu, wale ambao wamo katika lile agano jipya.
Bila shaka, imani katika dhabihu ya Yesu ni ya muhimu kwa wote ambao wangepata msamaha wa Mungu na uhai wa milele, uwe ni uhai mbinguni au uhai katika dunia-paradiso. Kristo alionyesha jambo hilo kwenye Yohana 6:51-54, NW: “Mimi ndimi mkate hai ambao ulikuja chini kutoka mbinguni; ikiwa ye yote anakula baadhi ya mkate huu ataishi milele; . . . mkate ambao mimi nitatoa ni mnofu wangu kwa niaba ya uhai wa ulimwengu [wa aina ya wanadamu wenye kukomboleka] . . . Yeye ambaye anajilisha mnofu wangu mimi na kunywa damu yangu mimi ana uhai wa milele.”
Hata hivyo, inastahili kuangaliwa kwamba Yesu alisema maneno hayo kwa wengine zaidi ya wanafunzi wake tu. Siku moja baada ya yeye kuwa amelisha maelfu kimuujiza, lile kutano la watu lilikuja kwa Yesu katika eneo la Kapernaumu. Kutano hilo la watu lilimhusisha yeye katika maongezi ambayo yalitia ndani maneno yake kwenye Yohana 6:51-54. Kwa hiyo Yesu hakuwa akisema hasa kwa wanafunzi wake wakati yeye aliposema kwamba yeye alikuwa ndiye ule ‘mkate ambao ulikuja chini kutoka mbinguni’ ulio wa mfano, ambao unaweza kuandaa matazamio ya uhai yenye kudumu zaidi ya ile mana ambayo ilikuwa imeliwa katika lile jangwa.—Yohana 6:24-34.
Katika kufikiria tukio hilo la kale katika iile jangwa, kumbuka ni nani ambao waiikuwa wametoka Misri kuingia katika lile jangwa. Walikuwa ni ‘wale wana wa Israeli wenye hesabu ya wanaume makakawana mia sita elfu wenye kutembea kwa miguu, bila kutia ndani wadogo-wadogo, na andamano-mchanganyiko lililo kubwa sana.’ (Kutoka 12:37, 38; 16:13-18, NW) Hilo “andamano-mchanganyiko” lilitia ndani Wamisri ambao walikuwa wameolewa na Waisraeli na Wamisri wengine ambao walikuwa wametupa kura yao pamoja na Waisraeli. Wote Waisraeli na lile “andamano-mchanganyiko” walihitaji mana ili kubaki hai. Ingawa hivyo, je! hilo “andamano-mchanganyiko,” lilikuwa na matazamio yale yale kama Waisraeli? Sivyo, hawakuwa nayo. Hata ingawa wao wangeweza kuabudu miongoni mwa Waisraeli na wangeweza kutumainia kuingia ile Nchi ya Ahadi, wao hawangeweza kamwe kuwa wafalme au makuhani chini ya lile agano la Sheria. Kwa hiyo kula ile mana halisi katika lile jangwa hakukumpa kila mmoja matazamio yale yale mamoja.
Huo ni mtofautisho wa kukumbuka wakati wewe unapofikiria mambo ambayo Yesu alisema kwa wanafunzi wake yapata mwaka mmoja baada ya yeye kusema yale maneno katika Yohana 6:51-54. Katika pindi hiyo ya baadaye, Yesu alikuwa akisimulia zoea jipya lenye kuhusisha ndani mkate na divai halisi ambavyo vingefananisha mnofu na damu yake. Wakati yeye alipokuwa akianzilisha ule mwadhimisho wa Chakula cha Jioni cha Bwana, Yesu alisema kwa wafuasi wake wa karibu hivi: “Kikombe hiki kinamaanisha lile agano jipya kwa uwezo wa damu yangu, ambayo itamwagwa chini kwa ajili yenu.” Kwa kikundi kidogo kile kile cha mitume, yeye aliongeza hivi: “Ninyi ndio wale ambao wameambatana pamoja na mimi katika majaribu yangu; na mimi nafanya agano pamoja na ninyi, kama vile Baba yangu amefanya agano pamoja na mimi, kwa ajili ya ufalme, ili mpate kula na kunywa katika meza yangu katika ufalme wangu, na kukalia viti vya enzi kuhukumu yale makabila kumi na mawili ya Israeli.”—Luka 22:20, 28-30, NW.
Ona kutokana na maneno hayo ya baadaye kwamba wale ambao wangekula mkate na divai halisi ikiwa ni mifano ya kufananisha mwili na damu ya Yesu ni wale wanafunzi walio katika “lile agano jipya.” Watu hao wangekuwa pia katika agano jingine, moja ambalo Yesu anafanya pamoja na wao ili kwamba wao wangeweza kushiriki utawala ‘katika ufalme wake.’ Kwa uwazi, hapa Yesu alikuwa akirejeza kwa wale ambao ‘wangefanywa kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, kutawala wakiwa wafalme juu ya dunia.’ (Ufunuo 5:10, NW) Katika karne ya kwanza, Mungu alianza kuchagua wale 144,000 ambao wangeshiriki katika ule Ufalme wa kimbingu. Wakristo katika Korintho walikuwa wa kikundi hicho, kwa maana wao walisimuliwa kuwa wale ambao walikuwa ‘wametakaswa katika muungano pamoja na Kristo Yesu, wakaitwa kuwa watakatifu.’ (1 Wakorintho 1:2; linganisha Warumi 1:7; 8:15-17, NW) “Watakatifu” hao wangepaswa kushiriki katika kile Chakula cha Jioni cha Bwana, wakishiriki kutwaa kwa uthamini sehemu ya ule mkate ulio kifananishi na pia ile divai yenye kumaanisha “lile agano jipya kwa uwezo wa damu [yake].”—1 Wakorintho 11:23-26, NW.
Leo limebaki duniani likiwa hai baki dogo tu la wale waliochaguliwa na Mungu kwa ajili ya uhai wa kimbingu. Ni hao tu ambao wamo katika “lile agano jipya” ambao wameruhusiwa kwa mamlaka kushiriki sehemu ya ile mifano, ule mkate na divai, wakati wa mwadhimisho wa kila mwaka wa Ukumbusho.
Bila shaka, Wakristo wote wa kweli leo ambao wanatazama mbele kuishi milele duniani chini ya utawala wa Ufalme wanajua kwamba jambo hilo linawezekana kwa kujizoeza imani katika dhabihu ya Yesu. Kama vile Yesu alivyoambia lile kutano la watu, yeye ndiye “mkate hai ambao ulikuja chini kutoka mbinguni.” (Yohana 6:51, NW) Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba wale waiio na lile tumaini la kidunia wanapaswa kushiriki sehemu ya ile mifano halisi ya Ukumbusho, kwa maana wao hawamo katika “lile agano jipya,” wala wao hawamo katika lile agano pamoja na Yesu kuwa ‘katika ufalme wake, wakiketi juu ya viti vya ufalme.’
Basi, kikundi kikubwa hicho kilicho na matumaini ya kidunia hakishiriki sehemu ya ile mifano, ule mkate na divai. Lakini jambo hilo halionyeshi kwa njia yo yote ukosefu wa imani katika au uthamini kwa mwili na damu ya Yesu. Kwa kweli, kwa sababu ya uthamini wao wa kina kirefu kwa ajili ya dhabihu yake na lile tazamio la kidunia linalopendeza lililo mbele yao, wao kwa uwazi kabisa wanakuwapo kila mwaka wakiwa watazamaji wenye staha kwenye mwadhimisho wa Chakula cha Jioni cha Bwana. Kwa njia hiyo, wao wanaonyesha imani yao wenyewe na kutoa ithibati yenye furaha kwamba lile baki la “kundi dogo” na wale “kondoo wengine” walio umati mkubwa wamo katika umoja mchangamfu.—Yohana 10:16.