Maisha na Huduma ya Yesu
Tajiri na Lazaro Wapatwa na Badiliko
YESU anasimulia kielezi juu ya tajiri na mwombaji maskini jina lake Lazaro. Tajiri anawakilisha viongozi wa kidini waliopendelewa kuwa na mapendeleo na nafasi za kiroho, na Lazaro anafananisha watu wa kawaida walio na njaa ya ulishaji wa kiroho. Yesu anaendeleza hadithi yake, akieleza badiliko la kutazamisha katika hali za wanaume hao.
“Halafu,” Yesu anasema, “yule masikini alikufa, akachukuliwa na malaika katika kifua chake Abrahamu; yule tajiri alikufa vilevile, akazikwa. Katika Hadeze akiwa katika azabu [mateso, UV], akanyanyua macho yake, akaona Abrahamu mbali na Lazaro katika kifua chake.”
Kwa kuwa tajiri na Lazaro si watu halisi bali wanafananisha jamii za watu, ni jambo la kiakili kuchukua vifo vyao kuwa vya ufananisho. Vifo vyao vinafananisha au kuwakilisha nini?
Yesu amemaliza sasa tu kuelekeza kwenye badiliko la hali kwa kusema kwamba ‘Torati na manabii zilikuwa hata Yoane Mbatizaji, lakini tangu wakati huo ufalme wa Mungu unahubiriwa.’ Kwa sababu hiyo, Yohana na Yesu Kristo wafanyapo kuhubiri kwao ndipo wote wawili tajiri na Lazaro wanapokufa kuhusu hali zao za kwanza.
Wale walio wa jamii ya Lazaro mnyenyekevu mwenye kutubu wanakufa kuhusu hali yao ya kwanza ya kunyimwa uhitaji wa kiroho na wanakuja ndani ya cheo cha upendeleo wa kimungu. Ijapokuwa mapema kidogo walitegemea viongozi wa kidini kwa kiasi chochote kidogo kilichoanguka kutoka meza ya kiroho, sasa kweli za Kimaandiko zinazotolewa na Yesu zinajaza mahitaji yao. Hivyo wanaletwa ndani ya kifua, au cheo chenye upendeleo, cha Abrahamu Mkubwa Zaidi, Yehova Mungu.
Kwa upande mwingine, wale wanaojumlika kuwa jamii ya tajiri wanakuja chini ya ukosefu wa upendeleo wa kimungu kwa sababu ya kukataa-kataa ujumbe wa Ufalme uliofundishwa na Yesu. Kwa njia hiyo wanakufa kuhusu cheo walichokuwa nacho cha kuonekana kama wenye upendeleo. Kwa uhakika, wananenwa kama kwamba wamo katika mteseko-teseko wa kitamathali. Sikiliza wakati tajiri anaponena:
“Baba Abrahamu, unirehemu, utume Lazaro atie [ncha] ya kidole chake katika maji apoleshe ulimi wangu; kwani ninateswa katika moto huu.” Jumbe zenye moto za hukumu ya Mungu zilizotangazwa na wanafunzi wa Yesu ndizo zinazotesa-tesa watu mmoja mmoja wa jamii ya tajiri. Wao wanataka wanafunzi waache kutangaza jumbe hizo, hivyo wakiwaandalia kadiri fulani ya kitulizo kutoka mteseko-teseko wao.
“Lakini Abrahamu alisema: Mwana, kumbuka ya kuwa ulipokea vitu vizuri katika maisha yako, kama vile Lazaro alivyopokea vitu vibaya; lakini sasa anafarijiwa, na wewe unateswa. Na zaidi ya maneno haya yote, shimo kubwa limewekwa kati yetu, sisi na ninyi; hata watu wanaotaka kutoka hapa kupita kwenu hawawezi, wala wanaotaka kutoka kule kupita hapa kwetu.”
Ni haki na inafaa kama nini badiliko hilo la kutazamisha litukie kati ya jamii ya Lazaro na jamii ya tajiri! Badiliko hilo la hali linatimizwa miezi michache baadaye kwenye Pentekoste 33 W.K., wakati nafasi ya agano la zamani la Sheria (Torati) inapochukuliwa na agano jipya. Ndipo inapoonekana wazi kwa njia isiyoweza kukosewa kwamba wanafunzi wanapendelewa na Mungu, wala si Mafarisayo na viongozi wengine wa kidini. Kwa hiyo “shimo kubwa” linalotenganisha tajiri na wanafunzi wa Yesu linawakilisha hukumu ya Mungu isiyobadilika, ya uadilifu.
Ndipo tajiri anapoomba “Baba Abrahamu” atume Lazaro “nyumbani mwa baba yangu, kwani nina ndugu watano.” Hivyo tajiri anaungama kuwa ana uhusiano wa karibu zaidi na baba mwingine, ambaye kwa kweli ni Shetani Ibilisi. Tajiri anaomba kwamba Lazaro atohoe uzito wa jumbe za hukumu za Mungu ili asitie “ndugu watano” zake, wafungamani wake wa kidini, katika “pahali hapa pa azabu [mateso, UV].”
“Abrahamu akamwambia: Wana Musa na manabii, wawasikilize wao.” Ndiyo, ikiwa “ndugu watano” hao wangetaka kuepuka kuteseka-teseka, la kufanya tu ni kuitii miandiko ya Musa na Manabii inayomtambulisha Yesu kuwa Mesiya halafu wawe wanafunzi wake. Lakini tajiri anaona haifai: “Sivyo, baba Abrahamu; lakini kama mumoja atakwenda kwao toka wafu, watatubu. Akamwambia: Wasiposikia Musa na manabii, hawatasadikishwa kama mumoja akifufuka toka wafu.” Mungu hataandaa ishara au miujiza maalumu kusadikisha watu wa jinsi hiyo. Ni lazima watu wasome Maandiko na kuyatumia ikiwa wangetaka kupata upendeleo wake. Luka 16:16, 22-31; Yohana 8:44, ZSB.
◆ Kwa nini ni lazima iwe vifo vya tajiri na Lazaro ni vya ufananisho, na vifo vyao ni picha ya nini?
◆ Mateso yaliyopata tajiri ni nini, naye anaomba yaondolewe kwa njia gani?
◆ Lile “shimo kubwa” linawakilisha nini?
◆ Ni nani baba halisi wa tajiri, na ndugu zake watano ni nani?