Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 1/15 uku. 30
  • Muono-Ndani Juu ya Habari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muono-Ndani Juu ya Habari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • “Si kwa Kuona”
  • Kufikiri Kubaya
  • Uhitaji Mkubwa Zaidi
  • Je, Sanda ya Turin Ndicho Kitambaa Ambacho Yesu Alifungwa Alipozikwa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Sanda ya Turin—Je, Ni Nguo ya Yesu ya Maziko?
    Amkeni!—1998
  • Kanisa La Kweli na Msingi Wake
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
  • Kanisa—Mabadiliko na Mvurugo
    Amkeni!—1993
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 1/15 uku. 30

Muono-Ndani Juu ya Habari

“Si kwa Kuona”

Michunguzo ya kisayansi ya hivi majuzi imethibitisha kwamba ile Shuka ya Turin ni kitu bandia cha karne ya 14. Hata hivyo, “Wakatoliki walitiwa moyo waendeleze heshima yao ya juu sana kwa shuka hiyo ikiwa mfano wenye kufananisha Kristo, ambaye bado anaweza kufanya miujiza,” inaripoti The New York Times. Anastasio Ballestrero, askofu mkuu wa Turin, alitaarifu hivi: “lle nguvu isiyo ya kawaida katika mfano huo wa Yesu Kristo ya kukumbusha hisia za wakati uliopita inapasa kuhifadhiwa.”

Hiyo inamaanisha nini? Inamaanisha kwamba ingawa kanisa limekiri kwamba ule mfano wenye madoa wa mwili wa mwanadamu katika shuka hiyo si ule wa Yesu Kristo, hata hivyo rai ambayo Wakatoliki waaminifu wanaendelea kuwa nayo ni kana kwamba mfano huo ndio Kristo na, hivyo, kana kwamba ni kitu kitakatifu. Kwa nini? Kulingana na Adam Otterbein, padri wa Roma Katoliki anayesimamia Udugu wa Shuka Takatifu, vikumbusha vitakatifu kama shuka hiyo vinaweza kusaidia waitikadi kumpa heshima yule ambaye mfano huo unawakilisha.

Haishangazi kwamba shuka hiyo ingebaki ikiwa kifananishi thabiti cha imani kwa Kanisa Katoliki, ijapokuwa haina uthibitisho wa kuwa ndiyo shuka ile ya kweli. “Sanamu-maumbo, picha za kupakwa rangi na aikoni . . . hupewa nafasi ya heshima kubwa sana katika zoea la Kikatoliki,” inasema The New York Times.

Je! Biblia inaunga mkono utumizi wa mifano ya jinsi hiyo katika ibada? Hapana! Neno la Mungu linasema wazi hivi: “Ikimbieni ibada ya sanamu.” (1 Wakorintho 10:14; linga Kutoka 20:4-6.) Wakristo hushauriwa waabudu Mungu “katika roho na kweli,” wala si kwa msaada wa mfano au kikumbusha fulani kitakatifu. (Yohana 4:24) Kwa kufaa, Paulo aliandika kwamba Wakristo wa kweli ‘wanaenenda kwa imani, si kwa kuona.’​—2 Wakorintho 5:7.

Kufikiri Kubaya

Kwa kupatana na elekeo la wazi kuhusu kulegezwa kwa viwango vya Kibiblia miongoni mwa wanadini, “hesabu inayoongezeka ya wanatheolojia wa United States wanatoa hoja ya kwamba makanisa ya Kikristo yanahitaji mapinduzi kuhusu ngono,” ndivyo inavyoripoti Star Tribune. Hiyo karatasi-habari ya Minnesota inataja rai zilizofafanuliwa na watu mashuhuri kama John Spong, askofu wa Newark kwa niaba ya Kanisa Episkopali la Amerika, na James Nelson, mstadi wa maadili yanayohusiana na ngono kwenye Seminari ya Muungamano wa Kitheolojia katika New Brighton. Karatasi-habari hiyo inadai kwamba wanatheolojia hao na wenginewo wanahisi kwamba makanisa yanapaswa “kuwabariki katika sherehe za kanisa wagoni-jinsiamoja wanaoishi pamoja kwa maisha ya uenzi, wakikiri kwamba watashikamana katika wajibu mmoja katika uhusiano wa kiadili, wenye upendo; . . . kuwapa baraka ya kanisa watu wazima vijana walioposana ikiwa wanaishi katika mahusiano yenye upendo, ya kujitia katika wajibu, ingawa hawajafunga ndoa”; na “kutoa idhini wakati watu wazima waliokomaa wanapofanya utendaji wa ngono kwa njia zinazojali madaraka, ingawa hawajaoana.” Kwa nini wanatheolojia hao wanaitikadi kwamba mabadiliko hayo yanahitajiwa? Spong anadai kwamba “sisi twatoa idhini ya kuwa na maisha ya ovyo-ovyo” ikiwa miungano hiyo haibarikiwi.

Hata hivyo, kile ambacho Spong na wengine wanashindwa kuona ni kwamba kule kubariki miungano hiyo ndiko kunakothibitisha kwamba makanisa yanatoa idhini ya hayo “maisha ya ovyo-ovyo.” Neno la Mungu linasema wazi. “Waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, . . . wala wazinzi, . . . wala walawiti [wanaume wanaolala na wanaume, NW].” Si kwamba wafuasi wa Kristo wanaamriwa ‘wasichangamane’ tu na watu wa jinsi hiyo bali wanaambiwa pia ‘wamwondoe yule mbaya’ miongoni mwao wenyewe.​—1 Wakorintho 5:11, 13; 6:9-11.

Uhitaji Mkubwa Zaidi

Mwaka huu, ripoti ya takwimu za Baraza la Mtangamano wa Makanisa Huru ya Uingereza imefunua kwamba zile madhehebu 15 zinazofungamana nalo zimekuwa na mshuko mwingine. Kwa mara ya kwanza, hesabu ya washiriki imeanguka chini ya milioni moja, ndivyo inavyoripoti Church Times, karatasi-habari ya Kanisa la Uingereza. Sababu ni nini? Ingawa makanisa yanasema kwamba wajibu wao ni kwa “walio wengi zaidi . . . ambao uhitaji wao mkubwa zaidi ni kukombolewa,” makala hiyo inasema kwamba “hayo Makanisa Huru yameendelea kutumia wakati na nishati nyingi mno kuhusu . . . shughuli za kijamii.” Kulingana na Church Times, “ikiwa Makanisa yanazorota, si kwa sababu ile minada yao ya mwaka haina mafanikio wala si kwa sababu hayapati wateja wa kuhudhuria tamasha zinazotayarishwa na sosaiti yao ya kitamthilia: ni kwa sababu yamekuwa hayachukui huduma yao ya ukombozi kwa uzito wa kutosha.”

Hata viongozi wa kidini wa siku ya Yesu hawakuchukua huduma yao kwa uzito. Yesu aliwachambua kwa haki kwa maana walikuwa ‘wamelitangua neno la Mungu’ kwa mapokeo yao. Alisema kwamba walikuwa wanafiki, ambao ‘waliheshimu Mungu kwa midomo yao, ila mioyo yao ilikuwa mbali naye.’​—Marko 7:6, 7, 13.

Hata hivyo, wahudumu wa kweli wa Yehova Mungu wamejitoa kwa bidii “kulihudumia lile Neno.” Wao wanachukua kwa uzito amri ya Yesu ‘kufanya wanafunzi,’ na wanafuata kielelezo cha mitume, ambao “hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.” Kwa Wakristo wa kweli, kazi hiyo ndiyo ya maana kubwa zaidi.​—Matendo 5:42; 6:4; Mathayo 28:19, 20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki