Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 kur. 4-7
  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mifano ya Jumuiya ya Wakristo​—Kutoka Wapi?
  • Kutetea Utumizi wa Mifano ya Kidini
  • Mifano—Kituo cha Rai ya Mwabudu
  • Biblia Inasema Nini?
  • Kuabudu ‘Katika Ukweli’
  • Je! Sanamu Zaweza Kukuleta Karibu Zaidi na Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Sanamu
    Amkeni!—2014
  • Je, Tumwabudu Mungu Kupitia Sanamu?
    Amkeni!—2008
  • Kuzipa Sanamu Heshima Kibishanio
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 kur. 4-7

Maoni ya Kikristo Juu ya Mifano

“NINYI mlivunja uhusiano na ibada ya sanamu . . . na mkawa watumishi wa yule Mungu halisi, aliye hai,” ndivyo alivyoandika mtume Paulo kwa Wakristo katika Thesalonike. (1 Wathesalonike 1:9a) Ndiyo, Wakristo wengi wa mapema walikuwa waabudu-sanamu wapagani wakati mmoja. (1 Wakorintho 6:9-11) Lakini walipokwisha kuwa Wakristo, walikomesha mazoea ya ibada ya sanamu.

Hata hivyo, kuinama mbele ya sanamu kulikuwa jambo la kawaida sana hivi kwamba Wakristo walifanyiwa mzaha kwa sababu waliabudu bila kutumia mifano. Wapagani fulani hata waliwashtaki wao juu ya kuwa watu wasioamini Mungu yuko! Basi, ni jinsi gani kule kustahi mno mifano kulivyokuja kuenea sana katika Jumuiya ya Wakristo baadaye?

Mifano ya Jumuiya ya Wakristo​—Kutoka Wapi?

Mazoea mengi ya kipagani yalijulishwa miongoni mwa “Wakristo” baada ya ule unaoitwa eti uongofu wa maliki Mroma Konstantino. “Kutoka siku za Konstantino,” anataarifu mwanahistoria wa kidini Edwyn Bevan katika kitabu chake Holy Images, “utumizi wa Msalaba kama ufananisho katika sehemu zote za ulimwengu wa Kikristo ulikuja kuwa wa kawaida na baada ya muda mfupi ukapewa staha nyingi.” Hii ilifungulia njia namna nyinginezo za ibada ya mifano. Kitabu hicho hicho kinaonelea hivi: “Linaelekea kuwa labda kabla ya picha na mifano kupewa staha nyingi, desturi ilikuwa imeingia ya kuutolea staha nyingi ufananisho wa Msalaba, ambao huo wenyewe . . . haupatikani juu ya vifaa vya kumbukumbu za Kikristo wala juu ya sanaa za kidini kabla ya Konstantino, kuweka kielelezo cha kufanya hivyo katika ile labaramu [beramu ya kijeshi yenye msalaba].”

Hali hiyo iliendelea. Katika karne ya nane W.K., John wa Dameski, aliyefikiriwa kuwa “mtakatifu” na makanisa Katoliki ya Roma na Orthodoksi ya Mashariki, aliandika hivi: “Kama vile ambavyo Mababa watakatifu walipindua-pindua mahekalu na sehemu takatifu za maibilisi, na kusimamisha katika mahali payo sehemu takatifu kwa kuziita majina ya Watakatifu, na sisi tunaziabudu, ndivyo pia walivyopindua-pindua mifano ya maibilisi, na badala yayo wakasimamisha mifano ya Kristo, na Mama ya Mungu, na Watakatifu.”

Thomas Aquinas, “mtakatifu” wa Katoliki ya Roma wa karne ya 13, aliongezea hivi kwa jambo hilo: “Kicho hicho hicho kinapasa kuonyeshwa kuelekea mfano wa Kristo na kuelekea Kristo Mwenyewe . . . Msalaba unastahiwa kwa mapenzi makuu kwa njia ile ile anayostahiwa Kristo, yaani, kwa staha nyingi mno ya latria [ambao ni ufafanuzi wa Kikatoliki wa namna ya ibada iliyo ya hali ya juu zaidi], na kwa sababu hiyo sisi tunausemesha Msalaba na kuuomba dua sawasawa na vile sisi tunavyomfanyia Msulibiwa Mwenyewe.”

Bado Wakatoliki wana rai ya kwamba Aquinas ana mamlaka nyingi juu ya “kustahi mno mifano.” Kulingana na New Catholic Encyclopedia, “kustahi mno mifano” kulilazimika kumngojea yeye “ili apate maelezo kamili kabisa juu ya jambo hilo lenyewe.” Hata hivyo, ni wazi kwamba ibada ya mifano “ya Kikristo” ilitumikia tu kuchukua mahali pa ibada ya mifano ya kipagani.

Kutetea Utumizi wa Mifano ya Kidini

Wengi leo ambao wanastahi mno mifano ya kidini wangekataa kuitwa waabudu-mifano. Hata hivyo, makatao yao kuhusu mtajo huo si jambo jipya. Katika karne ya nne, yule mwenye kuitwa eti Mtakatifu Augustino alizifanyia mzaha njia za kufikiria mambo za watu wasio Wakristo, wenye kuabudu sanamu, akisema: “Kuna mbishani fulani ambaye kwake mwenyewe anaelekea kuwa ni mtu mwenye elimu nyingi, na anasema, Mimi siabudu jiwe lile, wala mfano ule usio na akili; . . . Mimi siabudu mfano huu; lakini nastahi kwa mapenzi makuu kile ambacho naona, na natumikia yeye ambaye sioni.” Ndiyo kusema, wao walidai kuabudu mtu yule tu asiyeonekana ambaye sanamu zao ziliwakilisha. “Kwa kutoa utetezi huu kuhusu mifano yao,” Augustino aliongezea kwamba, “wao wanaelekea kwa maoni yao wenyewe kuwa ni wabishani hodari, kwa sababu wao hawaabudu sanamu, na hata hivyo wanaabudu maibilisi.”​—Expositions on the Book of Psalms kilichotungwa na Augustino, Zaburi 97:9.

Ingawa wanatheolojia wa Katoliki ya Roma wamekuwa na haraka ya kushutumu ibada ya sanamu ya kipagani, wakati utumizi wao wenyewe wa mifano unapohusika, mara nyingi wao wamegeukia kufanya majiteteo yale yale ambayo ule unaoitwa upagani umetumia. Mathalani, lile Baraza la Trent la karne ya 16 lilitangaza rasmi hivi kuhusu mifano ya Kristo, Mariamu, na “watakatifu”: “Heshima inayopasa na staha nyingi mno inapasa kupewa kwao; hata hivyo, sababu ya hiyo kupaswa kustahiwa mno si kwamba inaitikadiwa kuwa ndani yayo mna uungu wowote au nguvu zozote za wema.” Basi, kule kustahiwa mno ni kwa nini? “Ni kwa sababu ile heshima inayoonyeshwa mifano hiyo,” likaeleza baraza hilo, “inarejezwa kwenye vyanzo-asilia ambavyo hiyo inaviwakilisha, hivi kwamba kupitia mifano ambayo sisi tunabusu na ambayo mbele yayo sisi tunafunua vichwa na kujisujudisha wenyewe, tunastahi mno Kristo kwa mapenzi makuu na kuwastahi mno watakatifu, ambao wana sura yake.”

Mpaka leo hii Kanisa Katoliki la Roma linaendelea kutetea ibada ya sanamu kwa misingi ile ile: kwamba mifano ni njia tu ya kukaza fikira juu ya yule mmoja wa kimbingu anayewakilishwa nayo na kwamba hakuna wema wala nguvu zinazokaa ndani ya mifano. Ingawa hivyo, ni kwa kadiri gani imethibitika kuwa hivyo katika mazoea halisi? Je! wote ambao wanatumia mifano wanaitikadi kweli kweli kwamba hakuna ‘uungu wala nguvu za wema katika hiyo’?

Mifano—Kituo cha Rai ya Mwabudu

Katika Seville, Hispania, ushindani wa kushikilia kauli bila akili nzuri upo kati ya wafuasi wa yule Bikira la Macarena na Bikira de la Esperanza. Katika Kathedro ya Chartres, Ufaransa, mna Mabikira watatu​—Bwana Wetu wa Nguzo, Bwana Wetu wa Mazikio, na Bwana Wetu wa “Kioo Chenye Kuvutia”​—kila mmoja akiwa na wafuasi wake mwenyewe. Inaonekana kwamba waabudu wanasadiki kwamba kidogo mfano wao wa Madonna ni bora kuliko mifano ile mingine​—hata ingawa mifano yote mitatu inawakilisha mtu yule yule mmoja! Basi, kwa uwazi staha nyingi inapewa, si kwa kile kinachowakilishwa, bali kwa mifano yenyewe.

Kwa hiyo, kile ambacho Kanisa Katoliki ya Roma linatolea udhuru kuwa ni ibada ya kiasi tu, mara nyingi kinageuka kuwa ibada halisi ya mfano. Njia za theolojia za kutokeza vitofauti vidogo-vidogo ili kuonyesha kwamba sivyo ilivyo zinakosa umaana kwa kuelekeana na zile karne ambazo jambo hilo limefanywa kwa mazoea halisi.

Biblia Inasema Nini?

Shauri la Biblia linapinganisha nadharia za wanatheolojia. Mungu alielewesha wazi kwa Israeli wa kale kwamba ibada ya sanamu ilishutumiwa kabisa kabisa. (Kutoka 20:4, 5; Kumbukumbu 4:15-19) Ni kweli, viwakilishi fulani, kama yule nyoka-shaba ambaye Musa alifanyiza, viliruhusiwa. Ingawa hivyo, kuinamia vitu hivyo katika ibada kulikatazwa kata-kata.​—Hesabu 21:9; 2 Wafalme 18:1, 4.

Nyakati fulani Israeli walikosa kutii katazo hili juu ya ibada ya sanamu. Mathalani, kule Sinai, Israeli walifanyiza ndama-dhahabu kwa ajili ya ibada. Lilikuwa kufuru kama nini kwa wao ‘kubadilishana utukufu wa Mungu kwa kiwakilishi cha ndama, mla-majani’! (Zaburi 106:20) Lakini kama vile wanadini fulani leo, wao walidai kuabudu, si ndama yule, bali Mungu mwenyewe! “Hapa yupo Mungu wako, Israeli,’ wao walipaaza sauti ‘ambaye alikuleta wewe kutoka lile bara la Misri.’” (Kutoka 32:1-5) Hata hivyo, Yehova hakuvumilia ibada hii “ya kiasi,” huku kurudia dini ya Kimisri bila kujali. (Matendo 7:39-41) Kulivunja moja kwa moja agano ambamo wao walikuwa wameingia kule Sinai, na kukaleta Israeli ndani ya hatari ya kufutiliwa mbali kabisa.​—Kutoka 32:9, 10, 30-35; Kumbukumbu 4:23.

Ingawa hivyo, kwa nini Yehova Mungu alichukua msimamo imara hivyo dhidi ya mifano? Kwanza, mifano ni hoi; hiyo si kitu. (Kumbukumbu 32:21a; Zaburi 31:6) Yeremia alisema kwamba hiyo ilikuwa kama sanamu za kufukuza ndege shambani, zisizo na pumzi ndani yazo. (Yeremia 10:5, 14) Vilevile Isaya aliwadhihaki wale wanaotumia sehemu ya mti kufanyiza moto wa kupikia na sehemu nyingine kufanyiza mungu. Nabii anaonya kwamba hao waabudu-sanamu “hawajui kitu, hawaelewi kitu. Macho yao yamefungika kwa uonaji wote, moyo wao kwa uonaji wote wa sababu.”​—Isaya 44:13-18.

Hatari moja hususa iliyo ya kufisha inayohusiana na ibada ya mifano ni uwezekano wa mfano kutumika kama njia ya kupashana habari pamoja na kani za kishetani. Mtunga zaburi alisema hivi juu ya Waisraeli: “Wakitumikia sanamu-ibada za wapagani, wao walijikuta wametegwa ndani ya kudhabihu wana na binti zao wenyewe kwa roho wabaya.” (Zaburi 106:35-37; linganisha Walawi 17:7; Kumbukumbu 32:17.) Tokeo ni kwamba, njia ilifunguliwa ya mazoea mengine ya kishirikina, ya kuwasiliana na roho wabaya. Kielelezo kingine ni kile cha Mfalme Manase, ambaye alirudisha upya ibada ya sanamu katika Israeli. Kufuatia jambo hilo, “Yeye alijenga madhabahu kwa ajili ya mpangilio mzima wa mbinguni katika nyua mbili za lile Hekalu” na “akazoea ubashiri-matukio na mizungu.”​—2 Wafalme 21:1-6.

Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo yanaonya juu ya hatari zile zile. The New Bible Dictionary inasema hivi: “Ule ubishi wa Agano la Kale dhidi ya ibada ya sanamu . . . unatambua kweli zile zile mbili ambazo baadaye Paulo angekuja kuzitilia nguvu: kwamba sanamu-ibada haikuwa kitu, bali kwamba kulikuwa hata hivyo na kani-roho ya kishetani ya kupambana nayo, na kwamba kwa sababu hiyo sanamu-ibada ilikuwa tisho halisi la kiroho.” Paulo aliandika hivi: “Sisi tunajua kwamba kwa kweli sanamu-ibada hazipo katika ulimwengu na kwamba hakuna mungu isipokuwa yule Mmoja tu.” Lakini baadaye yeye alionya hivi: “Dhabihu ambazo wao wanatoa wanadhabihu kwa roho wabaya ambao si Mungu. Mimi sina tamaa kuona ninyi mkiwa katika ushirika pamoja na roho wabaya.”​—1 Wakorintho 8:4; 10:19, 20.

Ndiyo, kani za roho waovu zina hamu nyingi ya kuleta watu mmoja mmoja chini ya udhibiti wazo. Paulo aliandika hivi: “Kwa maana si dhidi ya maadui wa kibinadamu kwamba sisi tunalazimika kumenyana, bali ni dhidi ya Wenye-enzi-kuu na Nguvu za Kimamlaka ambao ndio wanaofanyiza asili ya giza lililo katika ulimwengu huu, jeshi la kiroho la uovu katika mbingu.” (Waefeso 6:12) Kwa hiyo ibada ya mifano ya namna yo yote inafisha fahamu za kiroho za mmoja, inatia moyo ushirikina, na kutoa nafasi ya kutumiwa na watawala wa ajabu za kimafumbo wa ulimwengu huu wenye giza, ulio mwovu.

Kuabudu ‘Katika Ukweli’

Watu wengi wenye moyo mweupe wanatumia mifano kujileta karibu zaidi na yule Msikiaji wa sala. Kujileta karibu na Mungu kunatamanika. Lakini je! sisi tuko huru kuchagua njia yetu wenyewe ya kumfikia? Kwa uhakika ni lazima sisi tutafute mfikio ambao unafurahisha Mungu, si wetu wenyewe. Yesu alisema: Mimi ni ile Njia, ule Ukweli na ule Uhai. Hakuna mmoja ambaye anaweza kuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.” (Yohana 14:6) Hii ingezuia kutumia mifano ya ibada ya sanamu. Yesu alizidi kufundisha hivi: “Lakini saa itakuja​—kwa uhakika tayari ipo​—wakati waabudu wa kweli wataabudu yule Baba katika roho na ukweli: hiyo ndiyo aina ya mwabudu ambaye Baba anataka. Mungu ni roho, na wale ambao wanaabudu lazima waabudu katika roho na ukweli.”​—Yohana 4:23, 24.

Je! mmoja ambaye ni roho anaweza kuwakiIishwa na mfano wenye mwili unaoonekana? Hata mfano uwe wa kuvutia kama nini, hauwezi kamwe kulanda utukufu wa Mungu. Kwa hiyo mfano wa Mungu haungeweza kamwe kuwa wa kweli. (Linganisha Warumi 1:22, 23.) Kwa hiyo je! mtu angekuwa ‘akiabudu katika ukweli’ ikiwa yeye angefikia Mungu kupitia mfano fulani ambao ni udanganyifu?

Mashahidi wa Yehova wamesaidia maelfu ya watu mmoja mmoja waache mazoea ya ibada ya sanamu na kuwa ‘aina ya waabudu ambao Baba anataka.’ Baada ya kuonyeshwa kutokana na Biblia jinsi Mungu anavyoona mifano, wengi wamesukumwa kuondolea mbali mifano kutoka kwenye maskani na namna yao ya ibada. (Linganisha Kumbukumbu 7:25.) Ni kweli, imekuwa si rahisi kwa watu hao kufanya hivyo sikuzote. Lakini wao wamesukumwa na tamaa ya moyo mweupe kushika sana Neno la Mungu Biblia, ambalo linahimiza Wakristo wa kweli hivi: “Watoto, iweni katika lindo dhidi ya miungu bandia [kwa uhalisi, sanamu-ibada].”​—1 Yohana 5:21, maelezo ya chini.

[Maelezo ya Chini]

a Isipokuwa kama yametiwa alama tofauti, manukuu yote ya Maandiko ni kutoka The Jerusalem Bible ya Kikatoliki.

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

Je! ‘Aikoni Haziwi Kamwe Ibada-Sanamu’?

“Aikoni” inarejeza kwenye mfano wa aina fulani ya wazi, yaani, michoro ya kidini inayostahiwa mno na washiriki wa Kanisa Orthodoksi la Mashariki. Mingine ya hiyo ni viwakilishi vya Kristo; mingine inawakilisha Utatu, Mariamu, “watakatifu,” au malaika. Kama Wakatoliki wa Roma, wanatheolojia Waorthodoksi wanatetea kwamba kuzistahi mno aikoni ni kitendo cha kiasi kinachopitisha bidii ya kujitoa imfikie yule mwakilishwa mmoja wa kimbingu. “Aikoni,” anadai mwanatheolojia Mrusi, Sergey Bulgakov, “inabaki kuwa kitu tu na haiwi kamwe sanamu-ibada wala chombo-kikaliwa-na-roho.”

Ingawa hivyo, wakati ule ule Kanisa Orthodoksi la Mashariki linafundisha kwamba aikoni inaweza kuleta manufaa za pekee kwa mwabudu anayesali mbele yayo, mradi aikoni hiyo ‘imetakaswa’ na kanisa. “Ile sherehe ya kidini ya kubariki aikoni,” anataarifu Bulgakov katika kitabu chake The Orthodox Church, “inaimarisha ufungamano fulani kati ya mfano ule na kile kinachofananishwa, kati ya kile kinachowakilishwa na kiwakilishi chenyewe. Kwa kule kubariki aikoni ya Kristo, inafanywa iwezekane kuwe na mkutano wa kifumbo wa waaminifu na Kristo. Ni hivyo hivyo kwa habari ya aikoni za yule Bikira na Watakatifu; huenda mtu akasema, aikoni zao zinarefusha maisha zao hapa chini.”

Zaidi ya hilo, aikoni nyingi za Mariamu zinaitikadiwa kuwa zina nguvu za kimwujiza. “Ingawa yeye anabaki akiwa mbinguni,” Bulgakov anakazania, “bado yeye anaishi pamoja na sisi maisha ya ulimwengu wetu, anateseka pamoja na mteseko wao, na kulia machozi pamoja na machozi yao. Yeye anakuwa katikati akifanyia ulimwengu upatanisho mbele ya kiti-ufalme cha Mungu. Yeye anajifunua mwenyewe kwa ulimwengu katika aikoni zake zenye kufanya maajabu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki