Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 12/15 kur. 3-5
  • Je! Biblia Inastahili Kufanyiwa Fasiri Yoyote Tu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Biblia Inastahili Kufanyiwa Fasiri Yoyote Tu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Acha Mtungaji Mwenyewe Ajisemee
  • Ni Nini Adhabu ya Dhambi?
  • Ni Nini Kitakachopata Dunia Mwishowe?
  • Sababu kwa Nini Haistahili Kufanyiwa Fasiri Yoyote Tu
  • Je, Kweli Habari Njema Imetoka kwa Mungu?
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Siku Ya Hukumu—Wakati wa Tumaini!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Kufasiriwa kwa Biblia Huathiriwa na Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Dunia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 12/15 kur. 3-5

Je! Biblia Inastahili Kufanyiwa Fasiri Yoyote Tu?

“WEWE unaruka-ruka tu katika Biblia, ukichagua-chagua maandiko yanayofaana na fasiri yako,” ndivyo alivyolalamika bibi yule kwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova aliyekuwa akizuru mlangoni pake.

Lakini je! kwa kweli kurejeza kwenye maandiko katika sehemu tofauti-tofauti za Biblia ni uthibitisho wa kwamba mtu anajaribu kuifasiri ili ifaane na mawazo yake mwenyewe? Na ikiwa ndivyo, je! hiyo inamaanisha kwamba Biblia inastahili kufanyiwa fasiri yoyote tu​—yoyote ile ikiwa halali sawasawa tu na ile nyingine?

Acha Mtungaji Mwenyewe Ajisemee

Ijapokuwa Biblia ina Mtungaji mmoja tu, Yehova Mungu, ina waandikaji wengi. Hawa waandikaji wa Biblia wapatao 40 hawapingani kamwe​—jambo ambalo, likitajwa kwa kupitia tu, ni uthibitisho wa kwamba mtungaji ni Mungu​—hata hivyo hakuna mwandikaji yeyote mmoja wa Biblia anayesema yote kuhusu habari yoyote moja. Kwa hiyo ili kuelewa Mtungaji wa Biblia anasema nini juu ya habari fulani, inahitajiwa kabisa kukusanya pamoja maandiko yote yanayohusiana na habari inayozungumziwa. Hivyo ndivyo alivyokuwa akijaribu kufanya Shahidi aliyetangulia kutajwa.

Yeye alikuwa akifanya lililo sawa. Mathalani, fungua Biblia yako kwenye Warumi sura ya 9. Hapo utapata kielelezo cha kutokeza wazi juu ya jinsi Paulo Mkristo mwaminifu alivyofanya jambo ilo hilo. Katika sura hiyo moja tu, Paulo ananukuu mara 11 kutokana na sehemu nyinginezo za Biblia. Huenda mchambuzi fulani hata akashtaki kwamba Paulo anafanya ‘uruka-rukaji’ mwingi sana. Akianza na kitabu cha kwanza cha Biblia, yeye anaruka kwenda kwenye kitabu cha 39, kabla ya kuendelea na cha 2, cha 28, na mwishowe, kitabu cha 23 cha Biblia.a

Bila shaka, lingalikuwa kosa Paulo kutumia maandiko kwa njia isiyopatana na habari zenye kuyazunguka na kuyapinda yafaane na mawazo yake mwenyewe ya kibinafsi. Lakini Paulo hakuwa na hatia ya jambo hilo. Hata hivyo, inaonekana kwamba Wakristo fulani wa mapema walikuwa na hatia hiyo kwa maana mtume Petro ananena juu ya “mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe.”​—2 Petro 3:16.

“Mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo” yanaweza kueleweka vibaya kwa urahisi. Hata kazi za waandikaji maarufu kama Shakespeare hutukia kwamba zikafanyiwa fasiri mbalimbali​—kwa uwazi zikiwa si zote zilizo sahihi. Kwa sababu hiyo, si ajabu kwamba ndivyo ilivyo kuhusu Biblia. Kama Shakespeare angalikuwa hai bado, sisi tungeweza kumuuliza hivi: “Wewe ulimaanisha nini hasa?” Hata hivyo, hiyo haiwezekani; wala haiwezekani sisi kuomba waandikaji wa Biblia watoe ueleweshaji zaidi. Jambo la kufurahisha ni kwamba, bado tunaweza kumuuliza Mtungaji wayo, kwa maana yeye yuko hai! (Zaburi 90:1, 2) Naye ameahidi kuwapa mwongozo huo wa kiroho watu wenye imani wanaomwomba huo.​—Luka 11:9-13; Yakobo 1:5, 6.

Alipokuwa Misri, Yusufu mtumishi mwaminifu wa Mungu alitambua umaana wa kuomba mwongozo wa kimungu alipoagizwa kufasiri ndoto moja ambayo Mungu alikuwa amempa mtawala wa Misri. “Kufasiri si kazi ya Mungu?” yeye akauliza. Baada ya Yusufu kutoa fasiri iliyo sahihi, moyo ulisukuma Farao kusema: “Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?” Halafu akasema hivi kwa Yusufu: “Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.”​—Mwanzo 40:8; 41:38, 39.

Unamna-namna wa fasiri zenye kupingana tunazopata leo miongoni mwa Wakristo si kosa la Mtungaji wa Biblia, wala si kosa la waandikaji wa Biblia. Wakiwa wanabii wa Mungu, wao “walisema kutoka kwa Mungu wakati walichukuliwa na roho takatifu.” (2 Petro 1:20, 21, NW) Ni kosa la waandikaji wa Biblia ambao wamekuwa hawakufuata miongozo ya roho ya Mungu katika kuruhusu Mungu afasiri Neno lake mwenyewe. Wao wameruhusu mawazo ya kibinafsi yawazuie kuona wazi yale yanayosemwa na Mtungaji mwenyewe wa Biblia. Acheni tuchukue vielelezo viwili.

Ni Nini Adhabu ya Dhambi?

Watu fulani wamefundishwa kuitikadi kwamba adhabu ya dhambi ni mtu kuteswa-teswa milele katika moto wa mateso hali akifahamu kuwa anatendwa hivyo. Huenda watu hao wakasoma Ufunuo 20:10, NW, ambao unanena juu ya Ibilisi ‘akivurumishwa ndani ya ziwa la moto na salfa,’ nao wanaupa fasiri ya kuunga mkono rai zao. Bila shaka, hiyo haiafikiani na Mhubiri 9:5, inayosema kwamba wafu “hawajui neno lo lote”; wala haiafikiani na Warumi 6:23, inayotaarifu kwamba “mshahara wa dhambi ni mauti,” wala si umizo-umizo lenye kuhisiwa na mtu akiwa na fahamu zake. Hata hivyo, huenda watu fulani wakauliza, Kwani Ufunuo 20:10 hausemi kwamba Shetani (na, inasemekana, watu waliodanganywa naye) “watateswa mchana na usiku milele na milele”?

Katika karne ya kwanza, neno la Kigiriki kwa ‘kuteswa’​—ambalo limetumiwa hapa na Yohana mwandikaji wa Biblia​—lilidokeza wazo zaidi lenye maana ya pekee. Kwa kuwa nyakati fulani wafungwa-gereza waliteswa-teswa (ingawa hiyo ilikuwa kinyume cha sheria ya Mungu), watunza-jela walikuja kujulikana kuwa watesaji.

Mwandikaji mwingine wa Biblia anarejeza kwenye jambo hilo anaponena juu ya mtumwa asiye mwaminifu ambaye bwana wake ‘alimpeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.’ (Mathayo 18:34) Ikitoa maelezo juu ya andiko hilo, The International Standard Bible Encyclopedia inasema hivi: “Labda kutiwa gerezani kwenyewe kulionwa kuwa ‘mateso’ (na ndivyo kulivyokuwa bila shaka), na haihitaji kumaanishwa kwamba ‘watesaji’ ni wengine bali ni watunza-jela tu.”

Hivyo tunaweza kuona kwamba kwa kulinganisha maandiko na kufikiria maana iliyo katika lugha ambazo Biblia iliandikwa kwazo, inawezekana kuwasili kwenye fasiri inayoafikiana na sehemu ile nyingine yote ya Biblia. Tukiwa bila mawazo yaliyotangulia kudhaniwa mapema, tunaweza kuona wazi kwamba Ufunuo 20:10 si uthibitisho wa kuteswa-teswa milele katika moto wa mateso. Litakalopata wote walio waasi dhidi ya Mungu ni ufungwa-gereza wa milele katika kifo. Uharibifu wao ni kamili kama kwamba wao walivurumishwa ndani ya ziwa la moto halisi.

Ni Nini Kitakachopata Dunia Mwishowe?

Kulingana na 2 Petro 3:10 (KJ), “dunia pia na kazi ambazo zimo humo itachomwa kabisa.” Watu fulani wanafasiri hilo kuwa linamaanisha kwamba tufe hili litaharibiwa, inawezekana katika mteketezo mkuu wa kinyukilia. Hata hivyo, kulingana na anayosema Mtungaji wa Biblia mahali penginepo, inawezaje kuwa hivyo? Kwenye Zaburi 104:5 (KJ) mtunga zaburi, akiwa chini ya uvuvio, alitaarifu kwamba Mungu “alilaza misingi ya dunia, kwamba isipaswe kuondolewa milele.” Mfalme Sulemani mwenye hekima, pia akinena chini ya uvuvio, alisema kwenye Mhubiri 1:4 (KJ) kwamba “kizazi kimoja hupitilia mbali, na kizazi kingine huja: lakini dunia hudumu milele.”

Je! huo ni mpingano? Sivyo, Mtungaji wa Biblia, aliye Mungu wa kweli, hawezi kujipinganisha mwenyewe. Basi mistari hiyo miwili inaweza kupatanishwa jinsi gani? Acheni tufikirie habari zinazozunguka 2 Petro 3:10.

Katika mistari 5 na 6 Petro ananena juu ya Gharika ya siku ya Noa na kuifananisha, katika mstari wa 7, na uharibifu ambao utakuja “siku ya hukumu na uangamivu kamili wa wanadamu wasiomcha Mungu.” Ni nini kilichoharibiwa katika Gharika? Mstari wa 6 unasema “ulimwengu ambao ulikuwako wakati huo . . . ulipotelea mbali.” Hili tufe-dunia halikupotelea mbali. Bali, uliofanya hivyo ni mfumo mbovu wa kilimwengu. Na wakati Mungu alipoahidi Noa, kwenye Mwanzo 9:11 (KJ), kwamba hakungekuwako tena “gharika ya kuharibu dunia,” ni wazi kwamba yeye hakuwa akinena habari za sayari yenyewe, kwa maana haikuwa imeharibiwa. Kwa hiyo “dunia” ambayo itaharibiwa, kulingana na 2 Petro 3:10, ni “dunia” ya aina ile ile iliyoharibiwa kwenye Gharika​—si Dunia sayari bali jamii ya kidunia ya watu waovu.​—Linganisha Mwanzo 11:1, ambapo “dunia” (“nchi,” UV) imetumiwa kwa njia inayofanana na hiyo.

Hata utafute kwa kadiri gani, hutapata andiko lolote la Biblia linalopinganisha fasiri hiyo. Basi lazima iwe kwamba hiyo ndiyo fasiri iliyo sahihi kutoka kwa Mtungaji mwenyewe wa Biblia.

Sababu kwa Nini Haistahili Kufanyiwa Fasiri Yoyote Tu

Mke mtunza nyumba angefikiri nini juu ya kitabu cha mapishi kinachostahili kufanyiwa fasiri yoyote tu? Au kungekuwa na manufaa gani kutumia pesa kununua kamusi yenye kuruhusu msomaji wayo afasiri maana ya maneno vyovyote tu ambavyo yeye angechagua? Je! hiyo ndiyo aina ya kitabu cha mwongozo ambayo tungetarajia Mungu awape viumbe wake? Kwa kweli, kama ingekuwa hivyo, je! ingefaa hata kukinena kuwa ni kitabu cha mwongozo?

Watu wafuataji haki, wenye kumcha Mungu, hawapendezwi na kupinda Maandiko “kwa uvunjifu wao wenyewe.” (2 Petro 3:16) Ili waepuke kufanya hivyo, wanatafuta maandiko yote yenye kushughulika na habari wanayojaribu kuelewa. Yanapopatikana maandiko yenye kuonekana wazi kuwa yakipinganisha rai walizoshikilia hapo kwanza, rai hizo zinatupiliwa mbali haraka, kwa maana haziwezi kuwa sahihi.

Kwa sababu ya kuwa na aina hiyo ya mwelekeo wa usikivu, mamilioni ya watu ambao hapo kwanza walikuwa wamegawanyika kidini wameingia katika muungamano wa kidini pamoja na Mashahidi wa Yehova. Badala ya kutaka kufasiri Biblia ili ifaane na mawazo ya kibinafsi, wao wamekuwa na nia ya kujipatanisha na fasiri ile ya wazi iliyofanywa na Mtungaji mwenyewe wa Biblia.

Ni vyema kama nini kujua kwamba Biblia haistahili kufanyiwa fasiri yoyote tu. Wakati sisi tunaporuhusu Mtungaji wayo aifasiri kwa ajili yetu, hapo inakuwa kikweli ‘yenye manufaa kwa kufundisha, kwa kukaripia, kwa kunyoosha mambo, kwa kutia nidhamu katika uadilifu.’ Hapo ndipo, na ni hapo tu, itatufanya ‘tuwe na uwezo wa kutosha, tayari kabisa kwa kila kazi njema.’​—2 Timotheo 3:16, 17, NW.

[Maelezo ya Chini]

a Manukuu hayo yanapatikana katika Warumi sura ya 9, mistari 7 (Mwanzo 21:12), 9 (Mwanzo 18:14), 12 (Mwanzo 25:23), 13 (Malaki 1:2, 3), 15 (Kutoka 33:19), 17 (Kutoka 9:16), 25 (Hosea 2:23), 26 (Hosea 1:10), 27, 28 (Isaya 10:22, 23), 29 (Isaya 1:9), na 33 (Isaya 28:16).

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki