Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 3/15 kur. 17-22
  • Muono-Ndani Ambao Yehova Ametoa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Muono-Ndani Ambao Yehova Ametoa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Mungu Ni Utatu?
  • Mahali Panapolifaa Jina la Mungu
  • Je! Nafsi ya Kibinadamu Ni Isiyoweza Kufa?
  • Mwenendo wa Kikristo Katika Ulimwengu Wenye Msukosuko
  • Matimizo ya Manabii ya Biblia
  • Tegemea Yehova Uwe na Muondo-Ndani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya Kweli
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
  • Twende Kwa Nani Isipokuwa Kwa Yesu Kristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1979
  • Yehova Analikweza Jina Lake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 3/15 kur. 17-22

Muono-Ndani Ambao Yehova Ametoa

“Kwa habari ya wale walio na muono-ndani miongoni mwa watu, wao watatia uelewevu kwa wengi.”​—DANIELI 11:33, NW.

1, 2. (a) Ingawa Waisraeli walikuwa wamejionea fadhili-upendo za Mungu, kwa nini walijiendesha kwa uasi? (b) Lingekuwa jambo la manufaa sisi tufanye nini? (Yeremia 51:10)

WATU wa Israeli ya kale walijua kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli. Walikuwa wameambiwa juu ya mishughuliko yake pamoja na baba zao watangulizi, na wao binafsi wakajionea fadhili-upendo zake. Lakini pindi nyingi, wao walitenda kwa ukosefu mkubwa wa muono-ndani. ‘Walijiendesha kwa uasi’ kuelekea Yehova na wawakilishi wake. Kwa nini? Kwa sababu ‘hawakukumbuka’ aliyokuwa amewafanyia. (Zaburi 106:7, 13, NW) Si kwamba hawakuyajua mambo hayo; wao hawakuyafikiria kwa uthamini. Tokeo ni kwamba, walithibitika kuwa “watu wa kutamani mabaya.”​—1 Wakorintho 10:6.

2 Katika siku yetu, njia kubwa ambayo Yehova amewatenga kando mashahidi wake wawe kikundi tofauti ni kwa muono-ndani ambao ameandaa kupitia tengenezo lake linaloonekana. Uthamini wetu wenyewe kwa njia ambayo Yehova anaongoza watu wake unaweza kuimarishwa kwa kufanya pitio la vielelezo fulani vya muono-ndani huo. Kimoja kinahusisha ndani kiini chenyewe hasa cha itikadi yetu​—utambulisho wa Mungu mwenyewe.

Je! Mungu Ni Utatu?

3. Ni nini kiliwezesha watumishi wa Yehova, zaidi ya miaka mia moja iliyopita, watambue ukweli juu ya utambulisho wa Mungu? (1 Wakorintho 8:5, 6)

3 Jumuiya ya Wakristo imeshikilia kwa uthabiti kwamba wale wasiotangaza kwa uhakika kwamba wanaitikadi katika Utatu ni wazusha-fitina. Lakini badala ya kutishwa na wanadamu, watumishi wa Yehova wametambua kwamba Maandiko Matakatifu ndiyo yanayoandaa kiwango cha kutambua yaliyo ukweli, wala si mapokeo na itikadi za wanadamu wasiovuviwa. Kwa kujenga juu ya msingi huu, kule nyuma katika 1882 wanafunzi hao wa Biblia waliojiweka wakfu walitaarifu wazi hivi katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza): “Wasomaji wetu wana habari kwamba ingawa sisi tunaitikadi katika Yehova Mungu na Yesu, na Roho takatifu, sisi tunakataa kuwa lisilo kabisa la Kimaandiko, lile fundisho la kwamba hawa ni Miungu watatu katika mtu mmoja, au kama vile wengine wanavyoweka wazo hilo, Mungu mmoja katika watu watatu.”​—Yohana 5:19; 14:28; 20:17.

4. (a) Kwa kuchunguza mambo kindani, watu wa Yehova walitambua nini juu ya msingi wa fundisho la Utatu na tokeo la fundisho la jinsi hiyo? (b) Kwa nini Yehova akawapa watumishi wake muono-ndani huo?

4 Hao wapenzi wa ukweli wa Biblia walikuwa wamechunguza kindani wakaona kwamba mizizi ya itikadi ya Utatu ilianza katika dini zisizo za Kikristo. Kwa kuchunguza Maandiko kwa uangalifu, wakawa pia wameng’amua kwamba wakati maandiko fulani ya Biblia yalipoonekana ni kama yanaunga mkono mawazo ya Utatu, ilikuwa hivyo kwa sababu ya maoni ya watafsiri yenye kuegemea upande mmoja, wala si kwa sababu ya mambo yaliyokuwa katika hati-mkono za zamani zaidi za lugha ya awali. Walitambua kwamba fundisho hili lenye kumheshimu Yesu kupita kiasi lilipinganisha mafundisho yake na kuondolea Yehova heshima. Hivyo, toleo lililotajwa juu la Mnara wa Mlinzi lilisema hivi: “Inatupasa sisi watafutaji wa ukweli, tufuate haki katika kushughulika pamoja na sisi wenyewe na pamoja na Neno la Baba yetu, linaloweza kutuhekimisha kikweli. Kwa hiyo, kwa kupuuza mapokeo na maoni ya kidini ya wanadamu na mifumo yenye ufisadi isiyo na uvuvio wa Mungu, acheni sisi tushike sana ile namna ya maneno timamu yaliyopokewa kutoka kwa Bwana wetu na Mitume.” Kwa sababu wao walipenda ukweli kihalisi na walielekeza fikira si kwenye mistari michache tu ya Biblia waliyoipendelea zaidi bali kwenye Neno zima la Mungu, Yehova aliwapa muono-ndani uliowatenganisha na Jumuiya ya Wakristo kwa njia yenye kuonekana wazi kabisa.​—2 Timotheo 3:16, 17; ona New World Translation Reference Bible, ukurasa 1580, kisehemu 6B.

Mahali Panapolifaa Jina la Mungu

5. Ni nini kimekuwa kichochezi cha elekeo la kuondoa jina la kibinafsi la Mungu lisiwe katika tafsiri za Biblia? (Ufunuo 22:18, 19)

5 Fikiria kielelezo cha pili: Wakati tafsiri nyingi zaidi na zaidi za Biblia zilipoficha au zikaacha nje kabisa jina la kibinafsi la Mungu, Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi ilitia mkazo mwingi hata zaidi juu ya umaana wa jina hilo. Jumuiya ya Wakristo ilibisha kwamba kuondolewa kwa jina Yehova kungeipa gospeli nguvu nyingi zaidi za kuvutia ulimwengu wote, lakini watumishi wapakwa mafuta wa Yehova wakamtambua aliyekuwa akichochea njama hiyo ya kuondoa katika Maandiko Matakatifu jina lililo la maana kupita yote. (Linganisha Yeremia 23:27.) Watu wa Mungu waling’amua kwamba njama hiyo ilichochewa na Ibilisi ili kufuta jina la Mungu mmoja tu wa kweli litoke katika kumbukumbu la kibinadamu.

6. Kwa utofautiano na mwendo wa Jumuiya ya Wakristo, watumishi wa kweli wa Mungu walifanya nini kutukuza jina lake? (Matendo 15:14)

6 Kwa utofautiano na mwendo wenye kufuatiwa na Jumuiya ya Wakristo, Mnara wa Mlinzi ulilipa umashuhuri jina la kimungu, YEHOVA, mwaka ule ule wa kwanza (1879) lilipoanza kutangazwa kwa chapa. Katika 1926 gazeti hili lilikazia makala “Ni Nani Ataheshimu Yehova?” (Zaburi 135:21) Katika 1931 wanafunzi wa Biblia wenye ushirika na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi walilikubali kwa moyo jina Mashahidi wa Yehova. (Isaya 43:10-12) Pia walipata kuthamini kikamili zaidi umaana mkubwa wa kutakaswa kwa jina la Yehova. (Isaya 12:4, 5) Katika 1944 walianza kuitangaza kwa chapa American Standard Version ya Biblia, ambayo inatia ndani jina Yehova zaidi ya mara 6,800. Hata hivyo, kuhusiana na kutangaza Biblia kwa chapa, jambo la kutokeza zaidi limekuwa ni kuchapishwa kwa New World Translation tangu 1950. Hiyo inalipa jina la kimungu mahali panapolifaa katika Maandiko ya Kiebrania na pia Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

7. Mkazo uliotiwa juu ya jina la Mungu na mambo yote yanayohusiana nalo umeathiri watu wengi kwa manufaa gani?

7 Mkazo ambao umewekwa hivyo juu ya jina la kibinafsi la Mungu umekuwa upendezo kwa mamilioni ya wapenzi wa uadilifu kuzunguka dunia yetu. Umewasaidia kumthamini Mungu wa kweli akiwa Mtu. Na kadiri ambavyo wamepata kujua njia zake, wameweza kujiendesha kwa busara, au wakiwa na muono-ndani.​—Mika 4:2, 5.

Je! Nafsi ya Kibinadamu Ni Isiyoweza Kufa?

8. Mapema katika historia yao ya ki-siku-hizi, Mashahidi wa Yehova walijifunza nini juu ya nafsi na hali ya wafu?

8 Sasa, kielelezo cha tatu: Mapema katika historia ya ki-siku-hizi ya watumishi wa Yehova, upendo kwa Neno la Mungu ulifungua macho yao yaone kweli nyingine za maana. Zaidi ya karne moja iliyopita, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” alielewa kwa usahihi kwamba nafsi si roho fulani yenye kuelewa mambo na yenye kubanduka na kutoka ambayo hukaa ndani ya wanadamu, bali ni mtu mwenyewe. (Mathayo 24:45-47) Katika 1880 Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) ulichanganua maneno ya lugha ya awali yaliyotoholewa kuwa Sheoli na Hadesi katika Biblia na likakata shauri kwamba maneno haya yanamaanisha kaburi. Pia lilionyesha wazi kwamba watu walioachwa waende Gehena waliharibiwa, hawakuteswa-teswa.​—Ona pia New World Translation Reference Bible, kurasa 1573-5.

9. Katika 1894, Mnara wa Mlinzi ulionyesha wazi nini kuhusu awali ya fundisho la kwamba kwa asili nafsi za kibinadamu huwa zimerithi kutokufa?

9 Katika 1894 Mnara wa Mlinzi ulitokeza swali hili, “Basi lilitoka wapi lile wazo lenye kufuatwa na wengi kwamba wanadamu wote wana hali ya kutokufa, katika asili yao, katika urithi wao?” Likiwa na muono-ndani, likajibu hivi: “Tunapotazama kwa makini kurasa za historia, tunapata kwamba, ingawa fundisho la kutokufa kwa binadamu halifundishwi na mashahidi wa Mungu waliovuviwa, hicho hasa ndicho kiini cha dini zote za watu waliokuwa hawajaerevuka. . . . Basi, si kweli kwamba Socrates na Plato walikuwa ndio wa kwanza kufundisha fundisho hilo: lilikuwa na mwalimu wa mapema kuliko wao, tena mwenye uwezo mwingi zaidi. Hata hivyo, wao waliling’arisha fundisho hilo . . . na kufanyiza falsafa kutokana nalo, na hivyo wakalifanya liwe na nguvu nyingi zaidi za utongozi na lenye kukubalika kwa jamii ya watu walioerevuka wa siku yao na wa tangu hapo. Kumbu-kumbu la maandishi ya kwanza ya fundisho hili bandia linapatikana katika historia ya zamani zaidi inayojulikana kwa mwanadamu​—Biblia. Huyo mwalimu bandia alikuwa Shetani.”a

10. Ni matokeo gani mabaya yametokana na uwongo wa kidini juu ya nafsi na hali ya wafu, lakini ilifanywa nini kusaidia watu wenye kusababu mambo vizuri?

10 Kwa kueneza propaganda za ubandia wa kwamba wanadamu wote wana nafsi isiyokufa na kwamba waovu watateswa-teswa milele katika moto wa mateso, Shetani amesingizia na kukufuru jina la Mungu. Mhariri wa kwanza wa Mnara wa Mlinzi, C. T. Russell, aling’amua hivyo. Yeye aliona watu wenye kuelewa mambo wakikataa wazo la mteseko wa milele, lakini kwa kuhuzunisha wakakataa Biblia pia kwa sababu walifikiri ilikuwa ndiyo chanzo cha fundisho hilo lisilo la kiakili. Ili kuuondoa ule moshi wa Enzi Zenye Giza uache kufunika akili za watu wenye kusababu mambo vizuri, kama vile yeye alivyoliweka wazo lenyewe, Ndugu Russell alitoa hotuba ya watu wote yenye kuvuta fikira, “Kwenda Hell na Kurudi! Walio Huko Ni Akina Nani.”

11. (a) Zoea la kuwasiliana na roho waovu lilipokuwa likianza kutokea wazi, ni onyo gani lililotangazwa na jamii ya “mtumwa mwaminifu”? (b) Ni nani wamenufaishwa na onyo hilo, na jinsi gani?

11 Hicho kilikuwa kipindi ambamo zoea la kuwasiliana na roho waovu lilikuwa likianza kutokea wazi. Lakini ikiwa na muono-ndani ambao Yehova Mungu alifanya uwezekane kupitia Neno lake, jamii ya “mtumwa mwaminifu” ilitambua kwamba zile zenye kudhaniwa kuwa ni roho zilizoacha miili ya watu waliokufa, ambazo watu walikuwa wakiwasiliana nazo, kwa kweli zilikuwa ni roho waovu. Hoja zenye nguvu za Kimaandiko zilitokezwa katika hotuba za watu wote na kwa namna ya maandishi ili kufungua macho ya wenye mioyo ya ufuataji haki yaone hatari ya kuhusika katika mazoea ya kuwasiliana na roho waovu. (Kumbukumbu 18:10-12; Isaya 8:19) Kama tokeo la huu muono-ndani ambao Yehova amewapa watumishi wake, maelfu mengi ya watu kuzunguka dunia wamewekwa huru kutoka hofu ya wafu, kutoka zoea la kuwasiliana na roho waovu, na kutoka desturi zinazoshusha tabia zinazoshirikishwa na kuwasiliana na roho waovu.

Mwenendo wa Kikristo Katika Ulimwengu Wenye Msukosuko

12, 13. (a) Eleza Danieli 11:32, 33. (b) Ni nini baadhi ya kweli za msingi za Biblia zinazoandaa msingi wa uelewevu unaotolewa na “wale walio na muono-ndani”?

12 Mnabii Danieli alionyesha kwamba watumishi wa Mungu wangedhihirisha muono-ndani kuhusiana na jambo jingine la nne, suala muhimu​—kutokuwamo. Baada ya kusimulia kwa urefu mng’ang’ano ulio kati ya sehemu mashuhuri za kisiasa zenye kuzozana za ulimwengu, Danieli 11:32, 33, NW, anasema: “Wale wanaotenda kwa uovu dhidi ya lile agano, yeye ataongoza ndani ya uasi-imani kwa njia ya maneno laini.” Yaani, mfalme wa kaskazini mwenye kutumia utawala-jumla dhidi ya watu anawaongoza ndani ya uasi-imani wale wanaodai kuwa ni Wakristo lakini wanaopenda ulimwengu, wanaotaka kibali chao, na kwa hiyo wanalitenda madharau agano la Yehova kuhusu Ufalme ambamo Yesu Kristo atatawala dunia yote. “Lakini,” Danieli anaendelea kusema, “kwa habari ya wale watu ambao wanajua Mungu wao, wao watashinda na kutenda kwa matokeo mazuri. Na kwa habari ya wale walio na muono-ndani miongoni mwa watu, wao watatia uelewevu kwa wengi.”

13 Muono-ndani unaohitajiwa ili kushughulika kwa hekima na hali zinazotuzunguka ambazo mara nyingi huwa zenye msukosuko unategemea kuthamini kweli za msingi za Biblia. Kwa mwelekezo wa Yehova, jamii ya “mtumwa mwaminifu” imetambua kweli hizo. Moja ni kwamba, kama Yesu alivyoonyesha, mtawala asiyeonekana wa ulimwengu huu ni Shetani Ibilisi. (Luka 4:5-8; Yohana 12:31) Kwa kupatana na ukweli huo, 1 Yohana 5:19, NW, inaongezea kwamba si sehemu fulani tu yenye mzozo bali “ulimwengu mzima [aina ya binadamu yote iliyo nje ya kundi la kweli la Kikristo] unalala katika nguvu za yule mwovu.” (Ufunuo 12:9) Kwa maana Yesu alisema kwamba wafuasi wake wangekuwa “si sehemu ya ulimwengu,” hii inawatokezea wito wa kutokuwamo kwa Kikristo.​—Yohana 17:16, NW.

14. (a) Fikira za watumishi wa Yehova zilielekezwa kwenye mambo gani ya wakati wake katika 1939 na 1941? (b) Muono-ndani huo umewasaidiaje Mashahidi wa Yehova kutenda kwa hekima?

14 Kwa hiyo, ilitukia kwa wakati wake kwamba wakati mawingu ya Vita ya Ulimwengu 2 yalipokuwa yakitia giza katika Ulaya, suala la kutokuwamo kwa Kikristo lilikaziwa katika Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) wa Novemba 1, 1939. Unaohusiana na jambo hili ni ukweli mwingine wa kimsingi​—ule umaana wa suala la enzi kuu ya ulimwengu wote mzima na fungu la Ufalme wa Kimesiya katika kutatua suala hilo. Kwa kufaa, katika 1941 suala hilo lilikaziwa katika hotuba moja kwenye mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova katika St. Louis, Missouri, U.S.A., na katika kitabu The New World mwaka uliofuata. Muono-ndani huo wa kimungu umeandalia watumishi wa Yehova ulinzi ulioje katika ulimwengu huu uliogawanyika na wenye vita! Ingawa mifumo ya kidini ya Jumuiya ya Wakristo imevunjika vipande-vipande kwa sababu imejiruhusu ijichangamanishe katika ugomvi wa kimataifa na katika harakati za wapiganaji-haramu ili kupindua serikali, Mashahidi wa Yehova katika mabara yote wameendelea kwa umoja kujitoa kutangaza Ufalme wa Yehova kuwa ndilo tumaini pekee kwa aina ya binadamu. Wameendelea kujishughulisha katika kazi ya kuokoa uhai ambayo Yesu Kristo alitabiri aliposema: “Habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.”​—Mathayo 24:14.

Matimizo ya Manabii ya Biblia

15. Kwa nini watumishi wa Yehova wamekuwa na muono-ndani?

15 Kwa nini watumishi wa Yehova wamekuwa na muono-ndani huo? Kwa sababu wana uhakika kamili katika Neno la Mungu lililoandikwa, wanalitii, na roho ya Yehova iko juu yao. Hiyo imewawezesha pia kuelewa manabii muhimu ya Biblia, na hilo ndilo jambo la tano tutakalofikiria.

16, 17. (a) Kwa nini nyakati fulani tarehe zinazotumiwa na Mashahidi wa Yehova hutofautiana na zile zinazotolewa na wanahistoria walimwengu? (b) Mashahidi wa Yehova wamenufaikaje kwa kuwa na uhakika katika Biblia kuhusu njia ya kuhesabu tarehe ya mwaka wa 20 wa Artazakse na wakati wa Yerusalemu kuharibiwa na Wababuloni?

16 Kwa kutegemea fasiri yao juu ya vitu ambavyo nyakati nyingine huwa ni vipande-vipande vya tableti zilizofukuliwa na wachimbuzi wa vitu vya kale, wanahistoria walimwengu wamekata shauri kwamba 464 K.W.K. ulikuwa ndio mwaka wa kwanza wa umaliki wa Artazakse Longimano na kwamba 604 K.W.K. ulikuwa ndio mwaka wa kwanza wa umaliki wa Nebukadreza 2. Kama hiyo ingekuwa kweli, mwaka wa 20 wa Artazakse ungeanza katika 445 K.W.K., na tarehe ambayo Yerusalemu ulifanywa ukiwa na Wababuloni (katika mwaka wa 18 wa kutawala kwa Nebukadreza) ingekuwa 587 K.W.K. Lakini mwanafunzi wa Biblia akitumia tarehe hizo anapohesabu utimizo wa unabii, atavurugika tu.

17 Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakipendezwa na mapato ya wachimbuzi wa vitu vya kale kwa kuwa vinahusiana na Biblia. Hata hivyo, mahali ambapo fasiri ya mapato hayo inapingana na taarifa za wazi zilizo katika Biblia, sisi tunakuwa na uhakika wa kukubaliana na yanayosemwa na Maandiko Matakatifu, kuhusiana na mambo ya orodha ya matukio au habari nyingine yoyote. Tokeo ni kwamba, kwa muda mrefu watumishi wa Yehova wametambua kwamba kipindi kilichoanza katika mwaka wa 20 wa Artazakse kilipasa kuhesabiwa kuanzia 455 K.W.K. na hivyo Danieli 9:24-27 ilielekeza kwa njia ya kutegemeka kwenye mwaka 29 W.K. kuwa ndio wakati wa kumpaka Yesu mafuta awe Mesiya.b Kwa sababu iyo hiyo, wameng’amua kwamba unabii ulio katika Danieli sura 4 kuhusu “nyakati saba” ulianza kuhesabika katika 607-606 K.W.K. na kwamba ulionyesha wazi kabisa ya kuwa mwaka 1914 W.K. katika vuli ndipo Kristo alipoketishwa katika kiti mbinguni akiwa Mfalme anayetawala, na ulimwengu huu ukaingia katika wakati wao wa mwisho.c Lakini wao wasingalitambua matimizo hayo yenye kusisimua ya unabii kama wangaliyumba-yumba katika uhakika wao wa kwamba Maandiko Matakatifu yalivuviwa. Hivyo, muono-ndani ambao wameuonyesha umehusiana moja kwa moja na tegemeo lao juu ya Neno la Mungu.

18. Isaya 65:13, 14 inaahidi nini kuhusu hali ya kiroho ya watumishi washikamanifu wa Yehova?

18 Akitofautisha hali ya kiroho ya watumishi wake washikamanifu na ile ya watu mmoja mmoja na vikundi vyenye haraka ya kusukuma Maandiko kando kwa kupendelea kitu chochote kile ambacho watu wengi wanakipenda kwa wakati uliopo, Yehova anasema hivi: “Tazama, watumishi wangu watakula, bali ninyi mtaona njaa; tazama, watumishi wangu watakunywa, bali ninyi mtaona kiu; tazama, watumishi wangu watafurahi, bali ninyi mtatahayarika; tazama, watumishi wangu wataimba kwa furaha ya moyo, bali ninyi mtalia kwa huzuni ya moyo; mtapiga kelele kwa sababu ya uchungu wa roho zenu.”​—Isaya 65:13, 14.

19. (a) Kwa msingi, “mtumwa mwaminifu mwenye akili” huandaa maelezo ya Maandiko kupitia njia gani? (b) Ni programu ya aina gani ya funzo itatuwezesha kunufaika kikamili na chakula cha kiroho?

19 Kama vile imeonyeshwa na pitio hilo fupi la historia, ni kupitia safu za Mnara wa Mlinzi kwamba “mtumwa mwaminifu mwenye akili” wa Yehova ametuandalia maelezo ya kweli muhimu za Kimaandiko. Mnara wa Mlinzi ndicho chombo kikuu kinachotumiwa na jamii ya “mtumwa” kugawa chakula cha kiroho. Je! wewe unanufaika nacho kikamili? Wewe husoma kila toleo, na je! programu yako ya kujifunza inatia ndani kufungua maandiko yaliyotajwa lakini bila kunukuliwa? Je! wewe hufanya liwe zoea lako kutafakari pia mambo ambayo umejifunza, kujenga uthamini kwayo, kufikiria yanavyopasa kuathiri mwelekeo wako, tamaa zako, utendaji wako wa kila siku, miradi yako maishani? Kufanya hivyo kunaweza kukusaidia sana kufanya maamuzi yanayotegemea muono-ndani wa kweli ambao ni Yehova peke yake ametoa.

[Maelezo Chini]

a Shetani aliongoza Hawa kuitikadi kwamba hangekufa hata kidogo katika mnofu. (Mwanzo 3:1-5) Kwa hiyo ni baadaye kwamba yeye alikuja kuanzisha lile fundisho bandia kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa ambayo huendelea kuishi mwili ukiisha kufa.​—Ona Mnara wa Mlinzi (Kiingereza), Septemba 15, 1957, ukurasa 575.

b Insight on the Scriptures, Buku 2, kurasa 614-16, 899-901.

c “Ufalme Wako Uje,” kurasa 186-9.

Wewe Unakumbuka Nini?

◻ Je! Mungu ni Utatu, na kwa nini wewe unajibu hivyo?

◻ Ni mahali gani panapolifaa jina la Mungu?

◻ Je! nafsi ya kibinadamu ni isiyoweza kufa?

◻ Yehova ameandaa muono-ndani gani kuhusu mwenendo wa Kikristo katika ulimwengu huu wenye msukosuko?

◻ Mashahidi wa Yehova wamepokea muono-ndani gani kuhusu matimizo ya manabii ya Biblia?

[Picha katika ukurasa wa 18]

Kupitia Mnara wa Mlinzi, ”mtumwa mwaminifu mwenye akili” huandaa muono-ndani juu ya maana ya Maandiko na utumizi wayo kuhusu siku yetu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki