Saa ya Hukumu ya Mungu Imewasili
Hofuni Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili.”—UFUNUO 14:7, NW.
1. Sura zinazofungua Ufunuo zinatia nini ndani?
KITABU cha Ufunuo kina manabii ya kusisimua yanayotimizwa siku yetu. Makala iliyotangulia ilizungumzia mengine, kutia na kufunguliwa kwa mihuri sita ya ufananisho. Mihuri hiyo iliyofunguliwa ilifunua upandaji wenye kuteketeza wa wale wapanda-farasi wanne wa apokalipsi katika hizi “siku za mwisho.” (2 Timotheo 3:1; Ufunuo 6:1-8) Pia ilieleza juu ya wale watakaotawala na Kristo mbinguni na wale watakaookoka ile “dhiki kubwa” waishi duniani milele. Mihuri sita hiyo inaonyesha kwamba “wakati uliowekwa” wa Mungu kufikiliza hukumu “u karibu.”—Ufunuo 1:3; 7:4, 9-17, NW.
2. Tarumbeta saba za ufananisho za Ufunuo sura ya 8 ni za kutumiwaje?
2 Lakini kuna muhuri mmoja zaidi, ule wa saba. Ufunuo 8:2 unatuambia linalofunuliwa wakati unapofunguliwa: “Na mimi nikaona malaika saba ambao husimama mbele za Mungu, na tarumbeta saba wakapewa wao.” Mstari wa 6 unasema: “Na malaika saba waliokuwa na tarumbeta saba wakajitayarisha kuzipuliza.” Nyakati za Biblia, tarumbeta zilitumiwa kuashiria matukio ya maana. Hivyo hivyo, mipulizo hiyo yenye kishindo ya tarumbeta saba inavuta fikira kwenye mambo yenye umaana wa kifo na uhai katika wakati wetu. Na ingawa malaika ndio wanaovumisha tarumbeta zile, Mashahidi wanadamu duniani wanafuatisha kwa kueneza kote kote habari muhimu zinazotangazwa na kila mpulizo wa tarumbeta wenye kishindo.
Maana ya Mipulizo ya Tarumbeta Yenye Kishindo
3. Ni nini maana ya mipulizo yenye kishindo ya tarumbeta saba?
3 Mipulizo hiyo yenye kishindo ya tarumbeta inatukumbusha tauni ambazo Yehova alimwagia Misri ya kale. Tauni hizo zilikuwa mawonyesho ya hukumu ya Yehova juu ya hiyo serikali kubwa ya kwanza ya ulimwengu na dini yayo bandia, lakini iliwafungulia watu wa Mungu njia ya kuponyoka pia. Vivyo hivyo, mipulizo yenye kishindo ya tarumbeta za Ufunuo ni tauni za ki-siku-hizi, wakati huu zikiwa juu ya ulimwengu mzima wa Shetani na dini yao bandia. Ingawa hivyo, si tauni halisi bali ni jumbe zenye tauni za hukumu za Yehova. Pia zinaonyesha wazi njia ya kuponyoka kwa watu wa Mungu.
4. Mipulizo yenye kishindo ya tarumbeta saba imepataje utimizo wakati wetu?
4 Kwa kupatana na hii mipulizo yenye kishindo ya tarumbeta saba, maazimio yenye kugonga sana yalikaziwa dhidi ya ulimwengu wa Shetani kwenye mikusanyiko maalumu ya kila mwaka ya watu wa Yehova kuanzia 1922 mpaka 1928. Nakala za maazimio ziligawanywa kwa mamia ya mamilioni. Hata hivyo, tarumbeta za jumbe hizo zenye kuunguza hazikupigwa miaka hiyo tu, bali zimeendelea muda wote wa siku za mwisho. Na leo zinatangazwa kwa nguvu kuliko wakati mwingine wowote, kwa kuwa mamilioni ya ule “umati mkubwa” wameongezea sauti zao kwenye kikosi kidogo cha wapakwa-mafuta ambao hapo kwanza ndio waliokuwa wakihubiri baada ya Vita ya Ulimwengu 1. (Ufunuo 7:9) Kila mwaka sasa, mamilioni hao wanatangaza wakiwa na kani na hesabu zenye kuongezeka kwamba ulimwengu wa Shetani utaangamizwa kabisa kabisa.
5. Ni nani “theluthi” ya ulimwengu inayohukumiwa vikali kwanza, na kwa nini?
5 Kwenye Ufunuo 8:6-12, NW, tarumbeta nne za kwanza zinavumishwa. Mawe-barafu, moto, na damu vinamiminwa, vikiteketeza “theluthi moja” ya ulimwengu. Kwa nini “theluthi moja” inatajwa kuwa sehemu ya ulimwengu iliyo na hatia yenye kupata hukumu kali kwanza? Kwa sababu ingawa mfumo wote wa Shetani una lawama kwa Mungu, sehemu moja ndiyo yenye lawama zaidi. Sehemu ipi? Sehemu iliyojichukulia jina la Kristo—Jumuiya ya Wakristo. Na wakati jumbe za hukumu ya Mungu zilipokuja dhidi yayo baada ya Vita ya Ulimwengu 1, wakati huo makao ya Jumuiya ya Wakristo yalikuwa yamechukua karibu theluthi moja ya aina ya binadamu.
6. Kwa nini Yehova ameachilia Jumuiya ya Wakristo ipate uharibifu?
6 Dini ya Jumuiya ya Wakristo ni tunda lililozaliwa na uasi-imani wa kuacha Ukristo wa kweli ambao umekuwapo kwa miaka 1,900, uliotabiriwa na Yesu na wanafunzi wake. (Mathayo 13:24-30; Matendo 20:29, 30) Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo wanajiwakilisha kuwa walimu wa Ukristo, lakini mafundisho yao yako mbali na ukweli wa Biblia, na vitendo vyao vya ufisadi vinaendelea kuingiza jina la Mungu katika sifa mbaya. Hatia yao ya damu kwa sababu ya kuunga mkono vita vya karne hii ya 20 imefunuliwa wazi. Jumuiya ya Wakristo yote ni sehemu ya mfumo wa mambo wa Shetani. Hivyo, inapokea jumbe zenye nguvu nyingi zinazopiga kama tauni kutoka kwa Yehova, zinazoonyesha haistahili upendeleo wowote wa kimungu. Yehova ameiachia uharibifu nyumba ya Jumuiya ya Wakristo sawasawa na alivyoifanya nyumba ya Kiyahudi ya karne ya kwanza!—Mathayo 23:38.
Warudishiwa Uhai Ili Kuhubiri Duniani Pote
7, 8. (a) Katika Ufunuo sura ya 9, mpulizo wa tarumbeta ya tano unafunua nini? (b) Nzige wanafananisha nani?
7 Kwenye Ufunuo 9:1 malaika wa tano anavumisha tarumbeta yake, na njozi inafunua nyota mmoja akishuka duniani. Nyota huyo ana ufunguo mkononi. Anautumia kufungua shimo lilimokuwa limezuiliwa bumba la nzige. Nyota huyo ni Mfalme wa Yehova wa kimbingu aliyetawazwa karibuni, Yesu Kristo. Nzige hao ni watumishi wa Mungu, walionyanyaswa na wakaonekana ni kama wameondolewa mbali wakati maofisa wao wenye kuongoza walipofungwa katika 1918. Lakini Kristo, sasa akiwa katika mamlaka ya Ufalme mbinguni, anawafungulia waweze kurudia kuhubiri peupe, hiyo ikihofisha na kutamausha makasisi, waliokuwa wamefanya hila kuua kazi yao.—Mathayo 24:14.
8 Kwenye Ufunuo 9:7, NW, nzige hao wanaelezwa kuwa hivi: “Na mifanano ya nzige ilishabihi farasi walio tayari kwa ajili ya pigano; na juu ya vichwa vyao palikuwa na kilichoonekana kuwa mataji kama dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.” Mstari wa 10 unaongeza hivi: “Pia, wao wana mikia na michomo kama nge.” Kwa kufaa nzige hao wanafananisha mabaki wa warithi wa Ufalme waliorudishiwa uhai wakiwa tena katika mwendo kuingia pigano la kiroho tangu 1919 na kuendelea. Wakiwa na nishati zilizofanywa upya, walitangaza jumbe za hukumu za Mungu zinazochoma, hasa dhidi ya Jumuiya ya Wakristo yenye ufisadi.
9, 10. (a) Mpulizo wa tarumbeta ya sita unafunua nini? (b) Yale mamiriadi ya farasi wenye nguvu nyingi ni kutia ndani nani pia?
9 Halafu, malaika wa sita anapuliza tarumbeta yake. (Ufunuo 9:13, NW) Hiyo inafunua kufunguliwa kwa majeshi ya askari wapanda-farasi. Mstari wa 16 unasema hesabu yao ni “mamiriadi mawili ya mamiriadi,” yaani milioni 200! Na katika mistari 17 na 19 wanaelezwa kuwa hivi: “Vichwa vya farasi vilikuwa kama vichwa vya masimba, na katika vinywa vyao moto na moshi na salfa vilitoka. . . . Mikia yao ni kama manyoka.” Majeshi hayo yanaruka kwenda nje kwa kishindo yakiwa chini ya mwelekezo wa Mfalme, Kristo Yesu. Nao ni tamasha ya kutia hofu kama nini!
10 Farasi hao wenye nguvu nyingi wanawakilisha nini? Kwa kuwa hesabu yao ni mamilioni, hawangeweza kuwa ni wale mabaki wapakwa-mafuta tu, ambao sasa ni 8,800 tu duniani. Lazima iwe mamiriadi hayo ya farasi ni kutia ndani “umati mkubwa” wa Ufunuo sura ya 7, wale walio na tumaini la kuishi milele duniani. Katika Biblia, mara nyingi neno “miriadi” huelekeza kwa hesabu kubwa sana, isiyo dhahiri. Hivyo, farasi hao wa ufananisho wangekuwa ni kutia ndani si ile hesabu inayopungua ya wapakwa-mafuta tu bali pia yale mamilioni yanayoongezeka yaliyo na sauti yenye nguvu ya “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wanaoendeleza kazi ya peupe iliyoanzishwa na mabaki wapakwa-mafuta walio kama nzige.—Yohana 10:16.
11. Kwa nini inasemwa kwamba “mamlaka ya farasi hao imo katika vinywa vyao,” na ni jinsi gani wao ‘hufanya dhara kwa mikia yao’?
11 Ufunuo 9:19, NW, unataarifu hivi: “Mamlaka ya farasi hao imo katika vinywa vyao,” na “kwa [mikia yao] wao hufanya dhara.” Ni jinsi gani mamlaka yao ilivyo katika vinywa vyao? Katika jambo la kwamba kwa makumi ya miaka, kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na mikutano mingine, watumishi wa Mungu wamefundishwa jinsi ya kuhubiri kimamlaka jumbe zake za hukumu kwa maneno ya kinywa. Nao hufanyaje dhara kwa mikia yao? Katika jambo la kwamba wamegawanya ulimwenguni pote mabilioni ya vichapo vinavyotegemea Biblia, hivyo wakiacha nyuma jumbe zenye kuchoma kwa uchungu dhidi ya ulimwengu wa Shetani. Kwa kweli majeshi hayo ya askari wapanda-farasi yanaonekana kwa wapinzani wao kuwa kama mamiriadi ya mamiriadi.
12. Ni lazima nzige na farasi wa ufananisho waendelee kufanya nini, na kwa tokeo gani?
12 Hivyo, ni lazima nzige na farasi wa ufananisho wavumishe jumbe za hukumu za Mungu waziwazi zaidi na kwa sauti kubwa siku yake ya kisasi ikaribiapo. Kwa wenye moyo wa kufuata haki, jumbe hizo ndizo habari bora zaidi duniani. Lakini kwa wale wanaopendelea zaidi ulimwengu wa Shetani, ziko kama habari mbaya, kwa maana zinamaanisha ulimwengu wao utaharibiwa karibuni.
13. “Ole ya tatu” inayoshirikishwa na mpulizo wenye kishindo wa tarumbeta ya saba inahusisha nini ndani, na ni jinsi gani ilivyo “ole”?
13 Nzige hao waleta tauni na yale majeshi ya askari wapanda-farasi wanaelezwa kuwa ndiyo ya kwanza na ya pili ya “ole” tatu zilizoamuliwa na Mungu. (Ufunuo 9:12; 11:14) “Ole ya tatu” ni nini? Kwenye Ufunuo 10:7, NW, tunaambiwa: “Katika siku za kuvumisha kwa malaika wa saba, . . . siri takatifu ya Mungu kulingana na habari njema ambazo yeye alijulisha wazi kwa watumwa wake mwenyewe wanabii kweli kweli huletwa kwenye tamati.” Hiyo siri takatifu inahusisha ndani “mbegu” iliyoahidiwa kwanza katika Edeni. (Mwanzo 3:15, NW) Kwa msingi “mbegu” hiyo ni Yesu lakini inawatia ndani pia washirika wake waliopakwa mafuta watakaotawala naye mbinguni. Kwa hiyo siri takatifu inahusu Ufalme wa Mungu wa kimbingu. Ufalme huo utaleta “ole” ya tatu iliyokusudiwa na Mungu, kwa maana utafikiliza hukumu za Mungu dhidi ya ulimwengu wa Shetani mpaka zimalizike kabisa.
Ufalme Wasimamishwa Imara
14. Mpulizo wenye kishindo wa tarumbeta ya saba ya Ufunuo 11:15 ulitangaza nini?
14 Ndipo jambo lenyewe linapotukia! Ufunuo 11:15, NW, unasema: “Na malaika wa saba akapuliza tarumbeta yake. Na sauti kubwa zikatukia katika mbingu, kusema: ‘Ufalme wa ulimwengu ulipata kuwa ufalme wa Bwana yetu [Yehova] na wa Kristo wake, na yeye atatawala akiwa mfalme milele na milele.’” Ndiyo, inatangazwa kwamba Ufalme wa Mungu ukiwa mikononi mwa Kristo ulisimamishwa imara mbinguni mwaka 1914. Na mabaki waliporudishiwa uhai baada ya Vita ya Ulimwengu 1, walitokeza mbele habari hiyo.
15. Katika 1922, ni tukio gani lililokuwa ishara ya kuchomosha mwendo mkubwa katika kuhubiri Ufalme?
15 Kwenye mkusanyiko wa 1922 wa watumishi wa Yehova katika Seda Pointi, Ohaiyo, U.S.A., maelfu wenye kuhudhuria walilisikia tangazo lile la kusisimua: “Hii ndiyo siku ya siku zote. Tazameni, Mfalme atawala! Nyinyi ndio mawakili wake wa utangazaji. Kwa hiyo tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mfalme na ufalme wake.” Hiyo ikachomosha mwendo mkubwa wa kule kuhubiri Ufalme peupe ambako kumetia ndani hukumu zilizotangazwa na malaika saba wapiga-tarumbeta. Leo, watumishi wa Yehova walio karibu milioni tatu na nusu katika makundi zaidi ya 57,000 kote ulimwenguni wanahusika katika huku kuhubiri Ufalme duniani pote. Ni mamiriadi kweli kweli!
16. Katika Ufunuo sura ya 12, ni tukio gani zaidi linalohusu mbingu na dunia lililofunuliwa na mpulizo wenye kishindo wa tarumbeta ya saba?
16 Lakini malaika wa saba ana mengi zaidi ya kufunua. Ufunuo 12:7, NW, unasema kwamba ndipo “vita ikafyatuka katika mbingu.” Mstari wa 9 unatupa sisi tokeo hili la kitendo kilichochukuliwa na Kristo Mfalme: “Hivyo chini yule drakoni mkubwa akavurumishwa, nyoka wa awali kabisa, mmoja ambaye huitwa Ibilisi na Shetani, ambaye anaongoza vibaya dunia nzima yote inayokaliwa; yeye akavurumishwa chini kwenye dunia, na malaika zake wakavurumishwa chini pamoja na yeye.” Mstari wa 12 unaongeza hivi: “Kwa minajili hii mwe na nderemo, nyinyi mbingu na nyinyi ambao hukaa ndani yazo!” Ndiyo, mbingu zilisafishwa sana uvutano wa Shetani, hiyo ikisababisha mshangilio mkubwa miongoni mwa malaika waaminifu. Lakini inamaanisha nini kwa aina ya kibinadamu! Mstari uo huo unajibu hivi: “Ole kwa ajili ya dunia na kwa ajili ya bahari, kwa sababu Ibilisi amekuja chini kwa nyinyi, akiwa na kasirani kubwa, akijua yeye ana kipindi kifupi cha wakati.”
17. Kwa nini inafaa kuonyesha serikali ya ulimwengu ikiwa kama “hayawani-mwitu” katika Ufunuo sura ya 13?
17 Ufunuo 12:3 unaeleza Shetani akiwa kama ‘drakoni mkubwa, mwenye vichwa saba na pembe kumi,’ mharibifu mkubwa sana wa kihayawani. Inaonyesha yeye ndiye aliyebuni “hayawani-mwitu” wa kisiasa duniani anayeelezwa katika sura ya 13, mistari 1 na 2. Hayawani huyo pia ana vichwa saba na pembe kumi, kwa kuiga Shetani. Mstari wa 2, NW, unasema: “Drakoni [Shetani] akampa hayawani nguvu zake na kiti cha ufalme chake na mamlaka kubwa.” Kwa uhakika inafaa kuonyesha serikali za kisiasa zikiwa kama hayawani-mwitu, kwa maana katika karne hii tu ya 20, watu zaidi ya milioni mia moja wameuawa katika vita vya mataifa.
18. Mnyama mwenye pembe mbili wa Ufunuo 13:11 ni nini, na vitendo vyake vinasaidiaje kumtambulisha?
18 Kama mstari wa 11 unavyosema, tamasha inayofuata katika Ufunuo 13 inafunua “hayawani-mwitu mwingine akipanda kutoka katika dunia, na yeye alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini yeye akaanza kunena kama drakoni.” Hayawani huyo mwenye pembe mbili ni muungano wa kisiasa wa Uingereza na Amerika. Huo ni kama kondoo kwa sababu unasingizia kuwa hauna madhara, kuwa namna ya serikali iliyo na nuru nyingi zaidi. Lakini unanena kama drakoni, kama Shetani, na unaitwa “hayawani-mwitu mwingine” kwa sababu vitendo vyao vya kutawala ni vya kihayawani. Huo hufinya watu na kuwatisha na hata kutumia jeuri mahali popote ambapo namna yao ya utawala haikubaliwi. Hauwatii moyo wajiweke chini ya Ufalme wa Mungu, bali waupe heshima nyingi mno ulimwengu wa Shetani. Ndiyo sababu mstari wa 14, NW, unasema: “Yeye huongoza vibaya wale ambao hukaa juu ya dunia.”
19, 20. (a) Ukamilifu wa watumishi wa Yehova unaonyesha nini? (b) Tunajuaje kwamba kwa uhakika mabaki wapakwa-mafuta watapata shangwe ya ushindi juu ya ulimwengu wa Shetani?
19 Ulimwengu huu ulio chini ya utawala wa Shetani ni mahali pagumu pa kuishi kwa wale ambao, kwa kupatana na amri ya Yesu kwa Wakristo wa kweli, si sehemu yao. (Yohana 17:16, NW) Hivyo, jambo la kwamba watumishi wa Yehova kote ulimwenguni wanashika ukamilifu na kuendeleza kwa umoja kutukuza Yehova na njia zake adilifu ni wonyesho wa kutokeza juu ya nguvu na baraka ya Yehova. Wao wanafanya hivyo wajapopatwa na upinzani mkali, mnyanyaso, na hata kifo.
20 Hasa mabaki wapakwa-mafuta wamekuwa shabaha za Shetani kwa sababu ndio watakuwa watawala-wenzi pamoja na Kristo. Lakini Ufunuo sura ya 14 unaonyesha kwamba hesabu kamili yao, 144,000, wanakusanywa kwa shangwe ya ushindi pamoja na Kristo katika mamlaka ya Ufalme. Wao wamemshikilia Bwana wao kwa ushikamanifu, kwa maana kama vile unavyosema mstari wa 4, NW: “Hawa ndio ambao hufuliza kufuata Mwana-Kondoo si kitu aenda wapi”—ujapokuwa mnyanyaso wa ukatili ambao Shetani ameleta juu yao.
Kupokea Hukumu za Mungu Kwanza
21, 22. (a) Malaika wanafanya matangazo gani kwenye Ufunuo 14:7, 8? (b) Kwa nini malaika anatangaza anguko la kidini la Babuloni wakati yeye angali yupo?
21 Kwenye Ufunuo 14:7, NW, malaika analia kwa sauti kubwa hivi: “Hofuni Mungu na kumpa yeye utukufu, kwa sababu saa ya hukumu kwa yeye imewasili, na hivyo abuduni yule Mmoja ambaye alifanyiza mbingu na dunia na bahari na vibubujiko vya maji.” Ni nani anayepokea kwanza hukumu kali ya Mungu? Mstari wa 8 unajibu hivi: “Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, kusema: ‘Ameanguka! Babuloni Mkubwa ameanguka, yeye ambaye alifanya mataifa yote yanywe divai ya kasirani ya uasherati wake!’” Hapa kwa mara ya kwanza, lakini si ya mwisho, Ufunuo unanena juu ya “Babuloni Mkubwa,” ile milki ya duniani pote ya dini bandia.
22 Kwa kuwa dini ingali ikijizoeza uvutano katika sehemu mbalimbali za dunia, kwa nini malaika anatangaza kwamba Babuloni Mkubwa amekwisha kuanguka? Basi, je! kulitokea nini katika 539 K.W.K. wakati Babuloni ya kale ilipoanguka lakini ikawa bado haijaharibiwa kabisa? Kumbe, watumishi watekwa wa Yehova walirudia bara la kwao miaka miwili baadaye na kurudisha ibada ya kweli! Kwa njia iyo hiyo, kurudishwa kwa watumishi wa Mungu kwenye utendaji uliofanywa upya na kwenye ufanisi wa kiroho ulioanza katika 1919 ni ushuhuda wazi kwamba wakati huo, katika 1919, kwa maoni ya Yehova Babuloni Mkubwa alibingirika akielekea chini. Hapo ndipo yeye alimshutumu kupata uangamivu kamili wa baadaye.
23. (a) Njia inaendeleaje kufanywa tayari kwa uharibifu wa Babuloni Mkubwa? (b) Ni manabii gani zaidi yatakayozungumziwa katika toleo linalokuja la Mnara wa Mlinzi?
23 Kwa utangulizi wa utowesho wake unaokaribia, Babuloni wa ki-siku-hizi amekwisha kuingia katika matata ya kina kirefu. Ufisadi wake, ukosefu wa adili, kutofuata haki, na kujiingiza-ingiza katika siasa, umefichuliwa kila mahali. Katika sehemu kubwa ya Ulaya, ni watu wachache wanaoendelea kwenda kanisani. Katika nchi nyingi za kisoshalisti, dini inaonwa kuwa ndiyo “kasumba ya watu.” Pia, Babuloni wa ki-siku-hizi anatiwa fedheha machoni pa wote wanaopenda Neno la Mungu la ukweli. Kwa hiyo sasa yeye ni kama amepanga mstari kungojea zamu yake ya kuuawa kunakomstahili. Ndiyo, “wakati uliowekwa u karibu” kwa matukio yenye kuvunja-vunja ulimwengu! Na katika toleo linalokuja la Mnara wa Mlinzi, makala zaidi za funzo zitazungumzia manabii yaliyo katika Ufunuo kuhusu uharibifu unaokaribia wa “kahaba” wa kidini, na pia wa mfumo mzima wa mambo ya Shetani.
Wewe Ungejibuje?
◻ Mipulizo yenye kishindo ya tarumbeta saba ambayo inaanza kwenye Ufunuo sura ya 8 ina maana gani kwa siku yetu?
◻ Kwa nini Jumuiya ya Wakristo inakuwa ya kwanza kuhukumiwa vikali?
◻ Katika Ufunuo sura ya 9 kazi ya kuhubiri ya mabaki wapakwa-mafuta na “umati mkubwa” inaelezwa kuwa jinsi gani?
◻ Tangazo kwenye Ufunuo 11:15 lilimaanisha nini kwa mbingu na dunia?
◻ Kama inavyoelezwa kwenye Ufunuo 14:8, Babuloni wa kidini aliangukaje katika 1919, na hiyo inamaanisha nini kwake?