Wewe Unaalikwa Kwenye “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya
YEHOVA Mungu, Muumba wetu mwenye upendo, ni Mwandalizi Mkuu kama nini! Kweli kweli, “kila zawadi njema na kila upaji mkamilifu” huwa unakuja kutoka kwake. (Yakobo 1:17, NW) Kwa kufaa, katika Zaburi 136 tunasoma mara 26 yale maneno: “Kwa maana fadhili za upendo zake ni kwa wakati usiojulikana.”
Miongoni mwa maandalizi yake mengi ya kiroho kwa ajili ya watu wake wa kale zilikuwamo sikukuu tatu za kila mwaka: Kupitwa na Sikukuu ya Keki Zisizochachwa; Sikukuu ya Majuma, au Pentekoste; na Sikukuu ya Vibanda, au Mkusanyo-ndani. Sikukuu tatu hizo zilionwa kwa mtazamio mkubwa, kwa maana zilikuwa pindi za kujenga kiroho na za shangwe kubwa pia.—Walawi 23:40-43.
Katika nyakati za ki-siku-hizi, vivyo hivyo Yehova Mungu ametia ndani ya mioyo ya watumishi wake kuwa na sikukuu tatu za kiroho za kila mwaka: ile siku ya pekee ya kusanyiko, kusanyiko la mzunguko la siku mbili, na ule mkusanyiko wa wilaya wa siku tatu au nne. Hizo pia zinatumikia kuwa pindi za kujengwa kiroho na za ushirika wenye shangwe nyingi. Kulingana na ripoti zilizopokewa wakati wa kuandika huku, 6,128,388 walihudhuria “Tumaini [Itibari] Katika Yehova” Mikusanyiko ya Wilaya iliyoanza katika Juni 1987, na 85,091 walibatizwa. Mwaka huu kila Shahidi anatazamia kuhudhuria “Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya.
“Haki ya Kimungu” ni kichwa kiadhimu na kisharifu kama nini! Tena ni cha maana kama nini! Kwani, hata wanadamu wasiokamilika wanautaja-taja kimdomo tu umaana wa haki. Hiyo ndiyo sababu wenye kuunda Katiba ya United States yapata miaka 200 iliyopita waliandaa, si matawi ya kiserikali ya ufikilizaji na utungaji sheria tu, bali pia baraza la hukumu ili kwamba ufuataji haki ufanywe. Hata hivyo, karne nyingi kabla ya hapo, Yehova Mungu mwenyewe aliandaa migawanyo mitatu ya serikali, na yote inakaa ndani yake. Hivyo, kwenye Isaya 33:22 (NW) tunasoma hivi: “Yehova ni Hakimu wetu, Yehova ni Mpaji-sheria wetu, Yehova ni Mfalme wetu.”
Kwa uhakika, sisi tunaambiwa kwamba haki ndilo lengo, mradi, au kusudi la serikali. Lakini ingawa wanatambua kanuni hii nzuri sana, wakati unapofika wa kuizoea, wanadamu wabinafsi na wasiokamilika wanapungukiwa kama nini! Namna zote za ubaguzi unaohusu rangi mbalimbali, taifa, na dini ni vielelezo vya visa vingi sana vya uvunjaji wa haki. Na ndivyo yalivyo matumizi yote mabaya ya nguvu, yawe yanafanywa na serikali, mashirika, mabaraza ya kidini, au watu mmoja mmoja.
Sisi tunaweza kuwa wenye shukrani kama nini kwamba Neno la Mungu linatuhakikishia juu ya ushindi wa mwisho kabisa wa haki na uadilifu, kwa maana Yehova ndiye anayewapita wote kwa kuwa Mungu wa haki! Hiyo ndiyo sababu Musa aliimba hivi juu yake: “Yule Mwamba, utendaji wake ni mkamilifu, kwa maana njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye kwake hakuna ukosefu wa haki; yeye ni mwadilifu na mnyofu.” (Kumbukumbu 32:4, NW) Yehova Mungu anastahi sana haki hivi kwamba alitoa Mwanaye mzaliwa wa pekee awe dhabihu ili kwamba Yeye aweze kuiletea uhai wa milele aina ya binadamu yenye utii. (Warumi 3:25, 26) Kwa kufaa, Yehova anapendelea wale ambao ni wapenda haki na uadilifu, hata kama vile tunavyosoma kwenye Zaburi 11:7, NW: “Yehova ni mwadilifu; yeye anapenda vitendo vya uadilifu. Wanyofu ndio ambao wataona uso wake.” Kulingana na tafsiri nyingine, yeye “ni mwenye haki na anapenda ushughulikaji wenye haki.”—New English Bible.a
“Haki ya Kimungu” Mkusanyiko wa Wilaya wetu utaimarisha imani yetu katika ushindi wa mwisho kabisa wa uadilifu. Pia utaimarisha kauli yetu nyakati zote na chini ya hali zote tutii ile amri kwenye Mika 6:8 (NW) ‘kujizoeza haki.’ Hilo ni takwa gumu kweli kweli kwa sababu ya maelekeo yetu tuliyorithi ya ubinafsi na vishawishi vya ulimwengu mbinafsi unaotuzunguka pande zote.
Katika sehemu zilizo nyingi, mkusanyiko utafunguka Alhamisi alasiri, na kila siku itakazia kichwa fulani kinachofaa, kichwa cha siku ya kwanza kikiwa “Wenye Furaha Ni Wale Wanaofuata Haki,” chenye kutegemea Zaburi 106:3, NW. Hotuba ya msingi itatilia nguvu kwamba ‘haki inakuwa katika njia zote za Mungu,’ na itafuatwa na ripoti kutoka kwa wafuataji-haki wa wakati wote, kama vile wamisionari kutoka nchi za kigeni.
“Pokea Nidhamu Inayotoa Mwono wa Ndani” (kikitegemea Mithali 1:3, NW) ndicho kichwa cha Ijumaa. Siku hii, mifululizo miwili itatia shada juu ya umaana wa kutia nidhamu na wa kukubali nidhamu. Drama ya ki-siku-hizi, “Waliotiwa Alama kwa Ajili ya Kuokoka,” itakazilia uhitaji wa kutambuliwa kuwa mmoja wa watumishi wa Yehova. Programu ya siku itamalizika kwa mashauri mazuri sana ya ‘Kutegemea Yehova kwa Mwono wa Ndani.’
Chenye kutuliza ni kichwa cha siku ya tatu, Jumamosi: “Hukumu Zake Ni za Kweli na Adilifu,” kilichotolewa katika Ufunuo 19:2, NW. Yenye kukaziwa asubuhi ni ile hotuba “Ubatizo Unaoongoza Kwenye Hukumu Inayopendeleka.” Programu ya alasiri itaanza kwa mfululizo utakaoshauri wazee “Tumikieni kwa Ajili ya Haki Yenyewe.” Hii itafuatwa na mfululizo mwingine, wenye kichwa “Wakati Uliowekwa Rasmi Uko Karibu,” ukishughulika na maunabii katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yenye kutabiri ushindi wa haki.
Jumapili, ile siku ya nne na ya hatima ya mkusanyiko, ina kichwa “Haki—Haki Ndiyo Mnapaswa Kufuatia.” (Kumbukumbu 16:20, NW) Yenye kutokeza katika programu ya asubuhi ni ile drama ya Kibiblia yenye kuvutia na ya wakati wake “Hukumu za Mungu Dhidi ya Watu Wenye Kukaidi Sheria.” Ujumbe wenye kuwafariji kweli kweli wote wapendao haki umo katika ile hotuba ya watu wote ya alasiri, “Haki kwa Wote Ikiletwa na Hakimu Mwekwa-Rasmi wa Mungu.” Wote watapata manufaa zaidi kutokana na hotuba hii ikiwa watajizoelesha Matendo sura ya 17. Kwa kufaa, katika hotuba ya kumalizia, wote waliopo wataonywa kwa upole, “Endeleeni Kufuatia Haki Wakati Upeo Ukaribiapo.”
Kweli kweli, karamu nono ya kiroho inangoja wote watakaohudhuria mmoja wa “Haki ya Kimungu” Mikusanyiko ya Wilaya. Kwa hiyo uje ukiwa na hamu kubwa ya kiroho, ukiujua kwa ukamili uhitaji wako wa kiroho. Onyesha meza ya Yehova uthamini ule ule ambao wewe unaonyesha wakati unapohudhuria mikutano ya kundi la kwenu kwa jinsi unavyojipamba, kwa kuwasili mapema vya kutosha kabla programu haijaanza, na kwa kubaki kwa ajili ya sala ya kumalizia ya kila siku. Sikiliza kwa makini sana kila sehemu ya programu. Andika mambo ya habari; si kwamba tu yatakupa kitu fulani cha kukumbuka mkusanyiko huu, bali pia yatakusaidia ukaze fikira juu ya habari zinapoendelea kutolewa.
Na acheni sisi tusikose kutazama ile kanuni iliyotaarifiwa na Yesu na kuandikwa kwenye Matendo 20:35, NW: “Kuna furaha nyingi katika kutoa kuliko zilivyo katika kupokea.” Kwa hiyo fanya sehemu yako kusaidia mkusanyiko ufanye kazi kwa ulaini na matokeo mazuri. Na uwe chonjo nyakati zote kuona fursa za kutoa ushuhuda wa vivi hivi. Uwe hasa mwenye kujua jambo hili, kwa sababu hakuna wakati ambao umewekwa kando kwa ajili ya ushuhuda wa nyumba kwa nyumba muda wa mkusanyiko. Katika njia zote hizo, unaweza kuonyesha kwamba kweli kweli wewe ni mfuataji haki mwenye furaha.
Unaweza kuwasiliana na Mashahidi wa Yehova wa kwenu upate habari juu ya mkusanyiko utakaokuwa karibu zaidi na eneo lako
[Maelezo ya Chini]
a Kwa msingi, hakuna tofauti iliyo wazi sana kati ya haki na uadilifu, ingawa mara nyingi haki inashirikishwa na mambo ya kisheria.—Linganisha 2 Timotheo 2:22; Yakobo 1:20, New World Translation na New English Bible.