Maisha na Huduma ya Yesu
Tajiri na Lazaro
YESU amekuwa akiongea na wanafunzi wake juu ya utumizi unaofaa wa mali za kimwili, akieleza kwamba hatuwezi kuwa watumwa wazo na wakati ule ule tuwe watumwa wa Mungu. Mafarisayo pia wanasikiliza, na wanaanza kumcheka Yesu kwa dharau kwa sababu wao ni wapenda pesa. Kwa hiyo yeye anawaambia: “Ninyi ndinyi mnaojidai haki [uadilifu, NW] mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu.”
Wakati umefika ili mambo yawageuke watu walio matajiri katika mali za kilimwengu, mamlaka ya kisiasa, na udhibiti na uvutano wa kidini. Wanapasa kushushwa cheo, na wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho wanahitaji kuinuliwa juu. Yesu anaelekeza kwenye badiliko hilo anapoendelea kusema hivi kwa Mafarisayo:
“Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana [Mbatizaji]; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu. Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati.”
Waandishi na Mafarisayo wana kiburicha kudai kwamba wao wanashika sana Sheria ya Musa. Kumbuka kwamba Yesu aliporudishia mtu fulani muono wa macho katika Yerusalemu, wao walijisifu hivi: “Sisi tu wanafunzi wa Musa. Sisi tunajua ya kuwa Mungu alisema na Musa.” Lakini sasa Sheria ya Musa imetimiza kusudi layo la kuongoza wanyenyekevu kwenye Mfalme aliyeonyeshwa na Mungu, Yesu Kristo. Kwa hiyo huduma ya Yohana inapoanza, watu wa aina zote, hasa wanyenyekevu na maskini, wanajikaza ili wawe raia za Ufalme wa Mungu.
Kwa kuwa sasa Sheria ya Musa inatimizwa, wajibu wa kuishika unapasa kuondolewa. Sheria hiyo inaruhusu talaka kwa sababu mbalimbali, lakini sasa Yesu anasema: “Kila mtu atakayemwacha [atakayetaiiki, NW] mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini.” Lo, hayo matamko rasmi lazima yawe yanawaudhi Mafarisayo kweli kweli, hasa kwa kuwa wao huruhusu talaka kwa sababu nyingi!
Akiendelea na maneno yake kwa Mafarisayo, Yesu anasimulia kielezi kinachohusu wanaume wawili ambao cheo au hali yao inabadilishwa sana hatimaye. Je! wewe unaweza kujua wanaume hao wanawakilisha nani na kinachomaanishwa na hali zao zilizogeuka zikawa kinyume?
Yesu anaeleza kwamba, “palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.”
Hapa Yesu anatumte tajiri huyo kuwakilisha viongozi wa kidini Wayahudi, kutia ndani si Mafarisayo na waandishi tu bali pia Masadukayo na wakuu wa makuhahi. Wao ni matajiri katika mapendeleo na fursa za kiroho, na wanajiendesha kama yule tajiri. Nguo zao za rangi ya zambarau iliyo ya kifalme zinawakilisha cheo chao chenye upendeleo, na ile kitani nyeupe ni picha ya kujiona kwao kuwa waadilifu.
Jamii hii ya tajiri mwenye kiburi inawadharau kabisa kabisa maskini wenye cheo cha kawaida tu, wakiwaita ‛am ha·’aʹrets, au watu wa dunia. Hivyo Lazaro mwombaji maskini anawakilisha watu ambao viongozi wa kidini wanawanyima ulishaji wa kiroho unaofaa na mapendeleo. Kwa sababu hiyo, kama vile Lazaro aliyejawa na vidonda, watu wa cheo cha kawaida wanadharauliwa kuwa na maradhi ya kiroho na wenye kufaa kushirikiana na mbwa tu. Hata hivyo, wale wa jamii ya Lazaro wana njaa na kiu kwa ajili ya ulishaji wa kiroho na kwa hiyo wako langoni wakitafuta kupokea makombo yoyote haba ya chakula cha kiroho ambayo huenda yakaanguka kutoka meza ya tajiri.
Sasa Yesu anaendelea kueleza mabadiliko katika hali ya tajiri na Lazaro. Hayo ni mabadiliko gani, na yanawakilisha nini Maswali hayo yatafikiriwa katika toleo linalofuata la gazeti letu. Luka 16:14-21; Yohana 9:28, 29; Mathayo 19:3-9; Wagalatia 3:24; Wakolosai 2:14.
◆ Huduma ya Yohana inapoanza, Yesu anaonyesha ni badiliko gani linalotukia?
◆ Ni kitu gani kitaondolewa wakati wa kifo cha Yesu, na hiyo itaathirije lile jambo la talaka?
◆ Katika kielezi cha Yesu, ni nani wanaowakilishwa na tajiri na Lazaro?
◆ Ni habari gani tunazoweza kutazamia katika toleo linalokuja la gazeti hili?