Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 5/15 kur. 21-23
  • Jinsi ya Kufaulu katika Huduma ya Painia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kufaulu katika Huduma ya Painia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uhusiano Wangu na Mungu Una Imara ya Kadiri Gani?
  • Mimi Napenda Watu Kadiri Gani?
  • Je! Mimi Nina Ratiba Iliyosawazika?
  • Je! Mimi Ni Mwalimu Mwenye Maendeleo?
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Upainia Huimarisha Uhusiano Wetu na Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mapainia Hutoa na Kupokea Baraka
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Utumishi wa Painia—Je, Wakufaa Wewe?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 5/15 kur. 21-23

Jinsi ya Kufaulu katika Huduma ya Painia

JE! HUDUMA ya painia ndiyo kazi-maisha yako? Ikiwa wewe ni painia, au mpiga mbiu wa wakati wote wa Ufalme, bila shaka unapendezwa na kupata mafanikio. Lakini mafanikio hutaka mengi kuliko kuweza tu kutumia wakati katika kazi fulani ya muda wote. Mtu mwenye mafanikio ni lazima akubali mazoezi na aendelee kusitawisha uwezo wake wakati wote.

Basi, je! ni jinsi gani wewe unaweza kuendelea si kuwa painia tu bali pia kufanya maendeleo katika kazi-maisha yako? Kuna maswali kadhaa makuu ambayo ungeweza kufikiria.

Uhusiano Wangu na Mungu Una Imara ya Kadiri Gani?

Moja la mambo yaliyo ya maana zaidi katika kufaulu kuwa painia ni uhusiano imara, wenye ukaribu, pamoja na Yehova Mungu. Katika habari hii, tunaweza kujifunza somo kwa mtunga zaburi Daudi. Yeye alisihi hivi: “Ee Bwana [Yehova, NW], unijulishe njia zako, unifundishe mapito yako, uniongoze katika kweli yako, na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, nakungoja [nimekutumaini, NW] Wewe mchana kutwa.”​—Zaburi 25:4, 5.

Daudi alimtegemea kabisa ‘Mungu wa wokovu wake.’ Alitamani kwamba Yehova amfundishe na ‘kumjulisha njia Zake.’ Je! wewe huwezi kuihisi tamaa ya Daudi yenye kumwaka sana akitaka kufurahisha Mungu? Huo haukuwa utakaji wa kikawaida tu, kwa maana Daudi alisema: ‘Nimekutumaini wewe mchana kutwa.’

Lakini unaweza kudumishaje uhusiano wa karibu jinsi hiyo pamoja na Yehova? Angalia kwamba yaliyotangulia yalisemwa na Daudi katika sala. Ndiyo, kuwasiliana kupitia sala ndio msingi wa uhusiano mwema pamoja na Mungu. Na sisi tunaweza kujipatia faraja kwa kujua kwamba hakuna uhitaji wa kupanga wakati rasmi wa kuongea na Baba yetu wa kimbingu. Tunaweza kumfikia wakati wowote. Kama alivyosema Daudi: “Nakulilia Wewe mchana kutwa.” (Zaburi 86:3) Hata Mwana wa Mungu mwenyewe, aliyetembea duniani akiwa mwanadamu mkamilifu, alitambua kwamba hangeweza kufaulu bila msaada wa Baba yake. Yesu alinena kwake katika sala siku nzima​—mapema asubuhi, mchana, na mpaka usiku.​—Marko 1:35; Luka 11:1; 6:12.

Sisi tulio Wakristo, tunahitaji kufuata kielelezo cha Yesu ikiwa tutafaulu katika huduma yetu. (Waebrania 5:7) Kuhusu sala, mwanamke mmoja Mkristo ambaye amekuwa painia mwenye mafanikio kwa miaka 30 alieleza hivi maoni yake: “Mimi hupata kwamba nahitaji sala kabisa ikiwa nitafaulu nikiwa painia. Imenisaidia kumtegemea Yehova kabisa, nikitambua kwamba singeweza kufaulu mimi peke yangu. Mimi humwomba Yehova daima anisaidie kuendelea.”

Ndiyo, ili kufaulu katika utumishi wa painia, unahitaji kudumisha uhusiano imara pamoja na Yehova, ukimtegemea yeye kabisa kupitia sala. Hata hivyo, linalofuata ni swali jingine la maana kujiuliza mwenyewe.

Mimi Napenda Watu Kadiri Gani?

Kupainia ni wonyesho wa upendo. Kwa nini? Kwa sababu huduma ya wakati wote inahusisha ndani roho ya kujidhabihu. Ukiwa painia, unakuwa ukitoa daima wakati na nishati zako kusaidia wengine. Lakini ikiwa utaendelea kufanya hivi, ni lazima uwe na upendezo halisi katika mahitaji ya wengine. Alipokuwa duniani, Yesu aliwaonyesha watu upendo wa jinsi hiyo. Kwa kielelezo, ilikuwako pindi ile ambapo yeye na wanafunzi wake walikuwa wakienda kwa mashua kuelekea mahali pasipokuwa na watu ili ‘wakapumzike kidogo.’ Hata hivyo, umati wa watu ulifika pale mbele yao. “Naye aliposhuka mashuani, akaona mkutano mkuu, akawahurumia; kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji; akaanza kuwafundisha mambo mengi.”​—Marko 6:30-34.

Kama Yesu, sisi tulio mapainia ni lazima tuwe na upendo wenye mizizi ya kina kirefu kwa watu. Upendo wa jinsi hiyo hutusukuma tujitoe sana kwa ajili yao. Kama vile mwandishi mmoja alivyosema kwa Yesu: “Na kumpenda [Mungu] kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko sadaka nzima za kuteketezwa na dhabihu zote pia.” (Marko 12:33) Maneno haya yanatusaidia kuthamini kwamba si yale tu tunayofanya katika huduma yetu yaliyo ya maana bali pia sababu ya sisi kuyafanya.

Wewe uliye painia, unatumia wakati mwingi katika kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kuliko wanavyofanya wengine walio wengi zaidi. Lakini pia unakutana na watu wengi zaidi. Wewe unahisije juu yao? Painia mmoja alisema: “Mimi najua kwamba upendo ni tunda la roho ya Mungu. Kwa hiyo bila hilo singekuwa katika ukweli hata kidogo, licha ya kufaulu nikiwa painia. Upendo hunifanya niwajali watu, niyajue mahitaji yao, nami huthamini kwamba watu huitikia upendo. Bila shaka, kuna nyakati ambapo upendo wako kwa watu utajaribiwa kwa sababu ya mielekeo au njia zao za kufikiri. Hapo hasa ndipo mimi hujaribu kusikiliza na kuwa mwenye saburi.”

Je! wewe unahisi hivyo juu ya watu katika eneo lako? Ili uwe painia mwenye mafanikio, ni lazima upende watu. (1 Wathesalonike 2: 6-8) Hata hivyo, ili uwe na matokeo katika kazi-maisha yako ya kupainia, unahitaji ratiba njema pia. Hivyo, jiulize hivi:

Je! Mimi Nina Ratiba Iliyosawazika?

Ili kuendelea kwa mafanikio katika huduma ya wakati wote, ni lazima painia awe amejipanga vizuri kitengenezo. Bila ratiba njema ya kibinafsi, huenda kupainia kukavuruga akili. Bila shaka, kuwa na ratiba inayoruhusu kutumia kiasi fulani hasa cha wakati katika huduma ya shambani siyo mambo yote yanayohusika.

Painia anahitaji kuwa na ratiba iliyosawazika. Je! wewe una moja? Ungeweza kujiuliza hivi: Je! mimi ninatumia kiasi kinachofaa cha wakati katika pande mbalimbali za huduma? Je! naweza kusema kwamba ninatia kila jitihada kuwafikia watu katika eneo? Je! ninafanya marekebisho yanayohitajiwa katika ratiba yangu ili kuzuru wakati wanapokuwa nyumbani? Je! mimi nafanya ziara za kurudia zenye matokeo? Yesu alisema: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu . . . kuwafundisha.” (Mathayo 28: 19, 20, NW) Yote mawili kuhubiri na kufundisha ni sehemu zinazohitajiwa kabisa za huduma yetu. Je! wewe unatosheka kuangusha vitabu, au unarudia wote wanaoonyesha kupendezwa, wawe walikubali au hawakukubali vitabu? Kwa ufupi, je! unatumia wakati wako kwa njia iliyo bora?

Je! Mimi Ni Mwalimu Mwenye Maendeleo?

Hilo ni swali jingine la maana. Kwenye 2 Timotheo 4:2, NW, Paulo aliandika hivi: “Lihubiri neno, fanya hivyo kwa haraka katika majira yanayofaa, katika majira yenye taabu, . . . kwa ustahimilivu wote na ustadi wa kufundisha.” Ili kulihubiri neno, iwe ni ndani au nje ya kundi, mapainia wenye mafanikio hujitahidi kujipatia na kuendeleza sana ustadi wa kufundisha. Kwa nini Paulo anaita kufundisha kuwa ni ustadi? Kwa sababu kufundisha kunataka ujuzi na mazoezi.

Utaendelezaje ujuzi wako ukiwa mwalimu? Mtume Paulo anajibu hivi: “Uyatafakari hayo; ukae katika hayo; ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote.” (1 Timotheo 4:15) Ndiyo, ni lazima mapainia watoe wakati kuhusu funzo la kibinafsi la Biblia, kuwaza, na kutafakari. Hii inatia ndani utumizi wenye mafaa wa madokezo yanayopatikana katika vichapo kama Reasoning From the Scriptures, Huduma ya Ufalme Yetu, na Kiongozi cha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.a

Kwa hiyo, ili kufaulu katika huduma ya painia, dumisha uhusiano wako wa kibinafsi ulio imara pamoja na Yehova. Hii, nayo, itakusukuma ujipatie na kuonyesha upendo wenye mizizi ya kina kirefu kwa watu. Bila shaka, ili kuonyesha upendo huu, si kwamba ni lazima wewe ujue kiasi cha wakati unaoumia katika huduma, bali ni lazima pia utake kutumia wakati wako kwa njia iliyo bora. Jinsi gani? Kwa kutia kila jitihada inayohitajiwa ili kufikia watu wengi iwezekanavyo ukiwa na ujumbe wa Ufalme. Mwisho, zidi kuwa na maendeleo ukiwa mwalimu kwa kujifunza njia tofauti za kufikia watu katika huduma na ujifunze Biblia kwa bidii-endelevu kwa kusudi la kuendeleza sana ustadi wako wa kufundisha.

[Maelezo ya Chini]

a Vinatangazwa kwa chapa na Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti ya New York.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki