Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/15 kur. 12-17
  • Tegemea Yehova Uwe na Muondo-Ndani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tegemea Yehova Uwe na Muondo-Ndani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yaliyo Katika Muono-Ndani
  • Jinsi Yoshua Alivyopata Muono-Ndani
  • Jinsi Yehova Anavyotoa Muono-Ndani Leo
  • Jilinde Dhidi ya Kupoteza Muono-Ndani
  • Muono-Ndani Ambao Yehova Ametoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mzoeze Mtoto Wako Amtumikie Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Hekima Ni Ulinzi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Yoshua 1:9—“Uwe Jasiri na Imara”
    Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/15 kur. 12-17

Tegemea Yehova Uwe na Muondo-Ndani

“Mimi nitafanya wewe uwe na muono-ndani na kukuagiza katika njia unayopaswa kuendea.”​—ZABURI 32:8, NW.

1. Ni nini baadhi ya mambo yanayoamua kama maamuzi tunayofanya yatakuwa ya hekima? (Linganisha Kumbukumbu 32:7, 29.)

KILA siku tunakabiliwa na maamuzi​—mengine yakionekana kama kwamba ni madogo, mengine yakionekana wazi kuwa ya maana. Je! maamuzi yetu yatakuwa ya hekima? Hiyo inategemea sana kama sisi ni watu wa kiherehere au sisi hufikiri kabla ya kunena au kutenda. Hata hivyo, mambo ni mengi ambayo kufanya maamuzi ya hekima kunataka tuweze kuona ng’ambo ya yale yanayoonekana wazi. Huenda hiyo ikatutaka tujue tokeo la matukio ya sasa ulimwenguni litakuwa nini, hata tuwe na habari juu ya yanayotukia katika makao ya roho. Je! tunaweza kufanya hivyo? Je! inawezekana mwanadamu yeyote afanye hivyo kwa njia isiyo ya kukisia tu?

2. Ili tujiendeshe kwa kufuata mwendo wenye mafanikio maishani, tunahitaji msaada gani, na kwa nini? (Mithali 20:24)

2 Wanadamu wamepewa nguvu za kiakili zilizo za kustaajabisha kweli kweli, lakini hawakufanywa wakiwa na uwezo wa kujiendesha maishani kwa mafanikio bila kukubali kwa unyenyekevu msaada kutoka kwa Mungu. Kama alivyoandika Yeremia mnabii aliyevuviwa: “Ee Bwana [Yehova, NW] najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.”​—Yeremia 10:23.

3. Tusipotegemea Yehova kwa mwongozo, tokeo litakuwa nini? (Linganisha Mwanzo 3:4-6, 16-24.)

3 Tokeo ni nini tukipuuza uhakika huo na kujitegemea sisi wenyewe au wanadamu wengine ili kujua mambo yaliyo au yasiyo ya hekima, yanayofaa au yaliyo makosa? Kwa sababu ya kuongozwa na fikira za kusababu mambo kwa njia ya mnofu, huenda kukawa na nyakati ambapo tutaliona kuwa jema lile ambalo Mungu anasema ni baya, ambapo huenda tukauona kuwa wenye hekima mwendo ambao Mungu anauita wa kipumbavu. (Isaya 5:20) Tujapofanya hivyo bila kukusudia, huenda tukawa kikwazo kwa wengine. (Linganisha 1 Wakorintho 8:9.) Kuhusu tokeo la mwisho kwa wale wanaoendelea kutotegemea Yehova kwa mwongozo, Neno lake linataarifu hivi: “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, lakini mwisho wake ni njia za mauti.”​—Mithali 14:12.

4. Ni msaada gani ambao Yehova anawaahidi watumishi wake kwa ukarimu? (Linganisha Yeremia 10:21.)

4 Kwa sababu hiyo, sisi tunahitaji nini? Kwa usemi rahisi, tunahitaji msaada ambao Yehova anatoa. Yeye anasema hivi kwa kutia moyo: “Mimi nitafanya wewe uwe na muono-ndani na kukuagiza katika njia unayopaswa kuendea. Mimi nitatoa shauri huku jicho langu likiwa juu yako.”​—Zaburi 32:8, NW.

Yaliyo Katika Muono-Ndani

5. “Muono-ndani” ni nini?

5 “Muono-ndani” unaotajwa katika Maandiko ni nini hasa? Ni uwezo wa kuona ndani ya hali fulani, kutazama ng’ambo ya jambo linaloonekana wazi. Kulingana na Theological Wordbook of the Old Testament, neno la Kiebrania lililofasiriwa “muono-ndani” linahusiana na “maarifa ya uelewevu mwingi juu ya sababu” ya mambo. Ni maarifa ya aina inayowezesha mtu atende kwa hekima na kupata mafanikio. Kwa kupatana na maana hiyo ya msingi na ili kuwa na ladha ile ile ya kitenzi cha Kiebrania, New World Translation hutumia maneno kama ‘tenda kwa uangalifu,’ ‘tenda kwa busara,’ na ‘kuwa na mafanikio,’ zaidi ya kufasiri ‘uwe na muono-ndani.’​—Zaburi 14:2.

6. Kwa nini “mwenye kutunza midomo yake” anaweza kusemwa kuwa anatenda kwa uangalifu, au kwa muono-ndani?

6 Hivyo, “mwenye kutunza midomo yake” anasemwa kuwa ‘akitenda kwa uangalifu,’ au kwa muono-ndani. (Mithali 10:19, NW) Yeye hufikiri kabla ya kunena, akiwaza jinsi wengine watakavyoelewa anayosema, pia juu ya kama jambo awezalo kusema juu ya mtu mwingine lingekuwa la hekima, la upendo, au lenye kuhitajiwa kabisa. (Mithali 12:18; Yakobo 1:19) Kwa sababu anasukumwa na upendo kwa njia za Yehova na tamaa halisi ya kusaidia mwanadamu mwenzake, analosema linajenga wengine.​—Mithali 16:23.

7. Ni nini kilichowezesha Daudi kupata sifa ya kuwa mtu aliyetenda kwa busara?

7 Kuhusu Daudi mwana wa Yese, imeandikwa hivi: “Kila alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili [busara, NW],” yaani, kwa muono-ndani. Daudi alitambua kwamba ni mambo mengi zaidi yaliyohusika katika kazi yake wala si pigano tu kati ya wanadamu walio mashujaa wa vita. Aling’amua kwamba yeye na wanaume waliokuwa pamoja naye walikuwa wakifanya vita vya Yehova. Hivyo, Daudi alitegemea Yehova kwa mwelekezo na baraka. (1 Samweli 17:45; 18:5; 2 Samweli 5:19) Tokeo ni kwamba shughuli za Daudi za kivita zilifanikiwa.

8. Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, ni mawazo gani mengine yanayotokezwa na kitenzi kinachotafsiriwa ‘kuwa na muono-ndani’?

8 Katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, kitenzi kilichotafsiriwa ‘uwe na muono-ndani’ kimefasiriwa pia, ‘pata maana ya’ na, ‘kuwa na ufahamivu.’ (Warumi 3:11; Mathayo 13:13-15; Waefeso 5:17, NW) Kile ambacho Mungu anaahidi watumishi wake ni uwezo wa kufanya mambo hayo. Lakini yeye anawapaje muono-ndani huo?

Jinsi Yoshua Alivyopata Muono-Ndani

9. Katika Israeli ya kale, Yehova aliwapaje watu muono-ndani?

9 Katika Israeli ya kale, Yehova aliagiza Walawi wafunze taifa Sheria yake. (Walawi 10:11; Kumbukumbu 33:8, 10) Sheria hiyo ilivuviwa na Mungu, na roho ya Yehova ilikuwa ikifanya kazi juu ya ule mpango wa kitengenezo uliopewa mgawo wa kuifundisha. (Malaki 2:7) Kupitia njia hiyo, Yehova ‘alifanya Waisraeli wawe na busara,’ au akawapa muono-ndani, kama inavyotaarifiwa kwenye Nehemia 9:20, NW.

10, 11. (a) Kama ilivyoonyeshwa kwenye Yoshua 1:7, 8, ni nini kingewezesha Yoshua kutenda kwa muono-ndani? (b) Ni uandalizi gani wa mafundisho uliokuwa wa maana Yoshua authamini? (c) Ni jitihada gani ya kibinafsi iliyotakwa kwa upande wa Yoshua pia?

10 Lakini je! watu mmoja mmoja ndani ya taifa hilo wangetenda wakiwa na muono-ndani? Ili wafanye hivyo, jambo fulani lilitakiwa kwao. Wakati Yoshua alipoitibarishwa daraka la kuongoza Israeli waingie Bara la Ahadi, Yehova alimwambia hivi: “Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana [kutenda kwa hekima, NW] kila uendako. Kitabu hiki cha torati [Sheria, NW] kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana [ndipo wewe utatenda kwa hekima, NW].’ Neno la Kiebrania lililotafsiriwa ‘kutenda kwa hekima’ hapa humaanisha pia ‘kutenda kwa muono-ndani.’​—Yoshua 1:7, 8.

11 Yehova angempaje Yoshua muono-ndani huo? Si kwa kuuingiza ndani yake kimuujiza. Ufunguo wa kuupata ulikuwa Neno la Mungu lililoandikwa. Yoshua alihitaji kulijaza katika akili na moyo wake, kulisoma na kulitafakari kwa ukawaida. Kama Yoshua alivyojua, Neno la Mungu lilisema kwamba mafunzo kutokana na Sheria yangetolewa na Walawi. Hivyo, Yoshua alihitaji kuthamini jambo hilo, bila kukaa mbali na wengine kama kwamba angeweza kuielewa yote peke yake kwa sababu alikuwa na cheo chenye daraka katika taifa. (Mithali 18:1) Lilikuwa jambo la maana Yoshua awe na bidii-endelevu katika kujifunza Neno la Mungu lililoandikwa. Akifanya hivyo, bila kuacha sehemu yoyote, na akiitii, ndipo yeye angetenda kwa muono-ndani.​—Linganisha 1 Wafalme 2:3.

Jinsi Yehova Anavyotoa Muono-Ndani Leo

12. Ili tunufaike na muono-ndani ambao Yehova hufanya tuweze kuupata, ni mambo gani matatu yanayotakwa?

12 Kuteremka kufikia wakati wetu, Yehova ameendelea kuandalia watumishi wake mwelekezo wanaohitaji iii kutenda kwa hekima. Ili kunufaika na mwelekezo huo, mambo kadhaa yanatakwa kwa sisi mmoja mmoja: (1) Tunahitaji kuthamini tengenezo la Yehova, kama Yoshua. Katika kisa chetu, uthamini huo unahusisha ndani kuonyesha ushirikiano pamoja na kundi la Kikristo la wapakwa-mafuta, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” pamoja na Baraza Linaloongoza lake. (Mathayo 24:45-47; linganisha Matendo 16:4.) Na uthamini huo unahusisha ndani ukawaida katika hudhurio la mikutano. (Waebrania 10:24, 25) (2) Lazima tuwe na bidii-endelevu katika kujifunza kibinafsi Neno la Mungu na vichapo vinavyoandaliwa na jamii ya “mtumwa,” vinavyotusaidia kulielewa. (3) Ni jambo la maana pia tuchukue wakati wa kutafakari jinsi mambo tunayojifunza yanavyoweza kutumiwa katika maisha zetu wenyewe na kutumiwa kusaidia wengine.

13. Ahadi iliyoandikwa kwenye Yeremia 3:15 ina maana gani?

13 Kwa habari ya aina ya uangalizi na ulishaji wa kiroho ambao angetuandalia katika siku yetu, Yehova alisema hivi, kwenye Yeremia 3:15: “Nitawapa ninyi wachungaji wanipendezao moyo wangu, watakaowalisha kwa maarifa na fahamu [muono-ndani, NW].” Kweli kweli, programu hiyo ya ulishaji ingetuandalia uwezo wa kustaajabisha wa kutazama jinsi hali zilivyo na kutambua mwendo wa kufuata ili kupata mafanikio. Ni nani chanzo cha muono-ndani huo? Ni Yehova Mungu.

14. Kwa nini jamii ya “mtumwa mwaminifu” ina muono-ndani?

14 Kwa nini jamii ya “mtumwa mwaminifu” ina muono-ndani huo? Kwa sababu wamehangaikia Neno la Mungu kwa moyo wa bidii na wanafuata mwelekezo walo. Tena, kwa sababu wao wamejiweka chini ya mwelekezo wa Yehova, yeye ameweka roho yake juu yao, akiwatumia kwa kupatana na kusudi lake. (Luka 12:43, 44; Matendo 5:32) Kama vile mtunga zaburi aliyevuviwa alivyoandika zamani za kale: “Mimi nimekuja kuwa na muono-ndani ulio zaidi ya walimu wangu wote, kwa sababu vikumbusho vyako ni hangaikio langu mimi.”​—Zaburi 119:99, NW.

15. (a) Ni nini wazo kuu la shauri ambalo jamii ya “mtumwa” hutupa sisi kwa upatani-patani? (b) Miaka mingi iliyopita, iliwezekanaje jamii ya “mtumwa” kuandaa “maarifa na muono-ndani” uliohitajiwa kuhusu maoni ya Kikristo juu ya kutiwa damu mishipani?

15 Kwa kujibu maulizo juu ya jambo linalofaa kufanywa, sikuzote “mtumwa mwaminifu mwenye akili” ameshauri hivi: ‘Tumia yaliyoandikwa katika Biblia. Itibari katika Yehova.’ (Zaburi 119:105; Mithali 3:5, 6, NW) Wakati kutiwa damu mishipani kulipokuja kuonwa kuwa utibabu uliokubaliwa kotekote na kukawa suala lenye kukabili Mashahidi wa Yehova, Mnara wa Mlinzi wa Julai 1, 1945, ulieleza maoni ya Kikristo kuhusu utakato wa damu. Ulionyesha kwamba damu ya wanyama na wanadamu pia ilitiwa katika lile katazo la kimungu. (Mwanzo 9:3, 4; Matendo 15:28, 29) Matokeo mabaya yenye kupata mwili hayakuzungumziwa katika makala hiyo; maarifa yalikuwa haba sana juu yayo wakati huo. Suala halisi lilikuwa kutii sheria ya Mungu, na lingali hivyo. Leo, watu wengi wanang’amua hekima inayotumika kwa mafaa ya kukataa kutiwa damu mishipani na wanafanya hivyo kwa idadi zinazoongezeka. Lakini muda wote ule Mashahidi wa Yehova wameweza kutenda kwa muono-ndani kwa sababu wanaitibari Muumba, anayejua mengi sana juu ya damu kuliko mwanadamu yeyote.

16. Kwa nini shauri lililo katika Mnara wa Mlinzi juu ya mambo kama vile maadili ya ngono, jamaa zenye mzazi mmoja, na mshuko wa moyo zilithibitika kuwa kitu kile hasa kilichohitajiwa?

16 Wakati mielekeo ya uendekevu kuhusu adili ya ngono imezidi kuonekana sana, badala ya kutetea mwendo ule wenye kufuatwa na walio wengi, Mnara wa Mlinzi umeandaa mwongozo timamu wa Kimaandiko. Mwongozo huo unasaidia wengi kulinda salama uhusiano wao wenye thamani kubwa pamoja na Yehova na kukaza fikira juu ya furaha ya kudumu badala ya kuzikaza juu ya raha inayopita haraka. Vivyo hivyo, makala za Mnara wa Mlinzi zenye kuelekezwa kwa jamaa zenye mzazi mmoja tu na kwa wale wanaopambana na mshuko wa moyo zimeonyesha muono-ndani unaowezekana kwa wale tu wanaothamini sana fikira za Yehova na kusali hivi kwa moyo wa bidii: “Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, kwa maana ndiwe Mungu wangu.”​—Zaburi 143:10; 139:17.a

17. (a) Makumi ya miaka mapema, watumishi wa Yehova walijua nini juu ya mwaka 1914? (b) Ingawa watu wa Mungu walikuwa wangali na maswali juu ya mambo mengi baada ya 1914, wao walijua nini kilichozipa maisha zao mwelekezo timamu?

17 Kupitia “mtumwa mwaminifu mwenye akili,” Yehova alisaidia watumishi wake kung’amua, makumi ya miaka mapema, kwamba mwaka 1914 ungekuwa alama ya mwisho wa Nyakati za Watu Wasio Wayahudi. (Luka 21:24) Walipokuwa wakiingia kipindi kilichofuata Vita ya Ulimwengu 1, bila shaka kulikuwa na maswali yaliyowafadhaisha. Lakini mambo waliyoyajua yalitosha kuwafanya watende kwa hekima. Walijua kutokana na Maandiko kwamba wakati wa Mungu ulikuwa umekaribia kuharibu mfumo wa zamani; kwa hiyo ingekuwa upumbavu kwao kuutumainia au kuacha viwango vyao vya kufanikiwa katika vitu vya kimwili visimamie maisha zao. Pia walijua kwamba Ufalme wa Yehova ndio utatuzi halisi kwa matatizo yote yanayosumbua aina ya binadamu. (Danieli 2:44; Mathayo 6:33) Waliona waziwazi kwamba ni daraka la Wakristo wote wa kweli kumtangaza Mfalme mpakwa-mafuta wa Yehova, Yesu Kristo, na Ufalme Wake. (Isaya 61:1, 2; Mathayo 24:14) Katika 1925, kupitia makala ya Mnara wa Mlinzi (wa Kiingereza) “Kuzaliwa kwa Taifa,” waliimarishwa kwa uelewevu wa wazi zaidi juu ya sura ya 12 ya Ufunuo; kwa hiyo sasa walielewa jambo lililokuwa limekuwa likitukia katika mbingu, bila kuonwa na macho ya kibinadamu. Muono-ndani huo ulitolea maisha zao mwelekezo timamu.

18. Tuna pendeleo na daraka gani sasa, na tunapaswa kujiuliza swali gani?

18 Wakati huo maelfu wachache waliokuwa wakitumikia Yehova wakiwa mashahidi wake walitenda kwa imani kwa kushika usukani katika kuhubiri katika sehemu zote za ulimwengu habari njema za Ufalme wa Mungu uliosimamishwa imara. Tokeo ni kwamba, mamilioni ya watu wamepata kumjua na kumpenda Yehova na wana tazamio la uhai wa milele. Sote ambao tumepokea ukweli kutokana na jitihada zao zenye upendo tumeonyeshwa kwamba sisi pia tuna pendeleo na daraka la kuishiriki kazi, kumpa ushuhuda kamili kila mtu tunayeweza kufikia na kuendelea kufanya hivyo mpaka Yehova aseme kazi imekwisha. (Ufunuo 22:17; linganisha Matendo 20:26, 27.) Je! njia unayotumia maisha yako inatoa ushuhuda wa kwamba wewe unathamini muono-ndani ambao Yehova ametoa kupitia tengenezo lake?

19. (a) Toa kielelezo cha mtu mmoja ambaye maisha yake huonyesha uthamini kwa muono-ndani ambao Yehova hutoa kupitia tengenezo lake. (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na kielelezo hicho?

19 Maisha za umati mkubwa wa watu mmoja mmoja katika sehemu zote za dunia yanashuhudiza kwamba katika kisa chao jibu ni ndiyo. Kwa kielelezo, fikiria John Cutforth. Miaka kama 48 iliyopita, yeye alithamini kwa moyo mashauri ya Kimaandiko ambayo jamii ya “mtumwa mwaminifu” ilikuwa ikiyaelekezea fikira wakati huo kama vile inavyofanya sasa, yaani: “Bali utafuteni [endeleeni kutafuta, NW] kwanza ufalme wake, na haki yake [uadilifu, NW]; na hayo yote mtazidishiwa. Basi msisumbukie ya kesho.” (Mathayo 6:33, 34) Baada ya miaka ya kujionea mengi katika utumishi wa Yehova, Ndugu Cutforth alisema: ‘Moja la mambo ambayo yamekazika akilini mwangu ni kwamba duniani Yehova ana tengenezo analoelekeza, kwamba mimi nikiwa mtu mmoja ningeweza kufanya kazi pamoja na tengenezo hilo, na kwamba kama ningefuata miongozo na mwelekezo walo kikamili, lingeniletea amani, uradhi, mtosheko, na rafiki wengi, kuongezea na baraka nyingi nyinginezo.’ Usadikisho huo umetiliwa-tiliwa nguvu huku yeye akipata shangwe ya maisha yenye baraka za kiroho katika United States, Kanada, Australia, na Papua New Guinea.b Kweli kweli, mwendo ulio wa hekima sisi sote tuufuate ni ule unaoonyesha uthamini kwa njia ya Yehova ya kuwapa watu wake muono-ndani.​—Mathayo 6:19-21.

Jilinde Dhidi ya Kupoteza Muono-Ndani

20, 21. (a) Watu fulani wamepotezaje muono-ndani wa kimungu waliokuwa nao? (b) Ni nini kitasaidia kutulinda salama dhidi ya mwendo wenye kuumiza?

20 Muono-ndani ambao Yehova huandaa ni hazina ya kutunzwa sana. Hata hivyo, inatupasa tuwe na habari kwamba tusipoendelea kufuata mwendo ambao umetuwezesha kujipatia muono-ndani wa kimungu, tunaweza kuupoteza. La kuhuzunisha ni kwamba, imetukia hivyo hasa kwa watu fulani. (Mithali 21:16; Danieli 11:35) Wao walijaribu kutetea walilokuwa wakifanya, wakikataa nidhamu iliyowagusa wao binafsi. Kiburi kikawa mtego kwao. Walianza kuliona kuwa jema lile ambalo Neno la Mungu linaonyesha ni baya, nao wakajivuta mbali na tengenezo la Yehova. Looo!

21 Hali za mtu wa jinsi hiyo zinaelezwa kwenye Zaburi 36:1-3, NW, tunaposoma hivi: “Kwa mwovu tamko la kukiuka yapasayo limo katikati ya moyo wake.” Yaani, fikira na tamaa zake mwenyewe za ubinafsi humwongoza kukiuka mambo yapasayo. “Hakuna kutetemekea Mungu mbele ya macho yake,” mtunga zaburi anaendelea kusema. “Kwa maana yeye ametenda kwa ulaini mno kwake mwenyewe asiweze kugundua kosa lake ili alichukie. Maneno ya kinywa chake ni uumivu na udanganyifu.” Na tokeo ni nini kwake? Yeye ‘hukoma kuwa na muono-ndani wa kutenda mema.’ Kwa kweli yeye hujisadikisha kwamba lile analotenda ni sawa, na hutongoza wengine wamfuate. Basi, ni jambo muhimu kama nini kwamba licha ya kuwa na muono-ndani tuulinde salama kwa kuthamini njia ambayo Yehova anatuwezesha kuupata!

[Maelezo ya Chini]

a Ona Watch Tower Publications Index 1930-1985, chini ya “Marriage” (Ndoa), “Families” (Jamaa), “Moral Breakdown” (Mvunjiko wa Maadili), na “Depression (Mental)” (Mshuko wa Moyo [wa Kiakili]).

b Ona Mnara wa Mlinzi (wa Kiingereza) wa Juni 1, 1958, kurasa 333-6.

Wewe Unakumbuka Nini?

◻ Ni nini kitatusaidia tufanye maamuzi yenye hekima?

◻ Ni mambo gani yanayohusika katika zi yenye hekim

◻ Yehova anawapaje watumishi wake muono-ndani katika wakati wetu?

◻ Ni nini kinachotakwa upande wetu ili tunufaike kikamili na muono-ndani ambao Yehova huandaa?

[Picha katika ukurasa wa 16]

Ili tunufaike na muono-ndani ambao Yehova hutoa, tunahitaji kuthamini tengenezo lake, kuwa wenye bidii-endelevu katika funzo la kibinafsi, na kutafakari juu ya Jinsi ya kutumia tunayojifunza

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki