Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 2/15 kur. 15-20
  • “Mkate wa Uzima” Upo kwa Watu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mkate wa Uzima” Upo kwa Watu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uandalizi wa Yehova Wenye Upendo
  • “Mkate wa Kweli Kutoka Mbinguni”
  • “Uzima Ndani Yenu Wenyewe
  • “Katika Muungano Pamoja na Kristo”
  • “Nitamfufua Katika Siku ya Mwisho”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Yesu​—“Mkate wa Uzima”
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • “Mkate wa Kweli Kutoka Mbinguni”
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 2/15 kur. 15-20

“Mkate wa Uzima” Upo kwa Watu Wote

“Mimi ndimi ule mkate ulio hai ulioshuka kutoka mbinguni; mtu ye yote akiula mkate huu ataishi milele; na kwa kweli, mkate ambao mimi nitatoa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”​—YOHANA 6:51, Biblia ya New World Translation.

1. Ni hali gani yenye msiba inayoelekea wanadamu leo?

KWA muda mrefu ulimwengu wa wanadamu umelishwa na mkate, chakula kinacholiwa mahali pengi zaidi ulimwenguni. Lakini leo njaa ya mkate imekuwa suala lenye msiba. Sasa njaa na ukosefu mkubwa sana wa chakula inapata robo moja ya wakaaji wa dunia. Hivi majuzi, kichapo The Globe and Mail cha Toronto, Kanada, kilisema, “Ukosefu mkubwa wa chakula, kama vita, hauna mipaka.” Gazeti hilo lilimnakili mtekelezaji wa shughuli za dharura za Umoja wa Mataifa katika Afrika kuwa akionya kwamba Afrika iko ukingoni mwa “moja la maafa makubwa zaidi ya kibinadamu moja la matatizo makubwa zaidi ya kibinadamu, ambalo tumepata kukabiliwa nalo.”

2, 3. (a) Upungufu wa chakula ni sehemu ya ishara gani? (b) Matatizo ya chakula yatatatuliwaje? (c) Ni mambo gani zaidi yanayohitajiwa, na ni uhakikisho gani wenye furaha unaotolewa na Isaya 25:8?

2 Yesu alitabiri kwamba upungufu wa chakula ungekuwa sehemu ya ishara ya kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme. (Mathayo 24:3, 7, 32, 33; 25:31, 32; Luka 21:11) Tunaweza kufurahi kama nini kwamba Ufalme wake umekaribia sana! Karibuni, Mfalme huyo mtukufu atawashinda adui wote wa wanadamu, aondolee mbali hali zote za udhalimu wa kisiasa na kiuchumi ambazo zimeleta taabu hizo zenye kuumiza sana. Ndipo watu wote watakapofurahi sana kupokea mkate wao wa kila siku.​—Mathayo 6:10, 11; 24:21, 22; Danieli 2:44; Mithali 29:2.

3 Chini ya serikali yenye uadilifu, dunia yetu nzuri itaweza kuzaa “mfuriko” wa chakula, kiasi kinachotosha kushibisha watu wengi zaidi ya idadi iliyopo sasa ulimwenguni. (Zaburi 72:12-14, 16, 18, NW) Yehova atafanyia watu wake “karamu” ya vitu vizuri. (Isaya 25:6) Lakini jambo fulani la ziada linahitajiwa. Kadiri miaka inavyoendelea kujisukuma mbele, je, wanadamu bado watakuwa wagonjwa na kufa? Jambo la kufurahisha ni kwamba andiko la Isaya 25:8 linaendelea kusema hivi juu ya Yehova: “Atameza kufa kusiwe tena milele. Na Bwana [Yehova] atapangusa machozi toka nyuso zote.” Jambo hilo linatukiaje?

Uandalizi wa Yehova Wenye Upendo

4. Ni uandalizi gani wenye upendo alioupanga Yehova katika Misri?

4 Yusufu alipokuwa msimamizi wa chakula katika Misri, kulikuwa na utele wa nafaka. Hiyo ni kwa sababu baada ya Yusufu kuwekwa rasmi na.Farao, yeye alitayarisha kwa hekima kwa ajili ya ile miaka saba iliyotabiriwa ya ukosefu mkubwa wa chakula, naye Yehova kwa upendo aliongeza baraka yake. (Mwanzo 41:49) Kulikuwako chakula tele kwa wote na kingine kikasaza. Walipomteremkia Yusufu Misri, Yakobo baba yake, ndugu zake. na jamaa zao, walifaidika sana kutokana na majaliwa hayo ya kimungu, Bila shaka Waisraeli hao wakiwa huko walipata kuzoeana sana pia na mkate uliotengenezwa kutokana na mkando wa ngano iliyochachishwa, kwa kuwa inaonekana asili ya mkate huo ilikuwa Misri.

5. (a) Yehova aliandaaje chakula jangwani? (b) Ni akina nani walioshiriki pamoja na Israeli katika baraka hii, na kwa sababu gani?

5 Baadaye, Yehova alifanyia watu wake uandalizi mwingine wenye upendo. Huo ni wakati ambao mamilioni ya Waisraeli walipoondoka Misri wakapitia jangwa la Sinai. Mkutano mkubwa huo ungeweza kupataje chakula katika jangwa hilo lisilowapa tumaini, la taabu? Ingawa Yehova alikuwa amekasirishwa na ukosefu wao wa imani, “aliifungua ile milango yenyewe ya mbingu. Naye akaendelea kunyesha juu yao mana ya kula, na nafaka ya mbingu aliwapa.” “Kwa mkate kutoka mbinguni aliendelea kuwatosheleza,” kwa muda wa miaka 40 kamili. (Zaburi 78:22-24; 105:40; Kutoka 16:4, 5, 31, 35, NW) Na usisahau kwamba Waisraeli hawakula mana peke yao. “Kundi kubwa la watu waliochangamana nao” wasio Waisraeli lilijizoeza imani katika Yehova likajiunga nao katika kutoka Misri. Mungu aliwapa hao mana pia.​—Kutoka 12:38.

6. (a) Ni uhitaji gani mkubwa zaidi alio nao mwanadamu, na kwa sababu gani? (b) Dhabihu za Israeli zilikazia nini, nazo zilitangulia kuwa kivuli cha kitu gani?

6 Lakini, wanadamu sikuzote wamekuwa na uhitaji mkubwa kuliko “mkate kutoka mbinguni” ulio wa halisi. Hata wale waliokula mana iliyoandaliwa kimuujiza walizeeka wakafa, kwa maana udhambi aliourithi mwanadamu unafanya kifo kiwe kisichoepukika, hata awe anakula vitu vya namna gani. (Warumi 5:12) Dhabihu za Israeli ziliandaa njia ya kudumisha uhusiano mwema pamoja na Mungu, lakini dhabihu hizo zilikazia pia udhambi wa taifa hilo. ‘Hazikuweza wakati wo wote kuondoa dhambi kabisa.’ Tena, matoleo hayo yalitangulia kuwa kivuli cha “dhabihu moja” ya Yesu, ambayo inafanya uandalizi wa kuondoa dhambi “daima.” Akiwa kwenye cheo chake kilichotukuzwa mbinguni, sasa Yesu anaweza kuutendesha kazi ustahili wa dhabihu hiyo​—Waebrania 10:1-4, 11-13, NW.

“Mkate wa Kweli Kutoka Mbinguni”

7. (a) Maneno ya Yesu katika Yohana sura ya 6 yanapasa kuonwa kulingana na hali gani mpya inayohusiana na sura hiyo? (b) Kwa sababu gani Yesu aliukemea mkutano wa watu?

7 Sasa tugeuze fikira kwenye Yohana sura ya 6. Maneno ya Yesu hapa si mwendelezo wa yaliyoandikwa katika sura ya 5. Hali ni tofauti, kwa maana mwaka mwingine mmoja umepita. Sasa ni mwaka 32 W.K. Yanayohusika hapa hayatendeki miongoni mwa Wayahudi wenye kujiona kuwa waadilifu katika Yerusalemu bali ni miongoni mwa watu wa kawaida tu katika Galilaya. Ni muda mfupi tu umepita tangu Yesu afanye muujiza wa kulisha wanaume 5,000 kutokana na mikate mitano ya shayiri na visamaki viwili. Kesho yake, mkutano wa watu unamfuata Yesu, wakitazamia mlo mwingine wa bure. Kwa hiyo Yesu anawaambia: “Ninyi mnanitafuta, si kwa sababu mliziona ishara. bali kwa sababu mlikula kutokana na ile mikate mkatosheka. Fanyieni kazi, si chakula kile kiharibikacho, bali chakula kile kibakicho kwa uzima wa milele.” Yesu alikuwa ametumwa na Baba yake kuandaa chakula cha namna hiyo kwa ajili ya wote ambao wangejizoeza imani katika yeye. Huo ungekuwa ndio “mkate wa kweli kutoka mbinguni,” ukiwa na faida zenye kudumu zaidi ya ile mana halisi waliyokula Waisraeli wa kale.​—Yohana 6:26-32, NW.

8. Mtu anaweza kuufikiaje uzima wa milele?

8 Yesu anaendelea kueleza faida zinazoweza kupatikana kwa “chakula” hicho, akiwaambia hivi: “Mimi ndimi ule mkate wa uzima. Yeye anayenijia mimi hataona njaa hata kidogo, na yeye anayejizoeza imani katika mimi hataona kiu kamwe. . . . Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mtu amwonaye Mwana na kujizoeza imani katika yeye awe na uzima wa milele, nami nitamfufua yeye ile siku ya mwisho.”​—Yohana 6:35-40, NW.

9, 10. (a) “Mkate wa uzima” unatofautianaje na mana? (b) Kulingana na Yohana 6:42-51, Yesu alitolea nani mwili wake? (c) Ni jinsi gani wao ‘wanaula mwili wake’?

9 Wayahudi hao wenye kuona mambo kwa maoni ya kimwili tu wanaanza matata kutokana na maneno hayo. Wanamwona Yesu kuwa mwana asiye mashuhuri wa Yusufu na Mariamu. Yesu anawaonya hivi: “Acheni kunung’unika miongoni mwenu wenyewe. Hakuna mtu anayeweza kunijia mimi isipokuwa kama Baba, aliyenituma mimi, amvuta yeye; nami nitamfufua yeye katika ile siku ya mwisho.” Halafu anarudia hivi: “Mimi ndimi ule mkate wa nzima. Baba zenu wa zamani waliila mana katika jangwa na bado wakafa. Huu ndio mkate unaoshuka kutoka mbinguni, ili kwamba mtu ye yote apate kuula na asife. Mimi ndimi ule mkate ulio hai ulioshuka kutoka mbinguni; mtu ye yote akiula mkate huu. ataishi milele; na, kwa uhakika, mkate ambao mimi nitampa ni mwili wangu kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.”​—Yohana 6:42-51, NW.

10 Hivyo, ni kwa ajili ya “uzima wa ulimwengu”​—ulimwengu mzima wa wanadamu wanaokomboleka​—kwamba Yesu aliutoa mwili wake. Na “mtu ye yote” wa ulimwengu wa wanadamu anayekula “mkate” huo wa mfano, kwa kuonyesha imani katika uwezo unaokomboa wa dhabihu ya Yesu, anaweza kuingia katika njia ya uzima wa milele. Hapa, “kundi kubwa la watu waliochangamana” ambalo lilishiriki pamoja na Waisraeli kuila mana jangwani lilitangulia kuwa kivuli cha mkutano mkubwa wa “kondoo wengine” wa Yesu ambao, pamoja na mabaki wapakwa mafuta wa “Israeli wa Mungu,” wanakula sasa mwili wa Yesu kwa njia ya mfano. Wanafanya hivyo. kwa kujizoeza imani katika dhabihu.yake.​—Wagalatia 6:16; Warumi 10:9, 10.

11. Ni maneno gani zaidi ya Yesu yaliyoshtua Wayahudi, na kwa sababu gani?

11 Kule Galilaya, wengi wa wasikilizaji wa Yesu wanashtuliwa na hotuba yake. Kwa hiyo anapokuwa bado akizungumza juu ya mwili wake, anaongeza maelezo mengine, akiwaambia: “Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywua damu yake, hamna uzima ndani yenu. Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.” (Yohana 6:53-55) Ni jambo la kushtua sana! Si kwamba tu wazo la kula binadamu m la kuchukiza sana kwa Wayahudi hao bali Torati kwenye Mambo ya Walawi 17:14 (NW) ilikataza kwa uthabiti kula “damu ya mwili wa aina yo yote.”

12. (a) Hapa Yesu anakazia nini? (b) Ni maandiko gani yanayoonyesha kwamba jambo hilo haliwahusu warithi washirika wa Yesu peke yao?

12 Bila shaka, hapa Yesu anakazia kwamba ni lazima mtu ye yote anayetaka kuufikia uzima wa milele afanye hivyo kwa msingi wa kujizoeza imani katika dhabihu aliyoitoa Yesu baadaye kwa toleo la mwili wake mkamilifu wa kibinadamu na kumwaga damu ya uhai wake. (Waebrania 10:5, 10; 1 Petro 1:18, 19; 2:24) Uandalizi huo si kwa ajili ya warithi washirika wa Yesu peke yao. Ni lazima pia utie ndani “mkutano mkubwa,” wanaoiokoka ‘dhiki kubwa,’ kwa maana “wamefua mavazi yao, na kuyafanya meupe katika damu ya Mwana-Kondoo.” Imani waliyo nayo katika dhabihu ya Yesu, inayoonyeshwa pia na kumtolea Mungu “utumishi mtakatifu,” inafanya wahifadhiwe kuupita wakati wa taabu kubwa kuliko zote ambazo zimewahi kuipata dunia. Vivyo hivyo, Rahabu alitangazwa kuwa mwadilifu na akaokoka wakati Yoshua alipouharibu Yeriko.​—Ufunuo 7:9, 10, 14, 15; Yoshua 6:16, 17; Yakobo 2:25.

“Uzima Ndani Yenu Wenyewe

13. (a) Katika kulinganisha Yohana 5:26 na Yohana 6:53, ni jambo gani linalofaa kuangaliwa? (b) Ni muundo gani wa kisarufi unaopatikana sana katika Kigiriki unaotusaidia kuelewa Yohana 6:53? (c) Kwa hiyo, maana yake nini kuwa na “uzima ndani yenu wenyewe,” na maneno hayo yanahusu nani?

13 Kwenye Yohana 6:53, 54, Yesu anaonyesha kwamba kuwa na “uzima wa milele” ni sawa na kuwa na “uzima ndani yenu wenyewe (NW) Kwa hiyo, kulingana na habari inayohusika hapa, maneno “uzima ndani yenu wenyewe” yanaelekea kuwa yana maana tofauti na ile Yesu aliyoisema katika Yohana 5:26. Maneno yenye muundo wa kisarufi unaofanana na ule unaosema kuwa na “uzima ndani yenu wenyewe” yanaonekana mahali penginepo katika Maandiko ya Kigiriki. Kwa mfano: “Mwe na chumvi ndani yenu wenyewe” (Marko 9:50 NW) na “kupokea ndani yao wenyewe malipo kamili” (Warumi 1:27, NW).a Katika mifano hiyo, kifungu hicho cha maneno hakimaanishi uwezo wa kuwapa wengine chumvi au malipo. Bali, jambo linaloonyeshwa ni kuwa na ukamili au ujazo wa ndani. Hivyo, kulingana na habari zinazozunguka Yohana 6:53, kuwa na “uzima ndani yenu wenyewe” kungemaanisha hapa kuingia mwishowe katika ujazo kamili wa uzima. “Kundi dogo” la warithi wa Ufalme linaingia katika hali hiyo wanapofufuliwa kuingia katika mbingu. Nao “kondoo wengine” ni baada ya mwisho wa miaka elfu, wakati wanapojaribiwa na kutangazwa kuwa waadilifu ili wapate uzima wa milele katika dunia-Paradiso.​—1 Yohana 3:2; Ufunuo 20:4, 5.

14. Ni akina nani wengine watakaofaidika na “mkate kutoka mbinguni,” na jinsi gani?

14 Wengine, pia, wanaweza kufaidika na “mkate kutoka mbinguni.” Yesu alisema hivi juu ya yule ‘anayekula mwili wake na kunywa damu yake’ kisha anakufa: “Nami nitamfufua siku ya mwisho.” Inafahamiwa kwamba Wakristo wapakwa mafuta ambao wanalala katika kifo wanainuliwa inapolia “tarumbeta ya mwisho.” ambayo inapigwa wakati wa “udhihirisho” wa Yesu Kristo katika utukufu wa Ufalme. (1 Wakorintho 15:52; 2 Timotheo 4:1, 8, NW) Lakini namna gani juu ya wale waliotazamiwa kuwa “kondoo wengine” wanaolala katika kifo? Maneno yaliyosemwa na Martha wakati wa kifo cha Lazaro yanafaa kuangaliwa hapa, kwa maana wakati huo Wayahudi wenye kumwogopa Mungu hawakuwa na tumaini jingine isipokuwa ufufuo wa kidunia. Martha alieleza imani yake kwa maneno haya: “Najua ya kuwa [Lazaro] atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.” (Yohana 11:24) Basi sisi tunaoishi sasa wakati wa kuwapo kwa Kristo tunaweza kutumainia kwamba waaminifu walio wa ule “mkutano mkubwa” wanaolala katika kifo watapata ufufuo wa mapema hapa duniani, ili waushiriki tena “mkate kutoka mbinguni,” wakiwa na tazamio la kupata uzima wa milele. Lo, tumaini bora kama nini, tumaini lenye kuhakikishwa na jambo la kwamba Yesu mwenyewe alifufuliwa kwa wafu!—1 Wakorintho 15:3-8.

“Katika Muungano Pamoja na Kristo”

15. Maneno ya Yesu “katika muungano pamoja na Kristo” yanatumika kwa nani, na kwa sababu gani wewe unajibu hivyo?

15 Yesu anaendelea kusema: “Yeye ajilishaye mwili wangu na kunywa damu yangu abaki katika muungano pamoja na mimi, nami katika muungano pamoja na yeye.” (Yohana 6:56, NW) Basi, hivyo ndivyo ilivyo kwa “mtu ye yote” anayejizoeza imani kwa njia hiyo katika dhabihu ya Yesu, akiwa na taraja la kuwa na ‘uzima ndani yake mwenyewe.’ Wote wanaodhihirisha imani ya namna hiyo wanaweza kupata kuwa “katika muungano pamoja na” Yesu. Bila shaka, “mkutano mkubwa,” ulio na matumaini ya kidunia, haumo “katika muungano pamoja na Kristo” katika maana ya kuwa warithi washirika pamoja naye, washiriki wa bibi-arusi wake wanaopokea ufufuo wa kimbingu ulio kama wake. (Warumi 8:1, 10; 1 Wakorintho 1:2; 2 Wakorintho 5:17; 11:2; Wagalatia 3:28, 29; Waefeso 1:1, 4, 11; Wafilipi 3:8-11, NW) Hata hivyo wote walio na matumaini ya kidunia wanaweza, na kwa kweli lazima wawe, katika upatano kamili pamoja na Baba na Mwana kwa kuyajua na kuyatenda ‘mapenzi makamilifu ya Mungu,’ sawa na vile ilivyo kwa lile “kundi dogo?’​—Warumi 12:2, NW; linganisha Yohana 17:21.

16. (a) Ni kwa njia gani za maana wote wanaojizoeza imani katika dhabihu ya Kristo wamo “katika muungano pamoja” na Yesu? (b) Umoja wao wa kusudi na jitihada unaonekana katika jambo gani?

16 Kwa hiyo, thamani ya dhabihu ya mwili na damu ya Kristo inaweza kupatwa na wale wote leo wanaojizoeza imani, na wote wanaojifaidi na thamani hiyo wanaweza, kwa njia zilizo za maana, kuwa “katika muungano pamoja” na Yesu. Wote wanapaswa kuwa sehemu ya jamaa ya ulimwengu mzima ya Yehova Mungu. Katika hizi “siku za mwisho” zilizo hatari, wanafurahia umoja wa ulimwenguni pote wa imani, kusudi, na utendaji. Kwa kujizoeza imani katika Yesu, wanawezeshwa ‘kufanya kazi kubwa’ zenye kuenea zaidi ya zile alizozifanya Yesu hapa duniani. Tena na iangaliwe kwamba mamilioni ya “mkutano mkubwa” sasa ni asilimia 99.7 ya wale wanaofanya kazi ya Yehova wakati huu. (Yohana 14:12; Warumi 10:18) Umoja huo wa kusudi na jitihada unaonekana katika ushahidi mkubwa wa duniani pote na katika jinsi programu za ujenzi za Sosaiti yetu zinavyoungwa mkono kwa moyo wa kupenda. (Zaburi 110:3) Haijulikani ni wangapi zaidi wa ulimwengu wa wanadamu watakaoamini waingie katika umoja huo wenye thamani kubwa. Ripoti ya hivi majuzi inaonyesha kuna Mashahidi watendaji 3,024,131.

17. Ni mambo gani yanayopasa kuthaminiwa na wote wanaohudhuria Ukumbusho?

17 Inatumainiwa kwamba watu wengi wanaopendezwa wataongezea hesabu ya wale watakaohudhuria mwadhimisho wa Ukumbusho mwaka 1986. Mamilioni ya “kondoo wengine” watakuwapo, pamoja na maelfu yanayoendelea kupungua ya lile “kundi dogo”​—wote wakiwa wanathamini sana uandalizi wenye upendo uliofanywa na Yehova kupitia Kristo, wakitambua kwamba mwili na damu ya Kristo ni vitu vya maana sana. Lakini, inawapasa wote wafahamu waziwazi wana msimamo gani. Kuishiriki mifano ya Ukumbusho hakumpi mtu uzima wa milele. Hivyo ni vifananishi vya dhabihu ya Yesu, ambayo kwanza inatumiwa kuhusiana na lije “agano jipya.” Wapakwa mafuta walioingizwa katika agano hilo ndio peke yao wanaoishiriki mifano kwa kufaa. Hakuna kushika mawili. Mtu anakuwa ama yumo ama hayumo katika agano jipya hilo. (1 Wakorintho 11:20, 23-26) Wale wasio katika agano jipya ambao Yesu hakuwaingiza katika agano kwa ajili ya ufalme hawaishiriki mifano ya Ukumbusho. lakini bado wanapaswa kutambua kwamba mwili na damu ya Yesu iliyotolewa dhabihu ni vitu vya maana sana. (Luka 22:14-20, 28-30) Dhabihu hiyo ndiyo njia ambayo kwayo wanaweza kupata uzima wa milele duniani.

18. Ni furaha gani inayotokana na kufahamu wazi-wazi mambo yote yanayomaanishwa na dhabihu ya Yesu?

18 Basi na tuifikilie pindi ya Ukumbusho unaokuja tukiwa tunafahamu waziwazi mambo yote ambayo dhabihu ya Yesu inamaanisha kwa wanadamu. Wale wa “kundi dogo” na wauthamini sana mwito wao, nao mkutano unaoongezeka wa “kondoo wengine” ufurahie sana taraja la kupata duniani ‘uzima ulio mkamilifu ndani yao wenyewe,’ huku wakiuthamini sana muungano walio nao, sasa hivi, pamoja na Baba, Mwana, na ile hesabu inayopungua ya mabaki wapakwa mafuta ambao wangali duniani. Sisi tuna furaha iliyoje kwamba sasa ule “mkate wa uzima” upo kwa watu wote!

[Maelezo ya Chini]

a Ona pia Mathayo 3:9; 9:3; 13:21; Marko 5:30; 6:51; Luka 7:39, 49; 12:17; 18:4; Yohana 5:42; 11:38; Matendo 10:17; 2 Wakorintho 1:9.

Maswali ya Kurudia

◻ Katika mwaka 32 W.K., Yesu alisema juu ya aina gani mbili za mana, kama zilivyoandaliwa kwa ajili ya nani?

◻ Ni akina nani ambao Yesu anakaribisha ‘wajilishe mwili wake na kunywa damu yake,’ nao wanafanyaje hivyo?

◻ Ni nini maana ya kuwa na“uzima ndani yenu wenyewe,” na ni jinsi gani na wakati gani uzima huo unapofikiwa?

◻ Ni furaha gani ambayo wote sasa wanaweza kushiriki kuhusiana na “mkate wa uzima”?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki