Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/15 kur. 4-6
  • Endelea Kutafuta Kama Hazina Zilizofichika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kutafuta Kama Hazina Zilizofichika
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kuendelea Kutafuta?
  • Utafutaji Hazina Ulio na Mafanikio
  • Vito vya Kiroho Ni Tele
  • Endelea Kutafuta!
  • “Bwana Huwapa Watu Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • “Heri Mtu Yule Aonaye Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Je! Unatafuta Hekima ya Kimungu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Hekima ya Kweli Inapaza Sauti Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/15 kur. 4-6

Endelea Kutafuta Kama Hazina Zilizofichika

VITO vya hekima inayopatikana katika Neno la Mungu, Biblia, ni vya bei kubwa isiyohesabika! Vito hivyo vinafunua kusudi la kimungu na kuweka mbele yetu matazamio yanayosisimua. Vinaandaa faraja na kutuonyesha jinsi ya kufurahisha Mungu. (Warumi 15:4) Vito hivyo vinatusaidia pia tutende kwa hekima katika shughuli zetu pamoja na wengine. Kweli kweli, hekima itokayo kwa Mungu hutusaidia tutembee katika “njia ya uzima” tukiwa na uradhi na furaha.​—Zaburi 16:11; 119:105.

Kwa kuwa hekima ina manufaa nyingi, tunapaswa kuithamini sana. “Maneno yote ya kinywa changu yana haki [uadilifu, NW],” yasema hekima yenye kufananishwa na mtu. “Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi. Yote humwelea yule afahamuye, yote huelekea mbele yao waliopata maarifa. Pokea mafundisho yangu, wala si fedha, na maarifa kuliko dhahabu safi. Maana hekima ni bora kuliko marijani; wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo.”​—Mithali 8:8-11.

Kwa Nini Kuendelea Kutafuta?

Kwa kawaida, utafutaji wa vito, dhahabu, au fedha iliyozikwa hauwi na matokeo. Haihitaji kuwa hivyo kuhusu utafutaji wa hekima ya kimungu. Lakini tunaweza kufauluje katika utafutaji huu? Basi, mafanikio yanategemea jinsi tamaa yetu ya hazina hiyo ilivyo kubwa na jinsi tutajibidiisha kuitafuta. Tukitambua ustahili halisi iliyo nao, tutaithamini kuliko vitu vingine vyote vyenye thamani. Ingawaje, “kupata hekima ni bora Wee kuliko dhahabu! Na kupata uelewevu kunafaa kuchaguliwa zaidi ya fedha.”​—Mithali 16:16, NW.

Mithali 2:1-6 inahimiza hivi: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba [kuyaweka kama hazina, NW] maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara, na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, na kuutafutia kama hazina iliyositirika; ndipo utakapofahamu kumcha Bwana [Yehova, NW], na kupata kumjua Mungu. Kwa kuwa Bwana [Yehova, NW] huwapa watu hekima; kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.”

Kwa kuwa hazina zilizozikwa zimefichika, inahitajiwa kabisa kuzitafuta. Wanapokuwa wakichimba, watu fulani hudhabihu wakati wa tafrija, chakula, na usingizi. Lakini jitihada hiyo inakuwa yenye kufaa wakati hazina inapopatwa. Sisi tunahitaji kufanya dhabihu kama hizo ili kutafuta na kupata hekima ya Mungu. Kwa kuwa kutafuta hazina zilizozikwa kunahitaji uchimbaji wa kujikaza sana, ndivyo utafutaji wa hekima unavyotaka uvumilio. Haitoshi kuipitia Biblia na vichapo vya Kikristo kijuu-juu. Wakati, utafiti, na utafakari unahitajiwa ili kupata vito vya kiroho. Lakini inafurahisha kama nini tunapopata muono-ndani katika Maandiko!​—Nehemia 8:13.

Utafutaji Hazina Ulio na Mafanikio

Ndiyo, furaha hutokana na kuchimba ndani ya Neno la Mungu na kupata vito vya hekima. (Mithali 3:13-18) Kwa kusudi hilo, sisi ni wenye hekima tukijenga maktaba nzuri ya kibinafsi au ya jamaa. Lakini inapasa kuwa na nini? Zaidi ya kuwa na kamusi nzuri, Mashahidi wa Yehova wanaona kuna manufaa kuwa na tafsiri mbalimbali za Maandiko, pamoja na vichapo vya Kikristo vya Biblia, kutia na nakala za kila mwaka za Mnara wa Mlinzi na jarida linaloandamana nalo, Amkeni! Bila shaka, ni lazima maktaba itumiwe ifaavyo ndipo itusaidie sisi watafuta-hazina.

Katika utafutaji wetu wa hekima, tunaweza kuangalia vile visehemu vya habari na Maandiko vya Watch Tower Publications Index au fahirisi nyingine zilizo nyuma ya vitabu au mabuku ya magazeti yaliyojalidiwa ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Hivyo ni vyombo vya msingi vya kutafutia hekima ya kimungu. Kwa uhakika, hivyo ni kama ramani inayoweza kutuongoza kwenye “hazina zilizofichika” za hekima ya kimungu. (Mithali 2:4, NW) Ikiwa hatuna vichapo fulani vinavyohitajiwa kwa utafiti, huenda vikapatikana kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova katika eneo letu.

Sasa, acheni tutoe kielezi cha utafutaji hazina ulio na mafanikio. Katika usomaji wetu wa Biblia, huenda tukashangaa Yuda Iskariote alikufaje baada ya kusaliti Yesu Kristo. Mathayo 27:5 inataarifu kwamba Yuda “akaenda, akajinyonga.” Lakini Matendo 1:18 inasema: “Akaanguka kwa kasi [kichwa kikitangulia mbele, NW] akapasuka, matumbo yake yote yakatoka.” Basi Yuda alikufaje? Jibu linaweza kupatikana kwa kuchunguza maorodhesho ya maandiko hayo katika “Fahirisi ya Maandiko” ya kichapo Insight on the Scriptures. Inatuambia hivi: “Inaonekana Mathayo inashughulika na njia iliyotumiwa kujaribu kujiua, hali Matendo inaeleza tokeo. Kwa kuunganisha masimulizi hayo mawili, inaonekana kwamba Yuda alijaribu kujinyonga juu ya genge fulani, lakini kamba au tawi la mti likakatika hivi kwamba yeye akaporomoka chini na kupasuka juu ya miamba ya huko chini. Mazingira ya nchi kandokando ya Yerusalemu yanafanya iweze kuaminiwa hivyo.” (Buku 2, ukurasa 130) Kuhusu Insight on the Scriptures, tafadhali ona ukurasa 10 wa gazeti hili.

Utumizi wa konkodansi unatuwezesha kupata maandiko ya Biblia. Bila shaka, tunapozungumzia andiko tunapaswa kuangalia habari zinazozunguka. Kwa kutoa kielezi, acheni tufikirie Zaburi 144:12-14. Mistari hiyo inawakilisha watu fulani kuwa wakisema hivi: ‘Wana wetu ni kama miche, binti zetu kama nguzo za pembeni zilizonakishiwa kwa kupamba hekalu (jumba la kifalme, NW), ghala zetu zimejaa, kondoo zetu wanazaa kwa maelfu, ng’ombe zetu wanachukua mizigo (bila kutoka mimba, NW).’ Huenda tukafikiri maneno hayo yanatumika kwa watu wa Mungu, lakini habari zinazozunguka zinaonyesha sivyo. Katika mstari 11, mtunga zaburi Daudi anasihi akombolewe kutoka wanaonena yasiyo kweli. Wao walijisifia wana wao, binti zao, kondoo, na ng’ombe zao. Kulingana na mstari 15, wakosaji hao walisema: “Heri watu wenye hali hiyo”! Hata hivyo, kwa kinyume Daudi akapaaza sauti hivi: “Heri [wenye furaha ni, NW] watu wenye Bwana [Yehova, NW] kuwa Mungu wao.”

Vito vya Kiroho Ni Tele

Kwa uhakika furaha hutokana na jitihada zenye mafanikio za kutafuta hekima. Na vito vya kiroho vinavyoweza kupatikana kupitia utafiti ni kutia ndani majibu yanayotosheleza maswali ya Biblia. Tunapata majibu yaliyoje tukiendelea kutafuta! Kwa kielelezo, Kaini alipata wapi mke wake? Mnara wa Mlinzi (Oktoba 1, 1981, Kiingereza) ulisema hivi: “Biblia inatuambia kwamba Adamu na Hawa walipata watoto wengi, si wawili tu [Kaini na Abeli]. ‘Siku za Adamu baada ya kumzaa Sethi [mwana mwingine] zilikuwa miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.’ (Mwa. 5:4) Ukiwa na habari hizo, ungesema Kaini alipata wapi mke wake? Ndiyo, lazima awe alioa mmoja wa dada zake. Leo huenda hiyo ikawa hatari kwa watoto wowote wanaozaliwa kwa wazazi wenye uhusiano wa karibu hivyo. Lakini karibu na mwanzo wa historia ya kibinadamu, wakati ambapo aina ya binadamu ilikuwa karibu zaidi na ukamilifu, hilo halikuwa tatizo.”

Tuseme tunasoma kitabu cha Biblia cha Mithali. Kwa kuangalia yanayosemwa kwenye Mithali 1:7, NW, huenda tukashangaa hivi: ‘“Kuogopa Yehova” ni nini?’ Utafiti huenda ukatuongoza kwenye Mnara uia Mlinzi wa Mei 15, 1987, uliosema hivi: “Ni ogopo, heshima nyingi mno ya kimungu, na hofu inayofaa ya kutofanya lisilompendeza yeye kwa sababu tunathamini [fadhili-upendo] na wema wake. ‘Woga [kwa] Yehova’ unamaanisha kukubali kwamba yeye ndiye Hakimu Mkuu Zaidi Sana na Mwenye Nguvu Zote, akiwa na haki na uwezo wa kuleta adhabu au kifo juu ya wale wasiomtii. Pia unamaanisha kumtumikia Mungu kwa uaminifu, [kumwitibari] yeye kabisa kabisa, na kuchukia yaliyo mabaya machoni pake.”

Endelea Kutafuta!

Mnara wa Mlinzi unatangazwa kwa chapa ili kusaidia watafutaji hekima wenye bidii wapate vito vya kiroho vyenye bei isiyohesabika. Sote tunahitaji hekima na uelewevu wa Neno la Mungu. Mithali 4:7, 8 inasema hivi: “Bora hekima, basi jipatie hekima; naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu. Umtukuze, naye atakukuza; atakupatia heshima, ukimkumbatia.”

Kwa kujipatia muono-ndani katika Maandiko na kutumia hekima ifaavyo ndipo tu tunapoweza kupata furaha ya kweli. Ndiyo, na ni kwa kujizoeza hekima ya kimungu tu kwamba tunaweza kufurahisha Yehova Mungu. Kwa hiyo usiache chochote kikuzuie kutafuta hekima kama hazina zilizofichika.

[Picha katika ukurasa wa 4, 5]

Kutafuta hazina zili. kunahitaji uchimbaji wa kujikaza sana. Je! haitupasi kuvumilia katika utafutaji wetu wa hekima ya kimungu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki