Kudumisha Umoja Wetu wa Kikristo
“WAZIA kwamba wewe unaitwa ndugu au dada,” akaandika mwandikaji mmoja Mkatoliki Domenico Mosso, “si na padri, bali na bwana mmoja wa makamo aliye karibu na wewe au na yule bibi kijana wa kupendeza ambaye amewasili sasa hivi akakaa upande wako wa kuume. ‘Eti umesema nini?’ ‘Nimesema, habari ya asubuhi ndugu.’ ‘Unathubutuje kusema hivyo . . . Mimi sikujui hata kidogo, sasa mbona wajifahamisha mno kwangu? Ingawaje, sisi tumo kanisani.’”
Uhalisi wa udugu unakosekana kweli kweli ndani ya makanisa ya Jumuiya ya Wakristo. Hiyo inaonyesha ukosefu wao wa muungamano wa Kikristo. Hata hivyo, sivyo ilivyo kuhusiana na Mashahidi wa Yehova. Sisi tunaweza kuitana ndugu na dada kwa uhuru, kama wafuasi wa mapema wa Yesu. (2 Petro 3:15) Hata twende wapi katika ulimwengu, upokezi mchangamfu wa kidugu unakuwa kwenye ukaribu ule ule ambao Jumba la Ufalme la karibu zaidi linapatikana. Muungamano unadhihirika pia katika uhakika wa kwamba makundi yote yanafuata kiolezo kile kile kimoja cha maagizo na kwamba Mashahidi wote wanajihusisha katika kuhubiri zile “habari njema za ufalme.”—Mathayo 24:14, NW.
Katika ule usiku wa kabla ya kufa kwake, Yesu Kristo alisali hivi: “Mimi nafanya ombi . . . kuhusu wale wanaotia imani katika mimi kupitia neno lao; ili kwamba wao wapate kuwa mmoja, sawa na vile wewe, Baba, ulivyo katika muungano pamoja na mimi na mimi katika muungano pamoja na wewe.” (Yohana 17:20, 21, NW) Kumbukumbu la maandishi ya Biblia linaonyesha kwamba Yehova Mungu alijibu sala ya Yesu. Miongoni mwa Wakristo wa mapema, uhasama wa muda mrefu kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi ulipotelea mbali kupitia ile kani yenye kuungamanisha ya mafundisho ya Kikristo.—Wagalatia 3:28.
Hata hivyo, ilichukua jitihada kudumisha muungamano huu. Mtume Paulo alisihi wafanya kazi wenzake ‘watembee kwa ustahiki wa ule mwito [wa kimbingu] . . . wakijitahidi kwa moyo wa bidii kushika ule umoja wa roho katika kifungo cha amani chenye kufanyiza muungamano.” Wao hawakugawanyika-gawanyika katika mafarakano mbalimbali. Sivyo, “kuna mwili mmoja, na roho moja, hata kama vile ambavyo ninyi mliitwa katika lile tumaini moja ambalo ninyi mliitwa kwenye hilo; Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja; Mungu mmoja na Baba ya wote.” Mitume, wachungaji, na walimu katika kundi waliandaliwa ili wasaidie wote “kufikia ule umoja katika imani.”—Waefeso 4:1-6, 11-14, NW.
Mashahidi wa Yehova katika nyakati za ki-siku-hizi wamedumisha kwa mafanikio “umoja” huu. Hata hivyo, mambo mbalimbali—roho ya kujitegemea, tofauti za kitamaduni na kirangi, dosari mbalimbali na makosa ya kutokamilika miongoni mwa Wakristo wenzi—yangeweza kutisha “umoja [wetu] katika ile imani.” Huo unaweza kudumishwa jinsi gani?
Kula Kwenye Meza Ile Ile Moja
Yehova hamulikii nuru kila Mkristo mmoja mmoja akiwa peke yake. Bali, Kristo aliweka rasmi jamii ya “mtumwa mwaminifu mwenye uangalifu” ili iandae habari za mafunzo ya Kimaandiko na mashauri ya wakati unaofaa kwa Wakristo katika sehemu zote za ulimwengu. (Mathayo 24:45-47, NW) Hivyo Mnara wa Mlinzi unatangazwa katika lugha 103 ili kutimiza uhitaji huo wa ulimwenguni pote.
Kula kwenye meza ya kiroho ile ile moja kumefanya mengi katika kutokeza na kudumisha umoja wa imani. Hata hivyo, nyakati fulani baadhi ya mashauri yale huenda yaonekane kuwa yasiyotumika kuhusu mabara fulani. Je! inatupasa tuhisi kwamba sisi hatuhitaji habari zile? Sivyo. Baadhi ya maonyo ya Paulo kwa Wakristo waliokuwa wanaishi katika lile jiji la Korintho lenye ukosefu wa adili na ibada ya sanamu huenda yakawa hayakuonekana kuwa yenye kutumika kikamili kwa Wakristo wenye kuishi mashambani. (1 Wakorintho 6:15, 16; 10:14) Hata hivyo, Wakristo kila mahali waliiona miandiko ya Paulo kuwa sehemu ya “yale Maandiko.”—2 Petro 3:16, NW.
Vilevile leo, makala fulani huenda zisionekane kuwa zinatumika kwa mastakimu za kienyeji kama vile nyingine zinavyotumika. Na bado inatupasa sisi tukaribishe onyo hilo la mapema, tukijua kwamba katika kizazi chetu cha mawasiliano ya kasi, maelekeo yasiyo ya kiafya yaliyoanza katika sehemu moja ya ulimwengu yanaweza kuenea kwa haraka!
Makosa ya Kutokamilika na Rai za Kupita Kiasi
Akasema mwanafunzi Yakobo: “Sisi sote tunajikwaa nyakati nyingi.” (Yakobo 3:2, NW) Kwa sababu ya kutokamilika, wanadamu wana maelekeo ya kupita kiasi katika mambo. Huenda hili lisionekane kuwa tatizo ikiwa watu wanashiriki rai (maoni) zile zile moja. Mathalani, watu wawili wanaojali sana mambo huenda wakawa na masikilizano katika mambo yao kwa uzuri kabisa. Lakini ikiwa mmoja ni mzembe-zembe na yule mwingine ni mwenye kujali sana mambo, hakungeweza kuwa na mwisho wa kuzozana!
Mashahidi wa Yehova wanatoka katika “mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na ndimi.” (Ufunuo 7:9, NW) Kama tokeo, watu mmoja mmoja miongoni mwetu huenda wakawa na maoni tofauti sana juu ya mambo kama vile ulaji, nguo, utunzaji wa kiafya, na hata kanuni za kiadabu kati ya watu. Rai hizo zenye kutofautiana hazihitaji kuingiza kati yetu kabari ya kututenganisha. Biblia inaonya dhidi ya mambo ya kupita kiasi na inatutia moyo tujitahidi kuelekea kuwa na usawaziko na kukubali sababu za mambo. “Hekima kutoka juu ni . . . yenye kuamanika, yenye kukubali sababu,” inasema Biblia.—Yakobo 3:17, NW.
Ni kweli, Biblia inashutumu wazi sana mazoea fulani. Lakini mara nyingi inatutia moyo tufuate mwendo ulio katikati ya mambo mawili yenye kupita kiasi. Fikiria yale ambayo Biblia inasema juu ya habari zinazofuata:
Kazi ya Kimwili: “Uvivu unasababisha usingizi wenye kina kirefu uingie, na nafsi ya ulegevu-legevu inaenda njaa.” (Mithali 19:15, NW) “Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.”—Mathayo 6:24.
Kuongea: “Mmoja anayefuliza kuchunga midomo yake anatenda kwa uangalifu.” (Mithali 10:19, NW) “Kwa kila jambo kuna wakati uliowekwa rasmi . . . wakati wa kufuliza kuwa mnyamavu na wakati wa kunena.”—Mhubiri 3:1, 7, NW.
Kufanya Starehe za Kirafiki: “Kwa hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa ninyi mna upendo miongoni mwa ninyi wenyewe.” (Yohana 13:35, NW) “Mguu wako usiingie katika nyumba ya jirani yako ila kwa kiasi; asije akakukinai.”—Mithali 25:17.
Kulea Watoto: “Mmoja ambaye anashikilia nyuma fimbo yake anachukia mwana wake, lakini mmoja ambaye anampenda ni yeye ambaye anamtafuta kwa nidhamu.” (Mithali 13:24, NW) “Msiwe mkichokoza-chokoza watoto wenu, ili kwamba wao wasiwe wenye kushuka moyo.”—Wakolosai 3:21, NW.
Kadiri ambavyo rai zetu zitazidi kuwa na usawaziko badala ya kupita kiasi, ndivyo uhitilafiano wetu na Wakristo wale wengine utakavyozidi kupungua. Lakini namna gani ikiwa hali za kutoafikiana zitatokeza kwa sababu ya kutokamilika? Kumbuka maneno ya Paulo kwenye Wakolosai 3:13, NW: “Endeleeni kuchukuliana mmoja na mwingine na kusameheana mmoja na mwingine kwa uhuru ikiwa mmoja ye yote ana kisababishi cha lalamiko.”
‘Yeye Alinikwaza’
Hata hivyo, watu fulani katika kundi huenda wakawa na elekeo la kugusika hisia ya hasira haraka kupita kiasi, wakichukulia wengine kuwa wanasema na kufanya mambo wakiwa na makusudio yasiyo na fadhili. Labda hiyo ni kwa sababu ya malezi ya kule nyuma. Vyo vyote ilivyo, ni jambo la kusikitisha kama nini wakati watu hao wenye kugusika hisia kwa urahisi mno wanapojiruhusu waudhiwe na vijikosa au, hata kwa ubaya zaidi, wanaposumbua-sumbua wengine kuhusu jambo hilo kwa kupanda mbegu za kukosa muungamano!
Ni kweli, Biblia inashutumu mwenendo ambao ungeweza kukwaza wanafunzi wengine. (Luka 17:1, 2) Na waliokomaa wanapaswa wawe wepesi wa kujali hisia za Wakristo wenzao. Wakati ule ule, Biblia inatushauri kwa imara dhidi ya kugusika hisia kwa urahisi mno na kukuza maudhia yaliyo katika akili yetu. (Mhubiri 7:9) Zaidi ya hilo, kueneza miongoni mwa ndugu zetu mnuno wa kukosa kuridhika kwa kufunua makosa ya mtu mwingine ni moja la mambo ambayo “Yehova anachukia.”—Mithali 6:16-19, NW.
Roho ya Mungu inaweza kutusaidia tushinde hali ya kugusika haraka mno hisia ya hasira. Badala ya kukaakaa tufikiria dosari za ndugu zetu, sisi tunaweza kufikiria mawazo ya mwelekeo chanya yenye kujenga, tukiwa na msaada wa ile roho. (Wafilipi 4:8) Hiyo inaendeleza muungamano.
Muungamano Si Unamnamoja
Hata hivyo, muungamano wa ulimwenguni pote haumaanishi kukandamiza vitabia vilivyo asili ya mtu mmoja mmoja wala kuvunjavunja ile hiari ya mtu kujichukulia hatua ya kwanza kujifanyia mambo. Mahali ambapo kanuni za Biblia zinatumika, sisi tunaterema kuacha violezo vya fikira za kujitegemea vya ulimwengu huu na kukubali uongozi wa roho ya Yehova. Na bado, katika kutekeleza utume wetu tukiwa wahubiri, mna nafasi nyingi ya mtu mmoja mmoja kuwa kama asili yake mwenyewe ilivyo naam, na kutumia uwezo wa kuwazia. Kweli kweli, mara nyingi ndugu zetu wanatumia umahiri mwingi katika kurekebisha njia zao za kutoa ushuhuda ili zilingane na mastakimu za kienyeji.
Halafu kuna uwanja mpana wa utendaji mbalimbali ambapo kanuni za Kimaandiko hazihusiki moja kwa moja, kutia na desturi fulani za kienyeji. Katika kontinenti ya Ulaya, watu hutikisana mikono mara nyingi kwa kusalimiana. Katika sehemu fulani za Mashariki ya Mbali, wao huinamiana. Lo lote la mambo hayo linakubalika kwa Wakristo. Au fikiria mavazi na kujipamba. Biblia inatoa miongozo ya msingi tu juu ya kiasi na usawaziko. Bila kuruka mipaka yayo, sisi tunaweza kufuata mambo tunayoyapendelea zaidi, huku tukijizoeza “utimamu wa akili.”—1 Timotheo 2:9, 10, NW.
Hivyo wazee wanakuwa waangalifu sikuzote kutoa shauri kwa kutegemea msingi thabiti wa kanuni za Biblia badala ya kutegemea mambo ambayo wao binafsi wanapendelea zaidi. Bila shaka, wakati mambo ya kiroho yanapohusika, wao watakuwa ndio wa mbele kabisa kuendeleza muungamano halisi. Sisi tunaweza kufanya sehemu yetu pia. Tunaweza ‘kufuliza kutahini kama sisi tumo katika ile imani’ kwa funzo la ukawaida la Biblia na vichapo vya ‘mtumwa mwaminifu.’ (2 Wakorintho 13:5, NW) Sisi tunaweza kudumisha umoja katika kazi kwa kufanya kijasiri “tangazo la peupe” la imani yetu.—Waebrania 13:15, NW.
Kwa njia hiyo sisi tutasikiza lile shauri lililovuviwa: “Sasa mimi natia moyo ninyi, akina ndugu, kupitia jina la Bwana yetu Yesu Kristo kwamba imepasa ninyi nyote kunena kwa mwafaka, na kwamba imepasa kusiwe migawanyiko miongoni mwenu ninyi, bali kwamba ninyi mpate kuungamanishwa kwa kufaa katika akili moja na katika mstari mmoja wa fikira.”—1 Wakorintho 1:10, NW.
[Picha katika ukurasa wa 30]
Kudumisha mahusiano mema, hata wakati mmoja anapokuwa na msingi wa kuudhika, ni muhimu kwa muungamano