Watangazaji wa Ufalme Waripoti
Yehova Abariki Washika-Ukamilifu Katika Saiprasi
YESU alisema kwa wafuasi wake hivi: “Ikiwa wao wamenitesa mimi, wao watawatesa ninyi pia.” (Yohana 15:20, NW) Na Yehova, kupitia nabii Isaya, alisema hivi: “Silaha yo yote ile ambayo itafanyizwa dhidi yako wewe haitakuwa na fanikio.” (Isaya 54:17, NW) Yote mawili ya hayo mafungu ya maneno yamethibitika kuwa kweli katika Saiprasi, ambako Mashahidi washika-ukamilifu wa Yehova ni wenye shughuli nyingi wakihubiri zile habari njema.
◻ “Kanisa Orthodoksi la Ugiriki limekuwa lenye utendaji sana likijaribu kubomoa kazi yetu,” inasema ripoti moja kutoka bara hilo. “Mapadri wanagawa-gawa vikaratasi vinavyotushtaki sisi juu ya mambo ya namna zote na kuwaambia watu waepuke mazungumzo pamoja na Mashahidi wa Yehova. Wao hata wanawazuru watu ambao wanajifunza Biblia pamoja na Mashahidi na kujaribu kuwavunja moyo. Katika Pafo, mwanatheolojia-padri alijaribu kusadikisha watu watatu tofauti waache kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kila mmoja wa watatu hao, akiwa mbali na wale wengine, alialika ndugu fulani kuwa na zungumzo pamoja na mwanatheolojia huyo. Jambo la kufurahisha ni kwamba, wote watatu sasa wanashiriki kwa utendaji pamoja na tengenezo.” Bila shaka, hiyo iliudhi padri yule naye akasema: “Mimi sitafanya tena zungumzo pamoja na Mashahidi wa Yehova.” Mapadri fulani hata walifikia hatua ya kuchapa baadhi ya akina ndugu wakati wao walipokuwa wakifanya huduma. Hata hivyo, kwa kawaida jitihada za viongozi wa kidini zinawarushia moto wao wenyewe, na watu walio wengi zaidi sasa wanachukua msimamo wao kwa ajili ya Yehova.
◻ Ono linalofuata kutoka Saiprasi linaonyesha kwamba kushika ukamilifu chini ya upinzani kunaleta mibaraka. Mume wa mwanamke mmoja aliuawa wakati wa ile vita ya 1974, hiyo ikimwacha akiwa na msichana mdogo wa kulea. Mwanamke huyo aliolewa upya. Alipozinduliwa macho kwa kuona unafiki wa viongozi wa kidini na kutokuwa na uhakika wa wakati ujao, yeye alikubali kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Yeye alifanya maendeleo kwa haraka sana na kuanza kuambia watu wa ukoo wake mambo mema aliyokuwa anajifunza. Upinzani ulianza. Mtihani ulio mkubwa zaidi ulikuja wakati binti yake mwenye umri wa miaka 15 aliposema: “Mimi nimepoteza baba yangu, na ikiwa wewe hutaacha kujifunza pamoja na Mashahidi, mimi nitakukataa kabisa usiwe mama yangu. Mimi nitakuwa yatima.” Hata hivyo, mwanamke huyo aliendelea kujifunza.
Siku moja msichana huyo alitembelea rafiki katika hospitali. Kwenye kitanda cha hospitali kilichokuwa karibu yake, Shahidi mmoja alikuwa akizuru mtu wa ukoo wake wakati padri mmoja alipokuja kuona mgonjwa huyo huyo. Maongezi yalianza kati ya ndugu huyo na padri. Ndugu yule alikuwa mtulivu na mwenye busara, akitumia Biblia kueleza msimamo wake. Kwa upande ule mwingine, padri alikuwa mtaka-ugomvi. Yeye aliinua sauti yake, lakini hakuna hata wakati mmoja alipofungua Biblia. Msichana yule alitazama tamasha ile na akavutwa na fadhili za ndugu yule na uhakika wa kwamba yeye alitumia Biblia. Jioni hiyo hiyo, wakati ndugu yule na mke wake walipomzuru mama ya msichana huyo kwa ajili ya funzo la Biblia, msichana yule alieleza jambo lililokuwa limetukia hospitalini na akawauliza: “Je! ninyi mnaweza kujifunza pamoja nami pia?” Sasa, msichana huyo anajifunza mara mbili kwa juma, na yule mume pia anajifunza. Yule mama ni mhubiri aliyebatizwa.
Kwa kweli, Yehova anabariki watumishi wake washika-ukamilifu katika Saiprasi!
[Picha katika ukurasa wa 7]
Mtume Paulo pia alikutana na upinzani katika Pafo