Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 2/1 kur. 4-7
  • Uzuri wa Kweli—Wewe Unaweza Kuusitawisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uzuri wa Kweli—Wewe Unaweza Kuusitawisha
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Badiliko la Utu
  • Sifa za Kikristo
  • Uzuri Katika Ulimwengu Wenye Sura Mbaya
  • Kusitawisha Ule Uzuri wa Kindani
  • Ulimwengu Mzuri Uko Mbele
  • Uzuri Huenda Ukawa wa Juujuu Tu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Urembo Ulio Bora Zaidi
    Amkeni!—2004
  • Uzuri wa Utu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Maoni Yanayofaa Kuhusu Mitindo
    Amkeni!—2003
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 2/1 kur. 4-7

Uzuri wa Kweli​—Wewe Unaweza Kuusitawisha

BIBLIA ina mashauri kwa ajili ya wanaume na wanawake pia katika jambo hili la uzuri wa sura. Kwa wanaume, inasema hivi: “Uzuri wa vijana wanaume ni nguvu yao.” (Mithali 20:29, NW) Ndiyo, nishati na siha ya vijana wanaume inaweza kuvutia sana. Lakini inakuwaje wakati sulubu ya ujana inapofifia? Mithali ya Biblia inasema hivi: “Kichwa chenye mvi ni taji ya utukufu, kama kikionekana katika njia ya haki [uadilifu, NW].” (Mithali 16:31) Uadilifu ni uso mmoja wa uzuri wa kindani. Kijana mwanamume akiusitawisha, atakuwa angali nao wakati atakapopoteza sulubu yake ya ujana yenye kuvutia.

Kwa habari ya wanawake Biblia inasema hivi: “Huenda uvutio ukawa wa bandia, na huenda uzuri wa sura ukawa wa ubatili; lakini mwanamke ambaye anahofu Yehova ndiye mwenye kujipatia sifa.” (Mithali 31:30, NW) Kijana mwanamke aliye mwenye sura nzuri na mwenye uvutio ni mwandamani wa kupendeza. Lakini namna gani ikiwa unafiki na ubatili wenye ubinafsi umejibanza nyuma ya uvutio huo wa kimwili? Hapo uzuri ule unakuwa wa juujuu tu, nao unaficha sura mbaya ya ndani. Ule uzuri wa sura unapofifia, kutabaki nini? Ingekuwa afadhali kama nini ile sura nzuri ikilandana na uzuri usiofifia wa kindani, ambao mizizi yao ni katika ‘kuhofu Yehova’!

Badiliko la Utu

Je! inawezekana kusitawisha uzuri huo wa kindani? Ndiyo. Kwa uhakika, huo ni wa lazima kwa Wakristo. Mungu huthamini uzuri wa kweli. “Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake.” (Mhubiri 3:11) Yeye hatakubali ibada ya wale ambao mwenendo wao unaonyesha wana sifa za kindani zisizopendeza.

Maneno ya mtume Paulo kwa Wakolosai yanagusia uhitaji wa kusitawisha uzuri wa kindani. Kwanza, yeye anawaonya kwa upole hivi: “Wekeni yote hayo mbali na nyinyi, hasira kisasi, kasirani, ubaya, uneni wenye matukano, na maongezi machafu yaondoke katika kinywa chenu. Msiwe mkisemezana uwongo. Uvueni utu wa zamani pamoja na mazoea yao.” Ndiyo, mtu yeyote anayezoea mambo hayo yenye sura mbaya ni chukizo kwa Mungu​—na kwa wanadamu wenye kufikiri sawasawa. Basi, Paulo anaendelea kusema: “Mjivike wenyewe utu mpya, ambao kupitia maarifa sahihi unafanywa mpya kulingana na mfano wa Yule aliyeuumba.” (Wakolosai 3:8-10, NW) Ni lazima sisi ‘tuvae’ njia ya kufikiri na kuhisi inayopatana na mapenzi ya Mungu. Ni tabia gani zilizo katika huo “utu mpya”?

Sifa za Kikristo

Biblia inaorodhesha sifa nyingi zenye uzuri zinazojumlika kuufanyiza. Lakini msingi wa uzuri huo wa kindani unaelezwa katika maneno ya Yesu: “‘Ni lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili zako zote.’ Hiyo ndiyo amri kubwa zaidi ya zote na ndiyo ya kwanza. Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Mathayo 22:37-39, NW) Upendo kwa Mungu unatuongoza tutake kuwa mtu wa aina inayomfurahisha. Upendo wa jinsi hiyo hutusukuma tunene juu yake kwa wengine, tukiwasaidia ili, nao pia, wapate kujua Muumba wao.​—Isaya 52:7.

Sifa nyingine zinazojumlika kufanyiza utu mpya zinaelezwa na mtume Paulo: “Upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujidhibiti. Dhidi ya mambo hayo hakuna sheria.”​—Wagalatia 5:22, 23, NW.

Kwa kuongezea, Biblia inasema waziwazi hivi kwa waume: “Mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa . . . Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake.” (Waefeso 5:23, 25) Na kwa wake, Biblia inasema hivi: “Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana . . . Mke asikose kumstahi mumewe.” (Waefeso 5:22, 33) Maisha ya jamaa yanavutia kama nini wakati mume anapotimiza madaraka yake kwa njia yenye upendo, isiyo ya ubinafsi, na yenye saburi! Tena inazidi kuwa rahisi kama nini mume kutimiza fungu lake ifaavyo wakati mke anapofunua uzuri wake wa kindani kwa kumtegemeza kwa upendo na kutoshindana naye au kutomchambua-chambua kupita kiasi. Maisha ya jamaa yanaweza kupendeza kweli kweli chini ya hali za jinsi hiyo.

Vielelezo vilivyotajwa katika makala iliyotangulia vilionyesha baadhi ya sifa hizo zikiwa katika kitendo. Yule msichana Mshulami alionyesha udumifu usio kigeugeu na upendo wa kina kirefu kwa mvulana wake mchungaji wakati alipokataa kumwacha yeye ili akawe na umerimeti wa jumba la Sulemani. Yusufu alionyesha wema ulio asilia yake ya ndani alipokataa kutenda dhambi dhidi ya bwana wake, Potifa. Pia alionyesha kujidhibiti alipokimbia badala ya kutongozwa na mke wa Potifa. Naye aliweka kielelezo cha upole, amani, na ustahimilivu alipokataa kuacha matukio makali katika maisha yake yamtie uchungu.

Uzuri Katika Ulimwengu Wenye Sura Mbaya

Je! sifa hizo zenye uzuri zina mafaa leo? Watu wengi wanafikiri hazina. Badala ya kuwa nazo, wao hutenda kwa kuitikia ulimwengu huu wanamoishi, wenye kujitafutia yake, na wenye unyakuzi, kwa kusitawisha sura ngumu. Wanahisi kwamba ili waendelee kuwa hai ni lazima wakose huruma, wajitakie makuu, wajitangulize na kunyakua vyote wawezavyo.

Tofauti na hivyo, Biblia inatia moyo hivi: ‘Usitende neno lolote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, hesabu mwenzako kuwa bora kuliko nafsi yako, ukiangalia si mambo yako mwenyewe, bali mambo ya wengine’ pia. (Wafilipi 2:3, 4) Jamii ya kibinadamu inazorota vibaya sana kwa sababu aina ya binadamu kwa ujumla haifuati shauri hilo zuri.

Kwa kuongezea, katika ulimwengu wa sasa, mafanikio ya mtu hupimwa kulingana na pesa zake au cheo chake. Mtu tajiri huonwa kuwa mtu mwenye mafanikio. Hata hivyo, kwa kadiri ambavyo thamani halisi zinahusika, si jambo la maana hata kidogo kama mtu ni tajiri au maskini. Kweli kweli, utajiri una hatari zao. Biblia inaonya hivi: “Wale wenye kupiga moyo konde wawe matajiri wanaanguka katika kishawishi na mtego na tamaa nyingi zisizo za akili na zenye kujaa madhara.” Inaongezea hivi: “Kupenda pesa ni mzizi wa mambo ya namna zote yenye kudhuru.”​—1 Timotheo 6:9, 10, NW.

Bila shaka, mara nyingi watu walio wabinafsi, wenye pupa, wenye kufuatia vitu vya kimwili, na wasio na huruma leo huona shangwe ya “mafanikio” kwa muda mfupi tu. Lakini hayo si mafanikio halisi, kwa kuwa gharama ya njia hiyo ya maisha yenye sura mbaya​—watu kuacha kupenda mtu binafsi, ndoa zilizovunjika-vunjika, afya mbaya, na mvurugiko wa akili kwa ujumla​—ni kubwa sana. Mwanadamu alifanyizwa kwa mfano wa Mungu, lakini wakati anapoasi kijeuri dhidi ya sifa ambazo Mungu alitia ndani yake hapo awali, hawezi kamwe kupata furaha ya kibinafsi.​—Mwanzo 1:27.

Kusitawisha Ule Uzuri wa Kindani

Basi, sisi tunaweza kukinzaje uvutano mbaya wa ulimwengu huu na kusitawisha sifa zenye usharifu, za kumcha Mungu? Wakati Paulo alipoorodhesha sifa za ‘upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, na kujidhibiti,’ aliziita “tunda la roho.” (Wagalatia 5:22, 23, NW) Kwa hiyo roho ya Mungu inahitajiwa kabisa ikiwa sisi tutasitawisha sifa hizo zenye uzuri wa kindani.

Jinsi gani? Basi, kujifunza Biblia, ambayo ilivuviwa kwa roho ya Mungu, kutatusaidia tutambue sifa hizo na tuimarishe tamaa yetu ya kuzisitawisha. (2 Timotheo 3:16) Mashahidi wa Yehova hufurahi sikuzote kusaidia katika mradi wa jinsi hiyo, kwa kuwa rai yao ni kwamba ni sehemu ya huduma yao kusaidia watu wajifunze Biblia. Kujichunguza wenyewe kwa njia ya ufuataji haki kutatuwezesha tuone tunapungukiwa wapi, nasi tunaweza kusali tuombe msaada wa roho ya Mungu katika maeneo hayo. Kufanya ushirika pamoja na waabudu wenzetu wa Mungu kutatupatia tegemezo tunalohitaji la watu wa marika yetu, na hapa pia, roho ya Mungu husaidia kwa sababu, kama vile Yesu alivyosema, “walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”​—Mathayo 18:20.

Ulimwengu Mzuri Uko Mbele

Kwa asili, hakuna yeyote kati yetu atakayeshinda kabisa hali zetu za kutokamilika, lakini tukijitahidi kusitawisha uzuri huu wa kindani, Mungu atabariki jitihada zetu. Na atatuthawabisha kwa njia nzuri ajabu. Biblia imetuwekea katika maandishi kusudi la Mungu kuleta hivi karibuni mfumo mpya wa mambo utakaokuwa tofauti kabisa na huu uliopo. Ndani yao, “wenye haki [waadilifu, 7NW] watairithi nchi [dunia, NW], nao watakaa humo milele.” (Zaburi 37:29) Yesu mwenyewe alisema: “Wenye furaha ni walio na tabia-moyo ya upole, kwa kuwa wao watarithi dunia.”​—Mathayo 5:5, NW.

Wakati huo, ule ushindani usiopendeza macho na ubinafsi wa huu mfumo wa mambo utaondolewa kisha kuwe na utulivu mwingi na ushwari. “Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua BWANA [Yehova, NW], kama vile maji yanavyoifunika bahari.” (Isaya 11:9) Kweli kweli, Mungu “atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”​—Ufunuo 21:4.

Je! hali za jinsi hiyo zinasikika kuwa za kuvutia? Zinaweza kupatikana kwa sababu tu wakaaji wa dunia wakati huo watakuwa na uzuri wa kindani wenye kutegemea msingi wa upendo kwa Mungu na kwa jirani. Na Mungu ameahidi kwamba wale wanaomtumikia yeye sasa, wakisitawisha ule “utu mpya” na kujitahidi sana kufuata viwango vyake, wataona utimizo wa ahadi hiyo. Sura nzuri, uzuri wa kimwili, haiwezi kamwe kuleta baraka za jinsi hiyo. Basi, kuna sababu nzuri kama nini ya kusitawisha huo uzuri wa kindani ulio tajiri zaidi, wenye kudumu muda mrefu zaidi, ulio na ufurahishi mwingi kwa wanadamu wenye kufikiri sawasawa na kwa Mungu mwenyewe!

[Picha katika ukurasa wa 6]

Watu wenye kuvutia kimwili wanapaswa kuepuka kuwa na ubinafsi na kutumia hali hiyo ili kufanya mambo yaende kivyao. Badala ya hivyo, wanapaswa kusitawisha uzuri wa kindani unaopendeza Mungu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki