Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 10/15 kur. 3-4
  • Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wafu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wafu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Je! Wafu Wako Hai?’
  • Je! Wafu Wataishi Tena?
  • Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Uhai Baada ya Kifo—Biblia Husema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Nafsi Yako Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Imani Yako Katika Ufufuo Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 10/15 kur. 3-4

Kuna Tumaini Gani kwa Ajili ya Wafu?

JAMAA changa ilikuwa ikisafiri kwenda kwenye pwani ya mashariki ya Afrika Kusini kwa ajili ya likizo. Wazazi wa mke walikuwa katika gari jingine hapo mbele tu. Kwa ghafula, mpira wa gurudumu ulipasuka. Walipokuwa wakijitayarisha kuubadili upande mmoja wa barabara, dereva mlevi alikuruza gari lake likayalima yale magari mawili. Mwanamume yule mzee-mzee na mke wake walikufa. Mwanamume aliye kijana kidogo alikufa siku chache baadaye. Mke wake alivunjika mbavu na akapata maumizo mengine. Mtoto wake mchanga alipata uharibifu wa ubongo ukamfanya apooze.

Loo, ni tanzia iliyoje kwa jamaa hii iliyopata msiba usiotazamiwa! Carolann, dada ya yule mke kijana, alipopata habari, aliduwaa kwa kulemewa na hisia. Tanzia kama hizi hutukia katika nchi zote. Watu wa ukoo na marafiki wenye kupigwa dharuba kali ya kihoro hushangaa wakijiuliza hivi, ‘Je! kweli wafu wamekufa,’ au . . .

‘Je! Wafu Wako Hai?’

Karibu dini zote hufundisha kwamba nafsi haifi. Kwa sababu hiyo, wafuasi wao huamini kwamba wale ambao hufa hawawi wafu kweli kweli bali wangali hai mbinguni, katika purgatori, au helo. Kama ifundishwavyo katika makanisa mengi, wale walio katika mahali hapa palipotajwa mwisho huteseka vibaya sana kwa umilele wote. Lakini je! kweli Mungu wa upendo angeleta mteseko huo juu ya viumbe wake?—1 Yohana 4:8.

Ingeonekana kwamba hangeuleta, lakini twawezaje kuwa na uhakika? Fikiria kwa uangalifu uthibitisho unaofuata wa Biblia. “Bwana [Yehova, NW] Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” (Mwanzo 2:7) Je! taarifa hii iliyovuviwa yasema kwamba mwanadamu wa kwanza, Adamu, alipewa nafsi? Sivyo, yeye alikuja kuwa nafsi, mtu hai. Hilo lahakikishwa na mtume Paulo, aliyeandika hivi: “Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai.” Paulo alikuwa akinukuu kutokana na kitabu cha Mwanzo. — 1 Wakorintho 15:45.

Je! nafsi ya kibinadamu yaweza kufa? Nabii Ezekieli aliandika hivi: “Nafsi zote—ni zangu mimi. Kama vile nafsi ya.baba kadhalika na nafsi ya mwana—ni zangu mimi. Ile nafsi inayofanya dhambi—hiyo yenyewe ndiyo itakayokufa.” (Ezekieli 18:4, 20, NW; Mhubiri 9:5, 10, NW) Kwa uwazi, ikiwa nafsi imekufa, basi mtu yule hajui lolote, na kwa sababu hiyo hawezi kuwa anateseka. Katika hotuba ya watu wote aliyoitoa kwanza baada ya Pentekoste 33 W.K., mtume Petro alijulisha wazi hivi: “Kweli kweli, nafsi yoyote ambayo haisikilizi Nabii huyo [Yesu] itaharibiwa kabisa kutoka miongoni mwa watu.” Kwa hiyo nafsi hufa.—Matendo 3:23, NW.

Je! Wafu Wataishi Tena?

Wote wale ambao waamini kwamba Biblia ni kweli wajua kwamba Yesu alikufa akafufuliwa siku ya tatu. (Matendo 10:39, 40) Hilo lingeweza kutukiaje? Kwa nguvu ya roho takatifu ya Mungu.

Je! ufufuo wa Yesu ulikuwa tofauti tu? Sivyo. Kama vile Paulo alivyoandikia kundi katika Korintho: “Kristo ameinuliwa kutoka kwa wafu, matunda ya kwanza ya wale ambao wamelala usingizi katika kifo. Kwa kuwa kifo ni kupitia mwanadamu, ufufuo wa wafu pia ni kupitia mwanadamu . . . Kristo.” (1 Wakorintho 15:20-22, NW) Kwa sababu hiyo, wengi watainuliwa kutoka kwa wafu. Pia Yesu alisema hivi: “Msione hili kuwa ajabu, kwa sababu ile saa inakuja ambayo katika hiyo wote wale walio katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na waje nje, wale waliofanya mambo mema kwenye ufufuo wa uhai.” (Yohana 5:28, 29, NW) Hiyo yatoa uhakikisho kamili juu ya ufufuo wa mamilioni.

Ikiwa uelezaji ulio juu umeamsha upendezi wako katika ufufuo, huenda wewe ukauliza ‘Ufufuo ni kwa ajili ya nani, na wakati gani?’ Acheni tufikirie maswali hayo muhimu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki