Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 11/15 kur. 24-27
  • “Bwana Huwapa Watu Hekima”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Bwana Huwapa Watu Hekima”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Tega Sikio Lako Usikie Hekima’
  • Je, Utajitahidi?
  • Hutashindwa
  • ‘Ujuzi Unapopendeza’
  • “Kukuokoa na Njia ya Uovu”
  • “Wanyofu Watakaa Katika Nchi”
  • Elekeza Moyo Wako Kwenye Ufahamu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je, Waweza Kusitawisha Ufahamu Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • “Heri Mtu Yule Aonaye Hekima”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Uongozi Timamu kwa Vijana wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 11/15 kur. 24-27

“Bwana Huwapa Watu Hekima”

UNATUMIA wakati wako na nguvu zako kufuatia mambo gani? Je, unahangaikia kujipatia sifa nzuri? Je, unatumia wakati wako kwa madhumuni ya kukusanya mali? Namna gani kufuatia kazi-maisha ya aina fulani au kuwa mtaalamu katika nyanja fulani? Je, kusitawisha mahusiano mazuri na wengine ni muhimu kwako? Je, hangaiko lako kuu ni kuwa na afya nzuri?

Yote hayo yaliyotangulia kutajwa huenda yakaonekana kuwa muhimu kwa kadiri fulani. Lakini ni jambo gani lililo muhimu zaidi? Biblia yajibu: “Bora hekima, basi jipatie hekima.” (Mithali 4:7) Hivyo, tunaweza kuipataje hekima, nayo ina manufaa gani? Sura ya pili ya kitabu cha Biblia cha Mithali hutoa majibu.

‘Tega Sikio Lako Usikie Hekima’

Kwa maneno yaliyo kama ya baba mwenye upendo, Mfalme Solomoni wa Israeli la kale ambaye alikuwa mwenye hekima, asema: “Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu, na kuyaweka akiba maagizo yangu; hata ukatega sikio lako kusikia hekima, ukauelekeza moyo wako upate kufahamu; naam, ukiita busara [“uelewevu,” “NW”], na kupaza sauti yako upate ufahamu; ukiutafuta kama fedha, na kuutafutia kama hazina iliyositirika; ndipo utakapofahamu kumcha BWANA, na kupata kumjua Mungu.”—Mithali 2:1-5.

Je, unatambua ni nani aliye na daraka la kutafuta hekima? Katika mistari hiyo, usemi “uki-” waonekana mara tatu. Ni wazi kwamba kila mmoja wetu ana daraka la kutafuta hekima na sifa nyingine zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu. Lakini, kwanza, twahitaji ‘kukubali’ na “kuyaweka akiba” akilini maneno ya hekima yaliyorekodiwa katika Maandiko. Ili kufanya hivyo, twahitaji kujifunza Biblia.

Hekima ni uwezo wa kutumia ifaavyo ujuzi tuliyopewa na Mungu. Nayo Biblia hutuwezesha kupata hekima kwa njia nzuri kama nini! Naam, ina maneno ya hekima, kama yale yaliyorekodiwa katika vitabu vya Mithali na Mhubiri, nasi twahitaji kuyakazia uangalifu. Katika Biblia sisi hupata pia mifano mingi ambayo huonyesha manufaa za kutumia kanuni za kimungu na hatari ya kuzipuuza. (Waroma 15:4; 1 Wakorintho 10:11) Kwa mfano, fikiria masimulizi juu ya Gehazi mwenye pupa, aliyekuwa mhudumu wa nabii Elisha. (2 Wafalme 5:20-27) Je, hayatufundishi hekima ya kuepuka pupa? Na namna gani matokeo yenye msiba ya ziara ambazo hazikuonekana kuwa hatari, wakati Dina binti ya Yakobo alipokuwa akiwazuru “binti za nchi” ya Kanaani? (Mwanzo 34:1-31) Je, hatutambui kwa urahisi upumbavu wa kuwa na mashirika mabaya?—Mithali 13:20; 1 Wakorintho 15:33.

Kuzingatia hekima kwahusisha kujifunza ufahamu na uelewevu. Kwa mujibu wa Webster’s Revised Unabridged Dictionary, ufahamu ni “nguvu au uwezo unaowezesha akili kupambanua mambo.” Ufahamu wa kimungu ni uwezo wa kupambanua mema na mabaya, kisha kuchagua mwenendo ufaao. ‘Tusipoielekeza mioyo’ yetu ipate ufahamu au tusipokuwa na hamu ya kujipatia ufahamu huo, tunawezaje kukaa katika ‘barabara iongozayo kuingia katika uhai’? (Mathayo 7:14; linganisha Kumbukumbu la Torati 30:19, 20.) Kujifunza na kutumia Neno la Mungu hutupa ufahamu.

Tunawezaje ‘kuita uelewevu’—uwezo wa kutambua jinsi sehemu mbalimbali za habari fulani zinavyohusiana kwa jumla? Bila shaka, umri na uzoefu ni mambo yawezayo kutusaidia tusitawishe uelewevu zaidi—lakini nyakati nyingi haiwi hivyo. (Ayubu 12:12; 32:6-12) “Ninao ufahamu kuliko wazee,” akasema mtunga-zaburi, “kwa kuwa nimeyashika mausia yako [Yehova].” Pia aliimba hivi: “Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga [“asiye na uzoefu,” NW].” (Zaburi 119:100, 130) Yehova ndiye “mzee wa siku,” naye ana uelewevu mkubwa zaidi kushinda binadamu yeyote. (Danieli 7:13) Mungu anaweza kumpa uelewevu mtu asiye na uzoefu, akimwezesha kuwa na uelewevu mwingi zaidi kushinda wazee. Hivyo, yatupasa kujitahidi kujifunza na kutumia Neno la Mungu, Biblia.

Neno “uki-” ambalo limerudiwa-rudiwa katika mafungu ya kwanza katika sura ya pili ya Mithali linafuatwa na semi kama “kubali,” “kuweka akiba,” “kuita,” “kutafuta,” “kutafutia.” Kwa nini mwandishi anatumia semi hizi zenye kukazia maana zaidi na zaidi? Kitabu kimoja cha marejezo chasema: “[Hapa] huyo mwenye hekima anakazia uhitaji wa kujitahidi kutafuta hekima.” Naam, ni lazima tujitahidi kutafuta hekima na sifa zinazohusiana nayo—ufahamu na uelewevu.

Je, Utajitahidi?

Jambo muhimu katika ufuatiaji wa hekima ni funzo la bidii la Biblia. Lakini funzo hilo lapaswa kutia ndani mengi zaidi ya kusoma tu ili kupata habari. Sehemu muhimu katika kujifunza Maandiko ni kupanga kutafakari yale tunayosoma. Kupata hekima na ufahamu huhusisha kutafakari jinsi tuwezavyo kutumia yale tunayojifunza katika kutatua matatizo na kufanya maamuzi. Kujipatia uelewevu kwahitaji kutafakari jinsi habari mpya inavyopatana na yale ambayo tayari tunajua. Ni nani awezaye kukanusha kwamba kujifunza Biblia kwa makini hivyo kunahitaji wakati na jitihada nyingi? Wakati na nguvu unazotumia zatoshana na zile zinazotumiwa ‘kutafuta fedha na kutafutia hazina iliyositirika.’ Je, utajitahidi inavyohitajiwa? Je, ‘utanunua kabisa wakati’ ili kufanya hivyo?—Waefeso 5:15, 16.

Fikiria hazina kubwa tutakazopata ikiwa kwa moyo mnyofu tunachimba sana katika Biblia. Kwani, tutapata “kumjua Mungu”—ujuzi kumhusu Muumba wetu ambao ni imara na wenye kutuletea uhai! (Yohana 17:3) ‘Kumcha BWANA’ pia ni hazina tuwezayo kujipatia. Kicho hicho chenye staha kina thamani iliyoje! Hofu ifaayo ya kutomkasirisha yapaswa iongoze maisha yetu yote, ikiongezea maana ya kiroho yale yote tufanyayo.—Mhubiri 12:13.

Hamu kubwa ya kutafuta na kuchimba kupata hazina za kiroho yapaswa kutuchochea. Ili kurahisisha utafutaji wetu, Yehova ameandaa vifaa bora vya kuchimbia—majarida ya wakati ufaao yenye habari za kweli, Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, na pia vichapo vingine vinavyotegemea Biblia. (Mathayo 24:45-47) Yehova pia ameandaa mikutano ya Kikristo ili tupate kufunzwa Neno lake na njia zake. Twahitaji kuhudhuria mikutano hiyo kwa ukawaida, kusikiliza kwa makini yale yanayosemwa, kujitahidi sana kukaza fikira na kushika mambo makuu, na kufikiria kwa uzito uhusiano wetu na Yehova.—Waebrania 10:24, 25.

Hutashindwa

Mara nyingi, utafutaji wa vito, dhahabu, au fedha iliyo chini ya ardhi haufanikiwi. Lakini sivyo ilivyo na kutafuta hazina za kiroho. Kwa nini? “BWANA huwapa watu hekima,” Solomoni atuhakikishia, “kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.”—Mithali 2:6.

Mfalme Solomoni alisifiwa kwa sababu ya hekima yake. (1 Wafalme 4:30-32) Maandiko yafunua kwamba alijua habari mbalimbali, kutia ndani mimea, wanyama, asili ya wanadamu, na Neno la Mungu. Ufahamu alioonyesha akiwa mfalme mchanga katika kusuluhisha mabishano kati ya wanawake wawili, kila mmoja wao akidai kuwa mama ya mtoto yuleyule, ulifanya asifiwe sana katika mataifa mengi. (1 Wafalme 3:16-28) Alipata wapi ujuzi wake mkubwa? Solomoni alisali kwa Yehova kupata “hekima na maarifa” na uwezo wa “kupambanua mema na mabaya.” Naye Yehova akampa sifa hizo.—2 Mambo ya Nyakati 1:10-12; 1 Wafalme 3:9.

Sisi pia twapaswa kusali kupata msaada wa Yehova tusomapo Neno lake kwa bidii. Mtunga-zaburi alisali hivi: “Ee BWANA, unifundishe njia yako; nitakwenda katika kweli yako; moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako.” (Zaburi 86:11) Yehova alikubali sala hiyo, kwa kuwa alifanya iandikwe katika Biblia. Tunaweza kuwa na hakika kwamba atajibu sala tutoazo mara nyingi na kwa bidii, tukiomba msaada wake ili tupate hazina za kiroho katika Biblia.—Luka 18:1-8.

Solomoni asema: “Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili; yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu; apate kuyalinda mapito ya hukumu, na kuhifadhi njia ya watakatifu wake. Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, na adili, na kila njia njema.” (Mithali 2:7-9) Huo ni uhakikisho ulioje! Yehova huwapa hekima ya kweli wale waitafutao kwa unyofu na pia huwalinda wanyofu kwa kuwa wao huonyesha hekima ya kweli na kushikamana kwa uaminifu-mshikamanifu na viwango vyake vya uadilifu. Na tuwe miongoni mwa wale ambao Yehova husaidia kuelewa “kila njia njema.”

‘Ujuzi Unapopendeza’

Si watu wengi hufurahia funzo la kibinafsi la Biblia ambalo ni takwa muhimu katika kutafuta hekima. Kwa mfano, Lawrence mwenye umri wa miaka 58 asema: “Sikuzote nimefanya kazi kwa mikono yangu. Kujifunza ni jambo gumu sana kwangu.” Michael mwenye umri wa miaka 24, ambaye hakufurahia kujifunza shuleni, asema: “Nilijilazimisha kuketi na kujifunza.” Hata hivyo, tamaa ya kujifunza yaweza kusitawishwa.

Fikiria vile Michael alivyofanya. Yeye asimulia: “Nilijitia nidhamu ili kujifunza kwa muda wa saa moja na nusu kila siku. Muda si muda nikaanza kuona matokeo ya kufanya hivyo katika mtazamo wangu, maelezo yangu kwenye mikutano ya Kikristo, na katika mazungumzo yangu na wengine. Sasa mimi hutazamia kwa hamu wakati wangu wa kujifunza, na sipendi jambo lolote liukatize. Naam, hatimaye sisi huja kufurahia funzo la kibinafsi tunapoona maendeleo tufanyayo. Lawrence pia alijitahidi kujifunza Biblia, na hatimaye, akatumikia akiwa mzee katika kutaniko la Mashahidi wa Yehova.

Jitihada yenye kuendelea inahitajiwa ili kufurahia funzo la kibinafsi. Na kuna manufaa nyingi. “Maana hekima itaingia moyoni mwako, na maarifa yatakupendeza nafsi yako,” asema Solomoni, “busara itakulinda; ufahamu utakuhifadhi.”—Mithali 2:10, 11.

“Kukuokoa na Njia ya Uovu”

Hekima, maarifa, busara, na ufahamu zinaweza kukulindaje? “[Zita]kuokoa na njia ya uovu,” asema Solomoni, “na watu wanenao yaliyopotoka; watu waziachao njia za unyofu, ili kuziendea njia za giza; wafurahio kutenda mabaya; wapendezwao na upotoe wa waovu; waliopotoka katika njia zao; walio wakaidi katika mapito yao.”—Mithali 2:12-15.

Naam, wale wanaothamini hekima ya kweli huepuka kushirikiana na yeyote ‘anenaye yaliyopotoka,’ yaani, mambo yasiyo ya kweli na yasiyofaa. Busara na ufahamu hutulinda dhidi ya wale wakataao kweli na kutembea katika njia za giza, na hutulinda pia dhidi ya wale waliopotoka na wanaofurahia matendo maovu.—Mithali 3:32.

Twashukuru kama nini kwamba hekima ya kweli na sifa zinazohusiana nayo pia hutulinda dhidi ya njia mbaya ya wanaume na wanawake wasio waadilifu! Solomoni aongezea kwamba sifa hizo ‘zitakuokoa na malaya [“mwanamke mgeni,” “NW”], naam, malaya mwenye kubembeleza kwa maneno yake; amwachaye rafiki wa ujana wake, na kulisahau agano la Mungu wake. Maana nyumba yake inaelekea mauti, na mapito yake yanakwenda kwenye wafu. Katika hao wamwendeao harudi hata mmoja, wala hawazifikilii njia za uzima.’—Mithali 2:16-19.

Huyo malaya, “mwanamke mgeni,” anasemwa kuwa mwanamke aachaye “rafiki wa ujana wake”—yaelekea mume wa ujana wake.a (Linganisha Malaki 2:14.) Amesahau ile sehemu ya agano la Sheria inayokataza uzinzi. (Kutoka 20:14) Njia zake zinaelekea kwenye kifo. Wanaoshirikiana naye huenda wasiweze kamwe ‘kuzifikilia njia za uzima,’ kwa kuwa huenda siku moja wakafikia hatua ambayo hali yao haiwezi kurekebishwa, yaani kifo, ambacho hakiwezi kubadilishwa. Mtu wa ufahamu na busara anajua mitego ya ukosefu wa adili naye huepuka kwa hekima kunaswa nayo.

“Wanyofu Watakaa Katika Nchi”

Akijumlisha kusudi la mashauri yake kuhusu hekima, Solomoni asema: “Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, na kuyashika mapito ya wenye haki.” (Mithali 2:20) Hekima inatimiza kusudi zuri kama nini! Inatusaidia kuishi maisha yenye furaha na yenye kuridhisha yanayokubalika kwa Mungu.

Fikiria pia baraka nyingi watakazopata wale ‘wanaokwenda katika njia ya watu wema.’ Solomoni aendelea kusema: “Maana wanyofu watakaa katika nchi, na wakamilifu watadumu ndani yake. Bali waovu watatengwa na nchi, nao wafanyao hila watang’olewa.” (Mithali 2:21, 22) Na uwe miongoni mwa wakamilifu watakaodumu milele katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu.—2 Petro 3:13.

[Maelezo ya Chini]

a Neno “mgeni” lilitumiwa kuwahusu wale waliokiuka Sheria, hivyo wakajitenga na Yehova. Hivyo, malaya—na si lazima mtu wa kutoka nchi ya kigeni—anaitwa “mwanamke mgeni.”

[Picha katika ukurasa wa 26]

Solomoni alisali apate hekima. Nasi twapaswa kufanya hivyo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki