Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 kur. 16-21
  • Vijana Lindeni Dhidi ya Kuendesha Maisha Maradufu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana Lindeni Dhidi ya Kuendesha Maisha Maradufu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Watu Fulani Wanaendesha Maisha Maradufu
  • Wazazi, Ninyi Mnaweza Kuchangia
  • Kile Ambacho Hasa Ni Maisha Maradufu
  • Jinsi ya Kuyaepuka!
  • Saidia Wengine Wayaepuke
  • Ninawezaje Kuacha Kuishi Maisha Maradufu?
    Vijana Huuliza
  • Kuishi Maisha Maradufu —Kwa Nini Nisifanye Hivyo?
    Amkeni!—1993
  • Kuwa na Nyuso Mbili—Kuna Ubaya Gani?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Naweza Kuachaje Maisha Maradufu?
    Amkeni!—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 kur. 16-21

Vijana Lindeni Dhidi ya Kuendesha Maisha Maradufu

“Shangilia, mwanamume kijana, katika ujana wako . . . Lakini jua kwamba kwa sababu ya yote haya Mungu wa kweli atakuleta wewe ndani ya hukumu.”​—MHUBIRI 11:9, NW.

1, 2. Kuna kielelezo gani kinachohusu kijana akiwa anaendesha maisha maradufu?

“KUTOKA utoto mchanga mimi nililelewa katika mazingira ya Kikristo, miongoni mwa Mashahidi wa Yehova,” akaandika kijana mmoja. “Na bado, maisha ambayo mimi niliishi, hata nilipokuwa kwenye maskani yetu, yalikuwa kinyume kabisa cha viwango na kufikiri kwa wazazi wangu. Maisha yangu kwa sehemu kubwa zaidi yalikuwa maisha ya ulegevu, maisha ya ulimwengu yasiyo na nidhamu.”

2 Kijana huyo alieleza zaidi hivi: “Hata kabla sijafika umri wa miaka kumi, nilianza kuendesha malimwengu yote mawili kwa kadiri bora ambavyo ningeweza​—ili nipate ukubaliwa na urafiki shuleni na bado nikubaliwe na wazazi wangu. Kwenye shule nilijipatanisha na mitindo na mwenendo wa huko kwa kadiri ambayo ningeweza . . . Lakini kwenye maskani yetu nilikuwa tofauti kabisa. Huko nilikuwa Mkristo mwenye mwenendo mzuri wa namna ile ambayo wazazi wangu walitarajia.”

3. (a) Ni uhakika gani tulio nao, hata hivyo tunang’amua nini? (b) Ni jambo gani linalotuchochea kuelekeza fikira kwa vijana?

3 Sisi tunang’amua kwamba mwenendo wa kijana huyu si kiwakilishi cha vile walio wengi kati yenu vijana mlivyo katika kundi. Sisi tuna uhakika kwamba mlio wengi kati yenu mnawaonyesha wazazi wenu na kundi jinsi mlivyo kwa haki, na jambo hili linachangamsha mioyo yetu. Wakati ule ule, sisi tunajua kwamba vijana fulani wanatokeza uso wa kuwa wanyofu lakini, kwa kadiri wawezavyo, wanaficha mwendo fulani wa kutenda makosa ili usionwe na watu wenye umri mkubwa. Kwa sababu hiyo swali ndilo hili: Je! wewe ni aina ya mtu yule ambaye wewe unafanya sisi tufikiri ndiye uliye, au wewe unaendesha maisha maradufu? Sisi hatuulizi jambo hili kwa roho ya kutafuta-tafuta makosa, bali kwa sababu sisi tunakupenda wewe kikweli na tunataka kukusaidia ufurahie ujana wako kwa kuishi kwa njia inayofurahisha Yehova.​—Mhubiri 11:9, 10; 12:14; 2 Wakorintho 5:10.

4. Ni jinsi gani watu wazima fulani pia wameendesha maisha maradufu, lakini ni jambo gani limeonwa hivi majuzi miongoni mwa vijana?

4 Na bado, huenda wewe ukauliza: ‘Kwa nini mtuonee sisi vijana? Namna gani watu wazima?’ Hakuna swali kwamba ni lazima wao pia walinde dhidi ya kuendesha maisha maradufu. Gehazi, hadimu wa Elisha, alitenda kwa udanganyifu, akijaribu kufunikiza uhakika wa kwamba yeye alikubali zawadi kutoka kwa Naamani. (2 Wafalme 5:20-26) Na Anania na Safira, ambao walikuwa watu wazima, walifanya ubandia kwa kusema kwamba walikuwa wamewapa mitume bei nzima ya lile shamba​—wakijaribu kujifanya waonekane wema​—hali kwa kweli wao walikuwa wamezuilia kiasi fulani cha pesa hizo kwa ajili yao wenyewe. (Matendo 5:1-4) Hata hivyo, sababu ambayo sisi tunaelekeza fikira kwa ninyi vijana ni kwamba inaonekana wazi kumekuwa na ongezeko katika mtukio wa tatizo hili miongoni mwenu.

Kwa Nini Watu Fulani Wanaendesha Maisha Maradufu

5. (a) Kwa nini vijana fulani wanaendesha maisha maradufu? (b) Mara nyingi vijana wanatendewa jinsi gani wakati wanapoishi maisha yanayostahili pongezi, na kwa hiyo vijana fulani hufanya nini?

5 Kwa nini iko hivi? Kijana mmoja alionyesha sababu moja kubwa iliyo halisi, akieleza hivi: “Mimi sikutaka kupoteza rafiki zangu kwa kuwa tofauti.” Ni kweli kwamba mara nyingi kuwa tofauti kwa njia yenye mafaa hufanya mmoja awe chombo cha dhihaka. (Linganisha 1 Petro 3:16; 4:4.) Ili kuepuka jambo hili, na ili wapate ukubaliwa wa marika yao, vijana fulani hata watalewa au wafanye mahusiano ya kingono. Msichana wa miaka 13 asiye Shahidi, ambaye alipata maksi za juu kabisa katika mambo yote na ambaye sikuzote alishiriki katika mazungumzo ya darasani, aliomboleza hivi: “Wavulana hawatapendezwa kamwe na mtu wanayejua wazi hufanya vizuri kama mimi. . . . Mimi nafikiria kuacha maksi zangu zishuke kidogo au nifanye jambo fulani ili sifa yangu ionekane wazi zaidi.”

6. Ni jinsi gani Petro alivyopatwa na uvutano wa kuingia katika mwenendo wenye kosa, na jambo hili linapasa kuathiri jinsi gani hukumu yetu juu ya vijana?

6 Ni jambo la maana kuangalia kwamba, wakati mmoja mtume Petro mwenyewe alifikiria jina, au sifa yake, zaidi ya kufanya lile alilojua lilikuwa sawa. Wakati Wakristo Wayahudi kutoka Yerusalemu walipozuru Antiokia, Petro alijiondoa kwenye ushirika pamoja na Wakristo wasio Wayahudi kwa sababu ya hofu ya kuchambuliwa na Wayahudi kwa kuchangamana na hawa wasio Wayahudi. (Wagalatia 2:11-14) Kwa kuwa hata Wakristo wakomavu wamejiacha hivyo washindwe na mkazo wa marika yao, je! ni ajabu kwamba huenda vijana wasio na ujuzi wakafanya hivyo pia?​—Mithali 22:15.

7. Ni jambo gani huenda likashawishi vijana fulani kuendesha maisha maradufu?

7 Sababu moja inayohusiana na hiyo ambayo inafanya vijana fulani waendeshe maisha maradufu ni kwamba wao wanaitikadi wanakosa raha fulani. Wao wanasikia vijana shuleni wakiongea juu ya utendaji wao​—jinsi kikaramu kilivyokuwa kizuri sana, ule muziki wa kupendeza ajabu, ule unywaji, zile dawa za kulevya, jinsi walivyokuwa na mfurahiko mkubwa! Au wanasikia ‘jinsi mvulana, au msichana yule anavyoweza kupiga busu na kufanya mapenzi.’ Kwa hiyo tamaa ya kuonja mambo haya inaamshwa, na vijana wanavutwa kujaribu kufanya ule ambao Biblia inauita “mfurahio wa muda wa dhambi.”​—Waebrania 11:24, 25; 1 Wakorintho 10:6-8.

8. Ni nini sababu ya msingi ya vijana kuendesha maisha maradufu?

8 Hata hivyo, sababu ya msingi inayofanya vijana fulani waishi maisha maradufu ni kwamba Yehova na ulimwengu mpya unaokuja si halisi kwao. Wao hawaitikadi ahadi za Yehova kikweli wala maonyo yanayotolewa kupitia Neno lake na tengenezo lake linaloonekana kuhusu matokeo ya kutotii Yehova. (Wagalatia 6:7, 8) Wao si kama Musa, ambaye Biblia inasema hivi juu yake: “Yeye alitazama kwa kukaza macho kuelekea lile lipo la thawabu [ya Mungu]. . . . Yeye aliendelea akiwa thabiti kama akiona yule Mmoja ambaye ni asiyeonekana.” Kwa Musa, Yehova na ahadi Zake alikuwa halisi. Lakini wale wanaoendesha maisha maradufu wana ukosefu wa imani hiyo. Wao wanaona kile tu ambacho Shetani anataka waone​—umetametaji wa mfumo huu. Na kwa hiyo wao wanafuatia mfurahio wa muda wa dhambi na bado, wakati ule ule, wanajaribu kutokeza uso wa kuwa na utakatifu.​—Waebrania 11:26, 27, NW.

Wazazi, Ninyi Mnaweza Kuchangia

9. (a) Ni jinsi gani wazazi wanaweza kuchangia kuendesha kwa watoto wao maisha maradufu? (b) Wengine walio na umri mkubwa wanahitaji kuthamini nini na kuwa chonjo kufanya nini?

9 Kijana aliyenukuliwa mwanzoni alionelea hivi: “Jambo lililofanya mimi nisipendwe na wengi shuleni ndilo lililoleta tabasamu ya ukubali kwenye maskani yetu. Lakini mimi nilihitaji zaidi ya hilo. Mimi nilihitaji mtu fulani ambaye ningeweza kushikamana naye, kuongea naye, na kumwambia siri zangu, na mimi sikuwa nikipata jambo hilo kutoka kwa wazazi wangu.” Wazazi, je! ninyi ni waangalifu msichangie watoto wenu kuendesha maisha maradufu? Je! ninyi mnawaandalia fikira za kibinafsi na mwongozo wanaohitaji? Ni lazima walio na umri mkubwa wathamini kuna mikazo mikubwa sana, yenye kufukua imani, ambayo vijana wetu wanakabili shuleni kisha wawe chonjo kufanya kila jambo linalowezekana ili kuwatia moyo na kuwasaidia.​—Zaburi 73:2, 3; Waebrania 12:3, 12, 13.

10. (a) Ni udadisi gani ambao wazazi wana daraka la kuutolea maelezo? (b) Mara nyingi tokeo ni nini wakati wazazi wanaposhindwa kuandaa mwongozo?

10 Mara nyingi maswali ya kijana yanazungukia mahusiano pamoja na washiriki wa jinsia ile tofauti, habari ambayo ni jambo la kusikitisha kwamba wazazi wengi huiepuka. “Wao hawakuwa kamwe na maongezi ya kinaganaga pamoja nami,” akasimulia mwanafunzi mmoja mrembo wa miaka 15 mwenye kuheshimiwa kwa kisomo kizuri. “Kila jambo ambalo mimi nilijifunza juu ya ngono nililazimika kujifunza mimi mwenyewe. . . . Mimi niliaibika mno kutokeza habari hiyo ingawa kuna mambo mengi sana niliyotaka kujua.” Tokeo lilikuwa nini? Yeye alisema: “Ule ukuta usioonekana ulizidi kuwa mnene kati ya wazazi wangu na mimi, na mimi nikawa msichana mdadisi sana mpumbavu na mwenye kugeuzwa-geuzwa na maoni ya watu.” Ndiyo, yeye alijiacha ashindwe na matongozi ya kingono ya mwanamume kijana, lakini wewe ungesema ni nani aliyeshiriki daraka kwa jambo hili?​—Mithali 22:3; 27:12,

11. (a) Ni jinsi gani wazazi wanavyoweza kuonyesha kwamba wanapenda watoto wao? (b) Inaelekea vijana wataitikia upendo huo jinsi gani?

11 Ni jambo muhimu wazazi waonyeshe vijana wao kwamba wao wanawapenda kikweli kwa kutumia wakati pamoja nao, kushiriki katika maongezi ya usiri, na kuwaandalia miongozo. (Mithali 15:22; 20:18) “Mimi nina hisia ya kwamba wao wangenijali mimi kweli kweli wangefanya sheria fulani-fulani,” akaonelea kijana mwingine. Hata ikiwa vijana wanaonea uchungu sheria na virekebi-rekebi vyenu sasa, baadaye wao watatazama nyuma kwa kuvithamini. Kijana mmoja aliandikia mama yake hivi: Nikiwa mmoja ambaye nilijaribu-jaribu mipaka daima, nikitafuta visehemu na njia zilizo rahisi kuponyokea zile sheria na virekebi-rekebi vigumu, mimi nashukuru sana kwamba wewe ulinibana sawasawa.” Kwa hiyo onyesha kwamba wewe unapenda watoto wako kwa kutaka kwamba wao wajipatanishe na miongozo yako. Usipate kamwe kuchangia kuendesha kwao maisha maradufu kwa kukosa kufungua njia za mawasiliano au kwa kukosa kuwapo wakati wanapokuhitaji wewe!

12. Ni mwelekeo gani usio wa hekima wa wazazi fulani ambao huchangia kuendesha maisha maradufu kwa watoto wao?

12 Wazazi wanaweza pia kuchangia kwa njia tofauti kuendesha kwa watoto wao maisha maradufu. Maelezo ya hakimu mmoja wa mahakama kuu ya New Jersey yanatoa kielezi. “Walimu,” akasema hakimu huyo, “wanajaribu kuwatia watoto nidhamu kwa makosa katika shule halafu wanagombezwa na wazazi badala ya kuungwa mkono.” Inaonekana kama wazazi fulani wanaitikadi kimakosa kwamba vijana wao hawawezi kufanya kosa lolote. Hata wakati wazee wa Kikristo au wengine wenye madaraka katika kundi wanapoleta kosa la watoto wao kwenye fikira zao, wazazi wanawapa sikio la uziwi. Kwa kufanya hivyo wanachangia mwenendo-maradufu wa vijana wao.

Kile Ambacho Hasa Ni Maisha Maradufu

13. Kwa kweli kuendesha maisha maradufu ni sawa na nini?

13 Hili ni jambo muhimu kufikiria: Kuendesha maisha maradufu kunakuwa kwa kweli ni sawa na kufanya ubandia​—kuwa mlaghai, mnafiki. (Zaburi 12:2; 2 Timotheo 3:13) Ni kuwa kama Shetani, ambaye “anaendelea kujigeuza umbile mwenyewe kuwa malaika wa nuru.” (2 Wakorintho 11:14, 15, NW) Inamaanisha pia kuwa kama hao viongozi wa kidini ambao Yesu alisema hivi juu yao: “Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu ninyi mnashabihiana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje-nje kweli kweli yanaonekana kuwa mazuri lakini ndani yamejaa mifupa ya watu wafu na ya kila namna ya ukosefu wa usafi. Katika njia hiyo ninyi pia, kwa nje-nje kweli kweli, mnaonekana waadilifu kwa wanadamu, lakini ndani ninyi mmejaa unafiki na uasi-sheria.” (Mathayo 23:27, 28, NW) Kwa uwazi, kuendesha maisha maradufu ni kosa zito dhidi ya Mungu.

14. Kwa nini mtu atake kuepuka kuendesha maisha maradufu?

14 Uhakika mwingine wa kufikiriwa kwa uzito ni huu: Mwendo wa kinafiki hauwezi kufichwa kwa wakati usio dhahiri. “Hata kwa mazoea yake mvulana hujifanya atambuliwe kwa habari ya kama utendaji wake ni wenye kutakata na mnyoofu,” Biblia inasema. (Mithali 20:11; Luka 12:1-3, NW) Ndiyo, utendaji wako, uwe ni mwema au mbaya, utakuja kujulikana mwishowe. Na Biblia inaonyesha kwamba Mungu ataadhibu wanafiki kwa ukali. (Mathayo 24:51) Kwa uhakika inakupasa wewe uepuke kuendesha maisha maradufu!

Jinsi ya Kuyaepuka!

15. Ni jambo gani ambalo litasaidia vijana kuepuka kuendesha maisha maradufu?

15 Njia moja ya kuepuka kuendesha maisha maradufu ni kuukabili uhakika wa jambo linalomaanishwa na maisha hayo halafu kujiuliza mwenyewe hivi: Je! hivyo ndivyo mimi nataka kukumbukwa, kuwa mnafiki, kuwa mwigaji wa Shetani na Mafarisayo? Bila shaka sivyo! Jambo jingine ambalo litakusaidia wewe kuepuka kuendesha maisha maradufu ni kufikiria umivu la kibinafsi na tanzia ambayo maisha kama hayo yatakuletea wewe. Kumbuka lililotukia kwa Gehazi kwa kujaribu kuishi kiuwongo. Ukoma wa Naamani ulimshika, na yeye alikuwa mkoma kwa muda wote uliobaki wa maisha yake. Na wote wawili, Anania na Safira, walipigwa na Mungu wakafa kwa kujaribu kuvaa kisingizio cha ukarimu.​—2 Wafalme 5:27; Matendo 5:5, 9, 10.

16. Ni jambo gani lililopata kijana mmoja ambaye alihusika ndani ya mtindo wa maisha ya kilimwengu?

16 Kuna vielelezo vya ki-siku-hizi pia. Kijana mmoja katika United States alikuwa ameanza kujifunza Biblia na kuhudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme. Lakini ndipo yeye alipoanza kujiingiza-ingiza katika mtindo wa maisha ya kilimwengu na akaacha ushirika. Miaka ilipita, na yeye akaandika hivi: “Karibu miezi miwili iliyopita niliomba Mungu anipelekee Shahidi mmoja kwa sababu mimi nilihisi nikitamani kuanza upya tena. Nilianza kujifunza tena wakati kombora lilipolipuka. Mwezi mmoja uliopita nilichunguzwa afya nikasemwa kuwa mwenye sarkoma ya Kaposi, ambayo ni sehemu ya ule ugonjwa mpya usiotibika wa UKIMWI.” Yeye alimalizia hivi: “Kama tu ningefuata na kutii maonyo ya Kimaandiko huko nyuma, singekuwa katika hali hii leo.” Kwa uhakika wewe unataka kuepuka matokeo yoyote hayo yenye kusikitisha! Kwa kweli ulimwengu hauna toleo la kitu chochote chenye thamani.​—1 Yohana 2 15-17.

17. Ni mfikirio gani zaidi unaopasa kusaidia vijana waepuke kuendesha maisha maradufu?

17 Jambo ambalo pia litakusaidia wewe uepuke kuendesha maisha maradufu ni kufikiria tokeo ambalo kufanya hivyo kutakuwa nalo juu ya jina la Yehova Kijana aliyetajwa katika utangulizi alisema kwamba mtu fulani aliyemwona akikubali sigareti alieleza hivi: “Mimi sikujua Mashahidi wa Yehova wangeweza kuvuta. Je! wewe si Shahidi?” Baadaye yeye alisema kwamba swali hilo lilimfanya ahisi vibaya sana kwa sababu alilokuwa akifanya lilikuwa likileta suto juu ya Yehova. Je! wewe unataka hivyo? Je! unamfikiria Mungu wetu kuwa mwenye thamani kidogo sana kama Israeli wa kale wasio waaminifu hivi kwamba utaleta aibu juu ya jina lake?​—Zaburi 78:36, 37, 41; Ezekieli 36:22.

18. (a) Wazazi wangetenda jinsi gani kama wangejua kwamba mtoto wao anaendesha maisha maradufu? (b) Kwa nini jambo hili linapasa kuzuia vijana wa Kikristo wasiendeshe maisha maradufu?

18 Zaidi ya hilo, fikiria jina na hisia za wazazi wako. “Siku ilikuja wakati wazazi wangu walipojua mimi nilikuwa nini kikweli,” akaandika kijana aliyetajwa juu. “Iliwashtua. Na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu niliona mama na baba wakilia. Wao waliumizwa sana na jambo nililokuwa nimefanya.” Labda wazazi wako wangelia, pia, kama wangejua wewe unaendesha maisha maradufu. Je! hivyo ndivyo wewe unataka? “Jina jema ni la kutamanika zaidi kuliko utajiri mkuu,” Biblia inasema. (Mithali 22:1, The Jerusalem Bible) Kwa kuendesha maisha maradufu, wewe unaangamiza jina jema lako mwenyewe. Lakini si hayo tu. Wewe pia unaharibu jina jema la wazazi wako na kuliburuta katika matope, ukiwasababishia mtwezo na kuona haya.​—Mithali 10:1; 17:21.

19. Mwenendo mbaya wa wana wa Yakobo ulileta sifa ya jinsi gani juu yake, na ni somo gani linaloweza kuchotwa kutokana na jambo hili?

19 Wana wa Yakobo wanatoa vizuri kielezi cha jinsi watoto wanavyoweza kuharibisha jina jema la wazazi wao. Wakati Dina binti ya Yakobo aliponajisiwa, ndugu zake waliwachinja wanaume wa jiji kisha wakanyakua vitu vya jiji hilo, wakisahabisha Yakobo aomboleze hivi: “Ninyi mmeniletea hali ya kukatalika miongoni mwa watu kwa kunifanya niwe uvundo kwa wakaaji wa bara.” Mungu hata alielekeza Yakobo aondoke kwenye eneo hilo. (Mwanzo 34:30; 35:1, NW) Wewe pia unaweza kusababisha jina la baba na mama yako livunde, ukiwafanya waaibike kuelekezea nyuso hata jirani na rafiki zao. Kweli kweli, ni kama vile Biblia inavyosema: “Mwana mpumbavu ni kero kwa baba yake na uchungu kwa huyo [mama] ambaye alimpa uzaliwa.”​—Mithali 17:25, NW.

20. Ni kipawa gani kikubwa ambacho wazazi wa Kikristo wamefanya kiweze kupatwa na watoto wao?

20 Hata hivyo, sisi tuna uhakika kwamba wewe hutaki wazazi wako wakereke na kuona uchungu. Kwa hiyo fikiria athari za vitendo vyako juu yao. Pia, ikiwa wewe una pendeleo la kuwa na wazazi wa Kikristo, fikiria kile ambacho wao wamekupa wewe​—si uhai tu​—bali kitu fulani chenye thamani kubwa zaidi. Biblia inasema hivi juu ya Yehova: “Fadhili-upendo zako wewe ni bora kuliko uhai.” (Zaburi 63:3, NW) Kwa kukulea katika ukweli, wazazi wako wamefanya fadhili-upendo za Mungu ziweze kupatikana na wewe, kukusaidia wewe uwe na uhusiano pamoja naye. Kuwa na kitu hicho ni bora kuliko kuwa na uhai wenyewe kwa sababu hata ijapo wewe ufe, Mungu atakurudisha kwenye uhai wa milele katika Paradiso.

Saidia Wengine Wayaepuke

21. (a) Vijana wanaojua juu ya kosa la wengine wana daraka gani? (b) Ni kielelezo gani kizuri ambacho mmoja mwenye umri wa miaka 13 aliandaa?

21 Namna gani ikiwa wewe unajua juu ya mtu fulani anayeendesha maisha maradufu? Kwanza, mtie moyo mtu huyo afikie wazee. Na namna gani ikiwa yeye anakataa kufanya hivyo? Basi ni daraka lako la Kimaandiko kuripoti jambo hilo. (Walawi 5:1) Sisi tunang’amua kwamba huenda hili lisiwe jambo rahisi, lakini ndilo jambo lililo sawa kufanya. “Majeraha yenye kutiwa na mpenzi ni ya uaminifu,” Biblia nasema. (Mithali 27:6, NW) Baada ya kusikia hotuba yenye kueleza daraka lake la Kimaandiko, msichana mmoja wa miaka 13 aliendea rafiki yake ambaye alijua alikuwa akijitia katika kosa akamwambia anapaswa kuungamia wazee. “Nilienda nikauliza nione kama yeye alikuwa ameongea na mzee yeyote,” msichana huyo anaandika. “Yeye hakuwa amefanya hivyo. Kwa hiyo nikaenda na kuongea na mmoja wao.” Kisichana huyo aliuliza: “Je! mimi nilifanya jambo lililo sawa kwa kumripoti ‘aliyekuwa rafiki yangu mkubwa zaidi?’” Bila shaka alifanya! Ingawa huenda matokeo ya mara hiyo ya kufanya hivyo yakawa yenye kutia kihoro, tokeo baadaye linaweza kuwa lenye kutia shangwe, hata lenye kuokoa uhai kwa mtenda kosa.​—Waebrania 12:11.

22. Ni mwendo gani wa hekima ambao vijana wanatiwa moyo wachukue, na tokeo lao litakuwa nini?

22 Hata hivyo mambo yote haya yanaweza kuepukwa ikiwa wewe huendeshi maisha maradufu pale mwanzo. Kwa hiyo uwe mwenye hekima. Sitawisha uhusiano imara wa kibinafsi pamoja na Mungu, kama vile ungefanya pamoja na rafiki wa karibu. Fanya hivi kwa kumpelekea sala kwa ukawaida, kwa kuomba msaada wake, na kwa kujifunza Neno lake, Biblia, kwa bidii-endelevu ili uje kuthamini kikweli sifa zake. Vijana, hapo ninyi mtakuwa wabarikiwa na mtafanya moyo wa wazazi wenu utereme. Lakini jambo lililo la maana hata zaidi, mtafanya moyo wa Yehova utereme.​—Mithali 27:11.

Wewe Ungejibu Jinsi Gani?

◻ Kwa nini vijana fulani huendesha maisha maradufu?

◻ Wazazi fulani wanachangia jinsi gani kuendesha maisha maradufu kwa watoto wao?

◻ Kwa kweli kuendesha maisha maradufu kunakuwa sawa na nini?

◻ Vijana wanaweza kuepukaje kuendesha maisha maradufu?

◻ Ni daraka gani ambalo vijana wanalo ikiwa wanajua juu ya vijana wengine ambao wametenda makosa mazito?

[Picha katika ukurasa wa 18]

Kuongea kwa usiri kunaonyesha upendo wa mzazi

[Picha katika ukurasa wa 20]

Ikiwa wewe unajua kwamba mwingine ametenda kosa zito, mtie huyo moyo aripoti jambo hilo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki