Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 3/15 kur. 15-18
  • Kutumikia Yehova Tukiwa Wafanya Kazi Wenzake Wenye Kuitibari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutumikia Yehova Tukiwa Wafanya Kazi Wenzake Wenye Kuitibari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Kujizoeza Haki’
  • ‘Penda Fadhili’
  • Mitihani ya Ushikamanifu
  • “Uwe Mwenye Kiasi Katika Kutembea Pamoja na Mungu Wako”
  • Kiasi Kinawafaa Vijana
  • Majibu Yako Ni Nini?
  • Yehova Anataka Nini Kwako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Kiasi Sifa Inayokuza Amani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Kusitawisha Kiasi cha Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • “Hekima I Pamoja na Wenye Kiasi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 3/15 kur. 15-18

Kutumikia Yehova Tukiwa Wafanya Kazi Wenzake Wenye Kuitibari

“Yeye amekuambia wewe, O mwanadamu wa dunia, yaliyo mema. Na Yehova anaomba umrudishie nini ila kujizoeza haki na kupenda fadhili na kuwa mwenye kiasi katika kutembea pamoja na Mungu wako?”—MIKA 6:8, NW.

1. Ni juu ya msingi gani wa Kimaandiko watumishi wote wa Yehova leo wanaweza kuitwa “wafanya kazi wenzi” wake?

MTUME Mkristo Yohana aliandika hivi: “Oneni ni upendo wa namna gani ambao Baba ametupa, ili kwamba sisi tupaswe kuitwa watoto wa Mungu; na ndivyo tulivyo.” (1 Yohana 3:1, NW) Na mtume Paulo alisema juu yake mwenyewe na Apolo mwandamani wake hivi: “Sisi ni wafanya kazi wenzi wa Mungu.” (1 Wakorintho 3:9, NW) Taarifa zote hizo mbili zilifanywa na wafuasi wapakwa-mafuta wa Yesu Kristo, tena ziliwahusu wao. Lakini kwa kanuni zinatumika kwa watumishi wote wa kweli wa Mungu. Kwa hiyo zingeweza kusemwa kwa ufupi hivi: ‘Oneni ni upendo wa namna gani ambao Baba ameweka juu yetu ili sisi tuwe wafanya kazi wenzi wa Yehova.’

2. Kwa sababu gani inawezekana watumishi wa Yehova kuwa wafanya kazi wenzake?

2 Inawezekana jinsi gani kwa wanadamu dhaifu, wasiokamilika, kuwa wafanya kazi wenzi wa Muumba mkuu, ambaye hana mipaka ya nguvu na hekima, aliye mkamilifu katika haki, na aliye kielelezo kizuri kabisa cha upendo-umbo-mtu? Hiyo inawezekana kwa sababu wazazi wetu wa kwanza walifanywa katika mfano na sura ya Muumba na ya mfanya kazi mwenzake, yule Neno, au Logosi. (Mwanzo 1:26, 27; Yohana 1:1) Kwa hiyo wazazi wetu wa kwanza walipewa kipimo fulani cha hekima, haki, nguvu, na upendo. Hiyo ndiyo sababu Yehova angeweza kuambia watumishi wake wa kidunia hivi kupitia nabii wake: “Yeye amekuambia wewe, O mwanadamu wa dunia, yaliyo mema. Na Yehova anaomba umrudishie nini ila kujizoeza haki na kupenda fadhili na kuwa mwenye kiasi katika kutembea pamoja na Mungu wako?”—Mika 6:8, NW.

3. Ni maana gani inayogusiwa kwenye Mika 6:8, na ni mambo gani yanayotakwa kwa mtu kabla yeye hajaweza kuwa mmoja wa wafanya kazi wenzi wa Yehova?

3 Wakati sisi tunaposoma yale maneno, “Yehova anaomba umrudishie nini ila . . . ?” maana inayogusiwa inaonekana kuwa kwamba yale yanayotajwa baada ya hapo yanatoa vizuri muhtasari wa daraka la ‘mwanadamu wa dunia’ kuelekea Mungu na wanadamu wenzake. Kadiri ambayo jambo hilo liko hivyo hasa itaonekana mazungumzo yetu yanapoendelea. Bila shaka, si mtu ye yote tu ambaye anaweza kutembea pamoja na Yehova. Pendeleo hilo limewekwa akibani kwa wale ambao ‘wamekutana naye kwa kuwekeana miadi,’ ikisemwa kwa njia ya mfano. (Amosi 3:3, NW) Jinsi gani hivyo? Kwa jambo la kwamba walikwisha kujitoa wakfu usio na masharti kwa Yehova na wakauonyesha kwa ubatizo katika maji, kama ilivyoonyeshwa katika makala iliyotangulia. Kwa hiyo, Mika 6:8 ina maana gani kwa hao watu mmoja mmoja?

‘Kujizoeza Haki’

4. Kwa msingi, ni nini maana ya “kujizoeza haki”?

4 Kwanza, kuna takwa la “kujizoeza haki.” Sisi wafanya kazi wenzi wa Yehova Mungu, ni lazima tushike dhamiri njema. “Kujizoeza haki” kunamaanisha kwa msingi kutenda yanayofaa, yanayotakwa kwetu na Mungu. Hiyo inamaanisha kwamba ni lazima sisi tutimize wajibu wetu mbalimbali, ule mkubwa zaidi ukiwa ni kumpa Yehova bidii ya kujitolea Yeye peke yake. (Nahumu 1:2) Yeye havumilii ushindani wo wote. Sisi hatuwezi kabisa kuwa watumwa kwa ajili ya mabwana-wakubwa wawili.—1 Wakorintho 10:22; Mathayo 6:24.

5. Yesu Kristo alionyesha jinsi gani kwamba yeye alipenda uadilifu na akachukia uovu?

5 Waaidha, ili “kujizoeza haki,” ni lazima sisi ‘tupende uadilifu na kuchukia uovu,’ kama vile Yesu Kristo alivyofanya. Kwa sababu ya kupenda kwake uadilifu, yeye alijitunza ‘bila hila yo yote, akatengwa na watenda dhambi.’ (Zaburi 45:7; Waebrania 7:26, NW) Na kwa sababu Yesu alichukia uovu, ilikuwa ni kwa ghadhabu yenye uadilifu kwamba yeye aliwashutumu vikali viongozi wanafiki na wenye pupa wa siku yake.—Mathayo 23:13-36; Yohana 8:44.

6. Kwa sababu gani sisi tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kukubali tu akilini kwamba inatupasa kuepuka jambo linalokatazwa kwa sababu ni baya?

6 Kama inavyoweza kuonwa kutokana na kielelezo cha Yesu, haitoshi kupenda uadilifu. Ni lazima sisi tuchukie—ndiyo, tukirihi, tunyarafu, tutake kutapika, tuwe na mchukio wa kukwepa kabisa—lililo baya. Kwa sababu miinamio yetu ya ndani ni mibaya tangu ujana wetu na kuendelea, na mioyo yetu ni midanganyifu na yenye hila, sisi tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kukubali akilini tu kwamba lililo baya limekatazwa. (Mwanzo 8:21; Yeremia 17:9) Sisi tusipopinga vikali maelekeo yenye dhambi na vishawishi, tutajiacha tushindwe na vivutio vyayo. Ni lazima sisi tuwe na ule mchukio wa kukwepa kabisa lililo baya, kama aliouonyesha Finehasi wakati alipotumia mkuki kudunga mwanamume na mwanamke waliounganika pamoja katika ibada ya Baali wa Peori yenye ukosefu wa adili.—Hesabu 25:5-8.

7. Sisi tuna ushuhuda gani kwamba Yehova hatumii watu wo wote walio waovu wawe wafanya kazi wenzake?

7 Yehova hataki kuwatumia na hatawatumia wawe wafanya kazi wenzake watu mmoja mmoja wo wote ambao ni waovu. Jambo hilo linaeleweshwa wazi kwenye Zaburi 50:16-18 (NW), ambapo tunasoma hivi: “Lakini kwa aliye mwovu Mungu atalazimika kusema: ‘Wewe una haki gani kutaja-taja wingi wa virekebishi vyangu, na kwamba wewe upate kuhimili agano langu katika kinywa chako? Kwani, wewe—wewe umechukia nidhamu, na wewe unaendelea kutupa maneno yangu nyuma yako wewe. Wakati wo wote wewe ulipoona mwivi, wewe hata ulipendezwa na yeye; na ushiriki wako ulikuwa pamoja na wazinzi.’”

8. Ni kisa gani kinachokazia suto ambalo sisi tunaweza kusababisha kwa kujiacha tushindwe na utendaji kosa?

8 Huenda sisi tukaendelea kujishughulisha katika utumishi wa Yehova, kuhubiri zile habari njema za Ufalme wa Mungu. Lakini ikiwa sisi si waangalifu sana kujizoeza kujiweza, huenda tukaruka mipaka kwa sababu ya udhaifu mbalimbali wa mnofu na kuleta suto juu ya jina la Yehova. Hivyo, miaka michache iliyopita mzee mmoja alifanya uzinzi pamoja na dada wa kiroho aliyekuwa na mume asiye mwitikadi. Jioni ile ambayo kutengwa na ushirika kwa huyo aliyekuwa mzee kulitangazwa, yule mume mwenye kiruu alipiga hatua za kishindo ndani ya Jumba la Ufalme akiwa na bunduki ya ufyatuzi wa karibu, akafyatua marisaa kuelekea watu hao wawili wenye hatia. Hakuna ye yote wao aliyeuawa, lakini kesho yake hiyo ndiyo iliyokuwa habari ya ukurasa wa mbele katika karatasi-habari iliyo kubwa zaidi ya zote katika United States! Kweli kweli, utendaji kosa unaleta suto.—Mithali 6:32.

9. Kulingana na Mithali 4:23, ni lazima tulinde nini salama, na kwa sababu gani?

9 Basi, kwa kufaa sisi tunashauriwa hivi: “Zaidi ya vyote vinginevyo ambavyo ni vya kulindwa, linda salama moyo wako, kwa kutoka huo ni vyanzo vya uhai.” (Mithali 4:23, NW) Ndiyo, ni lazima sisi tujitie nidhamu wenyewe juu ya mambo ambayo tunaacha mioyo yetu ya usemi wa mfano ikae-kae ikiyawazia. Zaidi na zaidi, televisheni, magazeti, na namna nyingine za vyombo vya utangazaji habari vinakazia mambo yasiyo safi, kutia na pornografia. Basi, ni lazima sisi tuwe wachaguzi juu ya mambo tunayotazama, tunayosikiliza, na tunayosoma. Uwezo wa kibinafsi wa kudhibiti fikira ni wa maana sana! Mathalani, huenda ikawa rahisi kujipatia raha kutokana na kuwazia-wazia katika akili zetu tukifanya mambo fulani ya ngono za kusisimua, mambo ambayo sisi hatungefikiria kujaribu kufanya kwa kitendo katika maisha halisi. (Mathayo 5:28) Lakini mara nyingi kufikiri jinsi hiyo kunatokeza vitendo vibaya. Basi, badala ya akili kukaakaa ikifikiria mambo hayo, acheni tuonyeshe tunda la roho takatifu ya kujiweza na kukaa juu ya mambo yaliyoorodheshwa kwenye Wafilipi 4:8.—Wagalatia 5:22, 23.

‘Penda Fadhili’

10, 11. (a) Ni upambanuzi gani unaoweza kufanywa kati ya uaminifu na ushikamanifu? (b) Mwana wa Mungu alionyesha uaminifu na ushikamanifu jinsi gani?

10 Takwa la pili ambalo limetajwa kwenye Mika 6:8 ni kwamba sisi ‘tupende fadhili.’ Hapa The New English Bible inasema “penda ushikamanifu.” Maelezo ya chini katika New World Translation Reference Bible yanaonyesha kwamba neno la Kiebrania cheʹsedh, ambalo limefasiriwa kuwa “fadhili,” lingeweza pia kufasiriwa kuwa “fadhili za upendo” au “upendo mshikamanifu.” Kulingana na wana-kamusi, “kuwa mshikamanifu kunamaanisha kuzuia kwa uthabiti kishawishi cho chote cha kutoroka au kusaliti.” “Kuwa mshikamanifu kunaongezea kuwa mwaminifu wazo la kutaka kusimama upande wa mtu au kitu na kupigania mtu au kitu hicho, hata dhidi ya magumu mazito.” Kwa kupendeza, katika Maandiko tunapata pia tofauti kidogo katika utumizi wa maneno hayo. Mathalani, neno “ushikamanifu” halitumiwi kamwe juu ya vitu visivyo na uhai. Lakini neno “uaminifu” linatumiwa hivyo tena na tena. Hivyo, mwezi unaitwa “shahidi mwaminifu katika zile anga.” (Zaburi 89:37, NW) Ndipo, pia, maneno ya Mungu yanasemwa kuwa maaminifu, yaani, yenye kutegemeka.a (Ufunuo 21:5; 22:6) Hata hivyo, sifa ya ushikamanifu inahesabiwa kwa Yehova Mungu na watumishi wake wakubaliwa peke yao. Kwa hiyo, kuhusu Yehova, sisi tunasoma hivi: “Kwa mtu mshikamanifu wewe utatenda kwa ushikamanifu.”—2 Samweli 22:26, NW.

11 Mwana wa Mungu alikuwa mwaminifu na mshikamanifu kwa Yehova mbinguni. Duniani, yeye alipita katika mitihani akiwa yule mwanadamu Yesu Kristo na akathibitisha kwa utii wake kwamba yeye alikuwa mwaminifu na mshikamanifu pia akiwa binadamu. Jambo hilo linaonyeshwa na Waebrania 5:7-9, NW, ambapo tunasoma hivi: “Katika siku za mnofu wake Kristo alipeleka juu toleo la dua na maombi rasmi kwa yule Mmoja ambaye aliweza kuokoa yeye kutoka ndani ya kifo, kwa milio mikali ya kupaaza sauti na machozi, na yeye alisikiwa kwa upendeleo kwa sababu ya woga wake wa kimungu. Ingawa yeye alikuwa Mwana, yeye alijifunza utii kutokana na mambo ambayo aliteseka; na baada ya yeye kufanywa mkamilifu akawa mwenye daraka kwa ajili ya wokovu wa milele kwa wote wale wanaotii yeye.”

Mitihani ya Ushikamanifu

12. Nyakati nyingine, huenda ushikamanifu wetu ukatahiniwa na kitu gani, na watu fulani wametendaje kwa kupatwa na mitihani hiyo?

12 Ushikamanifu kwa Yehova Mungu unataka kwamba sisi tuwe washikamanifu pia kwa watumishi wake duniani, Wakristo wenzetu. Mtume Yohana anaelewesha wazi jambo hilo wakati anapotukumbusha hivi: “Yeye ambaye hapendi ndugu yake, ambaye ameona, hawezi kuwa anapenda Mungu, ambaye yeye hajaona.” (1 Yohana 4:20, NW) Makosa ya kutokamilika kwa wengine huenda yakajaribu ushikamanifu wetu katika habari hiyo. Mathalani, wakati watu fulani wameudhiwa, wao wamedhihirisha udhaifu katika ushikamanifu wao kwa tengenezo la Yehova kwa kukaa mbali na mikutano ya Kikristo. Mtihani mwingine wa ushikamanifu wetu kwa ndugu zetu unatokea wakati wale ambao Yehova anatumia kuchukua uongozi wanapokosea katika hukumu. Muda kwa muda, makosa hayo yametumiwa na watu fulani kuwa udhuru wa kuingiwa na udhia na kujitenga na ushirika wa tengenezo lionekanalo la Yehova. Lakini je! mwendo wao unaweza kutetewa kuwa wa haki? Hata kidogo!

13. Kwa sababu gani kujitenga na tengenezo la Yehova si jambo linaloweza kutetewa kuwa la haki, na ni hali gani zinazojitokeza kwa hao wakosa ushikamanifu ili wachague kuzifuata?

13 Kwa sababu gani watu hao hawawezi kutetewa kuwa wana haki ya kuacha tengenezo la Mungu? Kwa sababu Neno lake linatuhakikishia hivi: “Wana amani nyingi waipendao sheria [ya Yehova], wala hawana la kuwakwaza.” (Zaburi 119:165) Waaidha, sisi tunaamriwa ‘tuwe na upendo mwingi sana kwa mmoja na mwenzake, kwa sababu upendo unafunika wingi wa dhambi.’ (1 Petro 4:8; Mithali 10:12, NW) Zaidi ya hilo, tuseme inakuja kuwa kwamba mtu fulani anajitenga mwenyewe na watu wa Yehova. Yeye angeweza kwenda wapi? Je! yeye haelekewi na suala lile lile lililokabili mitume wa Yesu wakati alipowauliza kama wao pia wangetaka kumwacha? Mtume Petro alijibu kwa kufaa hivi: “Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uhai wa milele.” (Yohana 6:68, NW) Hakuna mahali kwingineko kote kwa kwenda isipokuwa kwa “Babuloni Mkuu,” ile milki ya ulimwengu ya dini bandia, au kuingia ndani ya mibano ya “mnyama-mwitu” wa kisiasa aliye wa Shetani. (Ufunuo 13:1; 18:1-5, NW) Sana-sana, wakosa ushikamanifu ambao wameacha tengenezo lionekanalo la Yehova wamefanya shauri moja na wale walio katika “Babuloni Mkuu” mwenye kuvunjia Mungu heshima.

“Uwe Mwenye Kiasi Katika Kutembea Pamoja na Mungu Wako”

14, 15. (a) Neno “kiasi” lina maana zipi? (b) Hapa sisi tunahangaikia maana ipi ya “kiasi,” na kwa sababu zipi? (c) Kwa sababu gani inawapasa Wakristo ‘waweke kadirio lisilopita kipimo juu ya mambo wanayoyaweza au ustahili wao’?

14 Neno “kiasi” lina maana kadhaa. Linaweza kurejeza kwenye kitu ambacho si cha kusingizia tu, “chenye mipaka katika ukubwa, kadiri, au mweneo.” Au linaweza kuwa na maana ya usafi wa tabia, “kufuata mambo yanayofaa katika uvaaji mavazi na katika hali ya kujiendesha.” (1 Timotheo 2:9) Halafu kuna ile maana ya “kiasi” ambayo ndiyo hasa tunahangaikia, yaani, mtu kujua mipaka yake au “kuweka kadirio lisilopita kipimo juu ya mambo anayoyaweza au juu ya ustahili wake.” Sisi hatungeweza kamwe kuwa mmoja wa wafanya kazi wenzi wa Yehova kama tungekuwa na maoni ya kujifikiria ubora unaopita kadiri, tukivuta fikira kwetu wenyewe badala ya kuvuta fikira za kwanza kwa Yehova Mungu.

15 ‘Kuweka kadirio lisilopita kipimo juu ya mambo tunayoyaweza au ustahili wetu’ ndiyo inayoonekana kuwa maana tunayopaswa kuhusianisha na neno la Kiebrania lililofasiriwa “kiasi” kwenye Mika 6:8 (NW). Hiyo ni dhahiri kutokana na njia ambayo neno hilo limetumiwa mahali pale pengine pamoja tu ambapo linapatikana katika Maandiko ya Kiebrania. Kwenye Mithali 11:2 (AW) halitofautishwi na ukosefu wa adili katika ngono bali nakimbelembele, ambacho kinatokanana mtu kujifikiria ubora unaopita kadiri. Hapo tunasoma hivi: “Je! kimbelembele kimekuja? Ndipo kuvunjiwa heshima kutakuja; lakini hekima ina wale wenye kiasi.” Kuwa mwenye kiasi kunaambatana moja kwa moja na kuogopa Yehova, ambako pia kunashirikishwa na hekima. (Zaburi 111:10) Mtu mwenye kiasi anaogopa Yehova kwa sababu yeye anang’amua tofauti kubwa iliyopo kati yake na Mungu, kati ya uadilifu na nguvu za Yehova na kutokamilika kwake na udhaifu wake mwingi. Basi, mtu mwenye kiasi anajifanyia wokovu wake kwa woga na kutetemeka.—Wafilipi 2:12.

16. Ni nini baadhi ya maandiko yanayoonyesha sababu kwa nini Wakristo wanapaswa kuwa wenye kiasi?

16 Kuna sababu nyingi sana kwa nini wafanya kazi wenzi wa Yehova wawe wenye kiasi! Hata tuwe tuna hekima gani, hata tuwe tumejaliwa kuwa na imara gani ya kimwili, au tuwe tuna utajiri gani wa vitu vya kimwili, sisi hatuna sababu za kujisifu. (Yeremia 9:23) Kwa sababu gani sivyo? Kwa sababu ya ile kanuni iliyotaarifiwa kwenye 1 Wakorintho 4:7: “Ni nani anayekupambanua na mwingine? nawe una nini usichokipokea?” Sisi pia hatuna sababu yo yote ya kujisifu kwa sababu ya matunda ya huduma yetu, kwa maana tunasoma nini kwenye 1 Wakorintho 3:6, 7? Hapo Paulo alisema: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.” Maneno ya Yesu kwenye Luka 17:10 yanapasa pia yasaidie kutuendeleza tukiwa wenye kiasi, kwa maana yeye alisema: “Mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.”

17. Kwa sababu gani kuwa na kiasi ndio mwendo wa hekima kweli kweli?

17 Kuwa mwenye kiasi ni mwendo wa hekima kweli kweli. Kiasi kinatuwezesha kutosheka na mahali po pote ambapo sisi tumependelewa kutumikia. Ikiwa sisi ni wenye kiasi, hatutatafuta makuu kwa kujaribu kuonyesha umaarufu wetu, bali tutatosheka kujiendesha wenyewe kuwa “aliye mdogo.” (Luka 9:48) Halafu, pia, sisi tutakuwa na ule mwelekeo wa mtunga zaburi, ambaye alitangaza hivi: “Siku moja katika nyua zako ni bora kuliko elfu moja kwingineko. Mimi nimechagua kusimama kwenye kizingiti cha chini cha mlango katika nyumba ya Mungu wangu badala ya kuzurura-zurura katika hema za waovu.” (Zaburi 84:10, NW) Waaidha, ikiwa sisi ni wenye kiasi, tutakuwa na upendo ambao utatusukuma kuchukua uongozi katika kuonyesha wengine heshima.—Warumi 12:10, NW.

Kiasi Kinawafaa Vijana

18. (a) Kwa sababu gani kiasi kinawafaa vijana hasa? (b) Uhitaji wa kiasi unaonyeshwa wazi na kumbukumbu gani la matendo yanayohusu vijana wa ki-siku-hizi?

18 Hasa inafaa kwamba vijana Wakristo wajipambe wenyewe kwa lile vazi la kiasi. Elihu aliwawekea kielelezo kizuri kama nini! Ingawa yeye alikuwa na majibu yaliyofaa, yeye alikuwa na nia ya kungoja kwa staha mpaka wanaume wenye umri mkubwa zaidi walipokuwa wamesema. (Ayubu 32:6, 7) Mara nyingi, vijana wana maelekeo ya kuhisi kuwa na uhakika-binafsi, ya kutojua sana mipaka yao. Kwa sababu wao wana imara ya kimwili na wamejipatia maarifa fulani, huenda wao wakaelekea kudharau wazee wao. Lakini maarifa si kitu kimoja na hekima, hiyo ikiwa ni utumizi wa maarifa. Kielelezo halisi ni kumbukumbu ya matendo yenye kuhuzunisha ambayo vijana wa ki-siku-hizi wanaweka katika United States. Huko, asilimia 63 ya visa vya wenye kukamatwa kwa uhalifu mkubwa-mkubwa vinahusu vijana wa kufikia miaka 24, na asilimia 30 ni vya wale walio chini ya miaka 18. Pia inaripotiwa kwamba “uendeshaji magari katika hali ya kulewa au ya kutoona vizuri kwa sababu ya dawa za kulevya ndicho kisababishi kikuu cha kifo miongoni mwa Waamerika wa miaka 15-24.” Katika nchi hiyo, “ndoa nyingi zaidi na zaidi za utineja zinamalizika katika talaka,” hali inaripotiwa kwamba “ndoa zitaelekea zaidi kudumu ikiwa bibi-arusi na bwana-arusi wanakuwa wameishi miaka mingi ya kujipatia hekima wakati waendapo kwenye altare.”

19. Ni shauri gani la Kimaandiko ambalo ingewafaa vijana wathamini kwa moyo?

19 Kwa hiyo, ni lenye hekima kama nini shauri la Neno la Mungu! Kwa kufaa, hilo linaagiza vijana waheshimu baba yao na mama yao, na kuwatii katika kila jambo. (Waefeso 6:1-3; Wakolosai 3:20) Hasa inawapasa vijana wathamini kwa moyo lile shauri lenye hekima: “Itibari katika Yehova kwa moyo wako wote na usiegemee juu ya uelewevu wako mwenyewe. Katika njia zako zote mtie yeye maanani, na yeye mwenyewe atafanya vijia vyako viwe vinyoofu.”—Mithali 3:5 6,NW.

20. Ni thawabu gani ambazo watu wote waliojitoa wakfu na kubatizwa wanaweza kutazamia ikiwa wanatii Mika 6:8?

20 Ni thawabu gani ambazo sisi tunaweza kutazamia ikiwa, baada ya kuwa tumeonyesha itibari katika Yehova kupitia wakfu na ubatizo, ‘tunajizoeza haki, tunaonyesha upendo mshikamanifu, na tunakuwa wenye kiasi katika kutembea pamoja na Mungu wetu’? Jambo lililo la maana kupita yote ni kwamba, sisi tutapata kibali cha Yehova kwa sababu ya kutimiza matakwa yake na hivyo tutateremesha moyo wake kwa kushiriki katika utakaso wa jina lake kuu lenye kutia woga. (Mithali 27:11) Waaidha, sisi tutang’amua katika maisha zetu wenyewe ukweli wa ile kanuni ya kwamba “bidii ya kujitolea Mungu ina manufaa kwa mambo yote, kwa kuwa hiyo inatolea ahadi ya uhai wa sasa na ule ambao utakuja.’ —1 Timotheo 4:8, NW.

Majibu Yako Ni Nini?

◻ Kwa kupatana na Mika 6:8, ni nini kinachotakwa ili “kujizoeza haki”?

◻ Ushikamanifu kwa Yehova unahusuje uhusiano wetu na Wakristo wenzetu?

◻ Kwa sababu gani inatupasa tuwe ‘wenye kiasi katika kutembea pamoja na Mungu’?

◻ Kwa sababu gani kiasi kinawafaa vijana Wakristo hasa?

[Maelezo ya Chini]

a Katika sehemu ya magharibi ya United States, kuna chemchemi yenye kurusha maji-moto ambayo, kwa wastani, kwa miaka mingi ililipuka mara moja-moja kila dakika 65. Kwa njia hiyo ilijipatia jina layo, Yenye Uaminifu Tangu Zamani.

[Picha katika ukurasa wa 17]

Je! wewe unalinda salama moyo wako kwa kuwa mchaguzi juu ya mambo utakayotazama, kusikiliza, na kusoma

[Picha katika ukurasa wa 18]

Petro alijua kwamba hakukuwa na mahali kwingineko kwa kwenda kwa sababu Yesu alikuwa na “maneno ya uhai wa milele.”Je! wewe umepiga moyo konde kwa kadiri hiyo hiyo ili ubaki mshikamanifu kwa tengenezo la Yehova?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki