Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 9/1 kur. 3-4
  • Shetani Je! Yeye Ni Halisi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Shetani Je! Yeye Ni Halisi?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Bado Watu Fulani Wanaitikadi
  • Shetani
    Amkeni!—2013
  • Uwe Macho​—Shetani Anataka Kukumeza!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Adui wa Uzima wa Milele
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
  • Jihadhari na Adui Yako, Ibilisi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 9/1 kur. 3-4

Shetani Je! Yeye Ni Halisi?

JE! WEWE unaitikadi kwamba Shetani yuko? Ikiwa ndivyo, inaonekana wewe ni sehemu ya wachache wanaoendelea kupungua. “Kufikia miaka ya 1980 itikadi ya kwamba kuna Ibilisi ilikuwa imetoweka isipokuwa miongoni mwa Wakatoliki wasiopenda kubadili-badili kawaida zao, wakarisma, Waprotestanti wasiopenda kubadili-badili kawaida zao, Orthodoksi ya Mashariki, Waislamu​—na wachache wenye kufuata dini za kimafumbo.” Ndivyo kinavyotaarifu kitabu Mephistopheles​—The Devil in the Modern World, kilichotungwa na Jeffrey Burton Russell.

Ingawa hivyo, si kila mmoja ambaye ameacha kuitikadi kwamba Shetani ni halisi. “Ibilisi bado yuko hai na anafanya kazi katika ulimwengu,” akasema Papa John Paulo 2 katika hotuba moja ya hivi majuzi katika Italia.

Je! papa yuko sahihi? Ikiwa ndivyo, Shetani yumo katika msimamo mwema wa kutenda atakayo ulimwenguni. Ikiwa watu hawaitikadi kuwako kwake, wao hawatampinga. Si ajabu kwamba Kardinali Ratzinger, mkuu mwenye kuongoza sana mambo ya mafundisho katika Vatikani, alitaarifu hivi: “Ibilisi anaweza kupata kimbilio katika kitu kile akipendacho zaidi, kutojulikana yeye ni nani.”

Je! Shetani yuko kweli kweli? Ikiwa sisi tunaitikadi Biblia, ni lazima tujibu ndiyo! Shetani anarejezelewa mara nyingi kwa jina katika maandishi hayo ya kikumbukumbu yaliyovuviwa. Mathalani, Paulo mwandikaji wa Biblia, akionya juu ya “mitume bandia” na “wafanya kazi wadanganyifu” waliokuwa katika kundi la Kikristo, aliandika hivi: “Na si ajabu, kwa maana Shetani mwenyewe hufuliza kujigeuza umbo mwenyewe awe malaika wa nuru.” Paulo alikuwa na rai ya kwamba Shetani ni mtu mweledi, aliye mdanganyifu.​—2 Wakorintho 11:13, 14, NW.

Basi, kwa nini kuwako kwa Shetani hakuchukuliwi kwa uzito na watu walio wengi leo? Inaelekea kwamba, jambo hilo linaonyesha roho ya kizazi kilichopo. Kwa kuwa sisi tunaishi katika ule muda ambao watu fulani wameuita wa baada ya Ukristo, imani ya kwamba hakuna Mungu, imani ya kwamba raha ya pekee ni kula maisha tu, ufuatiaji wa vitu vya kimwili, na ukomunisti ni mambo ambayo yamechukua mahali pa imani ya kidini katika jamii nyingi za watu. Mamilioni ya watu hawaitikadi tena katika Mungu, wakiona kuwako kwake kuwa jambo lisilohitajiwa kabisa kuhusiana na falsafa zao za kibinafsi. Na wamemtupilia mbali Shetani pamoja na kumtupilia mbali Mungu. Ingawa wanadai kuitikadi katika Mungu, wanadini fulani katika Jumuiya ya Wakristo wanahisi kwamba itikadi katika Shetani imekuwa kuukuu katika karne hii ya 20.

Hata hivyo, inastahili kuangaliwa kwamba kukataa Mungu si jambo jipya hata kidogo. Yapata miaka 3,000 iliyopita, Daudi mshairi Mwebrania aliandika hivi: “Asiye na akili amesema katika moyo wake: ‘Hakuna Yehova.’ Wao wametenda kwa uangamivu, wao wametenda kwa makuruhi katika kushughulika kwao.” (Zaburi 14:1; 53:1, NW) Katika mahali pengine yeye alitaarifu hivi: “Kwa kulingana na utepetevu wake wa kimadharau aliye mwovu hafanyi utafutaji; mawazo yake yote ni: ‘Hakuna Mungu.’” (Zaburi 10:4, NW) Hata huko nyuma, watu walitenda kama kwamba Mungu hakuwako. Na lazima shauri lililokatwa kimantiki liwe lilikuwa kwamba, ikiwa hakuna Mungu, hakuwezi kuwa kuna Shetani.

Bado Watu Fulani Wanaitikadi

Hata hivyo, kama ilivyokwisha kutajwa, bado watu fulani wanakubali ile itikadi ya kwamba kuna Ibilisi wa kihalisi. Kuna wale wanaoitikadi lile fundisho la kale la Kizoroasta la muungano-maradufu, wakisema kwamba wema na uovu, Mungu na Ibilisi, lazima wawe walikuwako pamoja sikuzote mmoja akiwa kando ya mwingine. Wengine hata wanasema kwamba, wema na uovu, yote mawili ni nyuso za yule Mungukichwa. Na bado kuna wengi katika Jumuiya ya Wakristo na Uislamu wanaoitikadi kuwako kwa Shetani. Kweli kweli, kwa wengi wa hawa, yeye bado yuko akiwa kiwaji-roho chenye mabawa na pembe na mkia, kinachosimamia tukio la mwisho litakalopata zile “nafsi zisizokufa” zilizogawiwa kwenda kwenye “moto wa mateso,” kwa kulingana sana na jinsi inavyoonyeshwa katika kazi za yule mchora-vielezi mwenye sifa aliye Mfaransa Gustave Doré.

Kwa uhakika, kwa watu fulani itikadi katika Shetani inakuwa ni zaidi ya hapo. Wao wanamwabudu yeye​—ama kwa jina ama kwa kawaida za kishetani au za kipepo. Kwa mileani nyingi, uchawi na ulozi ni mambo ambayo yametambulishwa na ibada ya Shetani. Hata katika kizazi chetu cha ki-siku-hizi chenye kutia-tia mashaka, bado Shetani anasitawi sana. Kwa sababu hiyo, kabla hatujazungumzia yale ambayo Biblia inasema juu ya Shetani mwenyewe, acheni tufikirie baadhi ya mambo ya uhakika kuhusu Ushetani wa ki-siku-hizi.

[Picha katika ukurasa wa 3]

Picha ya Kibuddha ya kuwazia jinsi “moto wa mateso” wa kishetani ulivyo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki