Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 4/15 kur. 10-15
  • Katika Nyakati Zetu Zenye Hofu Ni Nani Unayeweza Kuitibari Kikweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Katika Nyakati Zetu Zenye Hofu Ni Nani Unayeweza Kuitibari Kikweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Itibari Inayopungua
  • Matazamio Mema Yaliyowekwa Pasipofaa
  • Mmoja Aliye wa Kuitibariwa kwa Ukamili
  • Maoni ya Mungu Juu ya Dini ya Ulimwengu
  • Fanya Yehova Awe Itibari Yako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kuwatumaini Wengine Ni Muhimu kwa Maisha Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Unaweza Kuwatumaini Ndugu Zako
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Mtumaini Yehova, Si Mwanadamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 4/15 kur. 10-15

Katika Nyakati Zetu Zenye Hofu Ni Nani Unayeweza Kuitibari Kikweli?

“Msitie itibari yenu katika washarifu, wala katika mwana wa mwanadamu wa dunia, ambaye kwake hakuna wokovu.”​—ZABURI 146:3, NW.

1. Ni nini tabia moja ya wakati wetu, na inaonyesha uhitaji gani?

TULIPOKUWA watoto, tulipoogopa tulienda kwa wazazi wetu wenye kujali ili tupate faraja na himaya kwa sababu tuliwaitibari. Tukiwa watu wazima, tunahitaji pia watu ambao sisi tunaweza kuitibari. Ndivyo ilivyo hasa siku hizi wakati ambapo mambo mengi yenye kuogofya yanatukia. Likieleza juu ya nyakati zetu, karatasi-habari moja ya Ujeremani ilisema: “Kama isivyopata kutukia kamwe, ulimwengu umejaa hofu.” Tena na tena, viongozi wa mataifa, waandikaji wa majarida, na wengine wameeleza hofu zao kuhusu matatizo mazito ambayo aina ya binadamu inakabili sasa.

2. Hofu na ukosefu wa itibari kwa kizazi hiki yalitabiriwa jinsi gani?

2 Maelezo hayo yanaonyesha kile ambacho Yesu Kristo alitabiri juu ya wakati wetu aliposema kwamba ungekuwa sana na “huzuni kuu ya mataifa, wasijue njia ya kutokea, . . . huku wanadamu wakizimia kwa sababu ya hofu na kwa kutazamia mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa.” (Luka 21:25, 26, NW) Biblia ilitabiri kwamba katika hizi “siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa” na kwamba watu wangekuwa ‘wajipenda wenyewe, wasio washikamanifu, wachongezi, na wasaliti.’ Maneno hayo yanaonyesha kwamba tabia moja ya wakati wetu ingekuwa ukosefu mkubwa wa itibari.​—2 Timotheo 3:1-4, NW.

Itibari Inayopungua

3. Kuna ithibati gani kwamba itibari inakosekana katika wakati wetu?

3 Katika nyakati hizi zenye hofu, tunahitaji sana wengine ambao tunaweza kuitibari, watu ambao watakuwa washikamanifu, wenye msaada katika wakati wa uhitaji. Lakini wengi wanahisi kuwa wanakatishwa tumaini na wale ambao waliwaitibari. Karatasi-habari katika bara moja ilitangaza hivi: “Watu Hawaitibari Mengi Ya Mashirika ya Serikali.” Wenye kuitibariwa kwa kadiri ndogo sana walikuwa ni viongozi wa kisiasa na kibiashara. Kutoitibariana kumeongezeka katika jamaa pia, kama inavyothibitiwa na talaka nyingi. Katika mataifa fulani, kuna talaka moja kwa kila ndoa tatu au hata moja kwa kila ndoa mbili. Katika nchi moja, asilimia 70 ya ndoa mpya zote zinapata talaka katika muda wa miaka kumi! Kwa hiyo kuitibariana kunaendelea kukosekana. Kutoitibariana kunachukua mahali pa kuitibariana. Limeacha kuwa lisilo la kikawaida lile elezo la mtu aliyesema: “Mimi siitibari tena mtu yeyote.”

4. Vijana wengi wanaathiriwa na hofu jinsi gani?

4 Kuna ukosefu mwingi sana wa kuitibariana kwa sababu huu ndio wakati wenye hofu kupita nyakati nyinginezo zote katika historia ya kibinadamu. Karne hii imeona vita vya ulimwengu viwili na vingine vingi ambavyo vimepoteza uhai wa watu zaidi ya milioni mia moja. Sasa, silaha za nyukilia zinatisha kufuta kabisa uhai wote duniani. Na jambo hilo linaathiri itibari ya hata walio wachanga sana. Jarida moja la kitiba liliripoti hivi: “Watoto zaidi na zaidi, hata watoto wadogo sana, wanaogofywa na tisho la maangamizi makuu ya kinyukilia.” Karatasi moja ya habari ya Kanada ilisema kwamba sasa kuna “hali ya kupuuza mambo, huzuni, uchungu na hisia ya kutojiweza” katika vijana wengi. Kijana mmoja alisema: “Sisi hatuhisi kamwe kuwa tuna himaya ya watu wazima. Huenda sisi tukakua na kupata kuwa kizazi chenye kupuuza mambo zaidi ya vizazi vyote ambavyo vimepata kuwako.”

5. Huenda ikawa kikundi cha wasio na hatia na wasiojiweza kingehisi jinsi gani, kama kingeweza kusema?

5 Na kikundi kingine cha vijana kingesema nini—kama wangeweza kunena—juu ya kutohisi wanapata himaya ya watu wazima? Tunamaanisha wale ambao wanauawa kwa kutolewa mimba kabla hawajazaliwa. Kadirio moja linaonyesha kwamba hesabu ya mimba zinazotolewa ulimwenguni pote ni kama milioni 55 kila mwaka. Huo ni ubaini ulioje kuelekea sehemu ya wanadamu wasio na hatia na wasiojiweza hata kidogo!

6. Uhalifu umeongezeaje kutoitibariana katika wakati wetu?

6 Kutoitibariana kumeongezeka kwa sababu ya hofu nyingine inayozidi katika siku yetu: hofu ya kuwa jeruhi wa uhalifu. Wengi sasa wanafanya kama mwanamke yule aliyesema kwamba yeye hulala akiwa na bastola chini ya mto wake. Mwanamke mwingine mwenye hofu alisema: “Mimi nachukizwa na jambo hili. . . . Nyanya yangu hakufunga kamwe milango yake kwa kufuli.” Hivyo, tahariri moja ya karatasi-habari katika Puerto Rico ilitangaza hivi: “Wanaofungwa gerezani ni sisi,” ndiyo, katika maskani zetu wenyewe zenye makomeo na zilizofungwa kwa kufuli.” Hofu hizi zina msingi mzuri. Inaelekea kwamba, katika United States, mathalani, mwanamke mmoja katika watatu ataingiliwa kwa nguvu wakati wa maisha yake. Mpasuaji mkuu huko alisema kwamba “Waamerika wapatao milioni nne wanapatwa na jeuri kubwa kila mwaka—kuuawa, kunajisiwa, kupigwa kwa wake, kutendwa vibaya kwa watoto, kuviziwa.” Uhalifu huo ni wa kikawaida katika bara nyingi, hiyo ikizidi kuharibu itibari ambayo watu wanayo katika wengine.

7. Kwa sababu gani hali mbaya za kiuchumi zinachangia kutoitibariana?

7 Katika mataifa yasiyositawi, watu walio wengi wanaishi katika umaskini. Ni wachache wanaoitibari kwamba kuna mtu ye yote atawaondoa katika huo. Rais wa bara moja kama hilo alisema kwamba katika mkoa mmoja, kati ya kila vitoto 1,000 vinavyozaliwa, 270 vinakufa kabla havijawa na umri wa mwaka mmoja. Ni nyumba moja tu kati ya kila 100 iliyo na maji. Serikali ya nchi nyingine inasema kwamba asilimia 60 ya watoto wayo ni wahitaji, na watoto milioni saba walioachwa “wanakua wakiwa wahuni wasioweza kusoma wala kuandika, walioachwa na wasioweza kuajiriwa.” Katika United States, hesabu ya vijana wasio na maskani inakadiriwa kuwa 500,000, lakini watu fulani wanasema tarakimu iliyo halisi ni ya juu zaidi. Ni itibari ya kadiri gani ambayo vijana hao wanaweza kuwa nayo katika wazazi wao, katika jamii, katika sheria na utengemano, au katika ahadi za viongozi?

8. (a) Uthibitifu wa mataifa yaliyo matajiri na uchumi wa duniani pote unatishwa jinsi gani? (b) Wastadi wanaweza kuitibariwa kwa kadiri gani ili watatue matatizo ya kiuchumi?

8 Matatizo ya kiuchumi yanakumba hata mataifa yaliyo matajiri. Hivi majuzi, United States ndiyo ilikuwa na visa vingi zaidi vya kufilisika kwa benki tangu ule Mshuko Mkubwa wa Thamani ya Pesa katika miaka ya 1930. Mtaalamu mmoja wa uchumi aliandika hivi: “Matokeo halisi ni mfumo wa kutunzia fedha ambao ni wenye kuharibika upesi leo kama ulivyokuwa katika miaka ya 1920,” kabla tu haujavunjika-vunjika. Mtazamaji mmoja alinena juu ya “dhoruba yenye uharibifu mkubwa inayoweza kuwa inakaribia” katika uchumi wa ulimwengu. Mwingine alisema: “Hisia ya kuona uharaka inatokea kwa sababu sasa mikazo hiyo katika mfumo wa kimataifa haikaribii tu; imekwisha kuwasili.” Je! wataalamu wa uchumi wanaweza kuitibariwa waongoze mataifa kutoka kwenye matata haya? Mmoja wao alisema kwamba maandishi ya matabiri yao “ni yenye kuogofya sana hivi kwamba hapana shaka kwamba wao sana-sana wanaeneza mvurugo.”

Matazamio Mema Yaliyowekwa Pasipofaa

9. (a) Ni jambo gani limepata matazamio mema yaliyokuwako mwanzoni mwa karne hii? (b) Kwa sababu gani Mashahidi wa Yehova wasingalitaka kutia sahihi katika hati ya Umoja wa Mataifa katika 1945?

9 Yote hayo yanatofautiana kama nini na matazamio mema yaliyokuwako wakati ulimwengu ulipoingia karne ya 20. Kulikuwa kumekuwa na miongo ya amani ya kadiri fulani, na ilihisiwa kwamba amani na ufanisi ungefikia vilele vipya. Lakini katika 1914 Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilivunja-vunja tazamio hilo. Katika 1945, baada ya vita ya ulimwengu ya pili yenye kuogofya zaidi, Mkataba wa Umoja wa Mataifa ulitiwa sahihi. Mataifa yaliandika njozi yao ya kuona ulimwengu wenye amani, ufanisi, na haki, baada ya vita. Ripoti ya hivi majuzi ilisema: “Hati ya mwisho ilitiwa sahihi na nchi 51, zikiwakilisha kila kontinenti, jamii ya watu na dini.” Hata hivyo kulikuwa na dini moja ambayo haikuwakilishwa, wala haikutaka kuwakilishwa, Mashahidi wa Yehova. Wao walijua kwamba ahadi hizo za amani, ufanisi, na haki hazingetimizwa na taifa lo lote la ulimwengu huu wala na shirika lo lote la mataifa hayo, kama vile Umoja wa Mataifa.

10. Uhakika wa mambo ni nini leo kwa kulinganishwa na ile ndoto ya Umoja wa Mataifa kule nyuma katika 1945?

10 Ripoti iyo hiyo inasema: ‘Miaka 40 baadaye linaonekana kuwa jambo linalofaa kuyapitia mambo ya hakika kwa kuyalinganisha dhidi ya yale ya kuwazika tu. Ushuhuda unahuzunisha. Mambo yaliyopo ni ulimwengu uliopungukiwa na haki, uliopungukiwa na usalama, na jeuri yenye kuongezeka. Idadi ya watu inayokosa chakula, maji, nyumba, utunzaji wa afya, na elimu, inaendelea kuwa kubwa bila kubadilika. Jambo hilo halikuwa ndoto katika 1945.’ Inaongeza hivi: ‘Miaka 40 baada ya mataifa kujiunga pamoja kuhakikisha kwamba watu wote wangeweza kuishi bila hofu na upungufu wa vitu, ulimwengu halisi wa miaka ya 1980 ni wenye umaskini unaolemea sana angalau robo moja ya wanadamu. Vifo vinavyohusianishwa na njaa ni vya wastani wa 50,000 kwa siku,’ Hata hivyo, mataifa yanatumia dola zaidi ya milioni mia moja kila saa kwa vita!

11. Ahadi za kibinadamu za ulimwengu bora zinastahili itibari kwa kadiri gani?

11 Kwa sababu ya hali hiyo yenye kuhuzunisha baada ya wanadamu kupata nafasi ya karne nyingi za kutatua matatizo hayo, je! sisi tunaweza kuitibari ahadi za kibinadamu kwamba watatatua matatizo haya? Ustahili wa kuitibariwa kwa ahadi hizo unakaribia kuwa kama yale maneno ya kapteni wa meli kubwa aliyesema hivi: “Mimi siwezi kuwazia hali yo yote ambayo ingesababisha meli [kubwa] izame. . . . Ufundi wa kisasa wa kuunda meli umefanya maendeleo yanayopita kiwango cha kuweza kuzama.” Mshiriki mmoja wa wafanya kazi katika chombo hicho alimwambia hivi baharia mmoja: “Mungu mwenyewe hawezi kuifanya meli hii izame.” Hata hivyo, meli hiyo, ile Titanic, ilizama katika 1912 ikipoteza uhai wa watu 1,500. Katika 1931 Shirika la Kitaifa la Elimu katika United States lilisema kwamba kupitia elimu “uhalifu utakaribia kumalizwa kabisa kabla ya 1950.” Katika 1936 mwanajarida Mwingereza aliandika kwamba “chakula, mavazi, na nyumba vitagharimu kiasi kidogo sana” kufikia 1960. Je! wewe hukubali kwamba magumu ya leo yanaonyesha ahadi hizo zilikuwa uwongo?

Mmoja Aliye wa Kuitibariwa kwa Ukamili

12. Ni nani ambaye sisi tunaweza kuitibari kwa ukamili, na ni mwongozo gani ambao yeye ametupa?

12 Kwa hiyo, tunahitaji sana chanzo ambacho tunaweza kuitibari ili kitusaidie kupitia nyakati hizi zenye hofu. Chanzo hicho hakiwezi kuwa cha kibinadamu. Aina ya binadamu imejiingiza yenyewe ndani ya matatizo makubwa sana hivi kwamba haiwezi kujiondoa humo. Chanzo kinachoweza kuitibariwa kwa ukamili ni Muumba wa wanadamu, Yehova Mungu. Yeye anajua kwa nini ulimwengu umo katika hali yao ya sasa, unaelekea wapi, na yeye atafanya nini kuhusu jambo hilo. Pia amefunua habari hizo katika kitabu ambacho yeye alitupa sisi kiwe mwongozo wetu, Biblia. Juu yacho, 2 Timotheo 3:16, 17 (NW) inasema hivi juu yacho: “Andiko lote liliongozwa na Mungu na ni lenye manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu, ili mtu wa Mungu apate kuwa na uwezo wa kutosha, aliye tayari kabisa kwa kila kazi njema.”

13. Mashahidi wa Yehova wanathamini nini juu ya Biblia?

13 Angalia taarifa hizo zenye mkazo. Neno la Mungu lililovuviwa linanyoosha mambo. Linatuambia yaliyo sawa. Linafanya sisi tuwe na uwezo wa kutosha. Linatuweka tayari kwa ukamili kwa ajili ya yaliyo mema. Ni kweli, watu wengi hawakubali Biblia kama ilivyo—Neno la Mungu. Lakini Mashahidi wa Yehova wanafanya hivyo. (1 Wathesalonike 2:13) Sisi tunathamini kwamba Muumba wa ulimwengu wote mzima wenye kutisha wa mabilioni ya magalaksi na kwintilioni za nyota hakika ana uwezo wa kutunga kitabu. Naye ana uwezo wa kuona kwamba usahihi wacho unahifadhiwa ili wanaotafuta ukweli wanufaike.​—1 Petro 1:25.

14. Biblia inapatana jinsi gani na uhakika wa mambo leo?

14 Katika nyakati zetu zenye hofu, Neno la Mungu linasema nini kuhusu habari hii ya itibari? Maelezo yalo yanapatana kwa ukamili na hali zenyewe zilizopo. Yeremia 10:23 inasema kwa usahihi hivi: “Ee BWANA [Yehova, NW], najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” Na Zaburi 146:3 (NW), inahimiza hivi kwa usawa: “Msitie itibari yenu katika washarifu, wala katika mwana wa mwanadamu wa dunia, ambaye kwake hakuna wokovu.”

15. Ni shauri gani ambalo Biblia inatupa sisi kuhusu itibari?

15 Neno la Mungu linatutia nadhari tusiitibari hata katika sisi wenyewe kwa sababu wanadamu ni wasiokamilika. (Warumi 5:12) Yeremia 17:9 inasema hivi: “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote.” Kwa sababu hiyo Mithali 28:26 (NW) inatangaza hivi: “Yeye ambaye anaitibari katika moyo wake mwenyewe ni mpumbavu, lakini yeye ambaye anatembea katika hekima ndiye ataponyoka.” Ni wapi ambapo sisi tunaweza kupata hekima hii inayoweza kuandaa mponyoko? Mithali 9:10 (NW) inajibu hivi: “Hofu kwa Yehova ndio mwanzo wa hekima, na maarifa ya kujua Mmoja Aliye Juu Zaidi ndio uelewevu.” Ndiyo, ni hekima ya Muumba tu inayoweza kutupa sisi mwongozo tupite katika nyakati hizi zenye hofu. Kwa hiyo, Mithali 3:5, 6 (NW) inashauri hivi: “Itibari katika Yehova kwa moyo wako wote na usiegemee juu ya uelewevu wako mwenyewe. Katika njia zako zote mtie yeye maanani, na yeye mwenyewe atafanya vijia vyako vinyooke.”

Maoni ya Mungu Juu ya Dini ya Ulimwengu

16. Ni dhana gani yenye makosa ambayo dini za ulimwengu huu zinafanya, kama walivyotenda Mafarisayo wakati wa Yesu?

16 Hekima hii kutoka kwa Mungu itatuwezesha tuepuke mtego unaoleta kifo ambamo dini za ulimwengu huu zimetumbukia. Wao wanajidhania kuwa waadilifu kwa sababu ni wanadini. Mwelekeo wao uko sana kama inavyoelezwa kwenye Luka 18:9, AW: “Sasa Yeye [Yesu] akanena kielezi hiki pia kwa watu fulani ambao waliitibari katika wao wenyewe kwamba wao walikuwa waadilifu.” Farisayo mmoja alishukuru Mungu kwamba yeye hakuwa mtenda dhambi, lakini mkusanya-kodi akaendelea kuomba-omba kimaskini hivi: “O Mungu, uwe mwenye neema kwangu mimi mtenda dhambi.” Yesu alisema: “Mimi naambia ninyi, Mwanamume huyu [mtenda dhambi] alishuka kwenda kwenye maskani yake akiwa amethibitishwa kuwa mwadilifu kuliko mwanamume yule [Farisayo]; kwa sababu kila mmoja ambaye anajikweza mwenyewe atanyenyekezwa, lakini yeye ambaye anajinyenyekeza mwenyewe atakwezwa.”​—Luka 18:10-14, NW.

17. Mungu anaziona jinsi gani jitihada za kidini kama za Mafarisayo?

17 Farisayo huyo hakujinyenyekeza mwenyewe mbele za Mungu. Badala ya hivyo, yeye alihisi kwamba kwa viwango vyake mwenyewe alikuwa mwadilifu. Lakini Mungu hakuona mambo jinsi hiyo. (Mathayo 23:25-28) Mtenda dhambi yule mnyenyekevu ndiye alionyesha yanayosemwa na Neno la Mungu kwenye Isaya 66:2: “Lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.” Viongozi wa kidini Wayahudi hawakutetemekea Neno la Mungu. Wao walilipuuza Walifanya yale ambayo wao walitaka kisha wakafikiri kwamba Mungu aliwakubali. Hata hivyo, Yesu aliwaambia hivi: “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”​—Mathayo 7:21-23.

18. Mungu atahukumu jinsi gani dini ambazo zinadai kumtumikia lakini ambazo hazijipatanishi na sheria zake?

18 Hao viongozi wa kidini katika karne ya kwanza hawakuitibari Mungu. Badala ya hivyo, wao walitia itibari yao katika mapokeo yaliyovunja sheria za Mungu. (Mathayo 15:3, 9) Hivyo Yesu aliwaambia: “Nyumba yenu imeachiwa hali ya ukiwa.” (Mathayo 23:38) Kama ithibati ya kwamba kweli Mungu alikuwa ameacha dini yao ya Kiyahudi, katika mwaka 70 wa Wakati wa Kawaida wetu, wao, mji mkuu wa taifa lao, Yerusalemu, na hekalu lao waliharibiwa na majeshi ya Waroma. Mambo si tofauti leo. Dini za ulimwengu huu zimeweka viwango vyazo zenyewe vya ibada ambavyo havipatani na viwango vya Mungu. Hivyo wao hawafanyi mapenzi yake bali yao wenyewe. Kwa sababu hiyo, wanaonekana kuwa wafanya kazi wa uvunjaji sheria machoni pa Mungu. (Tito 1:16) Kama uthibitisho wa kwamba Mungu ameacha dini hizo, karibuni zitaharibiwa na mataifa, sawa na vile Yerusalemu na hekalu lao ulivyoharibiwa na majeshi ya Kiroma katika karne ya kwanza.​—Ona Ufunuo, sura 17, 18.

19. Ni maswali gani ambayo huenda yakaulizwa kuhusu dini?

19 Je! mchanganuo huo kuhusu dini za ulimwengu ni mkali mno? Ni jinsi gani sisi tunaweza kuwa na uhakika kwamba hukumu za Mungu zitakuwa dhidi yao baada ya muda mfupi? Ni mambo gani ambayo lazima dini itende ili ipate kibali cha Mungu? Je! kuna vielelezo vya kihistoria vinavyoonyesha kwamba Yehova anahami wale wanaomgeukia kwa weupe wa moyo na kujiweka chini ya sheria zake? Makala inayofuata itaeleza juu ya maswali haya.

Maswali kwa Ajili ya Kupitia

◻ Ni jambo gani limechangia kutoitibariana katika wakati wetu?

◻ Kwa sababu gani matazamio mema ya ulimwengu huu yalikuwa na mwongozo mbaya?

◻ Ni nani ambaye sisi tunaweza kuitibari kwa ukamili, na ni mwongozo gani ambao yeye ametupa sisi?

◻ Kwa sababu gani haitupasi kuitibari katika sisi wenyewe wala wanadamu wengine?

◻ Ni jinsi gani Mungu anaziona dini za ulimwengu huu?

[Picha katika ukurasa wa 13]

Yule Farisayo alijichukulia kwamba alikuwa mwadilifu, lakini mwanamume yule mwenye dhambi aliombaomba kimaskini rehema ya Mungu kwa unyenyekevu

[Picha katika ukurasa wa 15]

Mungu anazihukumia mabaya dini ambazo hazitendi mapenzi yake, kama alivyoihukumia mabaya dini ya Kiyahudi katika karne ya kwanza wakati majeshi ya Kiroma yalipoharibu Yerusalemu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki