Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 9/15 kur. 28-30
  • Wakristo Imara Lakini Wenye Kupindikana

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wakristo Imara Lakini Wenye Kupindikana
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakati wa Kuwa Imara
  • Wakati wa Kuwa Mwenye Kupindikana
  • Wazee—Imara Lakini Wenye Kupindikana
  • Sitawisha Sifa ya Kukubali Sababu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mwige Yehova—Uwe Mwenye Usawaziko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 9/15 kur. 28-30

Wakristo Imara Lakini Wenye Kupindikana

ULE mti wenye fahari unaoitwa oak ni kifananishi halisi cha uimara. Wakati pepo imara zinapovuma, kwa kawaida huo hauwi na tatizo kubwa la kusimama dhidi yazo. Ingawa mti wa oak hubakia baada ya dhoruba nyingi kwa sababu una imara na ugumu au uthabiti kwa kulinganishwa na dhoruba hizo, kijinyasi kidogo hubakia pia lakini kwa sababu iliyo tofauti sana. Siri yacho ni nini? Ni kupindikana. Hicho kinapindika na hakivunjiki kinapopatwa na kani ya upepo.

Kupindikana au kuwa mgumu​—ni jambo jipi, basi, lililo la maana zaidi? Kwa kweli, Mkristo anahitaji mchanganyiko wa yote mawili. Hata hivyo, usawaziko wa uthabiti na kupindikana huenda nyakati nyingine ukawa umekosekana hata miongoni mwa baadhi ya watu wa Mungu. Wao wana kanuni za hali ya juu, lakini wachache kati yao wana elekeo la kutotaka kukubali kushindwa. Wengine wako kidogo kama ‘unyasi [tete, NW] unaotikiswa na upepo.’ (Mathayo 11:7) Wao wanajiacha washindwe na mifinyo na mavutano ya ulimwengu huu mwovu. Au huenda wao wakawa ni wenye kuvumilia mambo kufikia hatua ya kuwa waendekevu.

Kama vile Sulemani alivyosema: “Kwa kila jambo kuna majira yake.” (Mhubiri 3:1) Kwa hiyo, ni wakati gani ulio wa kuwa mgumu na ni wakati gani wa kuwa mwenye kupindikana?

Wakati wa Kuwa Imara

Wakati mmoja, Mfalme Sauli wa Israeli aliamriwa waziwazi hivi: “Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng’ombe na kondoo, ngamia na punda.” (1 Samweli 15:3) Waamaleki walikuwa na historia ya kupinga Mungu na watu wake pia na hivyo walistahiki kuuliwa mbali kabisa. (Kumbukumbu 25:17-19) Hata hivyo, “Sauli na watu wake wakamwacha hai [wakawa na huruma juu ya, NW] Agagi [mfalme wa Amaleki], na katika kondoo walio wazuri, na ng’ombe . . . , wala hawakukubali kuwaangamiza.” Kupinda kawaida za mwongozo ambako Sauli alifanya hakukukubalika kwa Yehova. “Angalia,” akatangaza mnabii Samweli, “Kutii ni bora kuliko dhabihu.”​—1 Samweli 15:9-22.

Somo lililo katika jambo hili liko wazi: Hakuwezi kuwako kupindikana wakati utii kwa Mungu unapohusika. “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu,” akasema mtume Yohana, “kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.” (1 Yohana 5:3) Yaliyopata Shadraki, Meshaki, na Abednego yanatoa kielezi juu ya umbali ambao watumishi wa Mungu lazima wawe na nia ya kufikia katika kuonyesha utii huu. Wao walikataa kuabudu ule mfano ambao Nebukadreza mfalme wa Babuloni alisimamisha. Kwa nini? Kwa sababu sheria ya Mungu ilishutumu waziwazi ibada ya sanamu. (Kutoka 20:4-6) Wao hawakusababu kwamba mastakimu zilitoa haki ya kupinda amri hii ya kimungu. Bali, wao walikataa kuacha msimamo wao kwa kupendelea kufa kuliko kukosa utii.​—Danieli 3:16-18.

Wakristo walio wengi hawana shida ya kujiweka chini ya sheria za Biblia zilizofafanuliwa wazi. Lakini Wakristo wanaambiwa hivi: “Iweni wenye kutii wale wanaoongoza kati yenu.” (Waebrania 13:17, NW) Huenda wazee wa kundi wakaonyesha nyakati fulani zilizotajwa wazi ili kundi likutane kwa ajili ya utumishi wa shambani. Au huenda wakasema waziwazi kwamba vifaa vya Jumba la Ufalme vinapasa kutumiwa kwa njia fulani. Ni kweli, hakuna andiko la Biblia linalotaja waziwazi jinsi kifaa cha upashaji joto kinapaswa kurekebishwa au ni nani anayepaswa kufanya urekebishaji huo. Hata hivyo, wakati wazee wanapofanya maamuzi hayo, je! si jambo zuri kufanya ushirikiano?

Vilevile, huenda mume akafanya maamuzi mbalimbali kwa ajili ya jamaa yake. Huenda mke Mkristo asiwe kwa lazima ameafikiana na hukumu yake katika jambo fulani, lakini yeye anatafuta kutii “sheria ya mume” wake. (Warumi 7:2) Kutii wazee, waume, wazazi, na waajiri-kazi hakupasi kukiukwa kwa kusingizia eti hali ya kupindikana ndiyo inayotafutwa kwa kufanya hivyo.​—Wakolosai 3:18-24.

Wakati wa Kuwa Mwenye Kupindikana

Hata hivyo, kuna wakati wa kuwa mwenye kupindikana pia. Mtume Paulo alionyesha hilo aliposema: “Acheni kiasi chenu kijulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5, NW) Neno la Kigiriki ambalo Paulo alitumia hapa linamaanisha “kutosisitiza juu ya nukta ya sheria; linaonyesha ule ufikirio unaotazama ‘mambo ya uhakika ya kisa fulani kwa huruma ya kibinadamu na kwa kiasi kinachofaa.’” (W. E. Vine, An Expository Dictionary of New Testament Words) Mara nyingi kuwa na kiasi kinachofaa ni jambo linalotegemea kuwa na nia ya kujirekebisha kulingana na mastakimu zilizopo.

Mathalani, misionari mmoja mwenye kutumikia katika nchi fulani ya kigeni huenda akang’amua kwamba kawaida za adabu zinazofaa katika mahali pale ni tofauti na zile za bara ambamo yeye alilelewa. Lakini ikiwa yeye anadharau njia za watu wa pale na kukataa kufanya marekebisho fulani, huduma yake itakuwa na matokeo mazuri kadiri gani? Kwa hiyo kwa hekima anajirekebisha kulingana na njia zenye manufaa za utamaduni ule mpya.​—1 Wakorintho 9:19-23.

Kwa kupendeza, mara tu baada ya kutaja wanawake wawili katika kundi ambao walikuwa na magumu ya kibinafsi, Paulo aliwatia moyo Wakristo Wafilipi wawe na kiasi kinachofaa. (Wafilipi 4:2-5) Ingawa Paulo hakutuambia hali ya ubishi wao, mara nyingi ukosefu wa kiasi kinachofaa unakuwa ndicho kiini cha mahusiano yenye mgogoro. Hakuna mmoja anayehisi kustareheka akiwa karibu na mtu fulani aliye mchambuzi au mwenye kudai kupita kiasi. “Usiwe na haki [uadilifu, NW] kupita kiasi,” Sulemani anatahadharisha, “wala usijiongezee hekima mno; kwani kujiangamiza mwenyewe?”​—Mhubiri 7:16.

Lazima Wakristo wafanye miruhusio kwa ajili ya hali za kutokamilika za wengine. Ni vizuri kama nini wakati tunapojaribu kutazama mambo kutokana na kituo cha rai ya mtu yule mwingine! Ingawa hivyo, jambo la kuhuzunisha ni kwamba Wakristo fulani katika Korintho wa kale walihangaikia sana “haki” zao za kibinafsi mpaka hata wakageukia kupeleka waitikadi wenzao mahakamani. Kwa kutangaza matatizo yao mbele ya wasioitikadi, si kwamba walileta suto juu ya kundi tu bali pia walipanua ule mwanya uliokuwa kati yao wenyewe.​—1 Wakorintho 6:1-6.

Kwa hiyo Paulo aliwatia moyo Wakristo Wakorintho walioudhika wawe na mwelekeo wa kukubali kushindwa. Yeye alihimiza hivi: “Basi imekuwa upungufu [ushinde, NW] kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang’anywa mali zenu?” (1 Wakorintho 6:7) Mkristo hufikiria kuwa ni pato kudumisha mahusiano mema pamoja na ndugu na dada zake wa kiroho.

Kuwa mwenye kiasi kunawafaa hasa wale walio na uzoezi wa kutumia mamlaka. Mathalani, huenda wazazi wakaweka wakati fulani ambao wana na binti zao lazima wawe nyumbani wakati wa jioni. Lakini tuseme mtoto anaomba apangiwe jambo lililo tofauti na ile kawaida ya mwongozo katika pindi moja? Je! haingefaa angalau kufikiria mastakimu za wazi zinazohusika? Na namna gani wazee wa Kikristo? Je! kiasi kinachofaa si moja ya sifa zao? (1 Timotheo 3:3) Ndiyo. Lakini ni wakati gani na jinsi gani inawapasa wadhihirishe sifa hiyo?

Wazee—Imara Lakini Wenye Kupindikana

Wakati mmoja mtume Petro alitofautisha wanaume “wenye kiasi” na wale ambao ‘ni vigumu kuwafurahisha.’ (1 Petro 2:18, NW) Huenda mzee akatoa madokezo fulani kusaidia ndugu afanyie maendeleo uwezo wake wa kuhutubu. Lakini ikiwa mzee anatumia kiwango kigumu sana na kukosa kufikiria elimu, uwezo mbalimbali, na mastakimu za ndugu yule, ni jambo gani ambalo lingeweza kutokea? Huenda ndugu yule akaona uchungu juu ya shauri lile au akavunjika moyo sana, akikata shauri kwamba wazee ni ‘wagumu mno kufurahishwa.’

Lazima wazee wawe wenye kupindikana juu ya kutumia kawaida za mwongozo katika kundi. Haiwapasi kamwe kuruhusu kawaida za miongozo ‘zitangue neno la Mungu’ kwa kuzipa kawaida hizo uzito mkubwa zaidi ya zile kanuni kamilifu za Neno la Yehova.​—Mathayo 15:6; 23:23.

Inafaa wazee wawe wenye kupindikana wakati kanuni za Kimaandiko zinapokuwa hazivunjwi na kupindikana huko. Mathalani, huenda wao wakaona kwamba kuweka akiba ya viti hukatazwa sana kwenye mikusanyiko mikubwa yenye kusongamana watu. Lakini je! ni lazima hiyo kawaida ya mwongozo ifikilizwe katika kundi dogo ambamo viti ni tele? Au huenda wazee wakahisi kwamba kwa ujumla namna fulani ya mavazi​—kama vile jaketi (koti) na tai kwa wanaume​—linafaa kwa kazi ya kuhubiri mlango kwa mlango. Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika kundi moja katika bara moja la Amerika ya Kusini. Hata hivyo, mzee mmoja huko akapata habari kwamba mwanamume kijana mmoja alikuwa akisita kushiriki habari njema pamoja na wengine. Sababu? Yeye hakuwa na pesa za kununua jaketi na tai. Mzee huyo alikata shauri kwamba ilifaa kupindikana na kwa hiyo akamtia moyo huyo mwanamume kijana aanze kushiriki imani yake pamoja na wengine.

Lazima kupindikana kuonyeshwe pia katika kushughulikia visa vya kihukumu katika kundi. Ingawa kosa lile lingestahikisha kutengwa na ushirika kwa mtenda-kosa, namna gani ikiwa toba inaonyeshwa? Yehova aliweka kiolezo kinachofaa katika shughuli zake pamoja na watu wa Ninawi. Mungu alikuwa amemwambia Yona hivi: “Zimebaki siku arobaini tu zaidi, na Ninawi utapinduliwa.” Hata hivyo, wakati watu walipodhihirisha toba, Yehova hakusisitiza juu ya kufuatiliza uharibifu uliotangazwa. Yeye alitambua kwamba mastakimu zilikuwa zimebadilika. (Yona 3:4, 10, NW) Vivyo hivyo, wazee wanapaswa kuona upendezo katika ‘kusamehe kwa njia kubwa’ mahali ambapo pana ithibati ya wazi ya toba ya kweli.​—Isaya 55:7, NW.

Si rahisi kudumisha usawaziko kati ya uimara na kupindikana. Kwa asili wanadamu wasiokamilika wanaonekana kuwa wana maelekeo ya kupita kiasi katika pande zote mbili. Hata hivyo, Wakristo wanaojitahidi kuwa imara lakini wenye kupindikana watathawabishwa kwa wingi. Kwa sababu wao wanajaribu kuwa wenye kupindikana, wao watafurahia mahusiano bora pamoja na wengine na wataepuka msukosuko mwingi wa hisia-moyo. Waaidha, kwa sababu wazee waliowekwa rasmi ni imara, wenye uthibitifu katika kazi zilizo njema wakiwa washika-ukamilifu, wao wanaweka kielelezo kinachovuta uhakika na ushirikiano wa kundi zima, huku wote wakisonga mbele pamoja wakiwa na lile tumaini la uhai wa milele.​—Isaya 32:2; 1 Wakorintho 15:58.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki