Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 6/15 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Habari Zinazolingana
  • “Mlinunuliwa Kwa Bei”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • ‘Kuishi Si Tena Kwa AJili Yetu Wenyewe’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Pambano la Muda Mrefu Dhidi ya Utumwa
    Amkeni!—2002
  • “Mtumikieni Yehova”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 6/15 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

■ Kulingana na maneno ya Yesu kwenye Yohana 15:15, je! inawapasa Wakristo wajione wenyewe kuwa “watumwa” wake, au tunaweza kujifikiria wenyewe kuwa “marafiki” zake?

Tunaweza na tunapaswa kuwa hali zote mbili. Ili tuone ni kwa nini, acheni tuangalie aliyosema Yesu hapo kwa mitume wake wenye imani usiku wake wa mwisho wa kuwa pamoja nao:

“Hakuna mmoja ambaye ana upendo mkubwa kuliko huu, kwamba mtu fulani apaswe kutoa nafsi yake kwa ajili ya rafiki zake. Ninyi ni rafiki zangu ikiwa ninyi mnafanya ninayowaamuru ninyi. Mimi siwaiti ninyi watumwa tena, kwa sababu mtumwa hajui anayofanya bwana-mkubwa wake. Lakini mimi nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu mambo yote ambayo mimi mmesikia kutoka kwa Baba yangu mmejulisha kwa ninyi.”​—Yohana 15:13-15, NW.

Kwanza, Yesu alimaanisha nini kwa kusema kwamba wanafunzi wake washikamanifu walikuwa watumwa? Yeye hakumaanisha watumwa katika maana ambayo wanadamu wote walio wazao wa Adamu wanazaliwa wakiwa wasiokamilika, hivyo wakiwa wameuzwa ndani ya dhambi au kufanywa watumwa wayo. (Yohana 8 34, Warumi 5:18, 19, 6:16:7:14) Kama vile kwa habari ya Wakristo tangu wakati huo, wakati mmoja mitume walifanywa watumwa kwa njia hiyo, lakini dhabihu ya Yesu ingeandaa njia ya kuwaweka huru, au kuwafungua. (1 Petro 1:18, 19: Wagalatia 4:5) Hata hivyo, baada ya hapo wao hawakuwa huru kabisa. Kama vile mtume Paulo alivyoandika baadaye, wao ‘walinunuliwa kwa bei,’ damu ya Yesu, kwa hiyo wao wakawa watumwa wa Mungu na wa Kristo.​—1 Wakorintho 6:20:7:22,23, NW.

Kwenye Yohana 15.15 Yesu hakuwa akidokeza kwamba wale mitume wenye imani ambao wangepokea roho takatifu baada ya muda mfupi na kuwa Wakristo waliopakwa mafuta hawakuwa tena watumwa. (Linganisha Yohana 15:20.) Bila shaka, utumikisho kwa Mungu kupitia Kristo si wa uonevu wala si wenye kuleta kifo. Ni wenye upendo na wenye kuhifadhi uhai. (2 Timotheo 4 8: Tito 1:1,2) Mkristo anayekubali thamani ya damu ya Kristo kwa mteremo na kuwa mtumwa wa Mungu akija baadaye kukataa dhabihu hiyo na kujitoa arudie dhambi, akiwa mtumwa wayo tena, hapo tu ndipo angeelekeana na kifo cha daima. (Wagalatia 1:10; 4:8, 9, Waebrania 6.4-6) Kwa sababu hiyo, wanafunzi wa Yesu wangeendelea kuwa watumwa wa Mungu na wa Kristo, lakini wao walikuwa ni zaidi hata ya watumwa. Kwa nini?

Yesu na mitume walielewa kwamba huko nyuma, katika uhusiano ambao kwa kawaida ulikuwa baridi-baridi au wa kirasmi kati ya bwana-mkubwa na mtumwa, ‘mtumwa hangejua anayofanya bwana-mkubwa wake.’ Kwa kawaida, bwana-mkubwa wa kibinadamu hangefanya mkutano wa mashauriano pamoja na mtumwa aliyemnunua, wala hangemfunulia mawazo na hisia zake za faragha.

Ingawa hivyo, sisi tunaweza kuona kutokana na maneno ya Yesu kwamba ilikuwa tofauti kuwahusu mitume. Yeye alisema: “Mimi nimewaita ninyi marafiki, kwa sababu mambo yote ambayo mimi mmesikia kutoka kwa Baba yangu mimi nimeyajulisha kwa ninyi.” (Yohana 15:15, NW) Ndiyo, kama ilivyo kawaida sana kati ya rafiki wapenzi, Yesu alikuwa amewafunulia wao habari za kirefu na maeleweko yaliyokuwa yamekuwa siri. (Mathayo 13:10-12; 1 Wakorintho 2:14-16) Ingawa wao walikuwa wangali ni watumishi, au watumwa, wa Mungu kupitia Yesu, mitume walifurahia uhusiano mchangamfu wa kindani ulioonyesha walikuwa marafiki wenye kuitibariwa. (Linganisha Zaburi 25:14.) Inaweza kuwa hivyo na ndivyo inavyopasa kuwa kwa habari yetu pia. Ni pendeleo kama nini kuwa na Mabwana-wakubwa katika mbingu wanaotutendea kama wasiri wenye kuitibariwa na kustahiwa, kama marafiki!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki