Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 5/1 uku. 7
  • Ukweli wa Biblia ‘Unatokeza Nguvu’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ukweli wa Biblia ‘Unatokeza Nguvu’
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Ushahidi Huzaa Tunda Nyumbani na Shuleni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Sababu kwa Nini Watu wa Namna Zote Wanakuwa Mashahidi wa Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Nguvu Yenye Kugeuza ya Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Umtazame Mtu Mnyofu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 5/1 uku. 7

Watangazaji wa Ufalme Waripoti

Ukweli wa Biblia ‘Unatokeza Nguvu’

ULIMWENGU huu unatumia wakati na pesa nyingi ukijaribu kuzuia vitendo vya watu wabaya. Sheria zinafikilizwa dhidi ya matendo ya uhalifu kama vile utumizi mbaya wa dawa za kulevya, wizi, na uuaji; lakini sheria hizi hazifanyi watu wabaya wawe wema. Kwa upande ule mwingine, Neno la Mungu, Biblia, lina nguvu za kugeuza watu, na wale ambao wanatumia sheria na kanuni zalo wanakuwa watu wanyofu, wafuataji haki, na wapole.​—Warumi 12:2.

◻ Mathalani, Mashahidi wawili katika Australia walifanya ziara ya kurudia kwa wanaume kadhaa vijana, wasioajiriwa kazi. Walipokuwa wakiingia nyumba walimokuwa wanaume hao, walikuja ndani ya chumba chenye giza, kilichojawa na moshi. Kulikuwa na vyombo vya matumizi ya bangi mezani na vibandiko vikubwa vya picha za waimbaji-roki vikiwa vimefuatana-fuatana kwenye zile kuta. Kando-kando ya upande mmoja wa chumba hicho vilikuwapo vipaaza-sauti vikubwa vya gitaa za kutumia umeme. Hicho kilikuwa chumba cha mazoezi ya kikoa cha upigaji muziki wa roki. Wao waliweza kuanza funzo la Biblia pamoja na watatu wa wanaume hawa waliokuwa ndugu za kimnofu. Miaka kadhaa mapema, mama yao alikuwa amejifunza Biblia pamoja na Mashahidi, na kwa msaada wa kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, yeye alikuwa amefundisha wavulana hao juu ya ahadi ya Mungu kuhusu paradiso ya wakati ujao. Ndipo jamaa ile ikahama, na funzo likaachwa. Sasa, upendo wao kwa ukweli ukiwa umefanywa upya, baada ya muda mfupi rafiki zao wawili walijiunga nao katika funzo lao.

Katika muda wa miezi mitatu, mmoja wao alikuwa akitoa ushuhuda, na mwezi mmoja baadaye wengine wawili wakajiunga naye. Waliacha kikoa kile cha muziki, na katika muda wa miezi minne, wote watatu wakawa wanashiriki katika kazi ya kuhubiri. Wakati uo huo, mama yao, ndugu yao mchanga zaidi, na dada yao mkubwa zaidi aliyeolewa walianza kujifunza Biblia. Muda si muda, rafiki mwingine akaomba funzo la Biblia. Ilikuwa shangwe kama nini kuona watano kati yao wakibatizwa siku ile ile moja kwenye kusanyiko la mzunguko! Wengine wawili wanajitahidi kuelekea ubatizo, huku yule mama na binti yake wakiendelea kufanya maendeleo mazuri. Kweli kweli, Neno la Mungu linatokeza nguvu.

◻ Mwanamume mmoja katika Ajentina alikuwa na mwajiriwa-kazi aliyekuwa mvivu na mdanganyifu, naye alikuwa na deni lake la pesa nyingi. Siku moja mfanya-kazi huyo alitoroka. Halafu, baada ya miaka kadhaa, katika barabara moja karibu na maskani yake mwanamume huyo alikutana na aliyekuwa mwajiriwa-kazi wake. Aliyekuwa mwajiriwa-kazi alimsalimu, akisema: “Sasa hivi tu ndio nilikuwa nikienda nyumbani kwako kulipa pesa unazonidai. Hizi ndizo pesa zako. Asante sana, na tafadhali nisamehe kwa kutozirudisha mapema zaidi.” Kwa kushangaa, mwanamume huyo alimuuliza kwa nini alifanya hivyo. Yeye akajibu: “Sasa mimi ninajifunza Biblia, na mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Biblia inasema kwamba haitupasi sisi kuwa na deni la kitu cho chote kwa mtu ye yote isipokuwa upendo. Hiyo ndiyo sababu mimi nimerudisha kilicho chako.” Mwanamume huyo akauliza: “Kwani Biblia ina nguvu gani za kutokeza badiliko kama hilo katika mwanamume?” Funzo la Biblia lilianzwa pamoja naye, na sasa yeye pia anajifunza ukweli, na hayo yote ni kwa sababu ya lile badiliko kubwa ambalo ukweli wa Biblia ulifanya katika huyo aliyekuwa mwajiriwa-kazi wake.

Watu wengi wenye mioyo ya ufuataji haki katika Ajentina wanakubali ukweli wa Biblia wenye kugeuza watu na wanabadili njia yao ya maisha, kama linavyoonyesha jambo lililoonwa lifuatalo.

◻ “Siku moja wakati sisi tulipobisha hodi kwenye mlango mmoja tukiwa katika utumishi,” anasimulia Shahidi mmoja, “tulisikia makelele yakitoka ndani ya nyumba ile. Kwa kujibu hodi yetu, mwanamume mmoja alikuja nje—akiwa amekasirika sana sana. Sisi tulianza kueleza kusudi la ziara yetu, lakini yeye akatisha kuturusha tutoke kwenye eneo lake. Tuliendelea kuongea kwa unyamavu na utulivu. Kidogo kidogo yeye akatulia. Kwa kuona hivyo, sisi tukamweleza mengi zaidi juu ya kusudi zuri ajabu la Yehova kwa ajili ya aina ya binadamu. Kwa kuvutwa na jambo hilo, mwanamume yule akatugutusha kwa kusema: ‘Mungu ndiye amewatuma ninyi hapa.’ Ndipo akatualika tuingie nyumbani. Humo, ‘mke’ na watoto wake walikuwa wamefinyana katika kona moja, wakilia. Ndipo yeye akaungama hivi: ‘Mlipokuja, nilikuwa karibu kuua jamaa yangu na mimi mwenyewe. Nina shida kubwa! Mimi nilipoteza kazi yangu, na sasa wanataka kutuondosha katika maskani yetu, nami nina madeni mengi ya kulipa.’”

Jambo hili lililoonwa lilikuwa na mwisho wenye kufurahisha. Dada mmoja alimtafutia kazi mwanamume huyo, na mwanamume huyo akapata nyumba nyingine. Yeye na “mke” wake walianza kujifunza Biblia na wakafunga ndoa baada ya kuishi pamoja kwa miaka 15.

Ukweli wa Biblia ‘unatokeza nguvu’ kama vile mambo haya yaliyoonwa yanavyoonyesha, na unaweza kufanyia hivyo mtu ye yote aliye na moyo wa unyenyekevu, ambaye atajifunza Biblia na kuitumia.

[Blabu katika ukurasa wa 7]

Neno la Mungu liko hai na linatokeza nguvu.”​—WAEBRANIA 4:12, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki