Wakati Ujao Mwangavu wa Dunia Chini ya Ufalme wa Mungu
BIBLIA inasema kwamba “imani ni taraja lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa.” (Waebrania 11:1, NW) Kama vile tulivyoona katika makala iliyotangulia, zaidi ya miaka 500 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo, Mungu alisababisha iandikwe katika kitabu cha Danieli mandhari ya kimapema ya unabii juu ya inuko na anguko la serikali kubwa za ulimwengu kutoka siku ya Danieli kuteremka mpaka siku yetu wenyewe. Usahihi wa manabii haya unatupa sisi uhakikishio, unatupa sababu imara ya kuwa na imani, kwamba mengine yote ya manabii ya Danieli yatatimizwa pia, na karibuni sana Ufalme wa Mungu chini ya Kristo Yesu utachukua mahali pa serikali za kibinadamu.
Hiyo itamaanisha badiliko lililoje kwa jamii ya kibinadamu! Akitazama mbele kwenye wakati huo, Mungu mwenyewe anasema: “Tazama! Mimi ninafanya vitu vyote kuwa vipya.” (Ufunuo 21:5, NW) Mfikirio wa baadhi ya manabii yaliyovuviwa na Mungu yanayofafanusha kwa ajili yetu hali ya wakati huo wenye furaha utatusaidia kuona ni kwa kadiri gani hasa mambo haya yatakuwa ‘mapya,’ ni kwa kadiri gani yatakavyotofautiana kikamili na yale tunayoona leo chini ya utawala wa kibinadamu. Kweli kweli, mambo ambayo Biblia inasema kuhusu wakati ujao wa dunia yetu na kuhusu uhai ulio juu yayo yatakuwa ya kustaajabisha vilivyo. Fikiria:
Uhalifu na jeuri vitaisha. “Kwa maana watenda maovu wenyewe watakatiliwa mbali, . . . aliye mwovu hatakuwapo tena.” Wale wenye kuishi “wataketi kwa kweli, kila mmoja chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, na hakutakuwa na mmoja wa kuwafanya wateteme; kwa maana kile kinywa chenyewe cha Yehova wa majeshi kimenena hilo.”—Zaburi 37:9, 10; Mika 4:4, NW.
Migawanyiko ya jamii za watu wa rangi mbalimbali na mataifa, na vita vinavyochochewa na migawanyiko hiyo, itakuwa imetoweka. “Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa, wala wao hawatajifunza vita tena kamwe.”—Isaya 2:4, NW.
Upungufu wa nyumba, ukosefu wa maskani, na ukosefu wa kuajiriwa kazi yatakuwa mambo ya wakati uliopita. Isaya alitabiri hivi: “Wao kwa uhakika watajenga nyumba na kuwa na ukaaji; na wao kwa uhakika watapanda viwanja vya mizabibu na kula uzao wa matunda yayo. . . . Na wachaguliwa wangu wataitumia kwa ujazi kazi ya mikono yao wenyewe.”—Isaya 65:21, 22, NW.
Njaa mbaya-mbaya sana, kama zile ambazo zimekumba sehemu za Afrika hivi majuzi, zitaondolewa kisha mahali pazo pachukuliwe na wingi wa chakula kwa ajili ya wote. “Kutakuja kuwa na nafaka tele juu ya dunia; juu ya kilele cha milima kutakuwa na mtiririko wa kuzidi.” “Dunia yenyewe kwa uhakika itatoa zao layo; Mungu, Mungu wetu, atatubariki.”—Zaburi 72:16; 67:6, 7, NW.
Kuongezea hilo, kutakuwa na afya na uhai wa kutumiwa kufurahia baraka hizi. Hata wakati wa huduma ya kidunia ya Yesu, ilisemwa kiukweli kwamba “vipofu wanapokea mwono, viwete wanatembea, wenye ukoma wanasafilishwa na viziwi wanasikia.” Hata hivyo, ahadi moja kubwa zaidi itahusika: “Yeye [Mungu] atafuta kila chozi kutoka kwenye macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala mpalizo wa kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe. Mambo ya hapo kwanza yamepitilia mbali.”—Luka 7:22; Ufunuo 21:4, NW.
Ni badiliko la uadhimifu mkubwa kama nini! Yote hayo yataleta kitulizo kama nini kwa aina ya binadamu iliyotaabika sana! Sisi tunakutia wewe moyo ujitiishe hata sasa kwa Ufalme wa Mungu, ili wewe pia upate kuvuna manufaa zitakazokuja kutokana na badiliko hili la nyakati zote katika utawala wa ulimwengu.
[Picha katika ukurasa wa 7]
Watu wanaoishi sasa wanaweza kutazama mbele kwenye baraka nzuri ajabu—kwisha kwa vita, uhalifu, umaskini, ugonjwa, na hata kifo. Je! wewe ungefurahia wakati ujao kama huo?