Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ijwbv makala 10
  • Yoshua 1:9—“Uwe Jasiri na Imara”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yoshua 1:9—“Uwe Jasiri na Imara”
  • Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana ya Yoshua 1:9
  • Muktadha wa Yoshua 1:9
  • Yoshua na Akusaidie Wewe Umtumikie Yehova kwa Uhodari!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Anataka Tufanikiwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Aliyokumbuka Yoshua
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Kitabu Cha Biblia Namba 6—Yoshua
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Mistari ya Biblia Yafafanuliwa
ijwbv makala 10

MISTARI YA BIBLIA YAFAFANULIWA

Yoshua 1:9—“Uwe Jasiri na Imara”

“Je, si mimi niliyekuamuru uwe jasiri na imara? Basi uwe jasiri na imara. Usitetemeke wala kuogopa, kwa maana mimi Yehova Mungu wako nipo pamoja nawe mahali popote utakapoenda.”—Yoshua 1:9, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

“Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.”—Yoshua 1:9, Union Version.

Maana ya Yoshua 1:9

Kupitia maneno hayo, Yehovaa Mungu alimhakikishia mtumishi wake mwaminifu Yoshua kwamba anaweza ‘kuwa jasiri na imara’ licha ya changamoto na matatizo mengi aliyokabili. Yoshua hakuwa na sababu yoyote ya kuogopa mambo yatakayotukia wakati ujao ikiwa angetii amri za Mungu, kwa sababu ingekuwa kana kwamba Yehova angekuwa kando yake akimsaidia ili afanikiwe. Mungu alikuwa pamoja na Yoshua kupitia miongozo na ushindi aliompa dhidi ya maadui zake.

Yoshua angewezaje ‘kuwa jasiri na imara’? Angeweza kuwa jasiri na imara kupitia maandiko matakatifu ambayo Yehova alikuwa ameandaa wakati huo. Maandiko hayo yalitia ndani ‘Sheria yote ambayo Musa mtumishi wa Yehova alimwamuru Yoshua.’b (Yoshua 1:7) Yehova alimwambia Yoshua ‘aisome kwa sauti ya chini [‘atafakari,’ Union Version] mchana na usiku.’ (Yoshua 1:8) Kusoma na kutafakari kulimsaidia Yoshua kuazimia moyoni kufanya mapenzi ya Mungu. Yoshua alihitaji pia kutenda kulingana na mambo aliyojifunza kutoka katika Neno la Mungu, ‘kufuata kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo.’ Ikiwa angefanya hivyo, basi angetenda kwa hekima na kufanikiwa. Hivyo ndivyo alivyotenda. Ijapokuwa alikabili changamoto mbalimbali, Yoshua aliishi maisha yenye kusudi na uradhi akiwa mtumishi mwaminifu wa Yehova.—Yoshua 23:14; 24:15.

Maneno hayo ya Yehova aliyomwambia Yoshua yanaendelea kututia moyo pia katika siku zetu. Yanaonyesha jinsi Yehova anavyowajali sana watumishi wake wote, hasa wanapokabili changamoto. Anataka wafanikiwe kama Yoshua! Na kama Yoshua, wanaweza ‘kuwa jasiri na imara’ kwa kusoma na kutafakari kwa ukawaida Neno la Mungu, Biblia, na kisha kutenda kulingana na mwongozo wake.

Muktadha wa Yoshua 1:9

Baada ya Musa kufa, Yehova alimwagiza Yoshua aongoze taifa la Israeli. (Yoshua 1:1, 2) Wakati huo, Waisraeli walikuwa wakijitayarisha kuingia katika Nchi ya Ahadi, nchi ya Kanaani. Hata hivyo, walikabili maadui wenye nguvu waliotaka kuwashambulia. Kwa mfano, Yoshua alihitaji kupigana vita na Wakanaani waliokuwa waovu kupita kiasi.c (Kumbukumbu la Torati 9:5; 20:17, 18) Pia, Wakanaani walikuwa wengi zaidi na wenye silaha bora zaidi za vita kuliko Waisraeli. (Yoshua 9:1, 2; 17:18) Lakini kwa ujasiri Yoshua alitii mwongozo wa Yehova. Na Mungu alikuwa pamoja naye kwa sababu Waisraeli waliwashinda maadui wengi katika kipindi cha miaka sita tu.—Yoshua 21:43, 44.

Soma Yoshua sura ya 1 pamoja na maelezo ya chini na marejeo ya pambizoni.

a Jina Yehova limetafsiriwa kutoka kwa jina la Mungu katika lugha ya Kiebrania lenye herufi nne za Tetragramatoni יהוה (YHWH). Tafsiri ya Union Version imetafsiri jina hilo kuwa “BWANA” katika mstari huu. Ili kujua mengi zaidi kuhusu Yehova na kwa nini baadhi ya tafsiri za Biblia hazitumii jina hilo, ona makala yenye kichwa “Yehova Ni Nani?”

b Huenda maandiko matakatifu yaliyopatikana wakati wa Yoshua na ambayo sasa tunaweza kuyapata katika Biblia, yalitia ndani vitabu vitano vya Musa (Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu, na Kumbukumbu la Torati), kitabu cha Ayubu, na zaburi moja au mbili.

c Ili upate habari zaidi ya kwa nini vita hivyo vilihitaji kupiganwa, ona makala yenye kichwa “Kwa Nini Mungu Aliwaamuru Waisraeli Wapigane Vita na Wakanaani?” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 2010.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki